7 Na wa kwanza akaipiga tarumbeta yake. Na kukatukia mvua ya mawe na moto+ uliochangamana na damu, nao ukatupwa duniani; na sehemu ya tatu ya dunia ikateketezwa,+ na sehemu ya tatu ya miti ikateketezwa, na mimea yote mibichi+ ikateketezwa.
8 Na malaika wa pili akaipiga tarumbeta yake. Na kitu fulani kama mlima+ mkubwa unaowaka moto kikatupwa ndani ya bahari.+ Na sehemu ya tatu ya bahari ikawa damu;+
10 Na malaika wa tatu akaipiga tarumbeta yake. Na nyota kubwa inayowaka kama taa ikaanguka kutoka mbinguni,+ nayo ikaanguka juu ya sehemu ya tatu ya mito na juu ya chemchemi za maji.+
12 Na malaika wa nne akaipiga tarumbeta yake. Na sehemu ya tatu ya jua ikapigwa na sehemu ya tatu ya mwezi na sehemu ya tatu ya nyota, ili sehemu ya tatu ya hizo itiwe giza+ na mchana usiwe na nuru kwa sehemu yake ya tatu,+ na usiku vivyo hivyo.
9Na malaika wa tano akaipiga tarumbeta yake.+ Nami nikaona nyota+ iliyokuwa imeanguka kutoka mbinguni mpaka duniani, naye akapewa ufunguo+ wa shimo la abiso.+
15 Na malaika wa saba akaipiga tarumbeta yake.+ Na sauti kubwa zikatokea mbinguni, zikisema: “Ufalme wa ulimwengu umekuwa ufalme wa Bwana+ wetu na wa Kristo+ wake, naye atatawala akiwa mfalme milele na milele.”+