Zaburi
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
2 Wale ambao wamepanga mambo mabaya moyoni mwao,+
Ambao mchana kutwa wanaendelea kushambulia kama katika vita.+
4 Unilinde, Ee Yehova, na mikono ya mwovu;+
Unilinde na mtu mwenye matendo ya jeuri,+
Wale ambao wamepanga hila ya kuzisukuma hatua zangu.+
5 Waliojiinua wenyewe wameficha mtego kwa ajili yangu;+
Nao wamezitandika kamba kama wavu kando ya njia.+
Wametega minaso kwa ajili yangu.+ Sela.
6 Nimemwambia Yehova: “Wewe ni Mungu wangu.+
Utege sikio, Ee Yehova, usikie sauti ya kusihi kwangu.”+
7 Ee Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu,+ nguvu za wokovu wangu,+
Umekinga kichwa changu katika siku ya jeshi lenye silaha.+
10 Makaa yanayowaka moto na yaangushwe juu yao.+
Na waangushwe motoni,+ ndani ya mashimo yenye maji, ili wasipate kusimama.+