Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Hesabu 27:12-14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Kisha Yehova akamwambia Musa: “Panda mlima huu wa Abarimu,+ uione nchi nitakayowapa Waisraeli.+ 13 Baada ya kuiona, utakufa pia na kuzikwa pamoja na watu wako,*+ kama Haruni ndugu yako alivyozikwa,+ 14 kwa sababu Waisraeli walipokuwa wakigombana nami katika nyika ya Zini, mliasi agizo langu la kunitakasa mbele yao nilipowapa maji.+ Hayo ndiyo maji ya Meriba+ huko Kadeshi+ katika nyika ya Zini.”+

  • Kumbukumbu la Torati 1:37
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 37 (Yehova alinikasirikia mimi pia kwa sababu yenu, akasema, “Wewe pia hutaingia humo.+

  • Kumbukumbu la Torati 3:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Lakini bado Yehova alikuwa amenikasirikia vikali kwa sababu yenu,+ naye hakutaka kunisikiliza. Badala yake Yehova aliniambia, ‘Imetosha! Usizungumze nami tena kamwe kuhusu jambo hili.

  • Kumbukumbu la Torati 32:51, 52
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 51 kwa sababu nyote wawili hamkuwa waaminifu kwangu miongoni mwa Waisraeli kwenye maji ya Meriba+ kule Kadeshi katika nyika ya Zini, kwa sababu hamkunitakasa mbele ya Waisraeli.+ 52 Utaiona nchi hiyo kwa mbali, lakini hutaingia katika nchi hiyo ninayowapa Waisraeli.”+

  • Kumbukumbu la Torati 34:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Kisha Yehova akamwambia hivi: “Hii ndiyo nchi ambayo nilimwapia Abrahamu, Isaka, na Yakobo, niliposema, ‘Nitaupa uzao wako* nchi hii.’+ Nimekuruhusu uione kwa macho yako mwenyewe, lakini hutavuka kuingia humo.”+

  • Yoshua 1:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 “Musa mtumishi wangu amekufa.+ Sasa jitayarishe, vuka Mto Yordani pamoja na watu hawa wote, mwingie katika nchi ambayo ninawapa Waisraeli.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki