-
Kumbukumbu la Torati 21:18-21Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
18 “Ikiwa mtu ana mwana ambaye ni mkaidi na mwasi na hamtii baba yake au mama yake,+ nao wamejaribu kumrekebisha lakini anakataa kuwasikiliza,+ 19 baba yake na mama yake wanapaswa kumshika na kumpeleka kwa wazee kwenye lango la jiji lake 20 na kuwaambia hivi wazee wa jiji lake: ‘Huyu mwana wetu ni mkaidi na mwasi, anakataa kututii. Ni mlafi+ na mlevi.’+ 21 Basi watu wote wa jiji lake watamuua kwa kumpiga mawe. Kwa hiyo ni lazima mwondoe uovu miongoni mwenu, na Waisraeli wote watasikia na kuogopa.+
-