-
2 Wafalme 22:18, 19Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
18 Lakini mwambieni hivi mfalme wa Yuda aliyewatuma kutafuta ushauri wa Yehova: “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Kuhusu maneno ambayo umesikia, 19 kwa sababu moyo wako ulikuwa msikivu,* nawe ukajinyenyekeza+ mbele za Yehova uliposikia mambo niliyosema dhidi ya mahali hapa na wakaaji wake—kwamba watakuwa kitu cha kutisha na laana—nawe ukayararua mavazi yako+ na kulia mbele zangu, mimi pia nimekusikia, asema Yehova.
-
-
Luka 15:22-24Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
22 Lakini baba yake akawaambia watumwa, ‘Leteni upesi kanzu bora zaidi na kumvika, pia mvisheni pete mkononi na viatu miguuni. 23 Vilevile, leteni ndama aliyenoneshwa, mchinjeni, nasi tule na tusherehekee, 24 kwa sababu huyu mwanangu alikuwa amekufa na sasa yuko hai;+ alikuwa amepotea naye amepatikana.’ Basi wakaanza kusherehekea.
-
-
Luka 18:13, 14Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 Lakini yule mkusanya kodi alikuwa amesimama mbali kidogo na hata hakutaka kutazama mbinguni, bali alijipigapiga kifuani akisema, ‘Ee Mungu, nihurumie* mimi mtenda dhambi.’+ 14 Ninawaambia, mtu huyu alishuka kwenda nyumbani akiwa mwadilifu mbele za Mungu kuliko yule Farisayo.+ Kwa sababu kila mtu anayejiinua atafedheheshwa, lakini yeyote anayejinyenyekeza atainuliwa.”+
-