Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 22:18, 19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Lakini mwambieni hivi mfalme wa Yuda aliyewatuma kutafuta ushauri wa Yehova: “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Kuhusu maneno ambayo umesikia, 19 kwa sababu moyo wako ulikuwa msikivu,* nawe ukajinyenyekeza+ mbele za Yehova uliposikia mambo niliyosema dhidi ya mahali hapa na wakaaji wake—kwamba watakuwa kitu cha kutisha na laana—nawe ukayararua mavazi yako+ na kulia mbele zangu, mimi pia nimekusikia, asema Yehova.

  • 2 Mambo ya Nyakati 33:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Aliendelea kusali kwa Mungu, naye akaguswa na sala yake ya kusihi, akasikia ombi lake la kutaka kibali, akamrudisha Yerusalemu kwenye ufalme wake.+ Ndipo Manase akajua kwamba Yehova ndiye Mungu wa kweli.+

  • Zaburi 22:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Kwa maana hajadharau wala kuchukizwa na mateso ya yule anayekandamizwa;+

      Hajauficha uso wake kutoka kwake.+

      Alipomlilia amsaidie, alisikia.+

  • Zaburi 34:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Yehova yuko karibu na wale waliovunjika moyo;+

      Huwaokoa waliopondeka roho.*+

  • Methali 28:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Anayefunika makosa yake hatafanikiwa,+

      Lakini yeyote anayeyaungama na kuyaacha ataonyeshwa rehema.+

  • Isaya 57:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Kwa maana Yule Aliye Juu na Aliyetukuka Sana,

      Anayeishi* milele+ na ambaye jina lake ni takatifu+ anasema hivi:

      “Ninaishi mahali palipo juu na patakatifu,+

      Lakini ninaishi pia na wale waliopondwa na wenye roho ya unyenyekevu,

      Ili kuihuisha roho ya watu wa hali ya chini

      Na kuuhuisha moyo wa wale wanaopondwa.+

  • Luka 15:22-24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Lakini baba yake akawaambia watumwa, ‘Leteni upesi kanzu bora zaidi na kumvika, pia mvisheni pete mkononi na viatu miguuni. 23 Vilevile, leteni ndama aliyenoneshwa, mchinjeni, nasi tule na tusherehekee, 24 kwa sababu huyu mwanangu alikuwa amekufa na sasa yuko hai;+ alikuwa amepotea naye amepatikana.’ Basi wakaanza kusherehekea.

  • Luka 18:13, 14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Lakini yule mkusanya kodi alikuwa amesimama mbali kidogo na hata hakutaka kutazama mbinguni, bali alijipigapiga kifuani akisema, ‘Ee Mungu, nihurumie* mimi mtenda dhambi.’+ 14 Ninawaambia, mtu huyu alishuka kwenda nyumbani akiwa mwadilifu mbele za Mungu kuliko yule Farisayo.+ Kwa sababu kila mtu anayejiinua atafedheheshwa, lakini yeyote anayejinyenyekeza atainuliwa.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki