Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 6:10-12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 “Yehova Mungu wenu atakapowaleta katika nchi aliyowaapia mababu zenu Abrahamu, Isaka, na Yakobo kwamba atawapa ninyi+—majiji makubwa na yenye kupendeza ambayo hamkujenga,+ 11 nyumba zilizojaa vitu vizuri vya aina mbalimbali ambavyo hamkufanya kazi ili kuvipata, visima ambavyo hamkuchimba, na mashamba ya mizabibu na mizeituni ambayo hamkupanda—nanyi mtakapokuwa mmekula na kushiba,+ 12 jihadharini msimsahau Yehova,+ aliyewatoa nchini Misri, kutoka katika nyumba ya utumwa.

  • Ayubu 31:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Ikiwa nilifanya dhahabu kuwa tumaini langu

      Au kuiambia dhahabu bora, ‘Wewe ni mlinzi wangu!’+

  • Ayubu 31:28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 Basi hilo ni kosa linalostahili adhabu kutoka kwa waamuzi,

      Kwa maana nitakuwa nimemkana Mungu wa kweli aliye juu.

  • Methali 11:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  4 Mali haitakuwa* na faida yoyote siku ya ghadhabu,+

      Lakini uadilifu ndio utakaookoa kutoka katika kifo.+

  • Methali 11:28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 Anayeutumaini utajiri wake ataanguka,+

      Lakini waadilifu watasitawi kama majani.+

  • Methali 23:4, 5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  4 Usijichoshe kupata utajiri.+

      Acha, na uonyeshe uelewaji.*

       5 Ukiutupia jicho, haupo,+

      Kwa maana hakika utaota mabawa kama ya tai na kuruka mbali angani.+

  • Mathayo 6:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 “Acheni kujiwekea hazina duniani,+ ambako nondo* na kutu hula na ambako wezi huvunja na kuiba.

  • Mathayo 6:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 “Hakuna anayeweza kuwatumikia mabwana wawili; kwa maana atamchukia mmoja na kumpenda mwingine,+ au atashikamana na mmoja na kumdharau mwingine. Hamwezi kutumikia Mungu na Utajiri.+

  • Marko 8:36
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 36 Kwa kweli, mtu atapata faida gani akiupata ulimwengu wote kisha apoteze uhai wake?*+

  • Luka 12:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Ndipo akawaambia: “Endeleeni kufungua macho yenu na mjilinde na kila aina ya pupa,*+ kwa sababu hata mtu anapokuwa na vitu vingi, uhai wake hautokani na vitu alivyo navyo.”+

  • 1 Timotheo 6:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Waagize* wale walio matajiri katika mfumo wa mambo* wa sasa wasijivune* wala wasiutumaini utajiri usiotegemeka,+ bali wamtumaini Mungu, ambaye hutupatia kwa wingi vitu vyote tunavyofurahia.+

  • 1 Yohana 2:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 kwa sababu kila kitu katika ulimwengu—tamaa ya mwili+ na tamaa ya macho+ na mtu kujionyesha mali zake maishani*—hakitokani na Baba, bali hutokana na ulimwengu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki