Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 15:1-5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Ee Yehova, ni nani anayeweza kuwa mgeni katika hema lako?

      Ni nani anayeweza kukaa katika mlima wako mtakatifu?+

       2 Yule anayetembea bila kosa,*+

      Anayezoea kutenda yaliyo sawa+

      Na kusema ukweli moyoni mwake.+

       3 Hachongei kwa ulimi wake,+

      Hamtendei jirani yake jambo lolote ovu,+

      Naye hawaharibii sifa* rafiki zake.+

       4 Humkataa mtu yeyote anayedharauliwa,+

      Lakini huwaheshimu wale wanaomwogopa Yehova.

      Havunji ahadi yake, hata ikimletea hasara.*+

       5 Hakopeshi pesa zake kwa faida,+

      Naye hakubali rushwa ili kumkandamiza asiye na hatia.+

      Yeyote anayefanya mambo hayo hatatikiswa kamwe.*+

  • Zaburi 27:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  4 Nimemwomba Yehova jambo moja

      —Ndilo nitakalolitafuta—

      Kwamba nikae katika nyumba ya Yehova sikuzote za maisha yangu,+

      Ili kuutazama uzuri wa Yehova

      Na kutazama kwa uthamini* hekalu lake.*+

  • Zaburi 84:1-4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 84 Jinsi linavyovutia sana* hema lako tukufu la ibada,+

      Ee Yehova wa majeshi!

       2 Nafsi yangu yote inatamani,

      Naam, ninazimia kwa kutamani,

      Nyua za Yehova.+

      Moyo wangu na mwili wangu humshangilia kwa sauti Mungu aliye hai.

       3 Hata ndege hupata makao huko

      Na mbayuwayu hujipatia kiota,

      Ambamo huyatunza makinda wake

      Karibu na madhabahu yako tukufu, Ee Yehova wa majeshi,

      Mfalme wangu na Mungu wangu!

       4 Wenye furaha ni wale wanaokaa katika nyumba yako!+

      Wanaendelea kukusifu.+ (Sela)

  • Zaburi 84:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Kwa maana siku moja katika nyua zako ni bora kuliko siku elfu moja kwingineko!+

      Ninachagua kusimama kwenye kizingiti cha nyumba ya Mungu wangu

      Badala ya kukaa katika mahema ya uovu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki