6 Kuna wale wanaomwaga dhahabu kwa wingi kutoka kwenye mikoba yao;
Wanapima fedha katika mizani.
Wanamwajiri mfua chuma, naye huitengeneza kuwa mungu.+
Kisha wanasujudu, naam, wanaiabudu.+
7 Wanaiinua na kujitwika mabegani;+
Wanaibeba na kuiweka mahali pake, nayo husimama papo hapo.
Haiondoki mahali pake.+
Wanaipazia sauti, lakini haiwajibu;
Haiwezi kumwokoa yeyote kutoka katika taabu yake.+