-
Isaya 11:11, 12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Siku hiyo Yehova ataunyoosha tena mkono wake, mara ya pili, ili kuwakomboa watu wake waliobaki kutoka Ashuru,+ kutoka Misri,+ kutoka Pathrosi,+ kutoka Kushi,+ kutoka Elamu,+ kutoka Shinari,*+ kutoka Hamathi, na kutoka katika visiwa vya bahari. 12 Atainua ishara* kwa ajili ya mataifa na kuwakusanya watu wa Israeli+ waliotawanywa, na watu wa Yuda waliotawanywa atawakusanya pamoja kutoka katika pembe nne za dunia.+
-