-
Isaya 13:11Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
Nitakikomesha kiburi cha wenye kimbelembele,
Nami nitayashusha majivuno ya waonevu.+
-
-
Yeremia 27:6, 7Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Na sasa mimi mwenyewe nimezitia nchi hizi zote mikononi mwa mtumishi wangu Mfalme Nebukadneza+ wa Babiloni; nimempa hata wanyama wa mwituni ili wamtumikie. 7 Mataifa yote yatamtumikia yeye na mwanawe na mjukuu wake mpaka wakati wa nchi yake utakapofika,+ wakati ambapo mataifa mengi na wafalme wakuu watamfanya kuwa mtumwa wao.’+
-
-
Yeremia 50:1, 2Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
50 Neno ambalo Yehova alisema kuhusu Babiloni,+ kuhusu nchi ya Wakaldayo, kupitia nabii Yeremia:
2 “Semeni jambo hili kati ya mataifa na mlitangaze.
Inueni ishara* na mlitangaze.
Msifiche jambo lolote!
Semeni, ‘Babiloni ametekwa.+
Beli ameaibishwa.+
Merodaki ameshikwa na hofu.
Sanamu zake zimeaibishwa.
Sanamu zake zinazochukiza* zimeshikwa na hofu.’
-