Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 13:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Nitaiadhibu* dunia inayokaliwa kwa sababu ya ubaya wake,+

      Na waovu kwa sababu ya uovu wao.

      Nitakikomesha kiburi cha wenye kimbelembele,

      Nami nitayashusha majivuno ya waonevu.+

  • Yeremia 25:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 “‘Lakini miaka 70 itakapotimia,+ nitamfanya mfalme wa Babiloni awajibike* na pia taifa hilo kwa sababu ya kosa lao,’+ asema Yehova, ‘nami nitaifanya nchi ya Wakaldayo kuwa mahame na ukiwa daima.+

  • Yeremia 27:6, 7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Na sasa mimi mwenyewe nimezitia nchi hizi zote mikononi mwa mtumishi wangu Mfalme Nebukadneza+ wa Babiloni; nimempa hata wanyama wa mwituni ili wamtumikie. 7 Mataifa yote yatamtumikia yeye na mwanawe na mjukuu wake mpaka wakati wa nchi yake utakapofika,+ wakati ambapo mataifa mengi na wafalme wakuu watamfanya kuwa mtumwa wao.’+

  • Yeremia 50:1, 2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 50 Neno ambalo Yehova alisema kuhusu Babiloni,+ kuhusu nchi ya Wakaldayo, kupitia nabii Yeremia:

       2 “Semeni jambo hili kati ya mataifa na mlitangaze.

      Inueni ishara* na mlitangaze.

      Msifiche jambo lolote!

      Semeni, ‘Babiloni ametekwa.+

      Beli ameaibishwa.+

      Merodaki ameshikwa na hofu.

      Sanamu zake zimeaibishwa.

      Sanamu zake zinazochukiza* zimeshikwa na hofu.’

  • Yeremia 51:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 “Isugueni mishale;+ chukueni ngao za mviringo.*

      Yehova ameichochea roho ya wafalme wa Wamedi,+

      Kwa sababu anakusudia kuiangamiza Babiloni.

      Kwa maana hiki ndicho kisasi cha Yehova, kisasi kwa ajili ya hekalu lake.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki