Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 30:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 “Nawe, mtumishi wangu Yakobo, usiogope,” asema Yehova,

      “Wala usihofu, Ee Israeli.+

      Kwa maana nitakuokoa kutoka mbali

      Na uzao wako kutoka katika nchi waliyopelekwa utekwani.+

      Yakobo atarudi na kuwa na utulivu bila usumbufu,

      Na hakuna yeyote atakayewaogopesha.”+

  • Ezekieli 34:28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 Hawatakuwa windo la mataifa tena, na wanyama wa mwituni wa dunia hawatawanyafua, nao wataishi kwa usalama, na hakuna mtu atakayewaogopesha.+

  • Ezekieli 39:25, 26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Nitawarudisha watu wa Yakobo waliotekwa+ na kuwaonyesha rehema watu wote wa nyumba ya Israeli;+ nami nitalitetea jina langu takatifu kwa bidii.*+ 26 Baada ya kufedheheshwa kwa sababu ya ukosefu wao wote wa uaminifu kunielekea,+ watakaa kwa usalama katika nchi yao, na hakuna mtu atakayewaogopesha.+

  • Hosea 2:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Siku hiyo nitafanya agano na wanyama wa mwituni kwa ajili ya watu wangu,+

      Pia na ndege wa angani na viumbe wa ardhini wanaotambaa;+

      Nitaondoa upinde na upanga na vita nchini,+

      Nami nitawafanya walale* kwa usalama.+

  • Mika 4:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  4 Wataketi,* kila mtu chini ya mzabibu wake na chini ya mtini wake,+

      Na hakuna yeyote atakayewaogopesha,+

      Kwa maana kinywa cha Yehova wa majeshi kimesema hayo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki