-
1 Wakorintho 11:23-25Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
23 Kwa maana nilipokea kutoka kwa Bwana kile nilichowapa ninyi pia, kwamba Bwana Yesu katika usiku+ ambao alisalitiwa alichukua mkate, 24 na baada ya kutoa shukrani, akaumega na kusema: “Huu unamaanisha mwili wangu,+ ambao ni kwa ajili yenu. Endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka.”+ 25 Akafanya vivyo hivyo na kile kikombe+ pia, baada ya wao kula mlo wa jioni, akisema: “Kikombe hiki kinamaanisha agano+ jipya kwa msingi wa damu yangu.+ Endeleeni kufanya hivi, kila mara mnapokinywa, kwa kunikumbuka mimi.”+
-