Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Mambo ya Nyakati 3
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

2 Mambo ya Nyakati—Yaliyomo

      • Sulemani aanza kujenga hekalu (1-7)

      • Patakatifu Zaidi (8-14)

      • Nguzo mbili za shaba (15-17)

2 Mambo ya Nyakati 3:1

Marejeo

  • +1Fa 6:1, 37
  • +Mwa 22:2, 14
  • +2Sa 24:25; 1Nya 21:18
  • +2Sa 24:18; 1Nya 21:22

2 Mambo ya Nyakati 3:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Kipimo cha kawaida cha mkono mmoja kililingana na sentimita 44.5 (inchi 17.5), lakini baadhi ya watu wanahisi kwamba “kipimo cha awali” kinarejelea kipimo cha mkono mrefu ambacho kililingana na sentimita 51.8 (inchi 20.4). Angalia Nyongeza B14.

Marejeo

  • +1Fa 6:2

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Ufahamu,

  • Fahirishi ya Machapisho

    bi12 1960

2 Mambo ya Nyakati 3:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mikono 20 kufikia upana wa nyumba.”

  • *

    Kipimo kisichojulikana.

Marejeo

  • +1Fa 6:3

2 Mambo ya Nyakati 3:5

Marejeo

  • +1Fa 6:15, 22
  • +1Fa 6:29
  • +1Fa 6:21

2 Mambo ya Nyakati 3:6

Marejeo

  • +1Nya 29:2, 8
  • +1Nya 29:3, 4

2 Mambo ya Nyakati 3:7

Marejeo

  • +Kut 26:29
  • +Kut 26:1; 1Fa 6:29

2 Mambo ya Nyakati 3:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “nyumba.”

  • *

    Talanta moja ilikuwa na uzito wa kilogramu 34.2. Angalia Nyongeza B14.

Marejeo

  • +Kut 26:33; 1Fa 8:6; Ebr 9:24
  • +1Fa 6:20

2 Mambo ya Nyakati 3:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Shekeli moja ilikuwa na uzito wa gramu 11.4. Angalia Nyongeza B14.

2 Mambo ya Nyakati 3:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “nyumba.”

Marejeo

  • +1Fa 6:23-28

2 Mambo ya Nyakati 3:11

Marejeo

  • +1Fa 8:6; 1Nya 28:18

2 Mambo ya Nyakati 3:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, zikielekea Patakatifu.

2 Mambo ya Nyakati 3:14

Marejeo

  • +Mt 27:51; Ebr 10:19, 20
  • +Kut 26:31, 33

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Ufahamu,

2 Mambo ya Nyakati 3:15

Marejeo

  • +2Fa 25:13
  • +1Fa 7:15-22; 2Fa 25:17; 2Nya 4:11-13; Yer 52:22, 23

2 Mambo ya Nyakati 3:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kusini.”

  • *

    Au “kaskazini.”

  • *

    Maana yake “Naye [yaani, Yehova] Aimarishe Kabisa.”

  • *

    Labda inamaanisha “Katika Nguvu.”

Tafsiri Mbalimbali

Bofya nambari ya mstari ili kuona mstari huo katika tafsiri mbalimbali za Biblia.

Jumla

2 Nya. 3:11Fa 6:1, 37
2 Nya. 3:1Mwa 22:2, 14
2 Nya. 3:12Sa 24:25; 1Nya 21:18
2 Nya. 3:12Sa 24:18; 1Nya 21:22
2 Nya. 3:31Fa 6:2
2 Nya. 3:41Fa 6:3
2 Nya. 3:51Fa 6:15, 22
2 Nya. 3:51Fa 6:29
2 Nya. 3:51Fa 6:21
2 Nya. 3:61Nya 29:2, 8
2 Nya. 3:61Nya 29:3, 4
2 Nya. 3:7Kut 26:29
2 Nya. 3:7Kut 26:1; 1Fa 6:29
2 Nya. 3:8Kut 26:33; 1Fa 8:6; Ebr 9:24
2 Nya. 3:81Fa 6:20
2 Nya. 3:101Fa 6:23-28
2 Nya. 3:111Fa 8:6; 1Nya 28:18
2 Nya. 3:14Mt 27:51; Ebr 10:19, 20
2 Nya. 3:14Kut 26:31, 33
2 Nya. 3:152Fa 25:13
2 Nya. 3:151Fa 7:15-22; 2Fa 25:17; 2Nya 4:11-13; Yer 52:22, 23
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Soma katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
2 Mambo ya Nyakati 3:1-17

Kitabu cha Pili cha Mambo ya Nyakati

3 Kisha Sulemani akaanza kujenga nyumba ya Yehova+ huko Yerusalemu juu ya Mlima Moria,+ mahali ambapo Yehova alikuwa amemtokea Daudi baba yake,+ mahali ambapo Daudi alikuwa ametayarisha kwenye uwanja wa kupuria wa Ornani Myebusi.+ 2 Alianza kujenga siku ya pili ya mwezi wa pili, katika mwaka wa nne wa utawala wake. 3 Na msingi ambao Sulemani aliweka kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya Mungu wa kweli ulikuwa na urefu wa mikono 60 na upana wa mikono 20,+ kulingana na kipimo cha awali.* 4 Ukumbi wa mbele ulikuwa na urefu wa mikono 20, nao ulilingana na upana wa nyumba,* na kimo chake kilikuwa 120;* naye akafunika upande wa ndani kwa dhahabu safi.+ 5 Alifunika nyumba kuu kwa mbao za miberoshi, kisha akaifunika kwa dhahabu bora,+ halafu akaipamba kwa michongo ya mitende+ na minyororo.+ 6 Pia, aliifunika nyumba hiyo kwa mawe maridadi yenye thamani;+ na dhahabu+ aliyotumia ilikuwa dhahabu kutoka Parvaimu. 7 Aliifunika nyumba, maboriti, vizingiti, kuta zake, na milango yake kwa dhahabu;+ naye akachonga makerubi kwenye kuta zake.+

8 Kisha akajenga chumba cha Patakatifu Zaidi;*+ urefu wake ulilingana na upana wa nyumba, mikono 20, na upana wake ulikuwa mikono 20. Akaifunika kwa talanta 600* za dhahabu bora.+ 9 Uzito wa dhahabu iliyotumiwa kutengenezea misumari ulikuwa shekeli 50;* naye alifunika vyumba vya darini kwa dhahabu.

10 Kisha akatengeneza mifano ya makerubi wawili katika chumba cha Patakatifu Zaidi,* akawafunika kwa dhahabu.+ 11 Kwa ujumla mabawa ya makerubi hao+ yalikuwa na urefu wa mikono 20; bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa mikono mitano nalo liligusa ukuta wa nyumba, na bawa la pili lilikuwa na urefu wa mikono mitano nalo liligusa bawa moja la kerubi wa pili. 12 Na bawa moja la kerubi wa pili lilikuwa na urefu wa mikono mitano nalo liligusa ukuta wa nyumba, na bawa la pili lilikuwa na urefu wa mikono mitano nalo liligusa bawa moja la yule kerubi wa kwanza. 13 Mabawa ya makerubi hao yalikuwa yamenyooshwa kufikia urefu wa mikono 20; nao walikuwa wamesimama kwa miguu yao, nyuso zao zikielekea ndani.*

14 Alitengeneza pia pazia+ kwa nyuzi za bluu, sufu ya zambarau, kitambaa chekundu, na kitambaa bora, na kulitarizi kwa mifano ya makerubi.+

15 Kisha akatengeneza nguzo mbili+ mbele ya nyumba hiyo, zenye urefu wa mikono 35, na kifuniko kilichokuwa juu ya kila nguzo kilikuwa na urefu wa mikono mitano.+ 16 Pia alitengeneza minyororo iliyokuwa kama mikufu, akaiweka juu ya nguzo hizo, kisha akatengeneza makomamanga 100 na kuyaweka kwenye minyororo hiyo. 17 Akasimamisha nguzo hizo mbele ya hekalu, moja upande wa kulia* na nyingine upande wa kushoto;* akaiita nguzo ya upande wa kulia Yakini* na nguzo ya upande wa kushoto Boazi.*

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki