Ayubu
21 Ayubu akajibu:
2 “Sikilizeni kwa makini ninayosema;
Na hii iwe faraja mnayonipa.
4 Je, ninamlalamikia mwanadamu?
Ikiwa ndivyo, je, nisingekosa* subira?
5 Niangalieni na kunikodolea macho kwa mshangao;
Funikeni kinywa chenu kwa mkono wenu.
6 Ninapofikiria jambo hilo, nashikwa na wasiwasi,
Na mwili wangu wote unatetemeka.
8 Huwaona watoto wao sikuzote,
Nao huendelea kuishi na kuwaona wazao wao.
10 Ng’ombe dume wao hawashindwi kuzalisha;
Ng’ombe wao huzaa na mimba haziharibiki.
11 Wavulana wao hukimbia nje kama kondoo,
Na watoto wao hurukaruka huku na huku.
14 Lakini wanamwambia Mungu wa kweli, ‘Tuache!
Hatutamani kuzijua njia zako.+
15 Mweza-Yote ni nani ili tumtumikie?+
Tutapata faida gani tukimfahamu?’+
16 Lakini ninajua kwamba hawaudhibiti ufanisi wao wenyewe.+
Mawazo ya waovu yako mbali nami.*+
17 Ni mara ngapi taa ya waovu huzimwa?+
Ni mara ngapi wanapopatwa na msiba?
Ni mara ngapi Mungu huwaangamiza kwa hasira yake?
18 Je, kuna wakati wowote wanapopeperushwa na upepo kama majani makavu
Na kama makapi yanayopeperushwa mbali na upepo wa dhoruba?
19 Mungu atawawekea watoto wa mtu mwovu adhabu ya mtu huyo.
Lakini Mungu na amlipe ili apate kujua hilo.+
21 Kwa maana, kwa nini ahangaikie kitakachoipata nyumba yake baada ya kifo chake
22 Je, kuna yeyote anayeweza kumfundisha Mungu ujuzi,*+
Wakati Yeye ndiye anayewahukumu hata walio juu zaidi?+
23 Kuna mtu anayekufa akiwa na nguvu zake zote+
Akiwa amestarehe kabisa na bila mahangaiko,+
24 Wakati mapaja yake yamenenepa kwa mafuta
Na mifupa yake ikiwa na nguvu.*
28 Kwa maana mnasema, ‘Iko wapi nyumba ya yule mtu maarufu,
Na liko wapi hema alimoishi yule mtu mwovu?’+
29 Je, hamjawauliza wasafiri?
Je, hamchunguzi kwa makini mambo waliyoona,*
30 Kwamba mtu mwovu huokolewa katika siku ya msiba
Na kuokolewa katika siku ya ghadhabu?
31 Ni nani atakayemuuliza kuhusu njia yake,
Na ni nani atakayemlipa kwa sababu ya mambo aliyotenda?
32 Anapopelekwa kaburini,
Kaburi lake litalindwa.
34 Basi kwa nini mnipe faraja isiyo na maana?+
Majibu yenu hayana lolote isipokuwa udanganyifu!”