Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Mambo ya Nyakati 1
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

2 Mambo ya Nyakati—Yaliyomo

      • Sulemani aomba hekima (1-12)

      • Utajiri wa Sulemani (13-17)

2 Mambo ya Nyakati 1:1

Marejeo

  • +1Nya 29:25; Mhu 2:9; Mt 6:28, 29; 12:42

2 Mambo ya Nyakati 1:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, ukoo wa upande wa baba.

2 Mambo ya Nyakati 1:3

Marejeo

  • +1Fa 3:4; 1Nya 21:29

2 Mambo ya Nyakati 1:4

Marejeo

  • +1Nya 13:5
  • +1Nya 16:1

2 Mambo ya Nyakati 1:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “walikuwa wakitafuta ushauri Wake hapo.”

Marejeo

  • +Kut 38:1, 2
  • +Kut 31:2-5

2 Mambo ya Nyakati 1:6

Marejeo

  • +1Fa 3:4

2 Mambo ya Nyakati 1:7

Marejeo

  • +1Fa 3:5-9

2 Mambo ya Nyakati 1:8

Marejeo

  • +2Sa 7:8
  • +1Nya 28:5; Zb 89:28, 29

2 Mambo ya Nyakati 1:9

Marejeo

  • +2Sa 7:12; 1Nya 28:6; Zb 132:11
  • +Mwa 13:14, 16

2 Mambo ya Nyakati 1:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “nitoke nje mbele ya watu hawa na kurudi ndani.”

Marejeo

  • +Met 2:6; Yak 1:5
  • +Zb 72:1, 2

2 Mambo ya Nyakati 1:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “siku nyingi.”

Marejeo

  • +1Fa 3:10-13, 28

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    The Watchtower,

    12/1/2005, uku. 19

  • Fahirishi ya Machapisho

    w05 12/1 19

2 Mambo ya Nyakati 1:12

Marejeo

  • +1Nya 29:25; 2Nya 9:22; Mhu 2:9

2 Mambo ya Nyakati 1:13

Marejeo

  • +1Fa 3:4

2 Mambo ya Nyakati 1:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wapanda farasi.”

  • *

    Au “wapanda farasi.”

Marejeo

  • +Kum 17:16; 1Fa 4:26
  • +2Nya 8:5, 6
  • +2Nya 9:25

2 Mambo ya Nyakati 1:15

Marejeo

  • +1Fa 10:21
  • +1Fa 10:27; 2Nya 9:27

2 Mambo ya Nyakati 1:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “kutoka Misri na kutoka Kue; wafanyabiashara wa mfalme waliwanunua kutoka Kue,” huenda ni Kilikia.

Marejeo

  • +2Nya 9:28
  • +1Fa 10:28, 29

Tafsiri Mbalimbali

Bofya nambari ya mstari ili kuona mstari huo katika tafsiri mbalimbali za Biblia.

Jumla

2 Nya. 1:11Nya 29:25; Mhu 2:9; Mt 6:28, 29; 12:42
2 Nya. 1:31Fa 3:4; 1Nya 21:29
2 Nya. 1:41Nya 13:5
2 Nya. 1:41Nya 16:1
2 Nya. 1:5Kut 38:1, 2
2 Nya. 1:5Kut 31:2-5
2 Nya. 1:61Fa 3:4
2 Nya. 1:71Fa 3:5-9
2 Nya. 1:82Sa 7:8
2 Nya. 1:81Nya 28:5; Zb 89:28, 29
2 Nya. 1:92Sa 7:12; 1Nya 28:6; Zb 132:11
2 Nya. 1:9Mwa 13:14, 16
2 Nya. 1:10Met 2:6; Yak 1:5
2 Nya. 1:10Zb 72:1, 2
2 Nya. 1:111Fa 3:10-13, 28
2 Nya. 1:121Nya 29:25; 2Nya 9:22; Mhu 2:9
2 Nya. 1:131Fa 3:4
2 Nya. 1:14Kum 17:16; 1Fa 4:26
2 Nya. 1:142Nya 8:5, 6
2 Nya. 1:142Nya 9:25
2 Nya. 1:151Fa 10:21
2 Nya. 1:151Fa 10:27; 2Nya 9:27
2 Nya. 1:162Nya 9:28
2 Nya. 1:161Fa 10:28, 29
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Soma katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
2 Mambo ya Nyakati 1:1-17

Kitabu cha Pili cha Mambo ya Nyakati

1 Sulemani mwana wa Daudi alizidi kuimarika katika utawala wake, na Yehova Mungu wake alikuwa pamoja naye, akamfanya kuwa mkuu sana.+

2 Sulemani aliagiza Waisraeli wote wakusanywe, wakuu wa maelfu na wa mamia, waamuzi, na viongozi wote wa Israeli, viongozi wa koo.* 3 Kisha Sulemani na Waisraeli wote wakaenda mahali pa juu kule Gibeoni,+ kwa maana hema la mkutano la Mungu wa kweli lilikuwa huko, hema ambalo Musa mtumishi wa Yehova alitengeneza nyikani. 4 Hata hivyo, Daudi alikuwa amelipandisha Sanduku la Mungu wa kweli kutoka Kiriath-yearimu+ na kulileta mahali ambapo Daudi alikuwa ametayarisha kwa ajili yake; alikuwa amepiga hema kwa ajili ya Sanduku hilo huko Yerusalemu.+ 5 Na ile madhabahu ya shaba+ ambayo Bezaleli+ mwana wa Uri mwana wa Huru alikuwa ametengeneza ilikuwa imewekwa mbele ya hema la ibada la Yehova; na Sulemani na Waisraeli wote walikuwa wakisali mbele yake.* 6 Kisha Sulemani akamtolea Yehova dhabihu mahali hapo, alitoa dhabihu 1,000 za kuteketezwa kwenye madhabahu ya shaba+ ya hema la mkutano.

7 Usiku huo Mungu akamtokea Sulemani na kumwambia: “Niombe unachotaka nikupe.”+ 8 Basi Sulemani akamwambia Mungu: “Umemtendea Daudi+ baba yangu kwa upendo mwingi mshikamanifu, nawe umeniweka kuwa mfalme baada yake.+ 9 Sasa, Ee Yehova Mungu, ahadi uliyompa Daudi baba yangu na ithibitike kuwa ya uaminifu,+ kwa maana umeniweka kuwa mfalme juu ya watu wengi sana kama chembe za mavumbi ya dunia.+ 10 Sasa nipe hekima na ujuzi+ ili niwaongoze watu hawa,* kwa maana ni nani anayeweza kulihukumu taifa hili lako lililo kubwa?”+

11 Kisha Mungu akamwambia Sulemani: “Kwa sababu moyo wako unatamani jambo hilo, nawe hukuomba mali, utajiri, wala heshima wala hukuomba wale wanaokuchukia wafe, wala hukuomba maisha marefu,* lakini umeomba hekima na ujuzi ili uwahukumu watu wangu ambao nimekuweka uwe mfalme wao,+ 12 nitakupa hekima na ujuzi; lakini nitakupa pia mali na utajiri na heshima, kuliko mfalme yeyote kabla yako na mfalme yeyote baada yako.”+

13 Basi Sulemani akatoka mahali pa juu huko Gibeoni,+ kutoka mbele ya hema la mkutano, akaja Yerusalemu; naye akatawala Israeli. 14 Sulemani akaendelea kukusanya magari ya vita na farasi;* akawa na magari 1,400 ya vita na farasi* 12,000,+ naye aliwaweka katika majiji ya magari ya vita+ karibu naye huko Yerusalemu.+ 15 Mfalme alifanya fedha na dhahabu huko Yerusalemu iwe nyingi kama mawe,+ na mbao za mierezi ziwe nyingi kama mikuyu katika Shefela.+ 16 Farasi wa Sulemani waliletwa kutoka Misri,+ na wafanyabiashara wa mfalme walinunua makundi ya farasi* kwa bei moja.+ 17 Kila gari kutoka Misri lilinunuliwa kwa vipande 600 vya fedha, na farasi alinunuliwa kwa vipande 150; kisha waliwauzia wafalme wote wa Wahiti na wafalme wa Siria.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki