Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bi12 3 Yohana 1-14
  • Barua ya Tatu ya Yohana

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Barua ya Tatu ya Yohana
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Barua ya Tatu ya Yohana

Barua ya Tatu ya Yohana

1 Mwanamume mzee,+ kwa Gayo, mpendwa, ambaye mimi nampenda+ kweli.

2 Mpendwa,+ mimi nasali kwamba uwe ukiendelea vema+ na kuwa na afya njema+ katika mambo yote, kama vile nafsi yako inavyoendelea vema.+ 3 Kwa maana nilishangilia sana wakati akina ndugu walipokuja na kutoa ushahidi kuhusu kweli ambayo wewe unashika, kama vile unavyoendelea kutembea katika kweli.+ 4 Sina sababu nyingine kubwa zaidi ya kuwa na shukrani kuliko mambo haya, kwamba niwe nikisikia watoto wangu wanaendelea kutembea katika kweli.+

5 Mpendwa, unafanya kazi ya uaminifu kwa yoyote yale unayofanya kwa ajili ya akina ndugu,+ tena walio wageni,+ 6 ambao wametoa ushahidi kuhusu upendo wako mbele ya kutaniko. Tafadhali uishughulikie safari ya hawa watu kwa namna inayomfaa Mungu.+ 7 Kwa maana wao walisafiri kwa ajili ya jina lake, bila kuchukua kitu chochote+ kutoka kwa watu wa mataifa. 8 Kwa hiyo, sisi tuna wajibu wa kuwakaribisha watu wa namna hiyo,+ ili tuwe wafanyakazi wenzi katika kweli.+

9 Niliandikia kutaniko jambo fulani, lakini Diotrefe, anayependa kuwa na mahali pa kwanza+ katikati yao, hapokei+ kwa heshima+ jambo lolote kutoka kwetu. 10 Hiyo ndiyo sababu, nikija, nitakumbusha matendo yake ambayo anaendelea kufanya,+ akipiga porojo juu yetu kwa maneno maovu.+ Pia, akiwa hatosheki na mambo haya, yeye mwenyewe pia hawapokei akina ndugu+ kwa heshima, na wale wanaotaka kuwapokea+ yeye hujaribu kuwazuia+ na huwatupa nje+ ya kutaniko.

11 Mpendwa, uwe mwigaji, si wa yaliyo mabaya, bali wa yaliyo mema.+ Yeye ambaye hutenda mema anatokana na Mungu.+ Yeye ambaye hutenda mabaya hajamwona Mungu.+ 12 Demetrio ametolewa ushahidi na wao wote+ na ile kweli yenyewe. Kwa kweli, sisi, pia, tunatoa ushahidi,+ nanyi mnajua kwamba ushahidi tunaotoa ni wa kweli.+

13 Nilikuwa na mambo mengi ya kukuandikia, lakini sitaki kuendelea kukuandikia kwa wino na kalamu.+ 14 Bali ninatumaini kukuona wewe moja kwa moja, nasi tutasema uso kwa uso.+

Na uwe na amani.+

Rafiki wanakutumia salamu+ zao. Wape rafiki salamu+ zangu kwa jina.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki