Mikutano Ya Utumishi Kwa Oktoba
ANGALIA: Huduma ya Ufalme Yetu itaratibu Mkutano wa Utumishi kwa kila juma wakati wa pindi ya mkusanyiko. Makundi yanaweza kufanya marekebisho kama inavyohitajiwa ili kuruhusu wakati wa kuhudhuria mkusanyiko wa wilaya halafu kuwe na pitio la dakika 30 kuhusu mambo makuu ya programu kwenye Mkutano wa Utumishi juma linalofuata. Pitio la siku baada ya siku laweza kugawiwa mapema ndugu wawili au watatu wanaostahili ambao wataweza kukazia mambo ya msingi. Pitio hilo lililotayarishwa vizuri litasaidia akina ndugu kukumbuka mambo ya msingi ili wayatumie kibinafsi na shambani. Maelezo kutoka kwa wasikilizaji na mambo yaliyoonwa yanayosimuliwa yapaswa kuwa mafupi na kutokeza wazo kuu.
Juma Linaloanza Oktoba 5
Dak. 10: Matangazo ya kwenu, Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu, na mambo makuu kutoka Habari za Kitheokrasi. Pitia makala zenye kutokeza kutoka kwa magazeti ya karibuni; kuwe na wonyesho mmoja au mawili mafupi kuonyesha jinsi magazeti yanavyoweza kutolewa baada ya kwanza kufanya mazungumzo ya Kimaandiko.
Dak. 15: “Sitawisha Utangulizi Wenye Kuchochea.” Toa hotuba ukizungumzia jinsi ya kutayarisha utoaji mbalimbali ukitumia makala za magazeti yaliyoonyeshwa. Panga wahubiri wawili au watatu wenye uwezo watoe wonyesho wa utoaji mbalimbali uliodokezwa; tia ndani utoaji mmoja ukitolewa na mhubiri mchanga.
Dak. 20: “Onyesha Hangaikio kwa Wanaopendezwa.” Zungumza pamoja na wasikilizaji. Unapozungumzia fungu 2, simulia mambo yaliyoteuliwa kutoka kwa Mnara wa Mlinzi la Julai 1, 1981, kurasa 4-6, (Kiingereza) ukieleza jinsi tunavyoweza kumwiga Yesu katika kuhangaikia wengine. Tia ndani maelezo juu ya jinsi ya kujaza rekodi ya nyumba kwa nyumba na jinsi inavyopaswa kutumiwa ili kufuatia kupendezwa. Toa wonyesho mfupi wa mojawapo ya madokezo. Baada ya mhubiri mwenye uwezo kutoa wonyesho wa njia iliyodokezwa, alika wasikilizaji watoe maelezo ya sababu zinazofanya hiyo iwe njia yenye matokeo ya kuanzisha mafunzo katika eneo lenu.
Wimbo 63 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 12
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu ya kila mwezi; toa pongezi kwa kutegemea 2 Wakorintho 9:6, 7. Waalike wahubiri waliojitayarisha wasimulie mambo yaliyoonwa yanayotokeza katika kutoa magazeti na maandikisho wakati wa Oktoba.
Dak. 15: “Tumia Magazeti Vizuri.” Maswali na majibu. Unapozungumzia fungu 6, toa madokezo juu ya jinsi ya kuanzisha njia ya kupelekea watu magazeti kwa ukawaida: Tumia njia ya utangulizi iliyo sahili na ya moja kwa moja; weka rekodi nzuri ya nyumba kwa nyumba; chochea kupendezwa katika matoleo ya wakati ujao kwa kutaja makala zinazokuja; uliza maswali yanayojibiwa na makala hizo; hakikisha kurudi kila baada ya majuma mawili.—8/84 km-SW uku. 6.
Dak. 15: “‘Wachukuaji Nuru’ Mkusanyiko wa Wilaya wa 1992”—Sehemu 1. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji juu ya mafungu 1-14. Huenda wahubiri wakataka kuzungumzia mambo yanayofaa pamoja na wanafunzi wao wa Biblia watakaohudhuria mkusanyiko.
Wimbo 88 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 19
Dak. 5: Matangazo ya kwenu. Eleza kifupi jinsi ya kujaza fomu za uandikishaji, na utambulishe ndugu aliye au waliogawiwa kupokea maandikisho.
Dak. 15: “Wasaidieni Watoto Wamtumikie Yehova Kutoka Moyoni.” Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Kazia uhitaji wa wazazi kutimiza daraka lao la kuweka mfano na kuwazoeza watoto wao kibinafsi katika huduma. Alika mzazi mmoja au wawili wasimulie yale ambayo wamefanya na kupata matokeo mazuri. Malizia kwa wonyesho wa mojawapo ya mazungumzo yaliyodokezwa ukitolewa na kijana.
Dak. 10: Sanduku la Swali. Zungumza pamoja na wasikilizaji. Kazia kwa nini ni jambo la maana kwa watoto kuwa na sifa ya mwenendo mwema na tamaa ya kweli ya kushiriki katika utumishi wa shambani ili kustahili kuwa wahubiri wasiobatizwa.
Dak. 15: “‘Wachukuaji Nuru’ Mkusanyiko wa Wilaya wa 1992”—Sehemu 2. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji juu ya mafungu 15-21 na pitio fupi la “Vikumbusho vya Mkusanyiko wa Wilaya.” Tia ndani vikumbusho vinavyofaa kwa kutegemea habari katika Mnara wa Mlinzi la Juni 15, 1989, kurasa 10-20. Tia moyo vikundi vya familia vipitie habari katika makala hizo kabla ya kuhudhuria mkusanyiko.
Wimbo 221 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 26
Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Watie moyo wote wafikirie kuhusu uwezekano wa kufanya upainia msaidizi wakati wa Novemba au Desemba wakati vipindi vya sikukuu vinapofanya kuwe na wakati wa ziada.
Dak. 12: Maelezo Kutoka kwa Wahubiri Wachanga. Waalike wahubiri wachanga waliojitayarisha waeleze jinsi walivyostahili kuwa wahubiri wasiobatizwa na kwa nini wanafurahia utumishi wa shambani na kutaka kuwa na ushiriki mkubwa zaidi. Wale wanaohojiwa wapaswa watoe maelezo yao wenyewe yanayofaa na si kurudia maneno ambayo wameombwa wakariri.
Dak. 15: Kutoa Biblia New World Translation na Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? wakati wa Novemba. Hotuba na wonyesho. Pitia mambo makuu ya habari juu ya “New World Translation” katika kitabu Kutoa Sababu, kurasa 248-51. Kisha onyesha jinsi dokezo la pili katika ukurasa 9 wa kitabu Kutoa Sababu laweza kutumiwa katika kuzungumza na mwenye nyumba.
Dak. 10: Je! Mipango Yako ya Kuhudhuria Mkusanyiko wa Wilaya ni Kamili? Mazungumzo yenye idili kati ya mzee na mtumishi wa huduma. (Tumia ndugu watakaohudhuria mkusanyiko pamoja na kundi lenu.) Zungumzia kwa nini sisi huhudhuria mikusanyiko. (Kum. 31:12, 13) Wote wanahitaji kusikiliza kwa uangalifu wakiwa na nia ya kuona jinsi wanavyoweza kutumia habari hiyo wao binafsi na katika utumishi wa shambani. Kuna uhitaji wa kufanya uchunguzi wa mwisho kuona kwamba wote wana mipango ya usafiri. Kuna tahadhari ambazo wote wanapaswa kukumbuka. Mtu yeyote asipangie kuburudika hadi usiku sana wakati wa mkusanyiko, kwa kuwa sote tunahitaji kupumzika vya kutosha. Tunapaswa tupange kutoa ushahidi. Kwa nani? Kwa watu tunaowakuta katika usafiri wa umma na kwenye stesheni za petroli, mikahawa, hoteli, na kadhalika.
Wimbo 111 na sala ya kumalizia.