Mikutano Ya Utumishi Kwa Machi
Juma Linaloanza Machi 1
Dak. 15: Matangazo ya kwenu na matangazo kutoka kwa Huduma ya Ufalme Yetu. Mazungumzo ya maswali na majibu ya makala “Kukubali, Kutumia, na Kunufaika na Neno la Mungu.” Tangaza tarehe ya kusanyiko la mzunguko lifuatalo na uwatie moyo wote wahudhurie.
Dak. 15: “Endeleeni Kusema: ‘Njoo!’” Makala ipitiwe kwa maswali na majibu. Unapozungumzia fungu la 4, mhubiri aliyejitayarisha vizuri akazie mambo machache kwenye sura 42 ya kitabu Upeo Wa Ufunuo katika, mafungu 6-10, yenye kushughulikia Ufunuo 21:4-6.
Dak. 15: “Uwe Mwenye Kubadilikana Katika Huduma Yako.” Hotuba na wasikilizaji wakishiriki. Tia ndani maonyesho mawili mafupi unapozungumzia mafungu 3-5. Unapoonyesha jambo kuu katika mafungu ya 4 na 5, onyesha jinsi mhubiri mwenye umri mkubwa na yule mchanga wanavyoweza kufanya kazi pamoja kwenye huduma ya mlango kwa mlango kama inavyoonyeshwa kwenye makala hiyo. Kazia uhitaji wa kupata shangwe katika huduma yajapokuwa matokeo.
Wimbo 114 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Machi 8
Dak. 7: Matangazo ya kwenu na mambo makuu ya Habari za Kitheokrasi. Taja idadi ya mapainia wasaidizi ambao wamekubaliwa kwa ajili ya Aprili. Tia moyo wanaopanga kupainia walete maombi yao mapema.
Dak. 18: “Je! Waweza Kufanya Zaidi Umheshimu Yehova?” Mazungumzo ya maswali na majibu ya mafungu 1 hadi 10.
Dak. 20: Kusaidia wanafunzi wetu wa Biblia. Mazungumzo na wasikilizaji yakikazia uhitaji wa kutoa msaada wa ziada kwa wanafunzi wa Biblia licha ya kuongoza tu funzo. (1 The. 2:8) Tumia wakati wa ziada kuchochea tamaa ya kuhisiwa moyoni ya kuhudhuria na kushiriki mikutanoni. Tia uthamini kwa tengenezo na udugu wa ulimwenguni pote kwa kuelezea makusanyiko ya mzunguko, siku za mikusanyiko ya pekee, na mikusanyiko ya wilaya. Mwaweza kutazama pamoja video Jehovah’s Witnesses—The Organization Behind the Name, Purple Triangles, na The Bible—Accurate History, Reliable Prophecy, na kuwauliza wanafunzi maswali kutokana na yale ambayo wamejifunza. Kwa kuendelea onyesha jinsi ya kushiriki na wengine kivivi-hivi yale ambayo wamejifunza. Wanafunzi wa Biblia ambao wamestahili matakwa yanayoonyeshwa kwenye sura 98 na 99 za kitabu chetu cha Huduma Yetu na wana tamaa ya kushiriki katika huduma ya peupe wanapaswa kusaidiwa kuwa wahubiri wasiobatizwa. Ni jambo la maana kutumia wakati katika pindi ya kujifunza na baada ya hapo ili kusaidia wanafunzi wasitawishe tamaa ya wakfu na ubatizo. Unaweza kuonyesha wanafunzi makala za picha au magazeti ya ubatizo katika mikusanyiko yetu. Wonyesho: Mhubiri asaidia mwanafunzi wa Biblia kutoa ushahidi wa vivi-hivi. Achagua madokezo kwenye kitabu Kuishi Milele na kusema: “Itakuwa vizuri kushiriki jambo hili na baadhi ya watu wa ukoo au majirani wako. Unaweza kuwatajia kwamba ulijifunza jambo fulani katika Biblia ambalo hukuwa umepata kujua.” Watie moyo wahubiri wasaidie wanafunzi wa Biblia, wakionyesha upendo hata baada ya ubatizo.
Wimbo 123 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Machi 15
Dak. 10: Matangazo ya kwenu, kutia ndani ripoti ya hesabu na shukrani za mchango. Elekeza kwenye “Ujumbe wa Wakati Unaofaa” kwenye ukurasa wa 7. Watie moyo wote waandike kichwa cha hotuba ya pekee ya Machi 28 na waalike wenye kupendezwa wahudhurie.
Dak. 15: “Kusaidia Wote Ambao Wameonyesha Kupendezwa” hotuba na wasikilizaji wakishiriki. Fikiria Maandiko yaliyotajwa wakati ukiruhusu. Toa wonyesho wa dokezo katika fungu la 3. Onyesha uhitaji wa kufuatia kupendezwa kwa wanaohudhuria kwa mara ya kwanza.
Dak. 20: “Je! Waweza Kufanya Zaidi Umheshimu Yehova?” Mazungumzo ya maswali na majibu ya mafungu 11 hadi 22.
Wimbo 32 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Machi 22
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Sanduku la Swali. Watie moyo wote wapangie kushiriki katika huduma iliyoongezeka wakati wa Aprili.
Dak. 20: Kuwatunza Wazee-Wazee. Mazungumzo na mahoji yanayofanywa na ndugu wawili. Katika Mkusanyiko wa Wilaya wa “Wachukuaji Nuru,” mfululizo uliotolewa Jumapili ulikuwa na kichwa: “Kujali Mmoja na Mwenzake Katika Nyumba ya Kikristo.” Sehemu ya kumalizia “Kwa Kujali Walio Wazee–Wazee” ilikazia mchango wa maana ambao watu wazee wanafanya ndani ya familia na kundi. (Mit. 16:31) Twaweza kusaidia wazee-wazee kwa njia zipi? Familia ina daraka la kwanza. (1 Tim. 5:3, 4, 8, 16) Uvumilivu na huruma vyahitajiwa. Watoto walio watu wazima na wajukuu wana fursa ya kuonyesha uthamini kwa miaka ya upendo, kazi na utunzaji ambao wazazi wao na nyanya zao waliwatolea wakati uliopita. (w87-SW 6/1 13-18) Kundi pia laweza kusaidia wazee-wazee. Wengine huenda wakahitaji msaada ili wastahili kwa ajili ya msaada wa serikali. Waonyesheni ukaribishaji-wageni kwa kuwaalika kwenye mlo na kwenye vikusanyiko. (Rum. 12:13) Wasaidieni katika huduma ya shambani. Watoleeni usafiri wa mikutano na makusanyiko. Wasaidieni kufanya ununuzi na kutunza makao yao. (w87-SW 6/1 4-7) Onyesheni heshima sikuzote kwa wazee-waze. (1 Tim. 5:1, 2) Hoji moja au wawili ambao ni wazee-wazee walio mfano mzuri. Onyesha jinsi wanavyonufaika na fadhili wanayoonyeshwa na familia zao na kundi.
Dak. 15: Mzee ahoji wahubiri watatu au wanne ambao watakuwa wakipainia katika Aprili au waliofanya hivyo wakati uliopita. Ni nini kimewasukuma kupainia? Ni mipango gani wamefanya kwa ajili ya Aprili? Upainia msaidizi umewasaidiaje wao binafsi? Watie moyo wote ambao wanapanga kufanya upainia msaidizi mwezi ujao wajipatie fomu ya ombi na kuirudisha upesi.
Wimbo 172 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Machi 29
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wote wakaribishe watu wenye kupendezwa na wanafunzi wa Biblia kwenye mwadhimisho wa Ukumbusho. Tumieni vizuri vikaratasi vya mwaliko. Watie moyo wahubiri waandike vizuri saa ya Ukumbusho na mahali pa mwadhimisho kwenye kikaratasi cha mwaliko.
Dak. 25: “Kuadhimisha Kifo Kitoacho Tumaini la Uhai wa Milele.” Ipitiwe kwa maswali na majibu na mwangalizi-msimamizi. Tia ndani habari katika sanduku “Kujitayarisha Kwa Ajili ya Ukumbusho.” Baada ya kufikiria fungu la 5 la makala hiyo, kuwe na wonyesho ambapo mhubiri anamkaribisha mwanafunzi wa Biblia kwenye Ukumbusho. Mhubiri aelezea mpango wa kusoma maandiko ya Biblia yaliyoteuliwa kwa pindi ya Aprili 1-6 na ajitolee kutoa usafiri.
Dak. 10: Kutoa Mnara wa Mlinzi wakati wa Aprili. Onyesha mambo hususa ambayo yaweza kutajwa mwezi huo. Uwe chonjo kuelekezea mambo katika magazeti kila pindi.
Wimbo 87 na sala ya kumalizia.