Mikutano Ya Utumishi Kwa Novemba
Juma Linaloanza Novemba 7
Dak 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Taja jambo moja au mawili ya kuzungumzia katika kila ya magazeti ya karibuni yawezayo kutumiwa kwa kuyatoa.
Dak 18: “Neno la Mungu Lina Nguvu.” Maswali na majibu. Tia ndani maelezo juu ya umuhimu wa usomaji wa Biblia wa ukawaida kulingana na dibaji ya Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—1994.
Dak 17: “Biblia—Chanzo cha Faraja na Tumaini Katika Ulimwengu Wenye Masumbuko.” Zungumza pamoja na wasikilizaji. Panga kuwe na maonyesho mawili yakionyesha jinsi ya kutumia utoaji uliodokezwa.
Wimbo 24 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 14
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na shukrani za upaji wowote wa hiari.
Dak 17: “Wewe Huonyesha Roho ya Aina Gani?” Hotuba. Tia ndani maelezo kutoka toleo la Mnara wa Mlinzi la Novemba 15, 1977, ukurasa 511, mafungu 4 na 5.
Dak 18: “Njia za Kuboresha Kuhubiri Kwetu Ufalme.” Maswali na majibu. Wakaribishe wasikilizaji waeleze maono kuonyesha jinsi madokezo yaliyotolewa katika Huduma ya Ufalme Yetu yametumiwa kwa matokeo mazuri.
Wimbo 37 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 21
Dak 12: Matangazo ya kwenu. Sanduku la Swali. Hotuba. Ifanye ifae kwenu.
Dak 15: “Je! Kweli Ni Wizi?” Hotuba ikitolewa na mzee ikitegemea makala itokayo kwenye toleo la Mnara wa Mlinzi, Aprili 15, 1994, kurasa 19-21.
Dak 18: “Wasaidie Wasikie ‘Tena.’” Zungumza pamoja na wasikilizaji. Panga uwe na maonyesho mawili yaliyotayarishwa vizuri yakionyesha jinsi Biblia yaweza kutumiwa tunapoanzisha funzo.
Wimbo 52 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 28
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Shughulikia Habari za Kitheokrasi. Toa wonyesho wa njia za kutoa magazeti ya karibuni.
Dak 17: “Baraka Zitokanazo na Kuhubiri Pamoja na Wengine.” Maswali na majibu. Watie moyo wote waunge mkono mipango ya mikutano ya utumishi wa shambani iliyopangwa na kutaniko badala ya kufanya mipango ya kibinafsi sikuzote ili kwenda peke yao. Kuhubiri pamoja na kikundi hutokeza baraka za ziada, utumishi wenye matokeo zaidi, na kitia-moyo kwa wote.
Dak 18: Kutoa Kitabu Mtu Mkuu Zaidi Wakati wa Desemba. Kuna uhitaji mkubwa sana wa kitabu hiki. Mamia ya mamilioni ya watu wanakiri kuwa wafuasi wa Yesu nao wadai kuamini aliyofundisha. Watu wanahitaji kujua ni nini kilichomtofautisha na wanaume wengine wote—wokovu wao wakitegemea. Kitabu Mtu Mkuu Zaidi, sura 133, husema: “Mioyo yetu inasukumwa wakati tunapofikiria ujasiri wake mwingi sana na sifa zake za kiume, hekima yake isiyolinganika, uwezo wake mwingi sana akiwa mwalimu, uongozi wake wa ujasiri, na huruma zake nyororo na hisia zenye kusikitikia wengine.” Biblia humtambulisha waziwazi kuwa (1) Shahidi (Yn. 18:37), (2) Mwokozi (Mdo. 4:12), na (3) Mfalme (Ufu. 11:15). Panga uwe na mhubiri aliye na ustadi atoe wonyesho wa utoaji akitumia baadhi ya mambo haya. Watie moyo wote washiriki katika kugawanya kitabu hiki katika Desemba.
Wimbo 61 na sala ya kumalizia.