Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Babuloni Mkubwa Ameanguka!”
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Sura ya 30

      “Babuloni Mkubwa Ameanguka!”

      1. Malaika wa pili anatangaza nini, na “Babuloni Mkubwa” ni nani?

      NI SAA ya hukumu ya Mungu! Basi, sikiliza ujumbe wa kimungu: “Na mwingine, malaika wa pili, akafuata, kusema: ‘Ameanguka! Babuloni Mkubwa ameanguka, yeye ambaye alifanya mataifa yote yanywe ya divai ya kasirani ya uasherati wake!’” (Ufunuo 14:8, NW) Kwa mara ya kwanza, lakini si ya mwisho, Ufunuo unakaza uangalifu juu ya Babuloni Mkubwa. Yeye ni nani? Kama tutakavyoona, yeye ni milki ya tufe lote, yeye ni wa kidini, naye ni mfumo bandia wa Shetani ambao yeye hutumia kupiga vita dhidi ya mbegu ya mwanamke wa Mungu. (Ufunuo 12:17, NW) Babuloni Mkubwa ni mfumo wa ulimwengu mzima wote wa dini bandia. Yeye anatia ndani dini zote ambazo huhifadhi mafundisho na mazoea ya Babuloni la kale na zinazodhihirisha roho yalo.

      2. (a) Ikawaje kwamba dini ya Kibabuloni ikatawanywa kwenye sehemu zote za dunia? (b) Ni kisehemu kipi chenye kutokeza zaidi sana cha Babuloni Mkubwa, nacho kiliibuka lini kikiwa tengenezo lenye nguvu?

      2 Ilikuwa kwenye Babuloni, zaidi ya miaka 4,000 iliyopita, kwamba Yehova akavuruga ndimi za wale ambao wangekuwa wajenzi wa Mnara wa Babeli. Vikundi mbalimbali vya lugha vilitawanywa kwenye miisho ya dunia, vikichukua pamoja navyo itikadi na mazoea ya uasi-imani ambayo ndiyo misingi ya dini zilizo nyingi leo hii. (Mwanzo 11:1-9) Babuloni Mkubwa ndiyo sehemu ya kidini ya tengenezo la Shetani. (Linga Yohana 8:43-47.) Kisehemu chenye kutokeza zaidi sana ni Jumuiya ya Wakristo yenye kuasi imani, ambayo iliibuka katika karne ya nne baada ya Kristo, ikiwa tengenezo lenye nguvu, lenye kuasi sheria, likiwa na itikadi na kawaida zinazotokana, si na Biblia, bali sana sana na dini ya Kibabuloni.—2 Wathesalonike 2:3-12.

      3. Inaweza kusemwaje kwamba Babuloni Mkubwa ameanguka?

      3 Huenda ukauliza, ‘Kwa kuwa dini ingali inatumia uvutano mkubwa katika dunia, kwa nini malaika anatangaza kwamba Babuloni Mkubwa ameanguka?’ Basi, kulitokea nini baada ya 539 K.W.K. wakati Babuloni la kale lilipoanguka? Kwani, Israeli aliwekwa huru arudi kwenye bara la nyumbani kwake na kurudisha ibada ya kweli kule! Kwa hiyo urudisho wa Israeli wa kiroho katika 1919 kwenye ufanisi wa kiroho wenye kung’aa, ambao unaendelea na kupanuka hadi leo hii, unasimama ukiwa ithibati kwamba Babuloni Mkubwa alianguka mwaka huo. Yeye hana nguvu tena za kuzuia watu wa Mungu. Zaidi, yeye ameingia katika matata yenye kina ndani yake mwenyewe. Tangu 1919 ufisadi, utovu wa haki, na utovu wa adili wake umefunuliwa sana. Katika sehemu kubwa ya Ulaya watu wachache ndio huenda kanisani, na baadhi ya mabara ya kisoshalisti, dini inaonwa kuwa “kasumba ya watu.” Akiwa ameaibishwa machoni pa wote wapendao Neno la Mungu la ukweli, sasa Babuloni Mkubwa, ni kana kwamba yu kwenye mstari wa kifo, akingojea Yehova atekeleze juu yake hukumu yake ya uadilifu.

      Anguko Lenye Aibu la Babuloni

      4-6. Ni jinsi gani “Babuloni Mkubwa . . . alifanya mataifa yote yanywe ya divai ya kasirani ya uasherati wake”?

      4 Acheni tuchunguze kirefu zaidi hali zenye kuzunguka anguko lenye aibu la Babuloni Mkubwa. Malaika anatuambia hapa kwamba “Babuloni Mkubwa . . . alifanya mataifa yote yanywe ya divai ya kasirani ya uasherati wake.” Hii humaanisha nini? Huhusiana na ushindi. Mathalani, Yehova alimwambia Yeremia: “Chukua kikombe hiki cha divai ya hasira-kali kutoka mkono wangu, na wewe lazima ufanye mataifa yote ambayo kwayo mimi ninatuma wewe yanywe hicho. Na wao lazima wanywe na kuyumbayumba na kutenda kama watu wenye kichaa kwa sababu ya upanga ambao mimi ninapeleka miongoni mwao.” (Yeremia 25:15, 16, NW) Katika karne ya sita na ya saba K.W.K, Yehova alitumia Babuloni ya kale kumwaga kikombe cha ufananisho cha dhiki kwa ajili ya mataifa mengi yanywe kutia na Yuda yenye kuasi imani, hivi kwamba hata watu wake mwenyewe walipelekwa katika uhamisho. Kisha, kwa zamu yayo, Babuloni ikaanguka kwa sababu ya mfalme wayo kujitukuza mwenyewe dhidi ya Yehova, “Bwana ya zile mbingu.”—Danieli 5:23, NW.

      5 Babuloni Mkubwa amefanya ushindi mwingi, lakini kwa sehemu iliyo kubwa, huo umekuwa wa werevu zaidi. Yeye ‘amefanya mataifa yote yanywe’ kwa kutumia ujanja wa kahaba, kufanya uasherati wa kidini pamoja nao. Yeye ametongoza watawala wa kisiasa waingie ndani ya mafungamano na urafiki pamoja naye. Kupitia vivuta-macho vya kidini, yeye amefanya njama ya uonevu wa kisiasa, wa kibiashara na wa kiuchumi. Yeye amechochea minyanyaso ya kidini na vita na krusedi, pamoja na vita vya kitaifa, kwa sababu tu za kisiasa na za kiuchumi. Naye ametakasa vita hivyo kwa kusema eti ni mapenzi ya Mungu.

      6 Kujiingiza kwa dini katika vita na siasa za karne ya 20 ni jambo linalojulikana na watu wote—kama katika Japani ya Shinto, India ya Hindu, Vietnamu ya Kibudha, Ailandi Kaskazini ya Ukristo” Amerika ya Kilatini, na nyinginezo—bila kusahau wale makasisi wa kijeshi pande zote mbili za vita viwili vya ulimwengu katika kuhimiza wanaume vijana wachinjane. Kielelezo kimoja bora cha kujiingiza kwa Babuloni Mkubwa ni hisa aliyokuwa nayo katika Vita ya Hispania ya Wenyewe kwa Wenyewe ya 1936-39, ambayo katika hiyo angalau watu 600,000 waliuawa. Umwagaji-damu huu ulichochewa na waungaji-mkono wa viongozi wa kidini Wakatoliki na wafungamani wao, kwa sehemu, kwa sababu ukwasi na cheo cha kanisa vilitishwa na serikali halali ya Hispania.

      7. Ni nani ambaye amekuwa shabaha kuu ya Babuloni Mkubwa, naye ametumia njia zipi dhidi ya shabaha hii?

      7 Kwa kuwa Babuloni Mkubwa ndiyo sehemu ya kidini ya mbegu ya Shetani, sikuzote yeye amefanya “mwanamke” wa Yehova “Yerusalemu juu,” kuwa shabaha yake kuu. Katika karne ya kwanza, kundi la Wakristo wapakwa-mafuta lilitambulishwa waziwazi kuwa mbegu ya mwanamke. (Mwanzo 3:15; Wagalatia 3:29; 4:26, NW) Babuloni Mkubwa alijaribu sana kushinda kundi hilo safi kwa kulitongoza lifanye uasherati wa kidini. Mitume Paulo na Petro walionya kwamba wengi wangeshindwa na uasi-imani mkubwa ungetokea. (Matendo 20:29, 30; 2 Petro 2:1-3) Jumbe za Yesu kwa makundi saba zilionyesha kwamba kuelekea mwisho wa maisha ya Yohana, Babuloni Mkubwa alikuwa akifanya maendeleo fulani katika jitihada zake za kufisidi. (Ufunuo 2:6, 14, 15, 20-23) Lakini Yesu alikuwa tayari ameonyesha kadiri ambayo angeruhusiwa afike.

      Ngano na Magugu

      8, 9. (a) Fumbo la maneno la Yesu kuhusu ngano na magugu lilionyesha nini? (b) Ikawaje “wakati watu walikuwa wakilala”?

      8 Katika fumbo la maneno lake la ngano na magugu, Yesu alisema juu ya mtu ambaye alipanda mbegu nzuri katika shamba lake. Lakini “wakati watu walikuwa wakilala,” adui alikuja akapanda magugu kwa wingi. Kwa sababu hiyo, ngano ikaja kufichwa na magugu. Yesu alifafanua fumbo la maneno lake kwa maneno haya: “Mpanzi wa mbegu nzuri ni Mwana wa binadamu; shamba ni ulimwengu; kwa habari ya mbegu nzuri, hawa ni wana wa ufalme; lakini magugu ni wana wa mwovu, na adui aliyeyapanda ni Ibilisi.” Kisha akaonyesha kwamba “mbegu nzuri” na “magugu” vingeruhusiwa vikue pamoja mpaka “umalizio wa mfumo wa mambo,” wakati malaika ‘wangekusanya ili kuondoa’ magugu ya ufananisho.—Mathayo 13:24-30, 36-43, NW.

      9 Walichoonya Yesu na mitume Paulo na Petro kikawako. “Wakati watu walikuwa wakilala,” ama baada ya mitume kulala usingizi katika kifo ama wakati waangalizi Wakristo waliposinzia katika kulinda kondoo za Mungu, uasi-imani wa Kibabuloni ulichipuka mle mle ndani ya kundi. (Matendo 20:31) Upesi magugu yakazidi wingi wa ngano na kuificha isionekane. Kwa karne kadhaa huenda ikawa ilionekana kwamba mbegu ya mwanamke ilikuwa imefunikwa kabisa na marinda makubwa ya Babuloni Mkubwa.

      10. Ni nini kilichotukia kufikia miaka ya 1870, naye Babuloni Mkubwa alitendaje kuitikia hilo?

      10 Kufikia miaka ya 1870 Wakristo wapakwa-mafuta walianza kufanya jitihada za bidii wajiondoe wenyewe kutoka ushirika wa njia za kikahaba za Babuloni Mkubwa. Wao waliachana na mafundisho bandia ambayo Jumuiya ya Wakristo ilikuwa imeingiza kutoka upagani na kwa ujasiri wakatumia Biblia katika kuhubiri kwamba majira ya Mataifa yangekwisha 1914. Chombo kikuu cha Babuloni Mkubwa, viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo, kilipinga vichocheo hivi vya kurudisha ibada ya kweli. Wakati wa vita ya ulimwengu ya kwanza wao walitumia kwa faida yao ukichaa wa wakati wa vita wakajaribu kufutilia mbali kikundi hicho kidogo cha Wakristo waaminifu. Katika 1918, wakati utendaji wao ulikuwa karibu umekomeshwa kabisa, ilionekana kama Babuloni Mkubwa alikuwa amefaulu. Alionekana kama amewashinda.

      11. Ni nini kilichotokezwa na anguko la Babuloni wa kale?

      11 Kama tulivyoona wakati uliopita, jiji la Babuloni lenye kiburi lilipatwa na anguko la nguvu lenye msiba katika 539 K.W.K. Ndipo kilio hiki kikasikika: “Ameanguka! Babuloni ameanguka!” Kiti kikubwa cha milki ya ulimwengu kilikuwa kimeanguka kwa majeshi ya Umedi na Uajemi chini ya Sairasi Mkuu. Ijapokuwa jiji lenyewe liliokoka ushindi huo, anguko la nguvu zalo lilikuwa halisi, na lilitokeza kuachiliwa kwa mateka walo Wayahudi. Walirudi Yerusalemu wakarudishe ibada safi kule.—Isaya 21:9; 2 Nyakati 36:22, 23; Yeremia 51:7, 8.

      12. (a) Katika nyakati zetu, inaweza kusemwaje kwamba Babuloni Mkubwa ameanguka? (b) Ni nini kinachoonyesha kwamba Yehova amekatalia mbali kabisa Jumuiya ya Wakristo?

      12 Katika nyakati zetu pia kilio kimesikika kwamba Babuloni Mkubwa ameanguka! Ufaulu wa kitambo wa Jumuiya ya Wakristo ya Kibabuloni katika 1918 uligeuzwa upesi sana katika 1919 wakati baki la wale wapakwa-mafuta, jamii ya Yohana, liliporudishwa kupitia ufufuo wa kiroho. Babuloni Mkubwa alikuwa ameanguka kwa habari ya kuwa na uwezo wa kushikilia mateka ya watu wa Mungu. Kama nzige, ndugu wapakwa-mafuta wa Kristo walitoka mabumba-mabumba katika abiso, wakiwa tayari kwa tendo. (Ufunuo 9:1-3; 11:11, 12, NW) Wao walikuwa ndiye “mtumwa mwaminifu na mwenye uangalifu” wa ki-siku-hizi, na Bwana-Mkubwa aliwaweka rasmi juu ya mali yake yote duniani. (Mathayo 24:45-47, NW) Kutumiwa kwao katika njia hii kulithibitisha kwamba Yehova alikuwa ametupilia mbali kabisa Jumuiya ya Wakristo lijapokuwa dai layo la kuwa ndiyo mwakilishi wake duniani. Ibada safi iliimarishwa tena, na njia ilifunguliwa kwa kazi ya kukamilisha kutia muhuri baki la wale 144,000—wabakio wa mbegu ya mwanamke, adui wa zamani wa Babuloni Mkubwa. Yote haya yaliashiria ushinde wenye kuponda-ponda wa hilo tengenezo la kidini la kishetani.

      Uvumilivu kwa Watakatifu

      13. (a) Malaika wa tatu anatangaza nini? (b) Yehova anafanya hukumu gani juu ya wale wanaopokea alama ya hayawani-mwitu?

      13 Sasa malaika wa tatu anasema. Sikiliza! “Na malaika mwingine, wa tatu, akafuata wao, akisema kwa sauti kubwa: ‘Ikiwa yeyote huabudu hayawani-mwitu na mfano wake, na hupokea alama juu ya kipaji cha uso wake au juu ya mkono wake, yeye pia atakunywa ya divai ya kasirani ya Mungu ambayo humiminwa bila kutoholewa ndani ya kikombe cha hasira-kisasi yake.’” (Ufunuo 14:9, 10a, NW) Kwenye Ufunuo 13:16, 17, ilifunuliwa kwamba wakati wa siku ya Bwana wale wasioabudu mfano wa hayawani-mwitu wangeteseka—hata kuuawa. (Ufunuo 1:10, NW) Sasa tunajifunza kwamba Yehova ameazimia kuwaleta hukumuni wale “wenye alama, jina la hayawani-mwitu au nambari ya jina lake.” Wao watalazimika kunywa kikombe cha hasira-kisasi’ kichungu cha kasirani ya Yehova. Hiyo itamaanisha nini kwao? Katika 607 K.W.K., wakati Yehova alipolazimisha Yerusalemu kunywa “kikombe chake cha hasira-kali” jiji hilo lilipatwa na “mporo, mvunjiko, na njaa na upanga” mikononi mwa Wababuloni. (Isaya 51:17, 19, NW) Hali kadhalika, wapatapo kunywa kikombe cha hasira-kisasi ya Yehova, watukuzaji wa mamlaka za kisiasa za dunia na mfano wazo, Umoja wa Mataifa, tokeo kwao litakuwa baa. (Yeremia 25:17, 32, 33, NW) Wataharibiwa kabisa kabisa.

      14. Hata kabla ya uharibifu wa wale wanaoabudu hayawani-mwitu na mfano wake, ni lazima hao wapatwe na nini, na Yohana anaelezaje hilo?

      14 Ingawa hivyo, hata kabla ya kuwa hivyo wale walio na alama ya hayawani hupatwa na matokeo yenye kutesa ya kutokuwa na kibali cha Yehova. Akinena juu ya mwabudu hayawani-mwitu na mfano wake, yule malaika amwarifu Yohana: “Na yeye atateswa kwa moto na salfa katika mwono wa malaika watakatifu na katika mwono wa Mwana-Kondoo. Na moshi wa kuteswa kwao hupaa milele na milele, na mchana na usiku wao hawana pumziko, wale ambao huabudu hayawani-mwitu na mfano wake, na yeyote ambaye hupokea alama ya jina lake.”—Ufunuo 14:10b, 11, NW.

      15, 16. Ni nini maana ya maneno “moto na salfa” kwenye Ufunuo 14:10?

      15 Baadhi ya watu wameona mtajo hapa wa “moto na salfa” (“moto na kiberiti,” Union Version) kuwa ushuhuda wa kuwako kwa mahali pa moto wa mateso. Lakini mtazamo mfupi wa unabii unaofanana na huu huonyesha maana halisi ya maneno hayo katika muktadha huu. Huko nyuma katika siku za Isaya, Yehova alionya taifa la Edomu kwamba wao wangeadhibiwa kwa sababu ya uadui wao kuelekea Israeli. Yeye alisema: “Vijito vyake vitageuzwa kuwa lami, na mavumbi yake yatageuzwa kuwa kiberiti [salfa, NW] na ardhi yake itakuwa lami iwakayo. Haitazimwa mchana na usiku, moshi wake utapaa milele. Tangu kizazi hata kizazi itakuwa ukiwa; hapana mtu atakayepita kati yake milele na milele.”—Isaya 34:9, 10.

      16 Je! Edomu ilivurumishwa ndani ya mahali pa kifumbo penye moto ichomeke milele? Bila shaka sivyo. Badala ya hivyo, taifa hilo lilitoweka kabisa kutoka mandhari ya ulimwengu kana kwamba lilikuwa limeliwa kabisa na moto na salfa. Tokeo la mwisho la adhabu hiyo halikuwa mateso ya milele bali “utupu . . . ukiwa . . . si kitu.” (Isaya 34:11, 12) ‘Kupaa milele kwa moshi’ hutoa kielezi cha hili waziwazi. Nyumba inapoteketea, moshi huendelea kutoka katika majivu kwa wakati fulani baada ya miale kufa, ukiandalia watazamaji ithibati ya kwamba kulikuwako mteketezo wenye kuharibu. Hata leo watu wa Mungu hukumbuka somo wanaloweza kujifunza kutokana na uharibifu wa Edomu. Kwa njia hiyo ‘moshi wa kuchomeka kwayo’ ungali unapaa kwa njia ya ufananisho.

      17, 18. (a) Ni nini tokeo kwa wale ambao hupokea alama ya hayawani-mwitu? (b) Ni katika njia gani waabudu wa hayawani-mwitu huteswa? (c) Ni jinsi gani “moshi wa kuteswa kwao hupaa milele na milele”?

      17 Wale walio na alama ya hayawani-mwitu wataharibiwa kabisa pia, kana kwamba kwa moto. Kama unabii unavyofunua baadaye, miili yao mifu itaachwa bila kuzikwa iliwe na wanyama na ndege. (Ufunuo 19:17, 18) Kwa wazi, basi, wao hawateswi milele! Wao ‘huteswaje kwa moto na salfa’? Kwa njia ya kwamba mbiu ya ukweli huwafichua na kuwaonya juu ya hukumu ya Mungu inayokuja. Kwa hiyo wao wanasuta watu wa Mungu na, inapowezekana wanashawishi kwa uayari hayawani-mwitu wa kisiasa anyanyase na hata kuua Mashahidi wa Yehova. Ukiwa upeo, wanadini hao wenye kupinga wataharibiwa kama kwa moto na salfa. Ndipo “moshi wa kuteswa kwao hupaa milele na milele” katika njia ya kwamba hukumu ya Mungu kwao itatumika kuwa kiwango cha kupimia endapo wakati mwingine wowote uhalali wa enzi kuu ya Yehova unatiliwa shaka. Suala hilo litakuwa limemalizwa kwa umilele wote.

      18 Ni nani leo wanaopeleka ujumbe wenye kutesa? Kumbuka, wale nzige wa ufananisho wana mamlaka ya kutesa watu ambao hawana muhuri wa Mungu juu ya vipaji vya nyuso zao. (Ufunuo 9:5) Kwa wazi, hawa wakiwa chini ya mwelekezo wa kimalaika ndio ‘watesaji.’ Hao nzige wa ufananisho huendelea hivyo, hivi kwamba “mchana na usiku wao hawana pumziko, wale ambao huabudu hayawani-mwitu na mfano wake, na yeyote ambaye hupokea alama ya jina lake.” Na mwishowe, baada ya uharibifu wao, ithibati yenye kukumbusha kutetewa huko kwa enzi kuu ya Yehova, “moshi wa kuteswa kwao,” utapaa milele na milele. Jamii ya Yohana na ivumilie mpaka kutetewa huko kukamilishwe! Kama anavyomalizia malaika: “Hapa ndipo humaanisha uvumilivu kwa watakatifu, wale ambao hushika amri za Mungu na imani ya Yesu.”—Ufunuo 14:12, NW.

      19. Ni kwa nini uvumilivu unatakwa upande wa watakatifu, na Yohana anaripoti ni nini kinachowaimarisha?

      19 Ndiyo, “uvumilivu kwa watakatifu” humaanisha kuabudu kwao Yehova pekee kupitia Yesu Kristo. Ujumbe wao haupendwi na wengi. Unaongoza kwenye upinzani, mnyanyaso, hata kifo cha imani. Lakini wao huimarishwa na yale ambayo Yohana anafuata kuripoti: “Na mimi nikasikia sauti kutoka katika mbingu ikisema: ‘Andika: Wenye furaha ni wale wafu ambao hufa katika muungano pamoja na Bwana kutoka wakati huu na kuendelea. Ndiyo, yasema roho, acheni wao wapumzike kazi zao ngumu, kwa kuwa vitu walivyofanya huenda moja kwa moja pamoja nao.’”—Ufunuo 14:13, NW.

      20. (a) Ahadi inayoripotiwa na Yohana inapatanaje na unabii wa Paulo juu ya kuwapo kwa Yesu? (b) Wale wa wapakwa-mafuta wanaokufa baada ya Shetani kutupwa nje ya mbingu wanaahidiwa pendeleo gani la pekee?

      20 Ahadi hii inapatana vizuri na unabii wa Paulo kuhusu kuwapo kwa Yesu: “Wale ambao ni wafu katika muungano pamoja na Kristo watainuka kwanza. Baadaye sisi tulio hai ambao tunaendelea kuishi [wale wa wapakwa-mafuta ambao huendelea kuishi hadi ndani ya siku ya Bwana], pamoja na wao tutadakwa mbali katika mawingu ili kumkuta Bwana katika hewa.” (1 Wathesalonike 4:15-17, NW) Baada ya Shetani kutolewa nje ya mbingu, wale waliokuwa wafu katika muungano pamoja na Kristo waliinuka kwanza. (Linga Ufunuo 6:9-11.) Baadaye, wale wa wapakwa-mafuta ambao hufa wakati wa siku ya Bwana huahidiwa pendeleo la pekee. Ufufuo wao kwenye uhai wa roho katika mbingu ni wa papo hapo, “katika kufumba na kufumbua jicho.” (1 Wakorintho 15:52, NW) Lo! hiyo ni ajabu kama nini! Na kazi zao za uadilifu huendelea moja kwa moja katika milki ya kimbingu.

      Vuno la Dunia

      21. Yohana hutuambia nini juu ya “vuno la dunia”?

      21 Wengine watanufaika pia na hii siku ya hukumu, kama Yohana anavyoendelea kutuambia: “Na mimi nikaona, na, tazama! wingu jeupe, na juu ya wingu mtu fulani ameketi kama mwana wa binadamu, akiwa na taji la dhahabu juu ya kichwa chake na mundu mkali katika mkono wake. Na malaika mwingine [wa nne] akaibuka katika patakatifu pa hekalu, akilia kwa sauti kubwa kwa mmoja anayeketi juu ya wingu: ‘Tia ndani mundu wako na kuvuna, kwa sababu saa imewadia ili kuvuna, kwa kuwa vuno la dunia limeiva kabisa.’ Na yule mmoja anayeketi juu ya lile wingu akatia ndani mundu wake kwenye dunia, na dunia ikavunwa.”—Ufunuo 14:14-16, NW.

      22. (a) Ni nani anayevaa taji la dhahabu na kuketi juu ya wingu jeupe? (b) Upeo wa kazi ya kuvuna unatukia lini, na jinsi gani?

      22 Utambulisho wa mmoja anayeketi juu ya wingu jeupe hauna shaka. Kwa wazi, aketiye juu ya wingu jeupe, hushabihi “mwana wa binadamu” na mwenye taji la dhahabu, ni Yesu, Mfalme wa Kimesiya ambaye Danieli aliona pia katika njozi. (Danieli 7:13, 14; Marko 14:61, 62) Lakini ni vuno gani ambalo limetolewa unabii hapa? Alipokuwa duniani, Yesu alifananisha kazi ya kufanya wanafunzi na kuvunwa kwa shamba la ulimwengu wa binadamu. (Mathayo 9:37, 38; Yohana 4:35, 36) Upeo wa kazi hii ya kuvuna unakuja katika siku ya Bwana, wakati Yesu amevikwa taji akiwa Mfalme na anatekeleza hukumu kwa niaba ya Baba yake. Hivyo, wakati wake wa kutawala, tangu 1914, pia ni wakati wa shangwe kwa ajili ya kuleta ndani vuno.—Linga Kumbukumbu 16:13-15.

      23. (a) Neno la kuanza kuvuna hutoka kwa nani? (b) Ni kuvuna gani ambako kumetukia tangu 1919 hadi sasa?

      23 Ijapokuwa yeye ni Mfalme na Jaji, Yesu anangojea neno kutoka kwa Yehova Mungu wake kabla ya kuanza kuvuna. Neno hilo linakuja kutoka “patakatifu pa hekalu” kupitia malaika. Mara hiyo, Yesu anatii. Kwanza, kutoka 1919 kuendelea, yeye anaagiza malaika wake wamalize kazi ya kuvuna 144,000. (Mathayo 13:39, 43; Yohana 15:1, 5, 16) Halafu, kazi ya vuno la kukusanya ndani umati mkubwa wa kondoo wengine yatukia. (Yohana 10:16; Ufunuo 7:9) Historia huonyesha kwamba kati ya 1931 na 1935 idadi kubwa kidogo ya hawa kondoo wengine ilianza kutokea. Katika 1935 Yehova alifungulia jamii ya Yohana uelewevu wa utambulisho wa kweli wa huu umati mkubwa wa Ufunuo 7:9-17. Tangu hapo, mkazo mwingi uliwekwa juu ya kukusanya ndani huu umati. Kufikia mwaka 2005, idadi yao ilikuwa imepita alama ya milioni sita, na ingali inaongezeka. Hakika, mmoja aliye kama mwana wa binadamu amevuna vuno jingi lenye shangwe katika huu wakati wa mwisho.—Linga Kutoka 23:16; 34:22.

      Kukanyaga Mzabibu wa Dunia

      24. Ni kitu gani kilicho mkononi mwa malaika wa tano, na malaika wa sita anaita nini kwa mpaazo?

      24 Vuno la wokovu likiwa limekamilika, ni wakati wa vuno jingine. Yohana aripoti: “Na bado malaika mwingine [wa tano] akaibuka kutoka katika patakatifu pa hekalu palimo katika mbingu, yeye, vilevile, akiwa na mundu mkali. Na bado malaika mwingine [wa sita] akaibuka kutoka katika madhabahu na yeye alikuwa na mamlaka juu ya moto. Na yeye akaita kwa sauti kubwa kwa mmoja ambaye alikuwa na mundu mkali, akisema: ‘Tia ndani mundu wako mkali na kukusanya vichala vya mzabibu wa dunia, kwa sababu zabibu zao zimepata kuiva.’” (Ufunuo 14:17, 18, NW) Makundi mengi ya malaika yameaminishwa kazi nyingi ya kuvuna wakati wa siku ya Bwana, wakitenganisha wema na wabaya!

      25. (a) Ni nini kinachoonyeshwa na uhakika wa kwamba malaika wa tano anatoka katika patakatifu pa hekalu? (b) Ni kwa nini inafaa kwamba amri ya kuanza kuvuna inakuja kutoka kwa malaika ambaye “anaibuka kutoka katika madhabahu”?

      25 Malaika wa tano anakuja kutoka kuwapo kwa Yehova katika patakatifu pa hekalu, hivyo, vuno la mwisho pia linafanywa kulingana na penzi la Yehova. Huyo malaika anaamriwa aanze kazi yake kwa ujumbe unaowasilishwa kupitia malaika mwingine ambaye “akaibuka kutoka madhabahu.” Uhakika huu ni wa maana sana, kwa kuwa nafsi zenye uaminifu zilizokuwa chinichini ya madhabahu zilikuwa zimeuliza: “Ni mpaka lini, Bwana Mwenye Enzi Kuu mtakatifu na wa kweli, wewe unajizuia usihukumu na kulipiza kisasi damu yetu juu ya wale ambao wanakaa juu ya dunia?” (Ufunuo 6:9, 10, NW) Kwa kuvunwa kwa huu mzabibu wa dunia, kilio hiki cha kutaka kisasi kitatoshelezwa.

      26. Ni nini ulio “mzabibu wa dunia”?

      26 Lakini ni nini ulio “mzabibu wa dunia”? Katika Maandiko ya Kiebrania, taifa la Kiyahudi lilisemwa kuwa mzabibu wa Yehova. (Isaya 5:7; Yeremia 2:21) Hali kadhalika, Yesu Kristo pamoja na wale ambao watatumikia pamoja na yeye katika Ufalme wa Mungu wanasemwa kuwa mzabibu. (Yohana 15:1-8) Katika mazingira haya, tabia ya maana ya mzabibu ni kwamba unazaa tunda, na mzabibu wa kweli wa Kikristo umezaa tunda jingi kwa sifa ya Yehova. (Mathayo 21:43) Kwa hiyo, lazima “mzabibu wa dunia,” uwe, si huu mzabibu halisi, bali mwigo wa Shetani wa huo mzabibu, mfumo wake mfisadi uonekanao wa kiserikali juu ya aina ya binadamu, pamoja na “vichala” mbalimbali vyao vya tunda la roho waovu ambalo limezaliwa kwa muda wa karne zilizopita. Babuloni Mkubwa, ambaye Jumuiya ya Wakristo yenye kuasi imani ndiyo yenye kutokeza zaidi, ametumia uvutano mkubwa juu ya huu mzabibu wenye sumu.—Linga Kumbukumbu 32:32-35.

      27. (a) Kunatukia nini wakati malaika mwenye mundu anapokusanya “mzabibu wa dunia”? (b) Ni unabii gani katika Maandiko ya Kiebrania unaoonyesha kadiri ya vuno hilo?

      27 Lazima hukumu itekelezwe! “Na malaika akatia mundu wake ndani ya dunia na kukusanya mzabibu wa dunia, na yeye akavurumisha huo ndani ya shinikizo la divai kubwa la kasirani ya Mungu. Na shinikizo la divai likakanyagwa nje ya jiji, na damu ikaja nje ya shinikizo la divai mpaka juu kabisa kwenye hatamu za wale farasi, kwa kitalifa cha farlong’i elfu moja mia sita.” (Ufunuo 14:19, 20, NW) Ghadhabu ya Yehova dhidi ya mzabibu huu imetangazwa kwa muda mrefu uliopita. (Sefania 3:8) Unabii katika kitabu cha Isaya hauachi shaka lolote kwamba mataifa mazima mazima yataharibiwa wakati shinikizo la divai linapokanyagwa. (Isaya 63:3-6) Yoeli vilevile alitoa unabii kwamba “umati wa watu” mkubwa, mataifa mazima mazima, yangekanyagwa na kuharibiwa katika “shinikizo la divai,” katika “uwanda-bonde wa uamuzi.” (Yoeli 3:12-14, NW) Kwa kweli, ni vuno kubwa sana ambalo mfano walo hautatukia tena kamwe! Kulingana na njozi ya Yohana, si zabibu tu zinazovunwa bali mzabibu wote mzima wa ufananisho unakatwa na kutupwa ndani ya shinikizo la divai ukanyagwe. Hivyo mzabibu wa dunia utang’olewa wote na hautaweza kamwe kukua tena.

      28. Ni nani wanaokanyaga mzabibu wa dunia, na humaanisha nini kwamba shinikizo la divai ‘linakanyagwa nje ya jiji’?

      28 Mkanyago wa kinjozi hufanywa na farasi, kwa kuwa damu inayokanyagwa kutoka mzabibu inafika kwenye “zile hatamu za wale farasi.” Kwa kuwa usemi “wale farasi” mara nyingi hurejezea utendaji wa kivita, lazima huu uwe wakati wa vita. Yale majeshi ya kimbingu ambayo hufuata Yesu kwenye vita ya mwisho dhidi ya mfumo wa mambo wa Shetani wanasemwa kuwa wanakanyaga “shinikizo la divai ya kasirani ya hasira-kisasi ya Mungu Mweza Yote.” (Ufunuo 19:11-16, NW) Kwa wazi hawa ndio wanaokanyaga “mzabibu wa dunia.” Hilo shinikizo la divai ‘hukanyagwa nje ya jiji,’ yaani, nje ya Sayuni la kimbingu. Kweli kweli, inafaa huo mzabibu wa dunia ukanyagwe duniani. Lakini pia ‘utakanyagwa nje ya jiji, hivi kwamba hakuna dhara litakalopata wale wabakio wa mbegu ya mwanamke, wanaowakilisha Sayuni la kimbingu duniani. Hawa pamoja na umati mkubwa watafichwa kwa usalama ndani ya mpango wa Yehova wa tengenezo la kidunia.—Isaya 26:20, 21.

      29. Damu kutoka shinikizo la divai ina kina cha kadiri gani, hufika kwenye kitalifa gani, na hayo yote huonyesha nini?

      29 Njozi hii iliyo wazi sana ina ulingano na kule kupondwa-pondwa kwa falme za dunia kwa njia ya jiwe la Ufalme kunakoelezwa kwenye Danieli 2:34, 44. Kutakuwako kuuliwa mbali kabisa. Ule mto wa damu kutoka shinikizo la divai ni wenye kina sana, mpaka kwenye hatamu za wale farasi, na hufikia kitalifa cha farlong’i 1,600.a Tarakimu hii kubwa, inayotokezwa kwa kuzidisha mraba wa nne kwa mraba wa kumi (4 x 4 x 10 x 10), kwa mkazo huwasilisha ujumbe wa kwamba ithibati ya uharibifu itahusisha ndani dunia yote. (Isaya 66:15, 16) Uharibifu utakuwa kamili na usiogeuzika. Hasha, la hasha, mzabibu wa dunia wa Shetani hautatia mzizi tena!—Zaburi 83:17, 18.

      30. Ni matunda gani ya mzabibu wa Shetani, na azimio letu limepaswa kuwa nini?

      30 Sisi tukiwa tunaishi ndani sana ya wakati wa mwisho, hiyo njozi ya haya mavuno mawili ni yenye maana sana. Tunaloweza kufanya tu ni kutazama pande zetu zote tuone yaliyo matunda ya mzabibu wa Shetani. Utoaji-mimba na namna nyinginezo za uuaji kimakusudi; ugoni-jinsia-moja, uzinzi, na namna nyingine za utovu wa adili, utovu wa haki, utovu wa shauku asilia—mambo yote kama hayo hufanya ulimwengu huu kuwa mbaya sana machoni pa Yehova. Mzabibu wa Shetani huzaa “tunda la pando lenye sumu na pakanga.” Mwendo wao wa uangamivu, wenye kuabudu sanamu hukosa kuheshimu Muumba mtukufu wa aina ya binadamu. (Kumbukumbu 29:18; 32:5; Isaya 42:5, 8, NW) Lo! ni pendeleo lililoje kuwa tukishirikiana kiutendaji na jamii ya Yohana katika kuvuna tunda zuri ambalo Yesu anatokeza kwa sifa ya Yehova! (Luka 10:2) Sisi sote na tuazimie kwamba hatutatiwa mawaa kamwe na mzabibu wa ulimwengu huu, na hivyo sisi na tuepuke kukanyagwa pamoja na huo mzabibu wa dunia wakati hukumu mbaya ya Yehova inapotekelezwa.

      [Maelezo ya Chini]

      a Farlong’i 1,600 ni kama kilometa 300, au maili za Kiingereza 180.—Ufunuo 14:20, New World Translation Reference Bible, kielezi cha chini.

      [Picha katika ukurasa wa 208]

      ‘Divai ya Uasherati Wake’

      Sehemu Yenye Kutokeza ya Babuloni Mkubwa ni Kanisa Katoliki la Roma. Kanisa hilo linatawalwa na papa katika Roma nalo linadai kwamba kila papa ni mwandamizi wa mtume Petro. Yafuatayo ni baadhi ya mambo ya hakika yaliyochapishwa ya hawa wanaoitwa eti waandamizi:

      Formoso (891-96): “Miezi tisa baada ya kifo chake, mwili wa Formoso ulifukuliwa kutoka kaburi la mapapa na kushtakiwa ili kujaribiwa mbele ya baraza linalohukumu maiti, ambalo katika hilo Stefano [papa mpya] alisimamia. Huyo papa aliyekufa alishtakiwa kosa la kutaka makuu kupita kiasi kwa ajili ya cheo cha papa na matendo yake yote yalijulishwa wazi kuwa si halali. . . . Maiti hiyo ilivuliwa majoho ya kipapa; vidole vya mkono wa kulia vikakatwa.”—New Catholic Encyclopedia.

      Stefano 6 (896-97): “Kwa muda wa miezi michache [ya jaribio la maiti ya Formoso] tendo-mwitikio lenye jeuri lilikomesha upapa wa Papa Stefano; yeye alinyang’anywa nishani ya upapa, akatiwa gerezani, na akanyongwa.”—New Catholic Encyclopedia.

      Sergio 3 (904-11): “Watangulizi wake wawili wa karibu-karibu . . . walinyongwa gerezani. . . . Katika Roma yeye aliungwa mkono na jamaa ya Theofilakto, ambayo kwa mmoja wa mabinti yayo, Marozia, yeye anadhaniwa kuwa alikuwa amepata mwana (baadaye Papa John wa 11).”—New Catholic Encyclopedia.

      Stefano 7 (928-31): “Katika miaka ya mwisho ya upapa wake, Papa John 10 . . . amejiletea hasira-kisasi ya Marozia, aliyekuwa Donna Senatrix wa Roma, naye alikuwa ametiwa gerezani na kuuawa kwa hila. Ndipo Marozia akampa Papa Leo wa 6 upapa, ambaye alikufa miezi 6 1/2 katika ofisi. Stefano 7 akamwandamia, yaelekea kupitia uvutano wa Marozia. . . . Wakati wa miaka 2 yake akiwa Papa, yeye alikuwa hana nguvu chini ya utawala wa Marozia.”—New Catholic Encyclopedia.

      John 11 (931-35): “Stefano 7 alipokufa . . . , Marozia, wa Nyumba ya Theofilakto, alipata upapa kwa ajili ya mwanaye John, kijana katika miaka yake ya 20 na kitu. . . . Akiwa papa, John alitawalwa na mamaye.”—New Catholic Encyclopedia.

      John 12 (955-64): “Yeye alikuwa hajatimiza [miaka] kumi na minane, na ripoti za wakati wake hukubaliana juu ya kutopendezwa kwake na vitu vya kiroho, kuzoelea anasa zisizo za adabu, maisha ya ufasiki yasiyozuiliwa.”—The Oxford Dictionary of Popes.

      Benedikto 9 (1032-44; 1045; 1047-48): “Yeye alikuwa mwenye sifa mbaya ya kuuzia mdhamini wa ubatizo wake upapa na kisha kudai tena mara mbili cheo hicho baadaye.”—The New Encyclopædia Britannica.

      Hivyo, badala ya kufuata kielelezo cha Petro mwaminifu, hawa na mapapa wengine walikuwa uvutano mbovu. Wao waliachilia hatia ya damu na uasherati wa kiroho na wa kimwili, pamoja na uvutano wa Kiyezebeli, ufisidi kanisa walilotawala. (Yakobo 4:4) Katika 1917 kitabu The Finished Mystery cha Wanafunzi wa Biblia kilionyesha waziwazi sana kwa urefu mengi ya mambo haya ya hakika. Hii ilikuwa njia moja ambayo Wanafunzi wa Biblia katika siku hizo ‘walipiga dunia kwa kila aina ya tauni.’—Ufunuo 11:6; 14:8; 17:1, 2, 5, NW.

      [Picha katika ukurasa wa 206]

      Kristo aliyeketishwa juu ya kiti cha ufalme hufanya hukumu kwa kuungwa mkono na malaika

      [Picha katika ukurasa wa 207]

      Baada ya Babuloni kuanguka katika 539 K.W.K., wafungwa wayo waliachiliwa

  • Kazi za Yehova—Kubwa na za Ajabu
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Sura ya 31

      Kazi za Yehova—Kubwa na za Ajabu

      Njozi ya 10—Ufunuo 15:1–16:21

      Habari: Yehova akiwa katika patakatifu pake; mabakuli ya hasira-kisasi yake yamwagwa ndani ya dunia

      Wakati wa utimizo: 1919 hadi Har–Magedoni

      1, 2. (a) Ni ishara gani ya tatu anayoripoti Yohana? (b) Ni daraka gani la kimalaika ambalo watumishi wa Yehova wamejua kwa muda mrefu?

      MWANAMKE akizaa mtoto wa kiume! Drakoni mkubwa akitafuta kumeza huyo mtoto! Hizo ishara mbili za kimbingu, zikionyeshwa kitaswira kwa njia iliyo wazi sana katika Ufunuo sura ya 12, zilitusisitizia kwamba lile bishano la muda mrefu linalohusu Mbegu ya mwanamke wa Mungu na Shetani na mbegu yake ya roho waovu linafikia upeo walo. Katika kukazia vifananisho hivi, Yohana anasema? “Na ishara kubwa ilionwa katika mbingu . . . Na ishara nyingine ikaonwa.” (Ufunuo 12:1, 3, 7-12, NW) Sasa, Yohana anaripoti ishara ya tatu: “Na mimi nikaona katika mbingu ishara nyingine, kubwa na ya ajabu, malaika saba wakiwa na tauni saba. Hizi ndizo za mwisho, kwa sababu kwa njia yazo kasirani ya Mungu inaletwa kwenye tamati.” (Ufunuo 15:1, NW) Ishara hii ya tatu vilevile ina maana ya umuhimu kwa watumishi wa Yehova.

      2 Angalia madaraka ya maana waliyo nayo malaika katika kutimiza penzi la Mungu. Uhakika huu umejulikana na watumishi wa Yehova kwa muda mrefu. Kwani, chini ya uvuvio mwandikaji wa zaburi wa kale hata alinena kwa malaika kama hao, akiwahimiza: “Barikini Yehova, O nyinyi malaika zake, wenye uweza katika nguvu, mtimizao neno lake, kwa kusikiliza sauti ya neno lake”! (Zaburi 103:20, NW) Sasa, katika mandhari mpya hii, malaika wanapewa mgawo wa kumimina tauni saba za mwisho.

      3. Ni nini zilizo tauni saba, na kuzimimina kunaonyesha nini?

      3 Hizi ni tauni gani? Kama vile ile mipigo saba ya tarumbeta, hizo ni matamko makali ya hukumu yakitangaza peupe maoni ya Yehova ya sura tofautitofauti za ulimwengu huu na kuonya juu ya tokeo la mwisho la maamuzi yake ya kihukumu. (Ufunuo 8:1–9:21) ‘Kumiminwa kwazo kunaelekeza kwenye kutekelezwa kwa hukumu hizo, wakati vitu vya hasira-kisasi ya Yehova vinapoharibiwa katika siku ya kasirani yake yenye kuwaka. (Isaya 13:9-13; Ufunuo 6:16, 17) Hivyo, kwa njia yazo “kasirani ya Mungu inaletwa kwenye tamati.” Lakini kabla ya kueleza huko ‘kumiminwa kwa tauni,’ Yohana anatuambia juu ya binadamu fulani ambao hawataathiriwa vibaya nazo. Wakiwa wamekataa alama ya hayawani-mwitu, washikamanifu hawa wanaimbia Yehova sifa wanapopiga mbiu ya siku yake ya kisasi.—Ufunuo 13:15-17, NW.

      Wimbo wa Musa na wa Mwana-Kondoo

      4. Sasa ni kitu gani kinachokuja katika mtazamo wa Yohana?

      4 Sasa picha nzuri ajabu inakuja katika mtazamo wa Yohana: “Na mimi nikaona kilichoonekana kuwa kama bahari ya kioo yenye kutangamana na moto, na wale ambao hutoka wakiwa washindi wa hayawani-mwitu na mfano wake na nambari ya jina lake wakisimama karibu ya bahari ya kioo, wakiwa na vinubi vya Mungu.”—Ufunuo 15:2, NW.

      5. Ni nini inayotolewa picha na “bahari ya kioo yenye kutangamana na moto”?

      5 “Bahari ya kioo” ni ile ile ambayo Yohana aliona mapema zaidi, ikiwa mbele ya kiti cha ufalme cha Mungu. (Ufunuo 4:6, NW) Inafanana na “bahari ya kuyeyushwa,” au chombo cha kuwekea maji cha hekalu la Solomoni, ambamo makuhani walipata maji wajisafishe wenyewe. (1 Wafalme 7:23, NW) Hivyo hiyo ni kiwakilishi kizuri cha “mwosho wa maji,” yaani, Neno la Mungu, ambalo Yesu hutumia kusafisha kundi la kikuhani la Wakristo wapakwa-mafuta. (Waefeso 5:25, 26; Waebrania 10:22, NW) Hii “bahari ya kioo” ni “yenye kutangamana na moto,” kuonyesha kwamba wapakwa-mafuta hawa hutahiniwa na kutakaswa wanapotii kiwango cha juu walichowekewa. Na zaidi, hutukumbusha kwamba pia Neno la Mungu lina semi za hukumu zenye moto dhidi ya maadui wake. (Kumbukumbu 9:3; Sefania 3:8) Baadhi ya hukumu hizi zenye moto zinadhihirishwa katika tauni saba ambazo zi karibu kumiminwa.

      6. (a) Ni nani walio waimbaji wanaosimama mbele ya bahari ya kioo, na sisi tunajuaje? (b) Ni katika njia gani wao ‘wametoka wakiwa washindi’?

      6 Uhakika wa kwamba bahari ya kuyeyushwa katika hekalu la Solomoni ilikuwa ya kutumiwa na makuhani huonyesha kwamba wale waimbaji wanaosimama mbele ya bahari ya kioo ya kimbingu ni wa jamii ya kikuhani. Wana “vinubi vya Mungu,” na kwa hiyo sisi tunawatambulisha na wazee 24 na 144,000, kwa kuwa vikundi hivi viwili pia huimba kwa kufuatanisha na kinubi. (Ufunuo 5:8; 14:2) Waimbaji ambao Yohana huona “hutoka wakiwa washindi wa hayawani-mwitu na mfano wake na nambari ya jina lake.” Kwa hiyo lazima wao wawe wa wale 144,000 wanaoishi duniani wakati wa siku za mwisho. Wakiwa kikundi, kweli kweli wao hutoka wakiwa washindi. Kwa karibu miaka 90 tangu 1919, wao wamekataa kukubali alama ya hayawani-mwitu au kutegemea mfano wake kuwa tumaini pekee la binadamu kwa ajili ya amani. Wengi wao tayari wamevumilia kwa uaminifu mpaka kifo, na hawa, sasa wakiwa katika mbingu, pasipo shaka wanafuata kwa upendezi wa pekee wimbaji wa ndugu zao ambao wangali dunani.—Ufunuo 14:11-13.

      7. Kinubi kilitumiwaje katika Israeli wa kale, na kuwapo kwa vinubi vya Mungu kwapasa kutuathirije sisi?

      7 Washindi washikamanifu hawa wana vinubi vya Mungu. Katika hili, wao wako kama Walawi wa hekalu wa kale, ambao waliabudu Yehova kwa wimbo kwa kufuatanisha na vinubi. Baadhi yao walitoa unabii kwa kufuatanisha na kinubi. (1 Nyakati 15:16; 25:1-3) Zile sauti tamu za kinubi zilitia uzuri nyimbo za Israeli za shangwe na sala za sifa na za kutoa shukrani kwa Yehova. (1 Nyakati 13:8; Zaburi 33:2; 43:4; 57:7, 8) Katika nyakati za simanzi au utekwa, kinubi hakikusikiwa. (Zaburi 137:2) Kuwapo kwa vinubi vya Mungu katika njozi hii kwapasa kuchochee taraja letu la wimbo wa kuchachawa, wa ushindi wenye shangwe na sifa na utoaji-shukrani kwa Mungu wetu.a

      8. Ni wimbo gani unaoimbwa, na maneno yao ni yapi?

      8 Huo ndio anaoripoti Yohana: “Na wao wanaimba wimbo wa Musa mtumwa wa Mungu na wimbo wa Mwana-Kondoo, kusema: ‘Kubwa na za ajabu ni kazi zako, Yehova Mungu, Mweza Yote. Za uadilifu na za kweli ni njia zako, Mfalme wa umilele. Ni nani ambaye kwa kweli hatahofu wewe, Yehova, na kutukuza jina lako, kwa sababu wewe pekee ni mshikamanifu? Kwa maana mataifa yote yatakuja na kuabudu mbele zako wewe, kwa sababu amri zako za uadilifu zimefanywa zidhihirike.”—Ufunuo 15:3, 4, NW.

      9. Ni kwa nini kwa sehemu, wimbo huo huitwa “wimbo wa Musa”?

      9 Washindi hawa huimba “wimbo wa Musa.” yaani, wimbo kama ule alioimba Musa katika hali zilizo kama hizo. Baada ya Waisraeli kuwa wameshuhudia tauni kumi katika Misri na uharibifu wa jeshi lote la Misri katika Bahari Nyekundu, Musa aliwaongoza katika wimbo kama huo wa ushindi wenye shangwe kwa sifa ya Yehova, akipiga mbiu hivi: “Yehova atatawala akiwa mfalme kwa wakati usio dhahiri, hata milele.” (Kutoka 15:1-19, NW) Inafaa kama nini kwamba waimbaji katika njozi ya Yohana, wakiwa wametoka wakiwa washindi wa hayawani-mwitu na wakiwa wanahusika katika kupiga mbiu ya tauni za mwisho saba, wamepaswa pia kuimbia “Mfalme wa umilele”!—1 Timotheo 1:17, NW.

      10. Ni wimbo gani mwingine uliotungwa na Musa, na mstari wao wa mwisho unahusuje umati mkubwa wa leo?

      10 Katika wimbo mwingine, uliotungwa Waisraeli walipokuwa wakijitayarishia kushinda Kanaani, Musa mwenye umri wa uzee aliambia taifa hilo: “Mimi nitajulisha wazi jina la Yehova. Nyinyi mhesabieni ukuu Mungu wetu!” Mstari wa mwisho wa wimbo huu uliwapa pia kitia-moyo wasio Waisraeli, na maneno ya Musa yaliyovuviwa yanafika chini moja kwa moja mpaka kwenye umati mkubwa wa leo: “Iweni na nderemo, enyi mataifa, pamoja na watu wake.” Na kwa nini wawe na nderemo? Kwa sababu sasa Yehova “atalipiza kisasi cha damu ya watumishi wake, na yeye atarudisha kisasi kwa mahasimu wake.” Utekelezo huu wa hukumu ya uadilifu utaleta shangwe kwa wale wote ambao huitibari katika Yehova.—Kumbukumbu 32:3, 43; Waroma 15:10-13; Ufunuo 7:9, NW.

      11. Wimbo aliosikia Yohana unaendeleaje kuwa na utimizo?

      11 Jinsi Musa mwenyewe angalishangilia kuwa katika siku ya Bwana sasa, akiimba pamoja na korasi ya kimbingu: “Mataifa yote yatakuja na kuabudu mbele zako wewe”! Wimbo huo ulio bora unaendelea kuwa na utimizo mzuri ajabu leo kama tuonavyo, si katika njozi tu bali ukiwa uhalisi ulio hai, mamilioni kutoka “mataifa” ambao wanakuja makundi makundi kwa shangwe kwenye tengenezo la Yehova la kidunia.—Ufunuo 1:10, NW.

      12. Ni kwa nini wimbo wa washindi huitwa wimbo wa Mwana-Kondoo?

      12 Hata hivyo, huu si wimbo wa Musa tu bali pia “wa Mwana-Kondoo.” Jinsi gani hivyo? Musa alikuwa nabii wa Mungu kwa Israeli, lakini Musa mwenyewe alitoa unabii kwamba Yehova angeinua nabii mwingine kama yeye. Huyu alithibitika kuwa Mwana-Kondoo, Yesu Kristo. Ingawa Musa alikuwa “mtumwa wa Mungu,” Yesu alikuwa Mwana wa Mungu, kwa kweli, Musa Mkubwa Zaidi. (Kumbukumbu 18:15-19; Matendo 3:22, 23; Waebrania 3:5, 6, NW) Kwa sababu hiyo, waimbaji huimba pia “wimbo wa Mwana-Kondoo.”

      13. (a) Inakuwaje kwamba Yesu, ajapokuwa mkubwa zaidi ya Musa, yu kama yeye? (b) Sisi tunaweza kuunganaje na waimbaji hao?

      13 Kama Musa, Yesu aliimba sifa za Mungu peupe na akatoa unabii kuhusu ushindi Wake juu ya maadui wake. (Mathayo 24:21, 22; 26:30; Luka 19:41-44) Yesu vilevile alitazamia wakati ambapo mataifa wangekuja na kusifu Yehova, na akiwa “Mwana-Kondoo wa Mungu” mwenye kujidhabihu, yeye alilaza chini uhai wake wa kibinadamu ili kuwezesha hilo. (Yohana 1:29; Ufunuo 7:9; linga Isaya 2:2-4; Zekaria 8:23.) Na kama vile Musa alivyokuja kuthamini jina la Mungu, Yehova, na kuhimidi jina hilo, vivyo hivyo Yesu alifanya jina la Mungu lidhihirike. (Kutoka 6:2, 3; Zaburi 90:1, 17; Yohana 17:6) Kwa kuwa Yehova ni mshikamanifu, ahadi zake tukufu ni hakika zitatimizwa. Basi, hakika sisi tuna umoja na waimbaji hawa washikamanifu, pamoja na Mwana-Kondoo, na pamoja na Musa, katika kuchangia maneno ya wimbo: “Ni nani kweli ambaye hatahofu wewe, Yehova, na kutukuza jina lako?”

      Malaika Wenye Mabakuli

      14. Ni nani ambao Yohana huona wakiibuka kutoka patakatifu, na wanapewa nini?

      14 Inafaa tusikie wimbo wa hawa washindi wapakwa-mafuta. Kwa nini? Kwa sababu wametangaza peupe duniani hukumu zilizokuwa katika mabakuli yaliyokuwa yamejaa kasirani ya Mungu. Lakini kumiminwa kwa mabakuli haya kunahusu zaidi ya binadamu wa vivi hivi tu, kama Yohana aendeleavyo kuonyesha: “Na baada ya vitu hivi mimi nikaona, na patakatifu pa hema ya ushahidi palifunguliwa katika mbingu, na malaika saba wakiwa na tauni saba waliibuka kutoka patakatifu, wakiwa wamevaa kitani safi, nyangavu na wamefunga kifuani mishipi ya dhahabu. Na mmoja wa viumbe hai wanne akawapa malaika saba mabakuli saba ya dhahabu yaliyokuwa yamejaa kasirani ya Mungu, ambaye huishi milele na milele.”—Ufunuo 15:5-7, NW.

      15. Kwa nini haishangazi kwamba malaika saba huibuka kutoka patakatifu?

      15 Kwa habari ya hekalu la Israeli, ambalo lilikuwa na viwakilishi vya vitu vya kimbingu, ni kuhani mkuu pekee angeweza kuingia Patakatifu Zaidi Sana, panapoitwa hapa “patakatifu.” (Waebrania 9:3, 7, NW) Panawakilisha kuwapo kwa Yehova katika mbingu. Hata hivyo, katika mbingu yenyewe, si Kuhani Mkuu Yesu Kristo tu aliye na pendeleo la kuingia mbele za Yehova bali pia malaika hufanya hivyo. (Mathayo 18:10; Waebrania 9:24-26) Basi, haishangazi kwamba malaika saba wamepaswa kuonekana wakitoka katika patakatifu katika mbingu. Wao wana utume kutoka kwa Yehova Mungu mwenyewe: Mimineni mabakuli yanayojaa kasirani ya Mungu.—Ufunuo 16:1, NW.

      16. (a) Ni nini kinachoonyesha kwamba hao malaika saba wanastahili sana kufanya kazi yao? (b) Ni nini kinachoonyesha kwamba wengine wanahusika katika hii kazi kubwa ya kumimina mabakuli ya ufananisho?

      16 Malaika hawa wanastahili sana kufanya kazi hii. Wao wanavaa kitani safi, nyangavu, kuonyesha kwamba wao ni safi kiroho na ni watakatifu, waadilifu katika mwono wa Yehova. Pia, huvaa mishipi ya dhahabu. Kwa kawaida mishipi inatumiwa wakati mtu anapojifunga mwenyewe kwa ajili ya kazi inayopasa kutimizwa. (Walawi 8:7, 13; 1 Samweli 2:18; Luka 12:37; Yohana 13:4, 5) Kwa hiyo malaika wamejifunga mishipi kwa ajili ya kutimiza mgawo. Zaidi ya hayo, mishipi yao ni ya dhahabu. Katika tabenakulo ya kale, dhahabu ilitumiwa kuwakilisha vitu vya kimungu, vya kimbingu. (Waebrania 9:4, 11, 12) Hiyo inamaanisha kwamba malaika hawa wana utume wa utumishi wa kimungu, wenye thamani sana kuufanya. Wengine wanahusika vilevile katika kazi hii kubwa. Mmoja wa viumbe hai wanne anawapa mabakuli yenyewe. Pasipo shaka, huyu alikuwa kiumbe hai wa kwanza, ambaye alishabihi simba, kufananisha ujasiri na ushujaa usiotishika unaohitajiwa ili kupiga mbiu ya hukumu za Yehova.—Ufunuo 4:7, NW.

      Yehova Katika Patakatifu Pake

      17. Yohana hutuambia nini sasa juu ya patakatifu, na hilo hutukumbushaje sisi juu ya patakatifu katika Israeli wa kale?

      17 Mwishowe, akimaliza sehemu hii ya njozi, Yohana anatuambia: “Na patakatifu pakajawa na moshi kwa sababu ya utukufu wa Mungu na kwa sababu ya nguvu zake, na hakuna mmoja ambaye aliweza kuingia ndani ya patakatifu mpaka tauni saba za malaika saba zilipokuwa zimekwisha.” (Ufunuo 15:8, NW) Kulikuwako vipindi katika historia ya Israeli wakati wingu lilifunika patakatifu halisi, na udhihirisho huu wa utukufu wa Yehova ulizuia makuhani kuingia humo. (1 Wafalme 8:10, 11; 2 Nyakati 5:13, 14; linga Isaya 6:4, 5.) Hizi zilikuwa nyakati Yehova alipokuwa anahangaikia sana matukio duniani.

      18. Hao malaika saba watarudi lini kutoa ripoti kwa Yehova?

      18 Vilevile, sasa Yehova anapendezwa sana na vitu vinavyotukia duniani pia. Yeye anataka malaika saba watimize mgawo wao. Ni wakati wa upeo wa hukumu, kama inavyoelezwa kwenye Zaburi 11:4-6, NW: “Yehova yumo katika hekalu takatifu lake. Yehova—kiti cha ufalme chake kimo katika mbingu. Macho yake mwenyewe huona, macho yake mwenyewe yenye kung’aa huchunguza wana wa binadamu. Yehova mwenyewe huchunguza mwadilifu na pia mwovu na yeyote mwenye kupenda jeuri nafsi Yake hakika huchukia. Yeye atanyesha chini juu ya waovu mitego, moto na salfa na upepo wenye kuunguza, kuwa aria ya kikombe chao.” Mpaka tauni saba hizi ziwe zimemiminwa juu ya waovu, malaika saba hawatarudi kwenye kuwapo kulikotukuka kwa Yehova.

      19. (a) Ni amri gani inayotolewa sasa, na inatolewa na nani? (b) Ni lazima kumiminwa kwa mabakuli ya ufananisho kuwe kulianza lini?

      19 Amri yenye kutia hofu yatokeza mngurumo: “Na mimi nikasikia sauti kubwa kutoka patakatifu ikisema kwa malaika saba: ‘Endeni na kumimina mabakuli saba ya kasirani ya Mungu ndani ya dunia.’” (Ufunuo 16:1, NW) Ni nani anayetoa amri hii? Ni lazima awe Yehova mwenyewe, kwa kuwa mng’aro wa utukufu na nguvu zake ulizuia mwingine yeyote kuingia patakatifu. Yehova alikuja kwenye hekalu lake la kiroho kwa ajili ya hukumu katika 1918. (Malaki 3:1-5) Basi, lazima iwe ilikuwa muda mfupi baada ya tarehe hiyo kwamba yeye akatoa hiyo amri ya kumimina “mabakuli ya kasirani ya Mungu.” Kwa kweli, hukumu zilizo katika mabakuli ya ufananisho zilianza kupigiwa mbiu kwa mkazo mkubwa katika 1922. Na leo ukubwa wa sauti za mbiu yao unazidi kuongezeka.

      Mabakuli na Mipigo ya Tarumbeta

      20. Mabakuli ya kasirani ya Mungu yanafunua na kuonya juu ya nini, nayo humiminwaje?

      20 Mabakuli ya kasirani ya Mungu hufunua sura za mandhari ya ulimwengu kama Yehova anavyoziona na kuonya juu ya hukumu ambazo Yehova atatekeleza. Malaika humimina mabakuli kupitia uwakili wa kundi la Wakristo wapakwa-mafuta duniani, wanaoimba wimbo wa Musa na wa Mwana-Kondoo. Wanapokuwa wakipiga mbiu ya Ufalme kuwa habari njema, jamii ya Yohana imefunua kwa ujasiri yaliyomo ndani ya mabakuli haya ya kasirani. (Mathayo 24:14; Ufunuo 14:6, 7) Hivyo, kazi yao ya kuhubiri yenye sehemu mbili imekuwa yenye amani katika kupiga mbiu ya uhuru kwa aina ya binadamu lakini kama vita katika kuonya juu ya “siku ya kisasi upande wa Mungu wetu.”—Isaya 61:1, 2, NW.

      21. Shabaha za mabakuli manne ya kwanza ya kasirani ya Mungu hulinganaje na yale ya mipigo minne ya kwanza ya tarumbeta, na hutofautiana katika nini?

      21 Shabaha za mabakuli manne ya kwanza ya kasirani ya Mungu zinalingana na zile za mipigo minne ya kwanza ya tarumbeta, yaani, dunia, bahari, mito na vibubujiko vya maji, na machimbuko ya kimbingu ya nuru. (Ufunuo 8:1-12) Lakini mipigo ya tarumbeta ilitangaza tauni juu ya “theluthi moja,” hali sehemu nzima husumbuliwa na mmimino wa mabakuli ya kasirani ya Mungu. Hivyo, ingawa Jumuiya ya Wakristo, ikiwa ile “theluthi moja,” imepokea uangalifu wa kwanza wakati wa “siku ya Bwana,” hakuna sehemu moja ya mfumo wa Shetani iliyoepushwa isipate kusumbuliwa na jumbe za hukumu zenye kukera za Yehova na masikitiko zinayoleta.

      22. Ile mipigo mitatu ya mwisho ya tarumbeta ilikuwa tofauti jinsi gani, na inahusianaje na mabakuli matatu ya mwisho ya kasirani ya Mungu?

      22 Ile mipigo mitatu ya mwisho ya tarumbeta ilikuwa tofauti, kwa kuwa iliitwa ole. (Ufunuo 8:13; 9:12) Mbili za kwanza za hizo zilikuwa hasa zenye nzige na majeshi ya wapanda-farasi, hali wa tatu ulijulisha uzawa wa Ufalme wa Yehova. (Ufunuo 9:1-21; 11:15-19, NW) Kama tutakavyoona, mabakuli matatu ya mwisho ya hasira-kisasi yake pia huhusu baadhi ya pande hizi, yako tofauti kidogo na ole tatu. Acheni sasa tutoe uangalifu wa karibu sana kwa mafumbuo ya kidrama yanayotokana na kumiminwa kwa mabakuli ya kasirani ya Yehova.

      [Maelezo ya Chini]

      a Kwa kupendeza, katika 1921 ile jamii ya Yohana ilitoa msaada wa funzo la Biblia The Harp of God, uliopata mwenezo wa nakala zaidi ya milioni tano kwa lugha zaidi ya 20. Ulisaidia kuleta ndani waimbaji zaidi wapakwa-mafuta.

  • Kasirani ya Mungu Yaletwa Kwenye Tamati
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Sura ya 32

      Kasirani ya Mungu Yaletwa Kwenye Tamati

      1. Ni nini kitakuwa kimetukia wakati mabakuli saba yatakuwa yamemwagwa mpaka kwenye tamati na sasa ni maswali gani yanayozuka kwa habari ya mabakuli?

      YOHANA amekwisha julisha malaika waliopewa utume wa kumimina mabakuli saba. Yeye anatuambia kwamba “haya ndiyo ya mwisho, kwa sababu kwa njia ya hayo kasirani ya Mungu inaletwa kwenye tamati.” (Ufunuo 15:1; 16:1, NW) Tauni hizi, zenye kufunua adhabu zinazotolewa na Yehova kwa ajili ya uovu duniani, ni lazima zimiminwe mpaka kwenye tamati. Zikiisha kumiminwa, hukumu za Mungu zitakuwa zimetekelezwa. Ulimwengu wa Shetani utakuwa haupo tena! Tauni hizi huonya juu ya nini kwa aina ya binadamu na watawala wa huu mfumo mbovu uliopo? Wakristo wanaweza kuepukaje kusumbuliwa kwa tauni pamoja na ulimwengu huu uliohukumiwa maangamizi? Haya ni maswali muhimu, na sasa yatajibiwa. Wote wanaotamani sana ushindi wenye shangwe wa uadilifu watapendezwa sana na vitu ambavyo Yohana anafuata kuona.

      Hasira-Kisasi ya Yehova Dhidi ya “Dunia”

      2. Hutokea nini malaika wa kwanza anapomimina bakuli lake katika dunia, na ni nini kinachofananishwa na dunia?

      2 Malaika wa kwanza aanza kutenda! “Na wa kwanza akaenda zake na akamimina bakuli lake ndani ya dunia. Na donda lenye kuumiza na lenye kudhuru likaja kuwa juu ya watu ambao walikuwa na alama ya hayawani-mwitu na ambao walikuwa wakiabudu mfano wake.” (Ufunuo 16:2, NW) Kama katika kile kisa cha ule mpigo wa kwanza wa tarumbeta, hapa “dunia” hufananisha ule mfumo wa kisiasa ambao huonekana kuwa imara ambao Shetani alianza kujenga hapa duniani huko nyuma katika wakati wa Nimrodi, miaka zaidi ya 4,000 iliyopita.—Ufunuo 8:7, NW.

      3. (a) Serikali nyingi zimedaije kile kinachokuwa sawa na ibada kutoka kwa raia zao? (b) Mataifa yametokeza nini kuwa kibadala cha Ufalme wa Mungu, na tokeo ni nini kwa wale wanaokiabudu?

      3 Katika hizi siku za mwisho, serikali nyingi zimedai kile ambacho kimekuwa kama ibada kutoka kwa raia wazo, zikisisitiza kwamba lazima Serikali itukuzwe juu ya Mungu au ushikamanifu mwingine wowote. (2 Timotheo 3:1; linga Luka 20:25; Yohana 19:15.) Tangu 1914 imekuwa kawaida kwa mataifa kuandikisha vijana wao jeshini kwa nguvu ili kupiga vita, au kuwa tayari kupiga vita, aina ya vita ya ujumla ambayo imetia sana kurasa za historia ya ki-siku-hizi madoa ya damu. Wakati wa siku ya Bwana mataifa yametokeza pia, kuwa kibadala cha Ufalme wa Mungu, mfano wa hayawani—Ushirika wa Mataifa na mwandamizi wao, Umoja wa Mataifa. Ni kufuru kama nini kupiga mbiu, kama vile wamefanya mapapa wa hivi karibuni, kwamba baraza hili lililofanywa na mwanadamu ndilo tumaini pekee la mataifa kwa amani! Hupinga kwa uthabiti Ufalme wa Mungu. Wale wanaoliabudu wanakuwa wachafu kiroho, wenye vidonda, kama vile Wamisri waliopinga Yehova katika siku ya Musa walipigwa kwa tauni ya vidonda na majipu halisi.—Kutoka 9:10, 11.

      4. (a) Yaliyomo katika bakuli la kwanza la kasirani ya Mungu yanakazia nini kwa uthabiti? (b) Yehova huwaonaje wale wanaokubali alama ya hayawani-mwitu?

      4 Yaliyomo katika bakuli hili hukazia kwa uthabiti uchaguzi ulio mbele ya wanadamu: Ni lazima wapatwe na ama kutoidhiniwa na ulimwengu ama ghadhabu ya Yehova. Aina ya binadamu imeshurutishwa kukubali alama ya hayawani-mwitu, kwa kusudi la kwamba “yeyote asipate kuweza kununua au kuuza isipokuwa mtu aliye na alama, jina la hayawani-mwitu au nambari ya jina lake.” (Ufunuo 13:16, 17, NW) Lakini kuna hasara katika hili! Yehova huwaona wale wanaokubali hiyo alama kuwa wakipigwa na “donda lenye kuumiza na lenye kudhuru.” Tangu 1919 wao wametiwa alama peupe kuwa wamekataa Mungu aliye hai. Mipango yao ya kisiasa haina fanikio, nao hupatwa na maumivu makali. Kiroho, wao ni wachafu. Wasipotubu, ugonjwa huu “wenye kuumiza” utaleta kifo, kwa kuwa hii ni siku ya Yehova ya hukumu. Hakuna uwanja wa kutokuwamo kati ya kuwa sehemu ya huu mfumo wa mambo wa ulimwengu na kutumikia Yehova upande wa Kristo wake.—Luka 11:23; linga Yakobo 4:4.

      Bahari Yawa Damu

      5. (a) Hutukia nini wakati lile bakuli la pili linapomiminwa? (b) Yehova anawaonaje wale wanaokaa katika ile bahari ya mfano?

      5 Bakuli la pili la kasirani ya Mungu lazima sasa limiminwe. Itamaanisha nini kwa aina ya binadamu? Yohana atuambia: “Na wa pili akamimina bakuli lake ndani ya bahari. Na hiyo ikawa damu kama ya binadamu mfu, na kila nafsi hai ikafa, ndiyo, vitu vilivyo katika bahari.” (Ufunuo 16:3, NW) Kama mpigo wa pili wa tarumbeta, bakuli hili linaelekezwa dhidi ya “bahari”—tungamo la binadamu lenye kuvurugika, lenye kuasi, lililotenganishwa na Yehova. (Isaya 57:20, 21; Ufunuo 8:8, 9, NW) Machoni pa Yehova, “bahari” hii ni kama damu, isiyowafaa viumbe kuishi ndani yayo. Ndiyo sababu Wakristo lazima wawe si sehemu ya ulimwengu. (Yohana 17:14, NW) Kumiminwa kwa bakuli la pili la kasirani ya Mungu hufunua kwamba aina ya binadamu yote inayokaa katika bahari hii imekufa machoni pa Yehova. Kwa sababu ya daraka la jumuiya, aina ya binadamu ina hatia kubwa ya umwagaji-damu isiyo na hatia. Siku ya kasirani ya Yehova iwasilipo, wao watakufa kihalisi mikononi mwa majeshi yake ya kufisha.—Ufunuo 19:17, 18; linga Waefeso 2:1; Wakolosai 2:13.

      Kuwapa Damu Wanywe

      6. Hutukia nini wakati bakuli la tatu linapomiminwa, na ni maneno gani yanayosikiwa kutoka kwa malaika na kutoka madhabahu?

      6 Bakuli la tatu la kasirani ya Mungu kama mpigo wa tatu wa tarumbeta, huathiri machimbuko ya maji matamu. “Na wa tatu akamimina bakuli lake ndani ya mito na vibubujiko vya maji. Na hiyo ikawa damu. Na mimi nikasikia malaika aliye na amri juu ya maji akisema: ‘Wewe, Mmoja ambaye yuko na ambaye alikuwako, Mshikamanifu, u mwadilifu, kwa sababu wewe umekata maamuzi haya, kwa sababu wao walimimina damu ya watakatifu na ya manabii, na wewe umewapa damu wanywe. Wao hustahili hiyo.’ Na mimi nikasikia madhabahu ikisema: ‘Ndiyo, Yehova Mungu, Mweza Yote, ya kweli na ya uadilifu ni maamuzi yako ya hukumu.’”—Ufunuo 16:4-7, NW.

      7. Ni nini kinachotolewa picha na “mito na vibubujiko vya maji”?

      7 Hii “mito na vibubujiko vya maji” ni picha ya yale yaitwayo eti machimbuko ya kisasa hivi ya mwongozo na hekima ambayo hukubaliwa na ulimwengu huu, kama vile falsafa za kisiasa, kiuchumi, kisayansi, kielimu, kijamii, na kidini ambazo huongoza matendo na maamuzi ya binadamu. Badala ya kutegemea Yehova, kwa ajili ya ukweli wenye kutoa uhai, ambaye ndiye Kibubujiko cha uhai, wanadamu ‘wamejichongea wenyewe visima vilivyovunjika’ nao wamekunywa sana “hekima ya ulimwengu huu [ambayo] ni upumbavu kwa Mungu.”—Yeremia 2:13; 1 Wakorintho 1:19; 2:6; 3:19; Zaburi 36:9, NW.

      8. Ni katika njia zipi aina ya binadamu imejiletea hatia ya damu?

      8 “Maji” kama hayo yaliyochafuliwa yameongoza wanadamu kuwa na hatia ya damu, mathalani, katika kuwatia moyo wamwage damu kwa kadiri kubwa katika vita ambavyo karne iliyopita vilitwaa maisha zaidi ya milioni mia moja. Hususa katika Jumuiya ya Wakristo, ambako vililipuka vita viwili vya ulimwengu, wanadamu wamekuwa “katika uharaka wa kumwaga damu isiyo na hatia,” na hiyo imetia ndani damu ya mashahidi wa Mungu mwenyewe. (Isaya 59:7; Yeremia 2:34, NW) Aina ya binadamu imejiletea pia hatia ya damu kwa kutumia vibaya kiasi kikubwa mno cha damu kwa ajili ya kutia mishipani, katika kukiuka sheria za Yehova za uadilifu. (Mwanzo 9:3-5; Walawi 17:14; Matendo 15:28, 29) Kwa sababu hiyo, kupitia kutiwa damu mishipani, tayari wao wamevuna sikitiko la kuwa na UKIMWI, ugonjwa wa kufura ini, na magonjwa mengine. Lipo kamili kwa ajili ya hatia ya damu litakuja karibuni wakati wakiukaji watakapolipa adhabu iliyo kuu zaidi, wakikanyagwa katika “shinikizo la divai ya kasirani ya Mungu.”—Ufunuo 14:19, 20, NW.

      9. Kumiminwa kwa bakuli la tatu kunahusu nini?

      9 Katika siku ya Musa, wakati Mto Naili ulipogeuzwa kuwa damu, Wamisri waliweza kuendelea kuwa hai kwa kutafuta machimbuko mengine ya maji. (Kutoka 7:24) Ingawa hivyo, leo, katika pindi ya tauni hii ya kiroho, hakuna mahali katika ulimwengu wa Shetani ambako watu wanaweza kupata maji yenye kutoa uhai. ‘Kumiminwa’ kwa bakuli hili la tatu kunahusu kupiga mbiu kwamba “mito na vibubujiko vya maji” vya ulimwengu viko kama damu, vikileta kifo cha kiroho kwa wote wanaoyanywa. Watu wasipomwendea Yehova, wanavuna hukumu yake mbaya.—Linga Ezekieli 33:11.

      10. “Malaika aliye na amri juu ya maji” anajulisha nini, na ni ushahidi gani ambao “madhabahu” inaongezea?

      10 “Malaika aliye na amri juu ya maji,” yaani, malaika amiminaye bakuli hili juu ya maji, anatukuza Yehova kuwa ndiye Hakimu wa Ulimwengu Wote Mzima, ambaye maamuzi yake ya uadilifu ni kamili. Kwa hiyo, yeye anasema juu ya hukumu hii: “Wao hustahili hiyo.” Pasipo shaka, huyo malaika alijionea mwenyewe umwagaji-damu mwingi na ukatili uliochochewa na mafundisho bandia na falsafa za ulimwengu huu mbovu kwa muda wa maelfu mengi ya miaka. Kwa sababu hiyo, yeye anajua kwamba uamuzi wa hukumu wa Yehova ni wa haki. Hata “madhabahu” ya Mungu inasema kwa mpaazo. Kwenye Ufunuo 6:9, 10, nafsi za wale ambao waliuawa kiimani husemwa kuwa kwenye msingi wa madhabahu hiyo. Kwa hiyo “madhabahu” inaongeza ushahidi wenye nguvu nyingi kwa habari ya haki na uadilifu wa maamuzi ya Yehova.a Hakika, inawafaa wale ambao wamemwaga na kutumia vibaya damu wenyewe wanyweshwe damu kinguvu, kama ufananisho wa Yehova kuwahukumia kifo.

      Kuunguza Wanadamu kwa Moto

      11. Ni nini iliyo shabaha ya bakuli la nne la kasirani ya Mungu na hutukia nini linapomiminwa?

      11 Shabaha ya bakuli la nne la kasirani ya Mungu ni jua. Yohana atuambia sisi: “Na wa nne akamimina bakuli lake juu ya jua; na jua likapewa ruhusa ya kuunguza wanadamu kwa moto. Na wanadamu wakaunguzwa kwa joto kubwa, lakini wao walikufuru jina la Mungu, ambaye ana mamlaka juu ya tauni hizi na wao hawakutubu ili wampe yeye utukufu.”—Ufunuo 16:8, 9, NW.

      12. Ni nini lililo “jua” la ulimwengu huu, na jua hili la ufananisho lapewa ruhusa gani?

      12 Leo, kwenye huu “umalizio wa mfumo wa mambo,” ndugu za kiroho za Yesu ‘hung’aa kwa uangavu kama jua katika ufalme wa Baba yao.’ (Mathayo 13:40, 43, NW) Yesu mwenyewe ndiye “jua la uadilifu.” (Malaki 4:2, NW) Ingawa hivyo, aina ya binadamu, ina “jua” layo yenyewe, watawala wayo yenyewe ambao hujaribu kung’aa katika kupinga Ufalme wa Mungu. Ule mpigo wa nne wa tarumbeta ulitangaza kwamba ‘jua, mwezi, na nyota’ katika mbingu za Jumuiya ya Wakristo kwa kweli ni machimbuko ya giza, si ya nuru. (Ufunuo 8:12, NW) Bakuli la nne la kasirani ya Mungu huonyesha sasa kwamba “jua” la ulimwengu lingekuwa lenye joto sana isivyovumilika. Wale wanaotegemewa kuwa viongozi kama jua ‘wangeunguza’ aina ya binadamu. Hiyo ruhusa ingepewa kwa jua la ufananisho. Kwa maneno mengine, Yehova angeruhusu hilo kuwa sehemu ya hukumu yake yenye moto juu ya aina ya binadamu. Ni katika njia gani kuunguzwa huku kumetukia?

      13. Ni katika njia gani watawala wa ulimwengu huu walio ufananisho wa jua ‘wameunguza’ aina ya binadamu?

      13 Baada ya vita ya ulimwengu ya kwanza, watawala wa ulimwengu huu walifanyiza Ushirika wa Mataifa katika jitihada ya kutatua tatizo la ulimwengu la usalama, lakini huu ulishindwa. Kwa hiyo aina nyingine za utawala wa kujaribia zilionjwa, kama vile Ufashisti na Unazi. Ukomunisti uliendelea kupanuka. Badala ya fungu la aina ya binadamu kuwa bora, hao watawala walio kama jua katika mifumo hiyo wakaanza ‘kuunguza aina ya binadamu kwa joto kubwa.’ Vita vya wenyewe kwa wenyewe katika Hispania, Ethiopia, na Manchuria viliongoza kwenye vita ya ulimwengu ya pili. Historia ya ki-siku-hizi hurekodi kwamba Mussolini, Hitla, na Stalini wakiwa madikteta wakawa na daraka la moja kwa moja na lisilo la moja kwa moja la vifo vya makumi ya mamilioni, kutia ndani wengi wa wanataifa wao wenyewe. Hivi majuzi zaidi, mipambano ya kimataifa au ya wenyewe kwa wenyewe ‘imeunguza’ watu wa nchi kama vile Vietnamu, Kampuchea, Irani, Lebanoni, na Ailandi, pamoja na mabara mengine katika Amerika ya Kilatini na Afrika. Ongezea hayo ule mng’ang’ano wenye kuendelea kati ya mataifa yenye nguvu zaidi, ambayo silaha zayo za nyukilia zenye kutia hofu sana zinaweza kuteketeza aina ya binadamu yote. Katika hizi siku za mwisho, hakika binadamu wamewekwa katika hatari ya kuunguzwa na “jua,” watawala wao wasio waadilifu. Kumiminwa kwa bakuli la nne la kasirani ya Mungu kumelenga barabara mambo haya ya hakika ya historia, na watu wa Mungu wameyapigia mbiu kotekote duniani.

      14. Mashahidi wa Yehova wamefundisha nini bila ugeugeu kuwa ndio ufumbuzi pekee wa matatizo ya aina ya binadamu, na kwa itikio gani kwa aina ya binadamu kwa ujumla?

      14 Mashahidi wa Yehova wamefundisha bila ugeugeu kwamba ufumbuzi pekee wa matatizo magumu ya aina ya binadamu ni Ufalme wa Mungu, ambao kupitia huo Yehova anakusudia kutakasa jina lake. (Zaburi 83:4, 17, 18; Mathayo 6:9, 10) Hata hivyo, aina ya binadamu kwa ujumla imeziba sikio kwa ufumbuzi huu. Wengi ambao wanakataa Ufalme huo, wanakufuru jina la Mungu pia, hata kama vile Farao alivyofanya wakati alipokataa kukiri enzi kuu ya Yehova. (Kutoka 1:8-10; 5:2) Wakiwa hawapendezwi na Ufalme wa Kimesiya, wapinzani hawa wanachagua kutaabika chini ya “jua” kali lao wenyewe la utawala wa kibinadamu wenye uonevu.

      Kiti cha Ufalme cha Hayawani-Mwitu

      15. (a) Bakuli la tano lamiminwa juu ya nini? (b) Ni nini kilicho “kiti cha ufalme cha hayawani-mwitu,” na ni nini kinachohusika katika kumiminwa kwa bakuli juu yacho?

      15 Malaika anayefuata anamimina bakuli lake juu ya nini? “Na wa tano akamimina bakuli lake juu ya kiti cha ufalme cha hayawani-mwitu.” (Ufunuo 16:10a, NW) “Hayawani-mwitu” ni mfumo wa kiserikali wa Shetani. Hauna kiti cha ufalme halisi, kama vile hayawani-mwitu asivyo halisi. Hata hivyo, mtajo wa kiti cha ufalme, huonyesha kwamba huyo hayawani-mwitu ametumia mamlaka ya kifalme juu ya aina ya binadamu; hii inapatana na uhakika wa kwamba kila moja ya pembe za hayawani-mwitu ina taji la kifalme. Kwa kweli, hicho “kiti cha ufalme cha hayawani-mwitu” ndicho msingi, au chimbuko, la mamlaka hiyo.b Biblia hufunua hali ya kweli ya mamlaka ya kifalme ya huyo hayawani-mwitu wakati inaposema kwamba “drakoni akampa hayawani nguvu zake na kiti cha ufalme chake na mamlaka kubwa.” (Ufunuo 13:1, 2; 1 Yohana 5:19, NW) Hivyo, kumiminwa kwa bakuli juu ya kiti cha ufalme cha hayawani-mwitu kunahusu mbiu yenye kufunua daraka la kweli ambalo Shetani amekuwa nalo na ambalo angali nalo katika kuunga mkono na kuendeleza huyo hayawani-mwitu.

      16. (a) Mataifa yanatumikia nani, yawe yanajua hivyo au hayajui? Fafanua. (b) Ulimwengu huonyeshaje utu wa Shetani? (c) Kiti cha ufalme cha hayawani-mwitu kitapinduliwa lini?

      16 Uhusiano huu kati ya Shetani na mataifa unadumishwaje? Shetani alipomshawishi Yesu, yeye alimwonyesha falme zote za ulimwengu katika njozi na akamtolea “mamlaka yote hii na utukufu wazo.” Lakini lilikuwako sharti moja—kwanza Yesu alipaswa afanye tendo la ibada mbele ya Shetani. (Luka 4:5-7, NW) Je! sisi tunaweza kudhani kwamba serikali za ulimwengu zinapokea mamlaka yazo kwa bei ndogo zaidi ya hiyo? Hasha. Kulingana na Biblia, Shetani ndiye kamungu ka huu mfumo wa mambo, hivi kwamba, yawe mataifa yanajua au hayajui, yanatumikia yeye. (2 Wakorintho 4:3, 4, NW)c Hali hii inafunuliwa na muundo wa mfumo wa ulimwengu uliopo, ambao umejengwa juu ya utukuzaji taifa wa kijinga, chuki, na kujipendeza kibinafsi. Umeundwa kitengenezo namna Shetani anavyotaka—kufuliza kutunza aina ya binadamu chini ya udhibiti wake. Ufisadi katika serikali, pupa ya kutaka mamlaka, ubalozi wa uwongo-uwongo, shindano la kuunda silaha—hayo huonyesha utu wa Shetani uliotwezwa. Ulimwengu unachangia viwango vya Shetani vyenye utovu wa uadilifu, hivyo kumfanya yeye kuwa kamungu kao. Kiti cha ufalme cha hayawani-mwitu kitapinduliwa wakati huyo hayawani apatwapo na mzimiko na mwishowe Mbegu ya mwanamke wa Mungu imtiapo Shetani mwenyewe ndani ya abiso.—Mwanzo 3:15; Ufunuo 19:20, 21; 20:1-3, NW.

      Giza na Umivu Lenye Kugugunya

      17. (a) Kumiminwa kwa bakuli la tano huhusianaje na giza la kiroho ambalo sikuzote limefunika ufalme wa hayawani-mwitu? (b) Watu wanatendaje kwa kuitikia kumiminwa kwa bakuli la tano la kasirani ya Mungu?

      17 Ufalme wa hayawani-mwitu huyu umekuwa katika giza la kiroho tangu ulipoanza. (Linga Mathayo 8:12; Waefeso 6:11, 12.) Bakuli la tano linaleta tangazo la peupe lenye mkazo mkubwa juu ya giza hili. Hata linalifanyia drama, kwa kuwa bakuli hili la kasirani ya Mungu humiminwa juu ya kiti cha ufalme chenyewe cha hayawani-mwitu wa ufananisho. “Na ufalme wake ukatiwa giza, na wao wakaanza kugugunya ndimi zao kwa ajili ya maumivu yao, lakini wao wakamkufuru Mungu wa mbingu kwa ajili ya maumivu yao na kwa ajili ya vidonda vyao, na wao hawakutubu kazi zao.”—Ufunuo 16:10b, 11, NW.

      18. Kuna ulingano gani kati ya mpigo wa tano wa tarumbeta na bakuli la tano la kasirani ya Mungu?

      18 Mpigo wa tano wa tarumbeta si sawa kabisa na bakuli la tano la kasirani ya Mungu, kwa kuwa mpigo wa tarumbeta ulitangaza tauni ya nzige. Lakini angalia kwamba wakati wa kuachiliwa tauni hiyo ya nzige, kulikuwako na kutiwa giza kwa jua na hewa. (Ufunuo 9:2-5) Na kwenye Kutoka 10:14, 15 (NW), tunasoma hivi kuhusu wale nzige ambao kwa hao Yehova alipiga Misri: “Walikuwa wenye kulemea sana. Kabla ya wao kulikuwa hakujatokea kamwe nzige kama wao, na hakutatokea kamwe wengine katika njia hii baada yao. Na wao wakaenda wakifunika uso wote wenye kuonekana wa bara zima, na bara likapata kuwa giza ti.” Ndiyo, giza ti! Leo, giza la kiroho la ulimwengu limekuwa wazi sana likiwa tokeo la kuvumishwa kwa tarumbeta ya tano na kumiminwa kwa bakuli la tano la kasirani ya Mungu. Ujumbe wenye kuchoma kwa uchungu ambao umepigiwa mbiu na bumba la nzige wa ki-siku-hizi huleta mateso na maumivu kwa wale waovu ambao “wamependa giza badala ya nuru.”—Yohana 3:19, NW.

      19. Kupatana na Ufunuo 16:10, 11, kufichuliwa peupe kwa Shetani kuwa mungu wa huu mfumo wa mambo kunasababisha nini?

      19 Akiwa mtawala wa ulimwengu, Shetani amesababisha utofurahifu mwingi na mateso. Njaa kuu, vita, jeuri, uhalifu, matumizi mabaya ya dawa za kulevya, utovu wa adili, magonjwa yenye kupitishwa kingono, utovu wa haki, unafiki wa kidini—haya na zaidi ni alama za mfumo wa mambo wa Shetani. (Linga Wagalatia 5:19-21.) Hata hivyo, ufichulio wa peupe wa Shetani kuwa ndiye mungu wa huu mfumo wa mambo ulisababisha maumivu na tahayari kwa wale ambao huishi kwa viwango vyake. “Wao wakaanza kugugunya ndimi zao kwa ajili ya maumivu yao,” hasa katika Jumuiya ya Wakristo. Wengi huona uchungu moyoni kwa vile ukweli hufunua mtindo wao wa maisha. Baadhi yao huuona kuwa tisho, nao hunyanyasa wale wanaoutangaza. Wanakataa Ufalme wa Mungu na kutusi jina takatifu la Yehova. Hali yao ya kidini yenye ugonjwa na yenye madonda madonda inafunuliwa wazi, hivi kwamba wao wanakufuru Mungu wa mbingu. La, wao ‘hawatubu kazi zao.’ Kwa hiyo sisi hatuwezi kutazamia kuongolewa kwa tungamo la watu kabla ya mwisho wa huu mfumo wa mambo.—Isaya 32:6.

      Mto Eufrati Wakaushwa

      20. Mpigo wa sita wa tarumbeta na pia kumwagwa kwa bakuli la sita huhusishaje ndani mto Eufrati?

      20 Mpigo wa sita wa tarumbeta ulitoa habari ya kuachiliwa kwa “malaika wanne ambao wamefungwa kwenye mto mkubwa Eufrati.” (Ufunuo 9:14, NW) Kihistoria, Babuloni lilikuwa jiji kubwa ambalo lilikalia mto Eufrati. Na katika 1919 kuachiliwa kwa malaika wanne wa ufananisho kuliandamana na anguko la maana la Babuloni Mkubwa. (Ufunuo 14:8, NW) Basi, inastahili kuangaliwa kwamba, bakuli la sita la kasirani ya Mungu huhusisha ndani pia mto Eufrati: “Na wa sita akamimina bakuli lake juu ya mto mkubwa Eufrati, na maji yao yakakauka kabisa, ili njia iweze kutayarishwa kwa ajili ya wafalme kutoka zukio la jua.” (Ufunuo 16:12, NW) Hii vilevile ni habari mbaya kwa Babuloni Mkubwa!

      21, 22. (a) Maji yenye kinga ya mto Eufrati yalikaukiaje Babuloni katika 539 K.W.K.? (b) Maji ambayo Babuloni Mkubwa anaketia ni nini, na hata sasa maji haya ya ufananisho yanakaukaje?

      21 Katika wakati wa upeo wa Babuloni la kale, maji mengi ya Eufrati yalikuwa sehemu kubwa ya mfumo wa kinga yalo. Katika 539 K.W.K. maji hayo yalikaushwa wakati yalipogeuzwa kando kutoka njia yayo na Sairasi kiongozi Mwajemi. Hivyo, njia ikafunguliwa kwa Sairaisi Mwajemi na Dario Mmedi, wafalme kutoka “zukio la jua” (yaani, mashariki), waingie Babuloni na kulishinda. Katika ile saa ya hatari, mto Eufrati ulishindwa kuwa kinga ya hilo jiji kubwa. (Isaya 44:27–45:7; Yeremia 51:36, NW) Jambo fulani kama hilo linakaribia kutukia kwa Babuloni wa ki-siku-hizi, mfumo wa ulimwenguni pote wa dini bandia.

      22 Babuloni Mkubwa “huketi juu ya maji mengi.” Kulingana na Ufunuo 17:1, 15, (NW), hayo hufananisha “vikundi vya watu na umati wa watu na mataifa na ndimi”—magenge ya wafuasi ambao yeye huwaona kuwa himaya. Lakini “maji” yanakauka! Katika Ulaya Magharibi, ambako hapo kwanza alikuwa na uvutano mwingi, mamia ya maelfu wamepuuza dini waziwazi. Katika mabara fulani, kwa miaka mingi kulikuwa na sera iliyojulishwa wazi kujaribu kuharibu uvutano wa dini. Matungamo katika mabara hayo hayakuinuka kumsaidia. Hali kadhalika, ujapo wakati wa Babuloni Mkubwa kuharibiwa, hesabu yenye kupungua ya wafuasi wake haitathibitika kuwa himaya kwa vyovyote. (Ufunuo 17:16) Ingawa yeye hudai kuwa na washiriki mamia ya mamilioni, Babuloni Mkubwa atajikuta akiwa bila kinga dhidi ya “wafalme kutoka zukio la jua.”

      23. (a) Ni nani waliokuwa wafalme kutoka “zukio la jua” katika 539 K.W.K.? (b) Ni nani walio “wafalme kutoka zukio la jua” wakati wa siku ya Bwana, nao wataharibuje Babuloni Mkubwa?

      23 Hawa wafalme ni nani? Katika 539 K.W.K. wao walikuwa Dario Mmedi na Sairasi Mwajemi, ambao walitumiwa na Yehova kushinda jiji la kale la Babuloni. Katika hii siku ya Bwana, dini bandia ya Babuloni Mkubwa itaharibiwa pia na watawala wa kibinadamu. Lakini kwa mara nyingine tena, hii itakuwa hukumu ya kimungu. Yehova Mungu na Yesu Kristo, “wafalme kutoka zukio la jua,” watakuwa wametia katika mioyo ya watawala wa kibinadamu “fikira” wamgeukie Babuloni Mkubwa na kumharibu kabisa. (Ufunuo 17:16, 17, NW) Kumwagwa kwa bakuli la sita hupiga mbiu peupe kwamba hukumu hii inakaribia kutekelezwa!

      24. (a) Yaliyomo ndani ya mabakuli ya kwanza sita ya kasirani ya Mungu yametangazwaje wazi, na kukiwa na tokeo gani? (b) Kabla ya kutuambia juu ya bakuli libakilo la kasirani ya Mungu Ufunuo unafunua nini?

      24 Haya mabakuli ya kwanza sita ya kasirani ya Yehova yana ujumbe mzito. Watumishi wa Mungu wa kidunia, wakiungwa mkono na malaika, wamekuwa na shughuli wakitangaza peupe yaliyomo kwa kadiri ya ulimwenguni pote. Kwa njia hiyo, sehemu zote za mfumo wa ulimwengu wa Shetani zimepewa onyo zinalostahili, na Yehova ameandalia watu mmoja mmoja fursa ya kutafuta uadilifu wafulize kuishi. (Ezekieli 33:14-16, NW) Bado, labaki bakuli moja zaidi la kasirani ya Mungu. Lakini kabla ya kutuambia juu yalo, Ufunuo unafunua jinsi Shetani na mawakili wake wa kidunia wanavyojaribu kukanusha kutangazwa peupe kwa hukumu za Yehova.

      Mkusanyo Kuelekea Har–Magedoni

      25. (a) Yohana anatuambia nini juu ya semi chafu zilizovuviwa, zilizo kama vyura? (b) Kumekuwaje na msiba wenye kunyarafisha kama wa vyura wa ‘semi chafu zilizovuviwa’ katika siku ya Bwana, na tokeo likiwa nini?

      25 Yohana anatuambia: “Na mimi nikaona semi chafu tatu zilizovuviwa ambazo zilionekana kama vyura zinatoka katika kinywa cha drakoni na katika kinywa cha hayawani-mwitu na katika kinywa cha nabii bandia. Kwa hakika, hizo ni semi zilizovuviwa na roho waovu na hufanya ishara, nazo hutoka kwenda kwa wafalme wa dunia nzima yote inayokaliwa, kukusanya wao pamoja kwenye vita ya ile siku kubwa ya Mungu Mweza Yote.” (Ufunuo 16:13, 14, NW) Katika siku ya Musa Yehova alileta tauni makuruhu ya vyura juu ya Misri ya Farao, hivi kwamba “bara likaanza kuvunda.” (Kutoka 8:5-15, NW) Wakati wa siku ya Bwana, kumekuwako pia msiba wenye kunyarafisha kama wa vyura, ingawa ni kutoka chimbuko tofauti. Ndani ya huo mna ‘semi chafu zilizovuviwa’ za Shetani, kwa wazi zikifananisha propaganda zinazokusudiwa kuongoza kwa werevu watawala wote wa kibinadamu, “wafalme,” katika kumpinga Yehova Mungu. Hivyo Shetani anahakikisha kwamba wao hawaathiriwi na kule kumiminwa kwa mabakuli ya kasirani ya Mungu bali kwa imara wao wako upande wa Shetani wakati “vita ya ile siku kubwa ya Mungu Mweza Yote” inapoanza.

      26. (a) Propaganda ya kishetani hutoka kwenye machimbuko gani matatu? (b) “Nabii bandia” ni nini, nasi tunajuaje?

      26 Hiyo propaganda huja kutoka kwa “drakoni” (Shetani) na “hayawani-mwitu” (mpango wa Shetani wa kisiasa wa kidunia), viumbe ambavyo tumekwisha kupata habari zavyo katika Ufunuo. Ingawa hivyo, huyu “nabii bandia” ni nini? Huyu ni mja-leo kwa jina tu. Wakati uliopita, sisi tulionyeshwa hayawani-mwitu wa pembe mbili mithili ya mwana-kondoo ambaye alifanya ishara mbele ya hayawani-mwitu mwenye vichwa saba. Kiumbe huyu mwenye kudanganya alitenda kama nabii kwa ajili ya huyo hayawani-mwitu. Aliendeleza ibada ya hayawani-mwitu, hata akasababisha mfano wake ujengwe. (Ufunuo 13:11-14, NW) Huyu hayawani-mwitu mwenye pembe mbili mithili ya mwana-kondoo lazima awe ndiye yule yule “nabii bandia,” anayetajwa hapa. Kuthibitisha hili, sisi tunasoma baadaye kwamba “nabii bandia” kama hayawani-mwitu wa ufananisho mwenye pembe mbili, “alifanya mbele [ya hayawani-mwitu mwenye vichwa saba] ishara ambazo kwa hizo yeye aliongoza vibaya wale ambao walipokea alama ya hayawani-mwitu na wale ambao hutoa ibada kwa mfano wake.”—Ufunuo 19:20, NW.

      27. (a) Ni onyo gani la wakati unaofaa ambalo Yesu Kristo mwenyewe hutoa? (b) Ni onyo gani ambalo Yesu Kristo alitoa alipokuwa duniani? (c) Mtume Paulo alirudishaje mwangwi wa onyo la Yesu?

      27 Kukiwako na propaganda nyingi sana za kishetani, maneno ambayo Yohana anafuata kurekodi ni ya wakati unaofaa kweli kweli: “Tazama! Mimi ninakuja kama mwivi. Mwenye furaha ni mmoja ambaye hukaa ameamka na kutunza mavazi yake ya nje, ili asipate kutembea uchi na watu watazame aibu yake.” (Ufunuo 16:15, NW) Ni nani anayekuja “kama mwivi”? Yesu mwenyewe, akija kwa wakati usiotangazwa akiwa Mfishaji wa Yehova. (Ufunuo 3:3; 2 Petro 3:10) Alipokuwa angali duniani, Yesu pia alifananisha kuja kwake na kule kwa mwivi, akisema: “Fulizeni kutazama, basi, kwa sababu nyinyi hamjui ni siku gani Bwana yenu anakuja. Kwa sababu hiyo, nyinyi vilevile jithibitisheni wenyewe kuwa tayari, kwa sababu kwenye saa ambayo nyinyi hamfikiri kuwa ndiyo, Mwana wa binadamu anakuja.” (Mathayo 24:42, 44; Luka 12:37, 40, NW) Akirudisha mwangwi wa onyo hilo, mtume Paulo alisema: “Siku ya Yehova inakuja sawasawa kama mwivi katika usiku. Wakati wowote wanaposema: ‘Amani na usalama!’ ndipo uharibifu wa ghafula utakuwa juu ya wao papo hapo.” Shetani ndiye anayechochea mbiu zozote bandia za “amani na usalama!”—1 Wathesalonike 5:2, 3, NW.

      28. Yesu alitoa onyo gani juu ya kukinza mibano ya ulimwengu, na “siku hiyo” ni ipi ambayo Wakristo hawataki iwe juu yao “kama tanzi”?

      28 Yesu alionya pia juu ya aina ya mibano ambayo ulimwengu huu, wenye kulowa propaganda, ungetia juu ya Wakristo. Alisema: “Toeni uangalifu kwa nyinyi wenyewe kwamba mioyo yenu isipate kulemewa kamwe na kula kupita kiasi na kunywa sana na wasiwasi wa maisha, na ghafula siku hiyo iwe juu ya nyinyi papo hapo kama tanzi. . . . Fulizeni kuamka, basi, wakati wote mkifanya dua kwamba nyinyi mpate kufaulu katika kuponyoka vitu hivi vyote ambavyo vimekusudiwa kutukia, na katika kusimama mbele ya Mwana wa binadamu.” (Luka 21:34-36, NW) “Siku hiyo” ni “ile siku kubwa ya Mungu Mweza Yote.” (Ufunuo 16:14, NW) Kadiri “siku hiyo” ya kutetewa kwa enzi kuu ya Yehova ikaribiavyo, inazidi kuwa vigumu zaidi kupambana kwa kufaulu na “wasiwasi wa maisha.” Wakristo wanahitaji kuwa chonjo na wenye kutazama, wakikaa hali wameamka mpaka siku hiyo iwasilipo.

      29, 30. (a) Ni nini kinachodokezwa na onyo la Yesu kwamba wale wanaopatikana wakilala wangeona aibu kwa kupoteza “mavazi ya nje” yao? (b) “Mavazi ya nje” yanamtambulisha mvaaji kuwa nini? (c) Mtu anaweza kupotezaje mavazi yake ya nje ya ufananisho, na tokeo likiwa nini?

      29 Ingawa hivyo, ni nini kinachodokezwa na onyo la kwamba wale wanaopatikana wakilala wangeona aibu kwa kupoteza “mavazi ya nje” yao? Katika Israeli wa kale, kuhani au Mlawi yeyote aliyekuwa katika kazi ya lindo kwenye hekalu alikuwa na daraka zito. Waelezaji Wayahudi hutuambia kwamba ikiwa yeyote alikutwa akilala akiwa katika kazi kama hiyo, mavazi yake yangeweza kuvuliwa kutoka kwake na kuchomwa, hivi kwamba aliaibishwa hadharani.

      30 Yesu anaonya hapa kwamba jambo kama hilo laweza kutukia leo. Makuhani na Walawi walikuwa kivuli cha ndugu wapakwa-mafuta wa Yesu. (1 Petro 2:9) Lakini kwa upanuzi onyo la Yesu linatumika vilevile kuhusu umati mkubwa. Hapa mavazi ya nje yanayorejezewa hutambulisha mvaaji kuwa Shahidi Mkristo wa Yehova. (Linga Ufunuo 3:18; 7:14.) Ikiwa wowote wanaruhusu mibano ya ulimwengu wa Shetani iwabembeleze walale usingizi au waingie ndani ya kutotenda, wao wanaelekea kupoteza mavazi ya nje, kwa maneno mengine, wapoteze utambulisho wao safi wa kuwa Wakristo. Hali kama hiyo ingekuwa yenye aibu. Ingemweka mmoja katika hatari ya kupoteza kabisa kila kitu.

      31. (a) Ufunuo 16:16 unakaziaje uhitaji kwa Wakristo kukaa wakiwa wameamka? (b) Baadhi ya viongozi wa kidini wamekisiakisia nini kwa habari ya Har–Magedoni?

      31 Uhitaji kwa Wakristo kukaa wakiwa wameamka unakuwa wenye kusonga hata zaidi kadiri mstari unaofuata wa Ufunuo ukaribiapo utimizo: “Na hizo [semi zilizovuviwa na roho waovu] zikakusanya wao [wafalme wa kidunia, au watawala] pamoja kwenye mahali ambapo huitwa kwa Kiebrania Har–Magedoni.” (Ufunuo 16:16, NW) Jina hili, ambalo wengi zaidi hufasiri Armagedoni hutokea mara moja tu katika Biblia. Lakini limechochea wazo la aina ya binadamu. Viongozi wa ulimwengu wameonya juu ya uwezekano wa Armagedoni ya nyukilia. Armagedoni imefungamanishwa pia na jiji la kale la Megido, mahali pa vita vingi vya kukata maneno katika nyakati za Biblia, na kwa hiyo baadhi ya viongozi wa kidini wamekisiakisia kwamba ile vita ya mwisho duniani itapiganwa mahali hapo padogo. Katika hili, wako mbali sana na ukweli.

      32, 33. (a) Badala ya kuwa mahali halisi, jina Har–Magedoni, au Armagedoni, huwakilisha nini? (b) Ni semi gani nyingine za Biblia zinazofanana na “Har–Magedoni” au zinazohusiana nayo? (c) Utakuwa wakati gani kwa malaika wa saba kumimina bakuli la mwisho kabisa la kasirani ya Mungu?

      32 Neno hili Har–Magedoni lamaanisha “Mlima wa Megido.” Lakini badala ya kuwa mahali halisi, linawakilisha hali ya ulimwengu ambayo ndani yayo mataifa yote yanakusanywa katika upinzani na Yehova Mungu na ambapo mwishowe yeye atawaharibu. Hii ni ya kadiri ya kuenea tufe lote. (Yeremia 25:31-33; Danieli 2:44) Inafanana na “shinikizo kubwa la divai ya kasirani ya Mungu” na “uwanda-bonde wa uamuzi,” au “uwanda-bonde wa Yehoshafati,” ambamo mataifa yanakusanywa yakauawe na Yehova. (Ufunuo 14:19; Yoeli 3:12, 14, NW) Inahusiana pia na “udongo wa Israeli” ambako majeshi ya kishetani ya Gogu wa Magogu yanaharibiwa na kata iliyo “kati ya bahari tukufu na mlima mtakatifu wa Urembo” ambako mfalme wa kaskazini anakuja “njia yote mpaka mwisho wake” mikononi mwa Mikaeli mwana-mfalme mkuu.—Ezekieli 38:16-18, 22, 23; Danieli 11:45–12:1, NW.

      33 Wakati mataifa yamekwisha kuongozwa kwa werevu ndani ya hali hii kupitia propaganda yenye kukoroma inayotokana na Shetani na mawakili wake wa kidunia, utakuwa ndio wakati wa malaika wa saba kumimina bakuli la mwisho kabisa la kasirani ya Mungu.

      “Imetukia!”

      34. Malaika wa saba humimina bakuli lake juu ya nini, na ni mbiu gani ‘hutoka katika patakatifu na katika kiti cha ufalme’?

      34 “Na wa saba akamimina bakuli lake juu ya hewa. Ndipo sauti kubwa ikatoka katika patakatifu kutoka kiti cha ufalme, kusema: ‘Imetukia!’”—Ufunuo 16:17, NW.

      35. (a) “Hewa” ya Ufunuo 16:17 ni nini? (b) Katika kumimina bakuli lake juu ya hewa malaika wa saba huonyesha nini?

      35 “Hewa” ndiyo njia ya mwisho kabisa ya kuendeleza uhai kupata tauni. Lakini hii si hewa halisi. Hakuna jambo lolote kuhusu hewa halisi linaloifanya istahili hukumu mbaya ya Yehova kama vile dunia, bahari, machimbuko ya maji matamu, au jua halisi visivyostahili kupatwa na hukumu mkononi mwa Yehova. Badala ya hivyo, hii ni ile “hewa” ambayo Paulo alikuwa akizungumzia wakati alipomwita Shetani “mtawala wa mamlaka ya hewa.” (Waefeso 2:2, NW) Ni “hewa” ya kishetani ambayo ulimwengu hupumua leo, ile roho, au mbetuko wa akili wa ujumla, inayoonyesha tabia ya mfumo mbovu wake wote wa mambo, kule kufikiri kwa kishetani kunakoenea katika kila upande wa maisha nje ya tengenezo la Yehova. Hivyo katika kumimina bakuli lake juu ya hewa, malaika wa saba anaonyesha kasirani ya Mungu dhidi ya Shetani, tengenezo lake, na kila kitu kinachosukuma aina ya binadamu iunge mkono Shetani katika kukaidi enzi kuu ya Yehova.

      36. (a) Tauni saba huwa nini? (b) Ni nini linalodokezwa na mbiu ya Yehova: “Imetukia!”?

      36 Tauni hii na zile sita zilizotangulia hutoa jumla ya hukumu za Yehova dhidi ya Shetani na mfumo wake. Hizo ni ujulisho-wazi wa angamio la Shetani na mbegu yake. Wakati bakuli hili la mwisho kabisa linapomiminwa, Yehova mwenyewe hupiga mbiu hivi: “Imetukia!” Hakuna jambo zaidi la kusema. Wakati yaliyomo ndani ya mabakuli ya kasirani ya Mungu yamekwisha kutangazwa peupe kwa kutosheka kwa Yehova, hakutakuwa na ukawio katika kutekeleza kwake hukumu zinazopigiwa mbiu na jumbe hizi.

      37. Yohana anaelezaje kinachotukia baada ya kumiminwa kwa bakuli la saba la kasirani ya Mungu?

      37 Yohana huendelea: “Na meme na sauti na ngurumo zikatukia, na tetemeko la dunia kubwa likatukia kama ambalo halikuwa limetukia tangu watu walipokuja kuwa juu ya dunia, tetemeko la dunia lenye kuenea mno, kubwa mno. Na jiji kubwa likatengana kuwa sehemu tatu, na majiji ya mataifa yakaanguka; na Babuloni Mkubwa akakumbukwa katika mwono wa Mungu, ili kumpa yeye kikombe cha divai ya kasirani ya hasira-kisasi yake. Pia, kila kisiwa kikakimbia, na milima haikupatikana. Na mvua-mawe kubwa yenye kila jiwe la uzani wapata talanta ikashuka kutoka katika mbingu juu ya watu, na wale watu wakakufuru Mungu kwa sababu ya tauni ya mvua-mawe, kwa sababu tauni yayo ilikuwa kubwa isivyo kawaida.”—Ufunuo 16:18-21, NW.

      38. Ni nini kinachofananishwa na (a) “tetemeko la dunia kubwa”? (b) uhakika wa kwamba “jiji kubwa,” Babuloni Mkubwa, linatengana kuwa “sehemu tatu”? (c) uhakika wa kwamba “kila kisiwa kilikimbia, na milima haikupatikana”? (d) “tauni ya mvua-mawe”?

      38 Kwa mara nyingine tena, bila kukosea Yehova anatenda kuelekea aina ya binadamu, hii ikiwa inaashiriwa na “meme na sauti na ngurumo.” (Linga Ufunuo 4:5; 8:5, NW.) Aina ya binadamu itatikiswa kwa njia ambayo haijatukia kamwe kabla ya hapo, kana kwamba kwa tetemeko la dunia lenye kukumba. (Linga Isaya 13:13; Yoeli 3:16.) Mtikiso huu wenye kulipua kama bomu utabomoa “jiji kubwa,” Babuloni Mkubwa, hivi kwamba hutengana kuwa “sehemu tatu”—ufananisho wa kuanguka kwalo ndani ya uangamivu usiokomboleka. Pia, “majiji ya mataifa” yataanguka. “Kila kisiwa” na “milima”—mashirika na matengenezo yanayoonekana ni ya kudumu sana katika huu mfumo—yataenda. “Mvua-mawe kubwa,” kubwa zaidi ya ile iliyopiga Misri wakati wa tauni ya saba, kila jiwe-mvua likiwa na uzani upatao talanta, litapigapiga aina ya binadamu kwa maumivu mengi.d (Kutoka 9:22-26) Huu mmimino-chini wenye kuadhibu, wa maji yaliyogandamana yaelekea unatoa picha ya semi za maneno zilizo nzito isivyo kawaida za hukumu za Yehova zikiashiria kwamba mwisho wa huu mfumo wa mambo umewasili hatimaye! Vilevile, Yehova angeweza kutumia mvua-mawe halisi katika kazi yake yenye uharibifu.—Ayubu 38:22, 23.

      39. Ijapokuwa kumiminwa kwa tauni saba, walio wengi wa aina ya binadamu watachukua mwendo gani wa tendo?

      39 Hivyo, ulimwengu wa Shetani utakutana na hukumu za Yehova zenye uadilifu. Hadi mwisho, walio wengi wa aina ya binadamu wataendelea kukaidi na kukufuru Mungu. Kama vile Farao wa kale, mioyo yao haitalainishwa na tauni zenye kurudiwarudiwa wala na upeo wa kumalizia wenye kuleta kifo wa tauni hizo. (Kutoka 11:9, 10) Hakutakuwa na mabadiliko makubwa ya moyo katika dakika ya mwisho. Kwa pumzi yao ya wakati wa kufa, wao watalaumu vikali Mungu anayejulisha wazi: “Wao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.” (Ezekieli 38:23, NW) Hata hivyo enzi kuu ya Yehova Mungu itakuwa imekwisha tetewa.

      [Maelezo ya Chini]

      a Kwa ajili ya vielelezo vya vitu visivyo na uhai vikitumika kuwa shahidi au vikitoa ushahidi, linga Mwanzo 4:10; 31:44-53; Waebrania 12:24.

      b Utumizi ulio kama huo wa “kiti cha ufalme” huonekana katika maneno anayoambiwa Yesu kiunabii: “Mungu ndiye kiti cha ufalme chako kwa wakati usio dhahiri, hata milele.” (Zaburi 45:6, NW) Yehova ndiye chimbuko au msingi, wa mamlaka ya kifalme ya Yesu.

      c Ona pia Ayubu 1:6, 12; 2:1, 2; Mathayo 4:8-10; 13:19; Luka 8:12; Yohana 8:44; 12:31; 14:30; Waebrania 2:14; 1 Petro 5:8.

      d Ikiwa Yohana alikuwa akifikiria talanta ya Kigiriki, kila jiwe la mvua lingekuwa na uzani wa zaidi ya kilo 20. Ingekuwa dhoruba ya mvua-mawe yenye kukumba.

      [Picha katika ukurasa wa 221]

      “Ndani ya Dunia”

      Jamii ya Yohana imetangaza wazi hasira-kisasi ya Yehova dhidi ya “dunia” kwa taarifa kama zifuatazo:

      “Baada ya karne nyingi za jitihada, vyama vya kisiasa vimejithibitisha kutoweza kwavyo kukabiliana na hali za wakati uliopo na kutatua matatizo yenye kutaabisha. Watalaamu wa uchumi na wakuu wa serikali, wakichunguza swali hilo kwa bidii-endelevu, wanapata kwamba hawawezi kufanya kitu.”—Millions Now Living Will Never Die, 1920, ukurasa 61.

      “Hakuna serikali hata moja duniani leo inayotosheleza kisehemu cha ulimwengu kwa kadiri yoyote yenye kuridhisha. Mengi ya mataifa yanatawalwa na madikteta. Ulimwengu kwa ujumla karibu umefilisika.”—A Desirable Government, 1924, ukurasa 5.

      “Kukomesha taratibu ya mambo haya . . . ndiyo njia peke yake ya kuondoa uovu katika dunia na kuipa nafasi amani na haki kusitawi.”—“Habari Njema Hizi za Ufalme,” ukurasa 25.

      “Mpango uliopo sasa wa ulimwengu umejionyesha wazi namna ulivyo kwa kuzidi kutenda dhambi nyingi, mabaya na uasi juu ya Mungu na mapenzi yake. . . . Hauwezi kubadilishwa uwe mzuri. Kwa hiyo, lazima upotelee mbali!”—Mnara wa Mlinzi, Juni 15, 1982, ukurasa 6.

      [Picha katika ukurasa wa 223]

      “Ndani ya Bahari”

      Zifuatazo ni chache tu za taarifa zilizochapishwa kwa muda wa miaka iliyopita na jamii ya Yohana zikipiga mbiu ya hasira-kisasi ya Mungu dhidi ya “bahari” isiyotulia, yenye uasi ya aina ya binadamu isiyohofu Mungu iliyotenganishwa na Yehova:

      “Historia ya kila taifa huonyesha kwamba imekuwa ni mng’ang’ano kati ya matabaka. Imekuwa ni wachache dhidi ya wengi. . . . Ming’ang’ano hii imetokeza mapinduzi makubwa mengi, kuteseka kwingi na umwagaji-damu mwingi.”—Government, 1928, ukurasa 244.

      Katika ulimwengu mpya, “‘bahari’ ya mfano ya watu wasiotulia, wenye kuasi, wasiohofu Mungu ambao kutoka kwao hayawani-mwitu alipanda muda mrefu uliopita atumiwe na Ibilisi itakuwa imeenda.”—The Watchtower, Septemba 15, 1967, ukurasa 567.

      “Jamii ya sasa ya kibinadamu ni yenye ugonjwa kiroho. Hakuna mmoja wa sisi awezaye kuiokoa, kwa maana Neno la Mungu laonyesha kwamba ugonjwa wayo unaongoza kwenye mauti yake.”—Amani ya Kweli na Usalama wa Kweli—Kutoka Chanzo Gani?, 1974, ukurasa 131.

      [Picha katika ukurasa wa 224]

      “Ndani ya Mito na Vibubujiko”

      Tauni ya tatu imefunua “mito na vibubujiko vya maji” kwa taarifa kama zifuatazo:

      “Viongozi wa kidini, wanaodai kuwa walimu wa mafundisho [ya Kristo], wametakasa vita na kuifanya kuwa kitu kitakatifu. Wao wamependezwa kuwa na taswira zao na sanamu-umbo zionyeshwe kando kwa kando na zile za mashujaa wenye kumwaga damu.”—The Watch Tower, Septemba 15, 1924, ukurasa 275.

      “Uwasiliano na roho msingi wao ni utokweli mkubwa, uwongo wa kuendelea kuishi baada ya kifo na kutokufa kwa nafsi ya kibinadamu.”—What Do the Scriptures Say About “Survival After Death?,” 1955, ukurasa 51.

      “Falsafa za kibinadamu, wananadharia wa kisiasa, watengenezaji jamii, washauri wa kiuchumi na wateteaji wa mapokeo ya kidini hawakutokeza burudiko lolote halisi lenye kutoa uhai. Maji kama hayo hata yameongoza wanywaji kuhalifu sheria ya Muumba kuhusu utakatifu wa damu na kujitia katika minyanyaso ya kidini.”—Azimio lililokubaliwa kwenye “Habari Njema za Milele” Mkusanyiko wa Kimataifa, 1963.

      “Si wokovu wa kisayansi, bali uangamivu wa jamii ya kibinadamu ndilo jambo la kutarajiwa kutoka kwa mwanadamu mwenyewe. . . . Sisi hatuwezi kutegemea wasaikolojia na wasaikayatristi wote wa ulimwengu wabadili njia ya kufikiri ya aina ya binadamu . . . Sisi hatuwezi kutegemea kani ya polisi yoyote ya kimataifa ifanyizwe . . . kufanya dunia hii kuwa mahali salama pa kuishi.”—Saving the Human Race—In the Kingdom Way, 1970, ukurasa 5.

      [Picha katika ukurasa wa 225]

      “Juu ya Jua”

      Huku “jua” la utawala wa kibinadamu likiwa ‘limeunguza’ aina ya binadamu wakati wa siku ya Bwana, jamii ya Yohana, imekuwa ikivuta uangalifu kwenye yanayotukia, kwa taarifa kama zifuatazo:

      “Leo Hitla na Mussolini, madikteta wenye amri peke yao, wanatisha amani ya ulimwengu kwa ujumla, na wanaungwa mkono kikamili na jamii ya mapadri wa Katoliki ya Roma katika uharibifu wao wa uhuru.”—Fascism or Freedom, 1939, ukurasa 12.

      “Muda wote wa historia sera iliyofuatwa na madikteta wa kibinadamu imekuwa, Tawala au angamiza! Lakini kirekebi cha kutumiwa sasa na Mfalme aliyewekwa na Mungu, Yesu Kristo, kwenye dunia yote, ni, Tawalwa au uangamizwe.”—When All Nations Unite Under God’s Kingdom, 1961, ukurasa 23.

      “Tangu 1945 zaidi ya watu milioni 25 wameuawa katika vita 150 vilivyopiganwa kuzunguka dunia.”—Mnara wa Mlinzi, Julai 1, 1980, ukurasa 6.

      “Mataifa kuuzunguka ulimwengu . . . hayajali sana daraka la kimataifa au amri za mwenendo. Ili kutimiza miradi yao, mataifa mengine yana maoni ya kwamba yana haki kabisa kutumia njia zo zote yanazoziona kuwa lazima—kuchinja watu kwa wingi, kuua, kuteka nyara, kulipua makombora, na kadhalika . . . Ni kwa muda gani mataifa yataendelea kuvumiliana katika mwendo huo wa upumbavu na usiofaa?”—Mnara wa Mlinzi, Julai 15, 1985, ukurasa 4.

      [Picha katika ukurasa wa 227]

      “Juu ya Kiti cha Ufalme cha Hayawani-Mwitu”

      Mashahidi wa Yehova wamefichua kiti cha ufalme cha hayawani-mwitu na wakatangaza wazi shutumu la Yehova juu yacho kwa taarifa kama hizi:

      “Watawala na waongozi wa kisiasa wa mataifa wanavutwa na kani zisizo za kibinadamu, zenye makusudi mabaya, zinazowaendesha bila kupingwa katika mwendo wa ujiuaji kwenye mpambano wa kukata maneno wa Har–Magedoni.”—After Armageddon—God’s New World, 1953, ukurasa 8.

      “‘Hayawani-Mwitu’ wa serikali za kibinadamu zisizo za kitheokrasi alipata uwezo, mamlaka na kiti cha ufalme chake kutoka kwa Drakoni. Kwa hiyo lazima atii amri ya chama, amri ya Drakoni.”—After Armageddon—God’s New World, 1953, ukurasa 15.

      “Mataifa Yasiyo ya Kiyahudi yanaweza kujikuta yenyewe tu . . . upande wa Hasimu Mkuu wa Mungu, Shetani Ibilisi.”—Azimio lililokubaliwa kwenye “Ushindi wa Kimungu” Mkusanyiko wa Kimataifa, 1973.

      [Picha katika ukurasa wa 229]

      “Maji Yao Yakakauka Kabisa”

      Hata sasa, uungaji-mkono wa dini ya Kibabuloni unakauka kabisa mahali pengi, kuonyesha jambo litakalotukia wakati “wafalme kutoka zukio la jua” watakapofanya shambulio lao.

      “Uchunguzi wa maoni ya watu wa taifa zima ulipata kwamba asilimia 75 ya wale wanaoishi katika maeneo ya manispaa [ya Thailandi] hawaendi hata kidogo kwenye mahekalu ya Kibuddha kusikiliza mahubiri, hali hesabu ya wale wanaozuru mahekalu mashambani inazidi kupungua kufika yapata asilimia hamsini.”—Bangkok Post, Septemba 7, 1987, ukurasa 4.

      “Mzungu umekwisha katika Utao katika bara [China] ambako ulianzia zapata mileani mbili zilizopita. . . . Wakiwa bila vidude vya kufanyia mizungu ambavyo kwavyo wao na watangulizi wao walizoea kupata ufuasi mwingi, washiriki wa ukuhani wanajikuta wakiwa bila waandamizi, karibu wakikabili mzimiko wa Utao ukiwa imani iliyopangwa kitengenezo katika bara kuu.”—The Atlanta Journal and Constitution, Septemba 12, 1982, ukurasa 36-A.

      “Japani . . . ina mmojapo misongano mikubwa zaidi sana ya wamisionari wa kigeni ulimwenguni, karibu 5,200, hata hivyo . . . punde kuliko asilimia 1 ya idadi ya watu ni Wakristo. . . . Padri mmoja wa Kifransiska anayefanya kazi hapa tangu miaka ya 1950 . . . anaitikadi kwamba ‘siku ya wamisionari wa kigeni katika Japani imekwisha.’”—The Wall Street Journal, Julai 9, 1986, ukurasa 1.

      Katika Uingereza wakati wa miongo mitatu iliyopita, “karibu makanisa ya Kianglikana 2,000 kati ya yale 16,000 yamefungwa kwa sababu ya kutotumiwa. Hadhirina imepungua kuwa miongoni mwa zile za chini zaidi sana za nchi zinazokiri kuwa za Kikristo. . . . ‘Sasa hali ni kwamba Uingereza si nchi ya Kikristo,’ akasema [Askofu wa Durham].”—The New York Times, Mei 11, 1987, ukurasa A4.

      “Baada ya saa nyingi za majadiliano makali, Bunge [la Ugiriki] liliidhinisha leo sheria itungwe, ikiiwezesha Serikali ya Kisoshalisti itwae mali zenye mashamba makubwa mno zinazoshikiliwa na Kanisa Orthodoksi la Ugiriki . . . Zaidi ya hilo, sheria hiyo inawapa wasio viongozi wa kanisa udhibiti wa mabaraza ya kanisa na halmashauri zenye madaraka ya kusimamia vitega-uchumi vya kanisa vyenye thamani kubwa kutia ndani mahoteli, mashimo ya kuchimba marumaru na majengo ya maofisi.”—The New York Times, Aprili 4, 1987, ukurasa 3.

      [Picha katika ukurasa wa 222]

      Mabakuli manne ya kwanza ya kasirani ya Mungu huleta tauni kama zile zilizotokana na mipigo minne ya kwanza ya tarumbeta

      [Picha katika ukurasa wa 226]

      Bakuli la tano hufichua kiti cha hayawani-mwitu kuwa ndiyo mamlaka ambayo Shetani amempa hayawani-mwitu

      [Picha katika ukurasa wa 231]

      Propaganda ya roho waovu inakusanya watawala wa dunia kwenye hali ya pamoja, Har–Magedoni, ambapo hukumu za Yehova zitamiminwa juu yao

      [Picha katika ukurasa wa 233]

      Wale wanaosukumwa na “hewa” chafu ya Shetani lazima wapatwe na utekelezo wa hukumu za Yehova zenye uadilifu

  • Kuhukumu Kahaba Mwenye Sifa Mbaya
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Sura ya 33

      Kuhukumu Kahaba Mwenye Sifa Mbaya

      Njozi ya 11—Ufunuo 17:1-18

      Habari: Babuloni Mkubwa apanda hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu ambaye mwishowe amgeukia na kumteketeza

      Wakati wa utimizo: Kuanzia 1919 hadi dhiki kubwa

      1. Mmoja wa malaika saba anafunulia Yohana nini?

      KASIRANI ya Yehova ya uadilifu lazima imiminwe mpaka utimilifu, mabakuli saba yayo! Malaika wa sita alipomimina bakuli lake katika kata ya Babuloni wa kale, ilifananisha kwa kufaa tauni kwa Babuloni Mkubwa huku matukio yakienda kasi kuelekea vita ya mwisho kabisa ya Har–Magedoni. (Ufunuo 16:1, 12, 16) Yaelekea, malaika uyu huyu ndiye anayefunua sasa ni kwa nini na jinsi gani Yehova anatekeleza hukumu zake za uadilifu. Yohana anapatwa na mshangao kwa sababu ya anachofuata kusikia na kuona: “Na mmoja wa wale malaika saba ambao walikuwa na mabakuli saba akaja na kunena na mimi, kusema: ‘Njoo, mimi nitaonyesha wewe hukumu juu ya kahaba mkubwa ambaye huketi juu ya maji mengi, ambaye wafalme wa dunia walifanya uasherati na yeye, huku wale ambao huikaa dunia walifanywa kulewa divai ya uasherati wake.’”—Ufunuo 17:1, 2, NW.

      2. Kuna ithibati gani kwamba “kahaba mkubwa” (a) si Roma ya kale? (b) si biashara kubwa-kubwa? (c) ni dini?

      2 “Kahaba mkubwa”! Kwa nini jina lenye kugutusha hivyo? Yeye ni nani? Wengine wametambulisha kahaba huyu wa ufananisho kuwa Roma ya kale. Lakini Roma ilikuwa mamlaka ya kisiasa. Kahaba huyu hufanya uasherati na wafalme wa dunia, kwa wazi kutia ndani wafalme wa Roma. Mbali na hilo, baada ya kuharibiwa kwake, “wafalme wa dunia,” husemekana kuombolezea kufa kwake. Hivyo, yeye hawezi kuwa mamlaka ya kisiasa. (Ufunuo 18:9, 10) Kwa kuongezea, kwa kuwa anaombolezewa pia na wafanya biashara wa ulimwengu, yeye hawezi kufananisha biashara kubwa-kubwa. (Ufunuo 18:15, 16) Hata hivyo, sisi tunasoma kwamba, ‘kwa mazoea yake ya uwasiliano na roho mataifa yote yaliongozwa vibaya.’ (Ufunuo 18:23, NW) Hilo linafanya iwe wazi kwamba huyu kahaba mkubwa lazima awe dini ya ulimwenguni pote.

      3. (a) Kwa nini kahaba mkubwa lazima afananishe zaidi ya Kanisa Katoliki la Roma, au hata Jumuiya ya Wakristo yote? (b) Ni mafundisho gani ya Kibabuloni yanayopatikana katika dini nyingi za Mashariki na pia katika mafarakano ya Jumuiya ya Wakristo? (c) John Henry Newman kardinali Mkatoliki alikiri nini juu ya asili ya mafundisho, sherehe na mazoea mengi ya Jumuiya ya Wakristo? (Ona kielezi cha chini.)

      3 Dini ipi? Je! yeye ni Kanisa Katoliki la Roma, kama vile wengine wameshikilia? Au je! yeye ni Jumuiya ya Wakristo yote? Hapana, lazima yeye awe mpana hata zaidi ya hizi ikiwa yeye ataongoza vibaya mataifa yote. Kwa hakika yeye ni milki ya ulimwengu mzima wote ya dini bandia. Chanzo chake katika mafumbo ya Babuloni huonyeshwa kwa njia ya kwamba mengi ya mafundisho na mazoea ya Kibabuloni ni mambo ya kawaida ya dini nyingi kotekote duniani. Mathalani, itikadi ya kwamba nafsi ya kibinadamu ina kutokufa, moto wa mateso, na utatu wa miungu itapatikana katika dini nyingi za Mashariki pamoja na katika mafarakano ya Jumuiya ya Wakristo. Dini bandia, iliyoanguliwa miaka zaidi ya 4,000 iliyopita katika jiji la kale la Babuloni, imesitawi ikawa dubwana la ki-siku-hizi, ambalo kwa kufaa huitwa, Babuloni Mkubwa.a Ingawa hivyo, sababu gani anaelezwa kwa usemi usiopendeza “kahaba mkubwa”?

      4. (a) Ni katika njia zipi Israeli wa kale alifanya uasherati? (b) Ni katika njia gani ya kutokeza Babuloni Mkubwa amefanya uasherati?

      4 Babuloni (au Babeli, kumaanisha “Mvurugo”) lilifikia kilele chalo cha ukubwa wakati wa Nebukadneza. Lilikuwa dola la dini-siasa lenye mahekalu na vikanisa zaidi ya elfu moja. Ukuhani walo ulitumia nguvu kubwa. Ingawa muda mrefu tangu hapo Babuloni limeacha kuwa serikali ya ulimwengu, Babuloni Mkubwa wa kidini huendelea kuwapo, na kwa kufuata kigezo cha kale, yeye angali anatafuta kuvuta na kuunda mambo ya kisiasa. Lakini je! Mungu anatoa idhini ya dini kuwa katika siasa? Katika Maandiko ya Kiebrania, Israeli alisemwa kuwa alifanya ukahaba wakati alipojihusisha katika ibada bandia na wakati badala ya kuitibari katika Yehova, alifanya mafungamano na mataifa. (Yeremia 3:6, 8, 9; Ezekieli 16:28-30) Babuloni Mkubwa pia hufanya uasherati. Kwa kutokeza, yeye amefanya lolote analoona linafaa ili kupata uvutano na mamlaka juu ya wafalme wa dunia wenye kutawala.—1 Timotheo 4:1.

      5. (a) Viongozi wa kidini hufurahia umashuhuri gani? (b) Kwa nini kutamani umashuhuri wa kilimwengu kunapingana moja kwa moja na maneno ya Yesu Kristo?

      5 Leo, mara nyingi viongozi wa kidini hugombea cheo cha juu katika serikali, na katika mabara fulani, wanashiriki katika serikali, hata wakishikilia vyeo katika bunge. Katika 1988 viongozi wa kidini wa Kiprotestanti wawili wenye kujulikana sana waligombea cheo cha rais wa United States. Viongozi katika Babuloni Mkubwa hupenda umashuhuri; foto zao mara nyingi zitaonekana katika nyusipepa za umma wanapofuatana na wanasiasa mashuhuri. Kwa kutofautiana, Yesu aliepuka kujihusisha katika siasa na akasema hivi kwa habari ya wanafunzi wake: “Wao si sehemu ya ulimwengu, kama vile mimi si sehemu ya ulimwengu.”—Yohana 6:15; 17:16, NW; Mathayo 4:8-10; ona pia Yakobo 4:4.

      ‘Ukahaba’ wa Ki-Siku-Hizi

      6, 7. (a) Chama cha Nazi cha Hitla kilipataje mamlaka katika Ujeremani? (b) Itifaki ambayo Vatikani ilifanya pamoja na Ujeremani ya Nazi ilisaidiaje Hitla katika jitihada yake kubwa ya kutawala ulimwengu?

      6 Kupitia udukizi wake katika siasa, huyu kahaba mkubwa ameletea aina ya binadamu huzuni isiyoelezeka. Mathalani, fikiria mambo ya hakika yaliyomwezesha Hitla kuinuka kwenye mamlaka katika Ujeremani—mambo ya hakika yenye kuchukiza sana ambayo baadhi ya watu wangependa kuyafuta kutoka katika vitabu vya historia. Katika Mei 1924 Chama cha Nazi kilishikilia viti 32 katika Bunge la Ujeremani. Kufikia Mei 1928 vilikuwa vimepungua vikawa viti 12. Lakini, ule Mshuko Mkubwa wa Thamani ya Pesa ukagharikisha ulimwengu katika 1930; kufuata huo, Wanazi walipata nafuu yenye kutokeza, wakijipatia viti 230 kati ya 608 katika machaguzi ya Ujeremani ya Julai 1932. Hivyo, wakawa chama kikubwa zaidi ya vyote katika Bunge. Upesi baadaye, Franz von Papen, Mheshimiwa Kipapa, aliyekuwa Chansela hapo kwanza, akaja kusaidia Wanazi. Kulingana na wanahistoria, von Papen alikuwa na njozi ya Milki Takatifu ya Kiroma mpya. Muda wake mwenyewe mfupi wa kuwa Chansela ulikuwa umekuwa usiofanikiwa, hivyo sasa yeye alitumainia kujipatia mamlaka kupitia Wanazi. Kufikia Januari 1933, yeye alikuwa amepata uungaji-mkono kwa ajili ya Hitla kutoka kwa wenye viwanda, na kwa njama za hila yeye alihakikisha kwamba Hitla amekuwa Chansela wa Ujeremani katika Januari 30, 1933. Yeye mwenyewe alifanywa makamu wa Chansela na yeye alitumiwa na Hitla apate uungaji-mkono wa sehemu za Kikatoliki za Ujeremani. Kwa muda wa miezi miwili ya kujipatia mamlaka, Hitla alivunja bunge, akapeleka maelfu ya viongozi wapinzani kwenye kambi za mateso, na akaanza kampeni iliyo wazi ya kuwaonea Wayahudi.

      7 Katika Julai 20, 1933, upendezi wa Vatikani katika mamlaka iliyokuwa ikiinuka ya Unazi ulionyeshwa wakati Kardinali Pacelli (ambaye baadaye akawa Papa Pius 12) alipotia sahihi itifaki katika Roma kati ya Vatikani na Ujeremani ya Nazi. Von Papen alitia sahihi hati hiyo akiwa mwakilishi wa Hitla, na huko huko Pacelli akampa von Papen medali ya juu ya kipapa ya Msalaba Mtukufu wa Daraja la Pius.b Katika kitabu chake Satan in Top Hat, Tibor Koeves huandika juu ya hili, akitaarifu: “Itifaki ilikuwa ushindi mkubwa kwa ajili ya Hitla. Ilimpa uungaji-mkono wa kwanza wa kiadili aliokuwa amepokea kutoka ulimwengu wa nje, na huo kutoka chimbuko lililokwezwa zaidi sana.” Itifaki hiyo ilitaka Vatikani iondoe uungaji-mkono wayo kutoka kwa Chama cha Kati cha Kikatoliki, na hivyo kuidhinisha “serikali jumla” ya Hitla ya chama kimoja.c Zaidi, sehemu ya 14 yayo ilisema: “Uwekwaji rasmi wa maaskofu wakuu, maaskofu, na wengine kama hao utatolewa baada tu ya gavana, aliyewekwa na Serikali, kuhakikisha kabisa kwamba hakuna shaka lolote kwa habari ya mafikirio ya ujumla ya kisiasa.” Kufikia mwisho wa 1933 (uliotangazwa na Papa Pius 11 kuwa “Mwaka Mtakatifu”), uungaji-mkono wa Vatikani ulikuwa umekuwa umechangia sana jitihada kubwa ya Hitla kwa ajili ya utawala wa ulimwengu.

      8, 9. (a) Vatikani na pia Kanisa Katoliki na viongozi wa kidini wayo walitendaje katika kuitikia ukatili wa Nazi? (b) Ni taarifa gani ambayo Maaskofu Wakatoliki wa Ujeremani walitoa mwanzoni mwa Vita ya Ulimwengu 2? (c) Mahusiano ya dini-siasa yamekuwa na matokeo gani?

      8 Ingawa mapadri na watawa wa kike wachache waliteta dhidi ya matendo ya ubahaimu ya Hitla—na wakapata mateso kwa kufanya hivyo—Vatikani pamoja na Kanisa Katoliki na jeshi layo la viongozi wa kidini waliunga mkono ukatili wa Nazi ama kwa vitendo au kwa kutoteta, waliuona kuwa kinga dhidi ya kusonga mbele kwa Ukomunisti wa ulimwengu. Akijikalia kitako katika Vatikani, Papa Pius 12 aliachilia Uharibifu Mkubwa wa Wayahudi na unyanyaso wa ukatili juu ya Mashahidi wa Yehova na wengine uendelee bila kuchambuliwa. Ni kinyume kwamba Papa John Paul 2, alipozuru Ujeremani katika Mei 1987, alipaswa kutukuza msimamo wa padri mmoja mwenye moyo mweupe wa kupinga Unazi. Yale maelfu mengine ya viongozi wa kidini wa Ujeremani walikuwa wakifanya nini wakati wa utawala wa kuogofya wa Hitla? Barua moja ya uchungaji iliyotolewa na maaskofu wa Ukatoliki wa Ujeremani katika Septemba 1939 ilipotokea Vita ya Ulimwengu 2, inatoa nuru juu ya jambo hili. Kwa sehemu inasomwa hivi: “Katika saa hii ya kukata maneno sisi twashauri askari-jeshi Wakatoliki kufanya wajibu wao katika utii kwa Fuehrer na kuwa tayari kudhabihu nafsi nzima yao. Sisi tunasihi Waaminifu wajiunge katika sala zenye idili kwamba huu Mwongozo wa Kimungu uweze kupeleka vita hii kwenye ufanisi wenye baraka.”

      9 Ubalozi huu wa Katoliki unatoa kielezi cha namna ya ukahaba ambao dini imejitia ndani yao katika miaka zaidi ya 4,000 iliyopita katika kubembeleza Serikali ya kisiasa ili kupata mamlaka na faida. Mahusiano kama hayo ya dini-siasa yamesitawisha vita, minyanyaso, na taabu kwa aina ya binadamu kwa kadiri kubwa mno. Jinsi aina ya binadamu inavyoweza kuwa na furaha kwamba hukumu ya Yehova juu ya huyu kahaba mkubwa imekaribia karibu! Na itekelezwe upesi!

      Kuketi Juu ya Maji Mengi

      10. Ni “maji mengi” gani ambayo Babuloni Mkubwa hutegemea kuwa himaya, na yanapatwa na nini?

      10 Babuloni wa kale aliketi juu ya maji mengi—Mto Eufrati na mifereji mingi. Haya yalikuwa himaya yake pamoja na chimbuko la biashara iliyotokeza utajiri, mpaka yalipokaushwa usiku mmoja. (Yeremia 50:38; 51:9, 12, 13) Babuloni Mkubwa pia hutegemea “maji mengi” yampe himaya na kumtajirisha. Maji haya ya ufananisho ni “vikundi vya watu na umati wa watu na mataifa na ndimi,” yaani, maelfu ya mamilioni yote ya binadamu ambao juu yao yeye ametawala na ambao kutoka kwao yeye amechota msaada wa vitu vya kimwili. Lakini maji haya ya ufananisho yanakauka pia, au kuondoa msaada.—Ufunuo 17:15, NW; linga Zaburi 18:4; Isaya 8:7.

      11. (a) Jinsi gani Babuloni wa kale ‘alifanya dunia yote ilewe’? (b) Babuloni Mkubwa ‘amefanyaje dunia yote ilewe’?

      11 Na zaidi, Babuloni wa kale alielezwa kuwa “kikombe cha dhahabu katika mkono wa Yehova, akifanya dunia yote ilewe.” (Yeremia 51:7, NW) Babuloni wa kale alilazimisha mataifa jirani kumeza maonyesho ya kasirani ya Yehova alipoyashinda kijeshi, kuyafanya dhaifu kama wanadamu waliolewa. Katika njia hiyo, alikuwa chombo cha Yehova. Babuloni Mkubwa, pia, amefanya ushindi mwingi kwa kadiri ya kuwa milki ya ulimwenguni pote. Lakini yeye kwa uhakika si chombo cha Yehova. Badala ya hivyo, yeye ametumikia “wafalme wa dunia” ambao pamoja nao yeye hufanya uasherati wa kidini. Yeye hufurahisha wafalme hawa kwa kutumia mafundisho yake ya uwongo na mazoea yenye kutumikisha ili kuweka matungamo ya watu, “wale wanaoikaa dunia,” kuwa dhaifu kama wanadamu waliolewa, wakitii watawala wao bila kuwa na la kufanya.

      12. (a) Kisehemu kimoja cha Babuloni Mkubwa katika Japani kilikuwaje na daraka la kumwagwa kwa damu nyingi wakati wa Vita ya Ulimwengu 2? (b) Jinsi gani “maji” yenye kuunga mkono Babuloni Mkubwa yaliondolewa katika Japani, na kukiwa na tokeo gani?

      12 Japani ya Shinto hutoa kielelezo kinachostahili kuangaliwa cha jambo hili. Askari-jeshi Wajapani waliiona kuwa heshima ya juu zaidi sana kutoa uhai wao kwa ajili ya maliki—mungu mkuu wa Shinto. Wakati wa Vita ya Ulimwengu 2, askari-jeshi Wajapani wapatao 1,500,000 walikufa vitani; karibu kila mtu aliona kusalimu amri kuwa utovu wa heshima. Lakini likiwa tokeo la ushinde wa Japani, Maliki Hirohito alilazimika kukana dai lake la uungu. Hilo lilitokeza mwondoleo mkubwa wa “maji” yaliyounga mkono kisehemu cha Shinto cha Babuloni Mkubwa—loo! baada ya Ushinto kuidhinisha umwagaji wa ndoo nyingi za damu katika uwanja wa vita wa Pasifiki! Mdhoofisho huu wa uvutano wa Shinto ulifungua pia njia katika miaka ya juzi kwa ajili ya Wajapani 200,000, ambao walio wengi wao walikuwa hapo kwanza Washinto na Wabuddha, wawe wahudumu walio wakfu na waliobatizwa wa Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu.

      Kahaba Apanda Hayawani

      13. Ni mwono gani wenye kushangaza anaoona Yohana wakati malaika anapompeleka katika jangwa kwa nguvu ya roho?

      13 Unabii hufumbua nini zaidi kwa habari ya kahaba mkubwa na msiba wake? Kama Yohana anavyosimulia sasa, mandhari nyingine iliyo wazi sana yaonekana: “Na yeye [malaika] akapeleka mimi mbali kwa nguvu ya roho kuingia ndani ya jangwa. Na mimi nikaona mwanamke akiwa ameketi juu ya hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu ambaye alikuwa amejaa majina ya kufuru na ambaye alikuwa na vichwa saba na pembe kumi.”—Ufunuo 17:3, NW.

      14. Ni kwa nini inafaa kwamba Yohana alipelekwa jangwani?

      14 Ni kwa nini Yohana anapelekwa ndani ya jangwa? Tamko la mapema zaidi la uangamivu dhidi ya Babuloni wa kale lilielezwa kuwa “dhidi ya jangwa la bahari.” (Isaya 21:1, 9, NW) Hilo lilitoa onyo linalostahili kwamba, ujapokuwa ulinzi wake mwingi wa kimaji, Babuloni wa kale angekuwa ukiwa usio na uhai. Inafaa, basi, kwamba yampasa Yohana apelekwe katika njozi yake kwenye jangwa akaone msiba wa Babuloni Mkubwa. Yeye pia lazima awe ukiwa na utupu. (Ufunuo 18:19, 22, 23) Ingawa hivyo, Yohana anashangazwa na anachoona nje kule. Kahaba mkubwa hayuko peke yake! Yeye anaketi juu ya dubwana la hayawani-mwitu!

      15. Ziko tofauti gani kati ya hayawani-mwitu wa Ufunuo 13:1 na yule wa Ufunuo 17:3?

      15 Hayawani-mwitu huyu ana vichwa saba na pembe kumi. Basi, je! yeye ni hayawani-mwitu yule yule ambaye Yohana aliona mapema zaidi, ambaye pia alikuwa na vichwa saba na pembe kumi? (Ufunuo 13:1) La, ziko tofauti. Hayawani-mwitu huyu ni rangi-nyekundu-nyangavu na, tofauti na hayawani-mwitu aliyetangulia, hasemwi kuwa ana mataji. Badala ya yeye kuwa na majina ya kufuru juu ya vichwa vyake saba tu, yeye ‘anajaa majina ya kufuru.’ Hata hivyo, lazima pawe na uhusiano kati ya hayawani-mwitu mpya na yule aliyetangulia; mifanano kati yao ni mingi mno kuwa ya nasibu.

      16. Ni nini utambulisho wa huyo hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu, na imetaarifiwa nini kwa habari ya kusudi lake?

      16 Basi, hayawani-mwitu mpya rangi-nyekundu-nyangavu ni nini? Yeye ni lazima awe ule mfano wa hayawani-mwitu ambao ulitokezwa kwa himizo la hayawani-mwitu Uingereza-Amerika aliyekuwa na pembe mbili mithili ya mwana-kondoo. Baada ya mfano huo kuwa umefanywa, huyo hayawani-mwitu mwenye pembe mbili aliruhusiwa kuupa pumzi huo mfano wa hayawani-mwitu. (Ufunuo 13:14, 15) Yohana anaona sasa mfano ulio hai, unaopumua. Ni picha ya tengenezo la Ushirika wa Mataifa ambalo hayawani-mwitu mwenye pembe mbili alileta kwenye uhai katika 1920. Rais Wilson wa U.S. alikuwa na njozi ya kwamba Ushirika huo “ungekuwa baraza la kutolea watu wote haki na kufutilia mbali milele tisho la vita.” Lilipofufuliwa baada ya vita ya ulimwengu ya pili likiwa Umoja wa Mataifa, kusudi la katiba yalo lilikuwa “kudumisha amani na usalama wa kimataifa.”

      17. (a) Ni katika njia gani huyo hayawani-mwitu wa ufananisho rangi-nyekundu-nyangavu anajaa majina ya kufuru? (b) Ni nani anayempanda huyo hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu? (c) Dini ya Kibabuloni ilijifungamanishaje na Ushirika wa Mataifa na mwandamizi wao pale pale mwanzoni?

      17 Ni katika njia gani huyu hayawani-mwitu wa ufananisho anajaa majina ya kufuru? Katika njia ya kwamba wanadamu wameisimamisha sanamu hii ya kuabudiwa na mataifa mengi ikiwa kibadala cha Ufalme wa Mungu—itimize jambo ambalo Mungu husema ni Ufalme wake pekee unaoweza kutimiza. (Danieli 2:44; Mathayo 12:18, 21) Ingawa hivyo, jambo lenye kutokeza kuhusu njozi ya Yohana ni kwamba, Babuloni Mkubwa anapanda hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu. Kupatana na ukweli wa unabii, dini ya Kibabuloni, hasa katika Jumuiya ya Wakristo, imejifungamanisha yenyewe na Ushirika wa Mataifa na mwandamizi wao. Mapema kama Desemba 18, 1918, shirika ambalo sasa linajulikana kuwa Baraza la Taifa la Makanisa ya Kristo katika Amerika lilipitisha julisho-wazi lililojulisha wazi kwa sehemu hivi: “Ushirika kama huo si manufaa ya kisiasa tu; badala ya hivyo ni wonyesho wa kisiasa wa Ufalme wa Mungu duniani. . . . Kanisa linaweza kutoa roho ya nia njema, ambayo bila hiyo hakuna Ushirika wa Mataifa unaoweza kudumu. . . . Ushirika wa Mataifa una mizizi katika Gospeli. Kama Gospeli, lengo lao ni ‘amani duniani, nia njema kuelekea wanadamu.’”

      18. Viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo walionyeshaje uungaji-mkono wao kwa Ushirika wa Mataifa?

      18 Katika Januari 2, 1919, San Fransisco Chronicle lilikuwa na kichwa kikuu cha habari kwenye ukurasa wa kwanza: “Papa Asihi Ukubaliwe Ushirika wa Maitafa wa Wilson.” Katika Oktoba 16, 1919, ombi rasmi lililotiwa sahihi na makasisi wa vikundi mashuhuri 14,450 lilitolewa kwenye Seneti ya U.S., kuhimiza baraza hilo ‘liidhinishe mwafaka wa amani wa Paris uliotia ndani agano la ushirika wa mataifa.’ Ingawa Seneti ya U.S. ilishindwa kuidhinisha mwafaka huo, viongozi wa Jumuiya ya Wakristo waliendelea kufanya kampeni kwa ajili ya huo Ushirika. Na Ushirika huo ulizinduliwaje? Habari iliyopelekwa kutoka Uswisi, yenye tarehe ya Novemba 15, 1920, ilisomwa hivi: “Kufunguliwa kwa kusanyiko la kwanza la Ushirika wa Mataifa kulitangazwa kwenye saa tano asubuhi hii kwa kupigwa kengele zote za kanisa katika Geneva.”

      19. Wakati hayawani-mwitu alipotokea, jamii ya Yohana ilichukua mwendo gani wa tendo?

      19 Je! jamii ya Yohana, kikundi pekee duniani ambacho kilikubali kwa hamu nyingi Ufalme wa Kimesiya uliokuwa ukija, kilishiriki pamoja na Jumuiya ya Wakristo katika kumpa shikamoo huyo hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu? Mbali kabisa na hilo! Jumapili, Septemba 7, 1919, mkusanyiko wa watu wa Yehova kwenye Sida Pointi, Ohaiyo, ulikuwa na hotuba ya watu wote iliyokuwa na kichwa “Tumaini kwa Binadamu Wenye Kutaabika.” Siku iliyofuata, Star-Journal ya Sandusky iliripoti kwamba J. F. Rutherford, katika kuhutubia watu karibu 7,000, alikuwa “amesisitiza kwamba kutopendezwa kwa Bwana ni hakika kutajilia Ushirika . . . kwa sababu viongozi wa kidini—Wakatoliki na Waprotestanti—wakidai kuwa wawakilishi wa Mungu, wameacha mpango wake na wakakubali Ushirika wa Mataifa, wakiushangilia kuwa wonyesho wa kisiasa wa ufalme wa Kristo duniani.”

      20. Ni kwa sababu gani ilikuwa kufuru viongozi wa kidini kushangilia Ushirika wa Mataifa kuwa “wonyesho wa kisiasa wa Ufalme wa Mungu duniani”?

      20 Ushinde wenye kusikitisha sana wa Ushirika wa Mataifa ulipaswa kuashiria viongozi wa kidini kwamba vyombo hivyo vyenye kufanywa na mwanadamu si sehemu ya Ufalme wa Mungu duniani. Ni kufuru kama nini kudai hivyo! Hufanya ionekane kana kwamba Mungu alishiriki kufanyiza Ushirika wa Mataifa ambao ni kazi ya ovyo sana. Kwa habari ya Mungu “utendaji wake ni mkamilifu.” Ufalme wa Yehova wa kimbingu chini ya Kristo—wala si muungano wa wanasiasa wenye kuzozana, wengi wao wakiwa hawaitikadi kuwako kwa Mungu—ndiyo njia ambayo kwayo yeye ataleta amani na kufanya penzi lake lifanywe duniani kama katika mbingu.—Kumbukumbu 32:4; Mathayo 6:10, NW.

      21. Ni nini kinachoonyesha kwamba kahaba mkubwa anaunga mkono na kusifu mno mwandamizi wa Ushirika, Umoja wa Mataifa?

      21 Namna gani mwandamizi wa Ushirika, Umoja wa Mataifa? Tangu mwanzo wao, baraza hili limekuwa na kahaba akilipanda mgongoni mwalo, akishirikiana nalo waziwazi na akijaribu kuongoza liendako. Mathalani, katika ukumbusho wa mwaka wao wa 20 katika Juni 1965, wawakilishi wa Kanisa Katoliki la Roma na Kanisa Orthodoksi la Mashariki, pamoja na Waprotestanti, Wayahudi, Wahindu, Wabuddha, na Waislamu—waliosemekana kuwakilisha idadi ya watu wa dunia elfu mbili milioni—walikusanyika katika San Francisco kusherehekea uungaji-mkono na usifaji wao wa UM. Alipozuru UM Oktoba 1965, Papa Paul 6 alieleza habari zao kuwa “hilo tengenezo la kimataifa kubwa zaidi ya yote” na akaongeza: “Vikundi vya watu wa dunia vinategemea Umoja wa Mataifa kuwa ndilo tumaini la mwisho la itifaki na amani.” Mgeni mwingine wa kipapa, Papa John Paul 2, akihutubia UM katika Oktoba 1979, alisema: “Mimi natumaini Umoja wa Mataifa utadumu daima ukiwa ndilo baraza kuu la amani na haki.” Kwa uwazi sana, huyo papa alimtaja Yesu Kristo na Ufalme wa Mungu mara chache sana katika hotuba yake. Wakati wa ziara yake United States katika Septemba 1987, kama ilivyoripotiwa na The New York Times, “John Paul alisema kirefu juu ya daraka chanya la Umoja wa Mataifa katika kuendeleza . . . ‘ushirikiano mpya wa ulimwenguni pote.’”

      Jina, Fumbo

      22. (a) Ni hayawani wa aina gani ambaye kahaba mkubwa amechagua kupanda? (b) Yohana anaelezaje habari ya kahaba wa ufananisho Babuloni Mkubwa?

      22 Karibuni mtume Yohana atajifunza kwamba kahaba mkubwa amechagua kupanda hayawani hatari. Ingawa hivyo, kwanza uangalifu wake wageukia Babuloni Mkubwa mwenyewe. Yeye amepambwa kitajiri, lakini, oh, jinsi anavyokirihisha! “Na huyo mwanamke alikuwa amepambwa zambarau na nyekundu-nyangavu na alikuwa amerembwa kwa dhahabu na jiwe la thamani na lulu na katika mkono wake alikuwa na kikombe cha dhahabu ambacho kilikuwa kimejaa vitu vya kunyarafisha na vitu visivyo safi vya uasherati wake. Na juu ya kipaji cha uso wake paliandikwa jina, fumbo: ‘Babuloni Mkubwa, mama ya makahaba na ya vitu vya kunyarafisha vya dunia.’ Na mimi nikaona kwamba mwanamke alikuwa amelewa damu ya watakatifu na damu ya mashahidi wa Yesu.”—Ufunuo 17:4-6a, NW.

      23. Ni jina gani kamili la Babuloni Mkubwa, na maana yalo ni nini?

      23 Kama ilivyokuwa desturi katika Roma ya kale, malaya huyu anatambuliwa kwa jina lililo juu ya kipaji cha uso wake.d Ni jina refu: “Babuloni Mkubwa, mama ya makahaba na ya vitu vya kunyarafisha vya dunia.” Jina hilo ni “fumbo,” jambo fulani lenye maana iliyofichwa. Lakini kwa wakati wa Mungu fumbo hilo litafafanuliwa. Kwa kweli, malaika anampa Yohana habari ya kutosha kuruhusu watumishi wa Yehova leo wafahamu umaana kamili wa jina hili lenye maelezo. Sisi tunatambua Babuloni Mkubwa kuwa dini bandia yote. Yeye ndiye “mama ya makahaba” kwa sababu dini bandia zote moja moja katika ulimwengu, kutia ndani mafarakano katika Jumuiya ya Wakristo, ni kama mabinti wake, zikimwiga yeye katika kufanya ukahaba wa kiroho. Yeye pia ni mama ya “vitu vya kunyarafisha” katika njia ya kwamba yeye amezaa wazao wenye makuruhu kama vile ibada ya sanamu, uwasiliano na roho, kupiga ramli, unajimu, uaguzi wa kutazama vitanga vya mikono, kudhabihu binadamu, umalaya wa hekaluni, ulevi katika kuheshimu miungu bandia, na mazoea mengine machafu.

      24. Ni kwa sababu gani inafaa kwamba Babuloni Mkubwa amevalia “zambarau na rangi-nyekundu-nyangavu” na “amepambwa kwa dhahabu na jiwe la thamani na lulu”?

      24 Babuloni Mkubwa amevalia “zambarau na nyekundu-nyangavu,” rangi za jamaa ya kifalme, na “amerembwa kwa dhahabu na jiwe la thamani na lulu.” Inafaa kama nini! Fikiria tu yale majengo yote mazuri mno, sanamu-umbo na taswira azizi, aikoni zenye bei sana, na vikorokoro vingine vya kidini, pamoja na kiasi ambacho ni vigumu kuitikadi cha mali na pesa, kisichohesabika ambacho dini za ulimwengu huu zimerundika. Iwe ni katika Vatikani, katika milki ya uevanjeli wa TV ambao kitovu chayo ni United States, au katika misikiti na mahekalu yenye kuvutia ya Mashariki, Babuloni Mkubwa amerundika kama tungamo—na nyakati nyingine akapoteza—ukwasi mwingi mno.

      25. (a) Ni nini kinachofananishwa na “kikombe cha dhahabu ambacho kilijaa vitu vya kunyarafisha?” (b) Ni katika maana gani kahaba wa ufananisho amelewa?

      25 Tazama sasa alicho nacho kahaba huyu mkononi mwake. Haikosi Yohana alitweta kwa mshangao kukiona—kikombe cha dhahabu “kimejaa vitu vya kunyarafisha na vitu visivyo safi vya uasherati wake”! Hiki ndicho kikombe ambacho ndani yacho mna “divai ya kasirani ya uasherati wake” ambacho kwa hicho amefanya mataifa yote yalewe. (Ufunuo 14:8; 17:4) Kwa nje kinaonekana kuwa chenye utajiri, lakini yaliyomo ni yenye kunyarafisha, si safi. (Linga Mathayo 23:25, 26.) Ndani kina mazoea yote machafu na uwongo mwingi ambao huyo kahaba mkubwa ametumia kutongoza mataifa na kuwaleta chini ya uvutano wake. Lenye makuruhu hata kuchukiza zaidi, Yohana anaona kwamba huyo kahaba mwenyewe amelewa, amekunywa sana damu ya watumishi wa Mungu! Kwa kweli, baadaye sisi tunasoma kwamba “katika yeye ilipatikana damu ya manabii na ya watakatifu na ya wale wote ambao wamechinjwa juu ya dunia.” (Ufunuo 18:24, NW) Ni hatia ya damu kubwa mno kama nini!

      26. Kuna ithibati gani ya hatia ya damu upande wa Babuloni Mkubwa?

      26 Kwa muda wa karne zilizopita, milki ya ulimwengu ya dini bandia imemwaga damu nyingi kama bahari. Mathalani, katika Japani ya zamani za kale, mahekalu katika Kyoto yaligeuzwa kuwa ngome, na watawa-mashujaa-vita, wakiliitia “jina takatifu la Buddha,” walipigana vita mpaka barabara zikawa nyekundu kwa damu. Katika karne ya 20, viongozi wa kidini walipiga miguu wakiwa pamoja na majeshi ya nchi zao, na walichinjana, kukiwa na hasara ya angalau maisha milioni mia moja. Katika Oktoba 1987 Nixon aliyekuwa rais wa U.S. alisema: “Karne ya 20 imekuwa ndiyo yenye damu nyingi zaidi ya zote katika historia. Watu zaidi wameuawa katika vita vya karne hii kuliko katika vita vyote vilivyopiganwa kabla ya karne hii kuanza.” Dini za ulimwengu zimehukumiwa vibaya na Mungu kwa sababu ya ushiriki wazo katika yote haya; Yehova hukirihi “mikono ambayo inamwaga damu isiyo na hatia.” (Mithali 6:16, 17, NW) Mapema zaidi, Yohana alisikia kilio kutoka madhabahu: “Ni mpaka lini, Bwana Mwenye Enzi Kuu mtakatifu na wa kweli, wewe unajizuia usihukumu na kulipiza kisasi damu yetu juu ya wale ambao wanakaa juu ya dunia?” (Ufunuo 6:10, NW) Babuloni Mkubwa, mama ya makahaba na ya vitu vya kunyarafisha vya dunia, atahusika sana ujapo wakati wa kujibu swali hilo.

      [Maelezo ya Chini]

      a Akionyesha chanzo kisicho cha Kikristo cha mengi ya mafundisho, sherehe, na mazoea ya Jumuiya ya Wakristo iliyoasi imani, John Henry Newman kardinali Mkatoliki wa karne ya 19 aliandika hivi katika kichapo chake Essay on the Development of Christian Doctrine: “Utumizi wa mahekalu, na hayo yakiwa yamewekwa wakfu kwa watakatifu fulani, na pindi nyingine yakiwa yametiwa madoido ya matawi ya miti; uvumba, mataa, na mishumaa; matoleo ya kushuhudia wakfu baada ya kupata nafuu ya ugonjwa; maji matakatifu; nyumba za kutunzia mayatima na wenye shida; sikukuu na misimu, tumizi la kalenda, miandamano, kubarikia mashamba; mavazi ya makasisi, kipara utosini, pete katika ndoa, kugeukia Mashariki, mifano kwenye tarehe ya baadaye, labda wimbo wa kieklesia, na Kyrie Eleison [wimbo “Bwana, Urehemu”], chanzo cha yote ni upagani, yakatakaswa kwa kukubaliwa ndani ya Kanisa.”

      Badala ya kutakasa ibada ya sanamu kama hiyo, “Yehova Mweza Yote” huonya Wakristo “Ondokeni kutoka miongoni mwao, na kujitenga nyinyi wenyewe, . . . na acheni kabisa kugusa kitu kisicho safi.”—2 Wakorintho 6:14-18, NW.

      b Kitabu cha historia cha William L. Shirer The Rise and Fall of the Third Reich hutaarifu kwamba von Papen alikuwa “mwenye daraka zaidi ya mwingine yeyote katika Ujeremani la Hitla kupata mamlaka.” Katika Januari 1933 aliyekuwa chansela wa Ujeremani von Schleicher alikuwa amesema hivi juu ya von Papen: “Yeye alithibitika kuwa aina ya haini ambaye kando yake Yudasi Iskariote ni mtakatifu.”

      c Akihutubia Koleji ya Mandragone Mei 14, 1929, Papa Pius 11 alisema kwamba yeye angeshauriana na Ibilisi mwenyewe ikiwa faida ya nafsi nyingi ingetaka hivyo.

      d Linga maneno ya Seneka mtungaji-vitabu Mroma kwa kuhani wa kike mwenye kukosa (kama yalivyonukuliwa na Swete): “Wewe msichana, ulisimama, katika nyumba ya sifa mbaya . . . jina lako lilining’inia kutoka kipaji cha uso wako; ulikubali fedha kwa fedheha yako.”—Controv. i, 2.

      [Sanduku katika ukurasa wa 237]

      Churchill Afichua ‘Ukahaba’

      Katika kitabu chake The Gathering Storm (1948), Winston Churchill huripoti kwamba Hitla alimweka rasmi Franz von Papen kuwa waziri wa Ujeremani kwenye Vienna ili “kudhoofisha au kuvuta watu mashuhuri katika siasa za Austria.” Churchill hunukuu waziri wa U.S. katika Vienna kuwa akisema hivi juu ya von Papen: “Kwa jinsi ya ujasiri zaidi sana na ya kudharau zaidi sana . . . Papen aliendelea kuniambia kwamba . . . yeye alikusudia kutumia sifa yake akiwa Mkatoliki mwema apate uvutano pamoja na Waaustria kama Kardinali Innitzer.”

      Baada ya Austria kukubali ushinde na vikosi vya Hitla vyenye kushambulia ghafula vikiwa vimepiga gwaride kuingia Vienna, Innitzer kardinali Mkatoliki aliamuru kwamba makanisa yote ya Austria yapandishe bendera ya swastika, yapige kengele zayo, na yatoe sala kwa ajili ya Adolf Hitla kwa heshima ya ukumbusho wa siku ya kuzaliwa kwake.

      [Sanduku/Picha katika ukurasa wa 238]

      Chini ya kichwa hiki, makala inayofuata ilitokea katika chapa ya kwanza ya The New York Times ya Desemba 7, 1941:

      ‘SALA YA VITA’ KWA AJILI YA REICH

      Maaskofu wa Kikatoliki katika Fulda Waomba Baraka na Ushindi

      Kongamano la Maaskofu wa Kikatoliki wa Ujeremani lililokusanyika katika Fulda limependekeza ianzishwe ‘sala ya vita’ maalumu ambayo itasomwa mwanzoni na mwishoni mwa ibada zote za kimungu. Sala hiyo husihi Mungu abariki silaha za Ujeremani kwa ushindi na kutoa himaya kwa maisha na afya ya askari-jeshi wote. Maaskofu hao waliwaagiza zaidi makasisi wa Kikatoliki waweke na kukumbuka katika mahubiri maalumu ya Jumapili angalau mara moja kwa mwezi askari-jeshi Wajeremani ‘barani, baharini na hewani.’”

      Makala hii iliondolewa kwenye chapa za baadaye za nyusipepa hiyo. Desemba 7, 1941, ndiyo siku Japani, nchi fungamani na Ujeremani, iliposhambulia meli za U.S. kwenye Pearl Harbor.

      [Picha katika ukurasa wa 244]

      “Majina ya Kufuru”

      Hayawani-mwitu mwenye pembe mbili alipoendeleza Ushirika wa Mataifa baada ya Vita ya Ulimwengu 1, hawara zake wa kidini walitafuta mara hiyo kulipa tendo hilo idhini ya kidini. Kama tokeo, tengenezo jipya la amani ‘likajawa na majina ya kufuru.’

      “Ukristo unaweza kuandaa nia njema, nguvu-msukumo inayotendesha ushrika [wa mataifa], na hivyo kugeuza mwafaka huo kutoka kipande cha karatasi tu na kuwa chombo cha ufalme wa Mungu.”—The Christian Century, U.S.A., Juni 19, 1919, ukurasa 15.

      “Wazo la Ushirika wa Mataifa ni mpanuo kuelekea mahusiano ya kimataifa wa wazo la Ufalme wa Mungu ukiwa utaratibu wa ulimwengu wa nia njema. . . . Ndicho kitu ambacho Wakristo wote husali kwa ajili yacho wanaposema, ‘Ufalme wako uje.”—The Christian Century, U.S.A., Septemba 25, 1919, ukurasa 7.

      “Saruji ya Ushirika wa Mataifa ni Damu ya Kristo.”—Dakt. Frank Crane, Mhudumu Mprotestanti, U.S.A.

      Baraza [la Taifa la Makanisa ya Kongrigeshonali] huunga mkono Agano [la Ushirika wa Mataifa] kuwa ndicho chombo pekee cha kisiasa kinachopatikana sasa ambacho kwacho Roho ya Yesu Kristo inaweza kupata mweneo mpana zaidi katika utumizi wenye mafaa kwenye mambo ya mataifa.”—The Congregationalist and Advance, U.S.A., Novemba 6, 1919, ukurasa 642.

      “Kongamano lataka Wamethodisti wote wategemeze na kuendeleza sana mawazo bora [ya Ushirika wa Mataifa] kama yanavyoonyeshwa na wazo la Mungu Baba na watoto wa Mungu wa kidunia.”—Kanisa la Kimethodisti la Wesley, Uingereza.

      “Tunapoyafikiria malengo yale, mawezekano na maazimio ya mwafaka huu, sisi tunaona kwamba una moyo wa mafundisho ya Yesu Kristo: Ufalme wa Mungu na uadilifu wake . . . Si kitu kilicho punde ya huo.”—Mahubiri ya Askofu Mkuu wa Kantabari wakati wa kufunguliwa kwa Kusanyiko la Ushirika wa Mataifa katika Geneva, Desemba 3, 1922.

      “Shirika la ule Ushirika wa Mataifa katika nchi hii lina haki takatifu ile ile kama sosaiti ya kimisheni yoyote ya ufadhili-binadamu, kwa sababu kwa wakati uliopo ndicho chombo chenye matokeo zaidi sana cha utawala wa Kristo Mwana-Mfalme wa amani miongoni mwa mataifa.”—Dakt. Garvie, mhudumu Mkongrigeshonali, Uingereza.

      [Ramani katika ukurasa wa 236]

      (Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)

      Mafundisho bandia yanayoitikadiwa kotekote ulimwenguni chanzo chayo ni katika Babuloni

      Babuloni

      Utatu au utatuutatu wa miungu

      Nafsi ya kibinadamu huishi baada ya kifo

      Uwasiliano na roho—kuongea na “wafu”

      Utumizi wa mifano katika ibada

      Utumizi wa ulozi kutuliza roho waovu

      Utawala wa ukuhani wenye nguvu nyingi

      [Picha katika ukurasa wa 239]

      Babuloni wa kale aliketi juu ya maji mengi

      [Picha katika ukurasa wa 239]

      Kahaba mkubwa leo pia huketi juu ya “maji mengi”

      [Picha katika ukurasa wa 241]

      Babuloni Mkubwa anaketi juu ya hayawani-mwitu hatari

      [Picha katika ukurasa wa 242]

      Kahaba wa kidini amefanya uasherati na wafalme wa dunia

      [Picha katika ukurasa wa 245]

      Mwanamke “amelewa damu ya watakatifu”

  • Fumbo Lenye Kutia Hofu Lafumbuliwa
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Sura ya 34

      Fumbo Lenye Kutia Hofu Lafumbuliwa

      1. (a) Yohana anatendaje kama itikio anapoona kahaba mkubwa na mpandwaji wake mwenye kutia hofu, na kwa nini? (b) Jamii ya Yohana inatendaje leo kama itikio, matukio yanapokunjuka katika utimizo wa njozi ya kiunabii?

      TENDO-MWITIKIO la Yohana ni nini anapomwona “kahaba mkubwa” na mpandwaji wake mwenye kutia hofu? Yeye mwenyewe ajibu: “Basi, nilipoona yeye mimi nilistaajabu kwa staajabu kubwa.” (Ufunuo 17:6b, NW) Mawazo vivi hivi tu ya kibinadamu hayangeweza kutunga mwono kama huo. Hata hivyo ndio huo—mbali kule jangwani—malaya mpujufu akimpanda hayawani-mwitu wa kutisha mwenye rangi-damu-nyangavu! (Ufunuo 17:3) Jamii ya Yohana leo pia hustaajabu kwa staajabu kubwa matukio yanapokunjuka katika utimizo wa njozi ya kiunabii. Kama watu wa ulimwengu wangeweza kuiona, wao wangepaaza sauti kusema, ‘Haisadikiki!’ na watawala wa ulimwengu wangerudisha mwangwi wakisema, ‘Haifikiriki!’ Lakini njozi hiyo inakuwa uhalisi wenye kugutusha katika siku zetu. Tayari watu wa Mungu wamekuwa na ushiriki wenye kutokeza katika utimizo wa njozi hiyo, na hiyo inawahakikishia kwamba unabii huo utasonga mbele moja kwa moja mpaka upeo wao wenye kupiga butaa.

      2. (a) Katika kuitikia mshangao mkubwa wa Yohana, malaika anamwambia nini? (b) Jamii ya Yohana imefunuliwa nini, na hilo limefanywaje?

      2 Malaika anaona mshangao mkubwa wa Yohana. “Na hivyo,” Yohana aendelea, “malaika akasema kwa mimi: ‘Kwa nini wewe ulistaajabu? Mimi nitakuambia fumbo la mwanamke na la hayawani-mwitu ambaye anabeba yeye na ambaye ana vichwa saba na pembe kumi.’” (Ufunuo 17:7, NW) Aha, sasa malaika atalifumbua fumbo! Yeye amfafanulia Yohana mwenye kukodoa macho nyuso mbalimbali za njozi na matukio ya kidrama yanayokaribia kukunjuka. Hali kadhalika, inapotumikia chini ya mwelekezo wa kimalaika leo, jamiii ya Yohana yenye kutazama imefunuliwa uelewevu wa huo unabii. Je! “kufasiri si kazi ya Mungu?” Kama Yosefu mwaminifu, sisi tunaitikadi kwamba ni yake. (Mwanzo 40:8; linga Danieli 2:29, 30.) Watu wa Mungu wamewekwa kana kwamba wako katikati ya jukwaa, Yehova anapowafasiria maana ya njozi na matokeo yayo juu ya maisha zao. (Zaburi 25:14) Kwa wakati barabara, yeye amewafungulia uelewevu wao fumbo la mwanamke na hayawani-mwitu.—Zaburi 32:8.

      3, 4. (a) Ni hotuba gani ya watu wote iliyotolewa na N. H. Knorr katika 1942, nayo ilimtambulishaje hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu? (b) Ni maneno gani ambayo malaika alisema kwa Yohana yaliyozungumzwa na N. H. Knorr?

      3 Kutoka Septemba 18 kufika 20, 1942, wakati wa upeo wa Vita ya Ulimwengu 2, Mashahidi wa Yehova katika United States walikuwa na Ulimwengu Mpya wa Kitheokrasi Kusanyiko. Jiji kuu la kusanyiko, Cleveland, Ohaiyo, lilifunganishwa kwa waya za simu na majiji mengine zaidi ya 50 ya mkusanyiko, kukiwa na kilele cha hadhirina 129,699. Mahali ambako hali za wakati wa vita ziliruhusu, mikusanyiko mingine ilirudia programu hiyo kuzunguka ulimwengu. Wakati ule, wengi wa watu wa Yehova walitaraji kwamba vita hiyo ingeongezeka na kuwa vita ya Mungu ya Har–Magedoni; kwa sababu hiyo kile kichwa cha hotuba ya watu wote, “Amani—Je! Inaweza Kudumu?,” kiliamsha udadisi mwingi. N. H. Knorr, msimamizi mpya wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi angewezaje kuthubutu kuongea juu ya amani wakati kinyume kabisa ndilo jambo lililoelekea kuwa akibani kwa ajili ya mataifa?a Sababu ilikuwa kwamba jamii ya Yohana ilikuwa ikitoa “zaidi ya uangalifu wa kawaida” kwenye Neno la kiunabii la Mungu.—Waebrania 2:1; 2 Petro 1:19, NW.

      4 Hotuba “Amani—Je! Inaweza Kudumu?” ilitupa nuru gani juu ya unabii? Akitambulisha waziwazi hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu wa Ufunuo 17:3 kuwa Ushirika wa Mataifa, N. H. Knorr aliendelea kuzungumzia mwendo wao wenye msukosuko juu ya msingi wa maneno yafuatayo ya malaika kwa Yohana: “Hayawani-mwitu ambaye wewe uliona alikuwako, lakini hayuko, na bado yu karibu kupanda atoke ndani ya abiso, na yeye anapaswa kwenda zake ndani ya uharibifu.”—Ufunuo 17:8a, NW.

      5. (a) Ni jinsi gani kwamba “hayawani-mwitu . . . alikuwako” na kisha “hayuko”? (b) N. H. Knorr alijibuje swali “Je! Ushirika utabaki katika shimo?”

      5 “Hayawani-mwitu . . . alikuwako.” Ndiyo, alikuwa amekuwako akiwa Ushirika wa Mataifa kutoka Januari 10, 1920, na kuendelea, kukiwa na mataifa 63 yenye kushiriki kwa wakati mmoja au mwingine. Lakini, kwa zamu, Japani, Ujeremani, na Italia zilijiondoa, na nchi zilizokuwa Muungano wa Sovieti ziliondolewa kutoka Ushirika huo. Katika Septemba 1939 dikteta Mnazi wa Ujeremani alianzisha Vita ya Ulimwengu 2.b Ukiwa umeshindwa kuendeleza amani katika ulimwengu, Ushirika wa Mataifa ulitumbukia kabisa ndani ya abiso ya kutotenda. Kufikia 1942 ulikuwa haupo kabisa. Wala kabla ya hapo wala kwenye tarehe fulani ya baadaye Yehova hakufasiria watu wake kina kamili cha maana ya njozi hiyo, ila kwenye wakati huo hasa wenye hatari! Kwenye Ulimwengu Mpya wa Kitheokrasi Kusanyiko, N. H. Knorr angeweza kujulisha wazi, kupatana na unabii, kwamba “hayawani-mwitu . . . hayuko.” Kisha akauliza swali, “Je! Ushirika utabaki katika shimo?” Akinukuu Ufunuo 17:8, NW, yeye akajibu: “Ushirika wa mataifa ya kilimwengu utainuka tena.” Na ndivyo ikathibitika kuwa hasa—katika kutetea ukweli wa Neno la Yehova la kiunabii!

      Kupanda Kutoka Abiso

      6. (a) Ni lini hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu alipopanda kutoka abiso, na kwa jina gani jipya? (b) Ni kwa nini kwa kweli Umoja wa Mataifa ni uhuisho wa hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu?

      6 Hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu alipanda kweli kweli kutoka katika abiso. Katika Juni 26, 1945, kukiwa na kishindo cha sherehe ya vigelegele katika San Francisco, U.S.A., mataifa 50 yalipiga kura kukubali Katiba ya tengenezo la Umoja wa Mataifa. Baraza hili lilipaswa “kudumisha amani na usalama wa kimataifa.” Kulikuwako mifanano mingi kati ya Ushirika na UM. The World Book Encyclopedia hueleza: “Katika njia fulani, UM hushabihi Ushirika wa Mataifa, ambao ulipangwa kitengenezo baada ya Vita ya Ulimwengu 1 . . . Mengi ya mataifa yaliyoasisi UM yalikuwa pia yameasisi ule Ushirika. Kama Ushirika, UM ulisimamishwa kusaidia kutunza amani kati ya mataifa. Ala kuu za UM zafanana sana na zile za Ushirika.” Basi, UM kwa kweli ni uhuisho wa hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu. Uanachama wao wa mataifa yapatayo 190 unazidi kwa mbali sana ule wa Ushirika wenye mataifa 63; umechukua pia madaraka makubwa zaidi ya yale ya mtangulizi wao.

      7. (a) Ni katika njia gani wakaaji wa dunia wamestaajabu kwa kusifu mno huyo hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu aliyehuishwa? (b) Ni mradi gani ambao umetatiza UM, naye katibu mkuu wao alisema nini kwa habari hii?

      7 Mwanzoni, matumaini makubwa yalionyeshwa kwa ajili ya UM. Hiyo ilikuwa katika utimizo wa maneno haya ya malaika: “Na wakati wao waona jinsi hayawani-mwitu alikuwako, lakini hayuko, na bado atakuwapo, wale ambao hukaa juu ya dunia watastaajabu kwa kusifu mno, lakini majina yao hayajaandikwa juu ya hati-kunjo ya uhai tangu kuasisiwa kwa ulimwengu.” (Ufunuo 17:8b, NW) Wakaaji wa dunia wamesifu mno dude jipya hili, linalotenda kutoka makao makuu yalo yenye fahari kwenye East River wa New York. Lakini amani ya kweli na usalama vimetatiza UM. Katika sehemu kubwa ya karne ya 20, amani ya ulimwengu ilidumishwa tu kwa tisho la “angamizano hakika,” nayo mashindano ya kuunda silaha yameendelea kuongezeka kwa kadiri kubwa mno. Baada ya jitihada ya Umoja wa Mataifa ya miaka karibu 40, aliyekuwa katibu mkuu wao, Javier Pérez de Cuéllar, aliomboleza hivi katika 1985: “Sisi tunaishi katika enzi nyingine ya washupavu, na sisi hatujui la kufanya juu ya hilo.”

      8, 9. (a) Ni kwa nini UM hauna jawabu kwa matatizo ya ulimwengu, nao utapatwa na nini kulingana na amri ya Mungu? (b) Ni kwa nini waasisi na wasifaji wa UM hawakuandikisha majina yao katika “hati-kunjo ya uhai” ya Mungu? (c) Ufalme wa Yehova utatimiza jambo gani kwa kufaulu?

      8 UM hauna jawabu. Na kwa nini? Kwa sababu Mpaji uhai wa aina ya binadamu yote siye mpaji-uhai wa UM. Urefu wa maisha yao utakuwa mfupi, kwa kuwa kulingana na amri ya Mungu, ‘wapaswa kwenda zao ndani ya uharibifu.’ Waasisi na wasifaji mno wa UM hawakuandikisha majina yao katika hati-kunjo ya uhai ya Mungu. Watu wenye dhambi, wenye kufa, wengi wao wakiwa wadhihaki wa jina la Mungu, wangewezaje kufanikiwa kupata kupitia UM kitu ambacho Yehova Mungu amejulisha wazi kwamba yeye yu karibu kutimiza, si kwa njia za kibinadamu, bali kupitia Ufalme wa Kristo wake?—Danieli 7:27; Ufunuo 11:15.

      9 Kwa kweli UM ni kitu bandia chenye makufuru cha Ufalme wa Kimesiya wa Mungu kupitia Yesu Kristo, Mwana-Mfalme wa Amani wake—ambaye utawala wake wa kifalme hautakuwa na mwisho. (Isaya 9:6, 7, NW) Hata kama UM ungeweza kutiatia kama viraka amani fulani ya kitambo, vita vingefyatuka tena. Hiyo ni asili ya watu wenye dhambi. “Majina yao hayajaandikwa juu ya hati-kunjo ya uhai tangu kuasisiwa kwa ulimwengu.” Ufalme wa Yehova kupitia Kristo hautasimamisha tu amani ya milele duniani bali, juu ya msingi wa dhabihu ya ukombozi ya Yesu, utainua wafu, waadilifu na wasio waadilifu ambao wamo katika kumbukumbu la Mungu. (Yohana 5:28, 29; Matendo 24:15) Hii inatia ndani kila mmoja ambaye amebaki akiwa imara ijapokuwa mashambulizi ya Shetani na mbegu yake, na wengine ambao wangali watajionyesha wenyewe kuwa watiifu. Kwa wazi, hati-kunjo ya uhai ya Mungu haitakuwa kamwe na majina ya wafuasi washupavu wa Babuloni Mkubwa au ya wowote wanaoendelea kuabudu hayawani-mwitu.—Kutoka 32:33, NW; Zaburi 86:8-10; Yohana 17:3; Ufunuo 16:2; 17:5.

      Amani na Usalama —Tumaini la Bure

      10, 11. (a) UM ulipiga mbiu ya nini katika 1986, na itikio lilikuwa nini? (b) Ni “jamaa za kidini” ngapi zilizokusanyika katika Assisi, Italia, kusali kwa ajili ya amani, na je! Mungu anajibu sala kama hizo? Fafanua.

      10 Katika jitihada za kutegemeza matumaini ya aina ya binadamu, Umoja wa Mataifa ulipiga mbiu ya 1986 kuwa “Mwaka wa Amani ya Kimataifa,” ukiwa na kichwa “Kulinda Salama Amani na Wakati Ujao wa Binadamu.” Mataifa yenye kupiga vita yaliombwa yalaze silaha zayo, angalau kwa mwaka mmoja. Itikio layo lilikuwa nini? Kulingana na ripoti iliyotolewa na Taasisi ya Utafiti wa Amani ya Kimataifa, watu wapatao milioni tano walikufa kwa sababu ya vita wakati wa 1986 pekee! Ingawa sarafu kadhaa za pekee na stampu za mwadhimisho zilitolewa, mataifa yaliyo mengi yalifanya kidogo sana kwa habari ya kufuatia wazo bora la amani katika mwaka huo. Hata hivyo, dini za ulimwengu—zikitamani sikuzote kuafikiana na UM—zilianza kutangaza mwaka huo kwa njia mbalimbali. Katika Januari 1, 1986, Papa John Paul 2 alisifu kazi ya UM na akaweka wakfu mwaka mpya kwa ajili ya amani. Na katika Oktoba 27, akakusanya viongozi wa nyingi za dini za ulimwengu katika Assisi, Italia, ili kusali kwa ajili ya amani.

      11 Je! Mungu anajibu sala kama hizo kwa ajili ya amani? Basi, viongozi wa kidini hao walikuwa wakisali kwa Mungu yupi? Kama ungewauliza, kila kikundi kingekupa jibu tofauti. Je! kuna jamii ya mamilioni ya miungu inayoweza kusikia na kujibu maombi rasmi yaliyotolewa kwa njia nyingi mbalimbali? Wengi wa washiriki waliabudu Utatu wa Jumuiya ya Wakristo.c Wabuddha, Wahindu, na wengine walitoa sala zao kwa miungu isiyo na hesabu. Kwa ujumla, “jamaa za kidini” 12 zilikusanyika, zikiwa zinawakilishwa na watu mashuhuri kama Askofu Mkuu wa Kianglikana wa Kantabari, Dalai Lama wa Buddha, kasisi wa Orthodoksi la Urusi, Msimamizi wa Ushirika wa Patakatifu pa Shinto wa Tokyo, waabudu-mizimu wa Kiafrika, na Wahindi Waamerika wawili waliovalia vazi la kichwani la manyoya-manyoya. Kilikuwa kikundi chenye rangi za namna namna, bila kusema zaidi, kikifanyiza kipindi cha TV chenye kutazamisha. Kikundi kimoja kilisali bila kukoma kwa saa 12 katika wakati mmoja. (Linga Luka 20:45-47.) Lakini je! yoyote ya sala hizo ilipenya mawingu ya mvua yaliyoning’inia juu ya mkusanyiko huo? Kwa sababu zinazofuata, la:

      12. Ni kwa sababu zipi Mungu hakujibu sala za viongozi wa kidini wa ulimwengu kwa ajili ya amani?

      12 Tofauti na wale ambao “hutembea katika jina la Yehova,” hakuna mwanadini hata mmoja wa hao aliyekuwa akisali kwa Yehova, Mungu aliye hai, ambaye jina lake huonekana mara zapata 7,000 katika maandishi asilia ya Biblia. (Mika 4:5; Isaya 42:8, 12, NW)d Wakiwa kikundi wao hawakumwendea Mungu kwa jina la Yesu, walio wengi wao wakiwa hata hawaitikadi katika Yesu Kristo. (Yohana 14:13; 15:16) Hakuna baadhi yao wanaofanya mapenzi ya Mungu kwa ajili ya siku yetu, ambayo ni kupiga mbiu ulimwenguni pote ya Ufalme unaokuja wa Mungu—si UM—kuwa ndilo tumaini halisi kwa aina ya binadamu. (Mathayo 7:21-23; 24:14; Marko 13:10) Kwa sehemu iliyo kubwa zaidi matengenezo ya kidini yao yamejihusisha katika vita vyenye umwagaji-damu vya historia, kutia na vita viwili vya ulimwengu vya karne ya 20. Kwa hao, Mungu husema: “Hata ingawa nyinyi mnafanya sala nyingi, mimi sisikilizi; mikono yenu imejawa na umwagaji-damu.”—Isaya 1:15, NW; 59:1-3.

      13. (a) Ni kwa nini ni jambo la maana kwamba viongozi wa kidini wa ulimwengu wamepaswa kuungana mikono na UM katika kutoa mwito kwa ajili ya amani? (b) Vilio kwa ajili ya amani vitafikia upeo gani uliotabiriwa kimungu?

      13 Na zaidi, ni jambo la maana yenye kina kwamba viongozi wa kidini wamepaswa kuungana mikono na Umoja wa Mataifa katika kutoa mwito kwa ajili ya amani wakati huu. Wao wangependa kutumia uvutano juu ya UM kwa faida yao wenyewe, hasa katika enzi hii ya ki-siku-hizi wakati watu wao wanaacha dini. Kama viongozi wasio waaminifu katika Israeli wa kale, wao wanalia, “‘Kuna amani! Kuna amani!’ wakati hakuna amani.” (Yeremia 6:14, NW) Pasipo shaka vilio vyao kwa ajili ya amani vitaendelea, vikiwa vinainuka katika kuunga mkono upeo ambao kuhusu huo mtume Paulo alitolea unabii: “Siku ya Yehova inakuja sawasawa kama mwivi katika usiku. Wakati wowote wanaposema: ‘Amani na usalama!’ ndipo uharibifu wa ghafula utakuwa juu yao papo hapo kama maumivu makali ya ghafula ya taabu juu ya mwanamke mwenye mimba; na wao hawataponyoka kwa vyovyote.”—1 Wathesalonike 5:2, 3, NW.

      14. Huenda kilio cha “Amani na usalama!” kitakuwa cha namna gani, na mmoja anaweza kuepukaje kuongozwa vibaya?

      14 Katika miaka ya hivi karibuni, wanasiasa wametumia maneno “amani na usalama” kuelezea mipango mbalimbali ya wanadamu. Je! jitihada hizo za viongozi wa ulimwengu zinaonyesha mwanzo wa utimizo wa andiko la 1 Wathesalonike 5:3? Au je, Paulo alikuwa akizungumzia tukio hususa na lenye kutokeza sana hivi kwamba lingetambuliwa ulimwenguni? Kwa kuwa mara nyingi unabii wa Biblia hueleweka kikamili tu baada ya kutimia au wakati unapoendelea kutimia, itatubidi tungoje tuone itakuwaje. Kwa sasa, Wakristo wanajua kwamba hata ingawa huenda ikaonekana kana kwamba mataifa yamepata amani na usalama, hakuna kitu ambacho kwa kweli kitakuwa kimebadilika. Ubinafsi, chuki, uhalifu, mvunjiko wa jamaa, ukosefu wa adili, magonjwa, huzuni, na kifo bado vitakuwapo. Ndiyo sababu si lazima wewe uongozwe vibaya na kilio chochote cha “amani na usalama,” ikiwa umeamka kuona maana ya matukio ya ulimwengu na unatii maonyo ya kiunabii katika Neno la Mungu.—Marko 13:32-37; Luka 21:34-36.

      [Maelezo ya Chini]

      a J. F. Rutherford alikufa Januari 8, 1942, na N. H. Knorr alimfuata kuwa msimamizi wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi.

      b Katika Novemba 20, 1940, Ujeremani, Italia, Japani, na Hungary zilitia sahihi kwa ajili ya “Ushirika wa Mataifa mpya,” ikifuatwa siku nne baadaye na msambazo-redio wa Vatikani wa Misa na sala kwa ajili ya amani ya kidini na kwa ajili ya utaratibu mpya wa mambo. Huo ‘Ushirika mpya’ haukutokea.

      c Dhana ya Utatu ina shina kutoka Babuloni wa kale, ambako mungu-jua Shamashi, mungu-mwezi Sin, na mungu-nyota Ishta waliabudiwa wakiwa utatu. Misri ilifuata kigezo icho hicho, ikiabudu Osirisi, Isisi, na Horusi. Asshuri, mungu mkuu wa Ashuru, huonyeshwa taswira ya vichwa vitatu. Kwa kufuata kigezo hicho, mifano inapatikana katika makanisa ya Kikatoliki ikionyesha Mungu kuwa ana vichwa vitatu.

      d Webster’s Third New International Dictionary ya 1993 hufasili Yehova Mungu kuwa “mungu mkuu kupita wote anayetambuliwa na mungu pekee anayeabudiwa na Mashahidi wa Yehova.”

      [Picha katika ukurasa wa 250]

      Kinyume cha “Amani”

      Ingawa 1986 ulipigiwa mbiu na UM kuwa Mwaka wa Amani ya Kimataifa, shindano la ujiuaji la kuunda silaha liliongezeka. World Military and Social Expenditures 1986 hutoa fasili hizi zenye kumakinisha:

      Katika 1986 matumizi ya kijeshi ya tufe lote yalifikia dola milioni elfu 900.

      Matumizi ya kijeshi ya tufe lote ya saa moja yangetosha kuchanja watu milioni 3.5 ambao walikufa kila mwaka kutokana na magonjwa ya kuambukiza yenye kuzuilika.

      Ulimwenguni pote, mtu mmoja kati ya watano aliishi katika umaskini wenye kuumiza. Watu hao wote wenye kufa-njaa wangeweza kulishwa kwa mwaka mmoja kwa gharama ya kile kiasi ambacho ulimwengu ulitumia kwa ajili ya silaha katika siku mbili.

      Nishati ya baruti iliyo katika rundo la silaha za nyukilia za ulimwengu ilikuwa kubwa zaidi ya ule mlipuko wa Chernobyl kwa mara 160,000,000.

      Bomu moja la nyukilia lingeweza kupelekwa likiwa na nguvu za mlipuko mara zaidi ya 500 ya bomu lililoangushwa juu ya Hiroshima katika 1945.

      Maghala ya zana za nyukilia yalikuwa na nguvu za baruti zinazolingana na Hiroshima zaidi ya milioni moja. Yaliwakilisha mara 2,700 za nguvu za baruti zilizoachiliwa katika Vita ya Ulimwengu 2, wakati watu milioni 38 walikufa.

      Vita vilikuwa vikitokea mara nyingi zaidi na ni vyenye kufisha zaidi. Vifo kutokana na vita vilikuwa jumla ya milioni 4.4 katika karne ya 18, milioni 8.3 katika karne ya 19, milioni 98.8 katika miaka 86 ya kwanza ya karne ya 20. Tangu karne ya 18, vifo kutokana na vita vimeongezeka zaidi ya mara sita kuliko idadi ya watu ya ulimwengu. Kulikuwako vifo mara kumi kwa kila vita katika karne ya 20 kuliko ilivyokuwa katika karne ya 19.

      [Picha katika ukurasa wa 247]

      Kama unabii ulivyotolewa juu ya hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu Ushirika wa Mataifa ulitiwa katika abiso wakati wa Vita ya Ulimwengu 2 lakini ulihuishwa ukiwa Umoja wa Mataifa

      [Picha katika ukurasa wa 249]

      Katika kuunga mkono “Mwaka wa Amani” wa UM, wawakilishi wa dini za ulimwengu walitoa sala ya mvurugo katika Assisi, Italia, lakini hakuna mmoja wao aliyetoa sala kwa Mungu aliye hai, Yehova

  • Kufisha Babuloni Mkubwa
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Sura ya 35

      Kufisha Babuloni Mkubwa

      1. Malaika anaelezaje habari ya hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu, na ni hekima ya aina gani inayohitajiwa kuelewa mifananisho ya Ufunuo?

      KATIKA kueleza zaidi habari ya hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu wa Ufunuo 17:3, malaika anamwambia Yohana: “Hapa ndipo elimu iliyo na hekima inapofaa: Vichwa saba humaanisha milima saba, ambako mwanamke huketi juu ya kilele. Na wako wafalme saba: watano wameanguka, mmoja yupo, mwingine hajawasili bado, lakini yeye awasilipo lazima yeye abaki kitambo kifupi.” (Ufunuo 17:9, 10, NW) Malaika anawasilisha hekima kutoka juu, hekima pekee inayoweza kutoa uelewevu wa mifananisho katika Ufunuo. (Yakobo 3:17) Hekima hii inaipa jamii ya Yohana na waandamani wayo nuru juu ya hatari ya nyakati tunamoishi. Inajenga katika mioyo yenye kujitoa uthamini wa hukumu za Yehova, ambazo sasa karibu kutimizwa, na inakaza kikiki hofu yenye afya kuelekea Yehova. Kama Mithali 9:10, NW inavyotaarifu: “Hofu ya Yehova ndio mwanzo wa hekima, na maarifa ya kumjua Mmoja Aliye Mtakatifu Zaidi Sana ndio uelewevu.” Hekima ya kimungu inatufunulia nini juu ya hayawani-mwitu?

      2. Ni nini maana ya vichwa saba vya hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu, na inakuwaje kwamba “watano wameanguka, mmoja yupo”?

      2 Vichwa saba vya hayawani-mwitu mkali sana husimamia “milima” saba, au “wafalme” saba. Semi zote mbili hutumiwa Kimaandiko kurejezea mamlaka za kiserikali. (Yeremia 51:24, 25; Danieli 2:34, 35, 44, 45) Katika Biblia, serikali za ulimwengu sita hutajwa kuwa zikiathiri mambo ya watu wa Mungu: Misri, Ashuru, Babuloni, Umedi-Uajemi, Ugiriki, na Roma. Kati ya hizi, tano zilikuwa tayari zimekuja na zikaenda kufikia wakati Yohana alipopokea Ufunuo, lakini Roma ilikuwa ingali sana serikali ya ulimwengu. Hii inalingana vizuri na maneno haya, “watano wameanguka, mmoja yupo.” Lakini namna gani juu ya “mwingine” aliyekuwa akitazamiwa kuja?

      3. (a) Milki ya Roma ilikujaje kugawanywa? (b) Ni matukio gani yaliyotukia katika Magharibi? (c) Milki Takatifu ya Roma yapasa ionweje?

      3 Milki ya Roma ilidumu na hata ikapanuka kwa mamia ya miaka baada ya siku ya Yohana. Katika 330 W.K. Maliki Konstantino alihamisha jiji kuu lake kutoka Roma kwenda Bizanshamu, ambalo alilipa jina Konstantinopo. Katika 395 W.K., Milki ya Roma iligawanywa ikawa sehemu za Mashariki na Magharibi. Katika 410 W.K., Roma liliangushwa na Alariki, mfalme wa Wavisigothi (kabila la Kijeremani ambalo lilikuwa limeongolewa kuwa la “Ukristo” wa aina ya Aria). Makabila ya Kijeremani (ya “Kikristo” pia) yalishinda Hispania na eneo lililo kubwa zaidi la Roma katika Afrika Kaskazini. Zilikuwako karne za misukosuko, kutotulia, na kujirekebisha upya katika Ulaya. Wamaliki wenye sifa waliinuka katika Magharibi, kama vile Charlemagne, ambaye alifanya fungamano na Papa Leo 3 katika karne ya 9, na Frederick 2, ambaye alitawala katika karne ya 13. Lakini milki yao, ingawa iliitwa Milki Takatifu ya Roma ilikuwa ndogo zaidi ya ile Milki ya Roma ya mapema zaidi, wakati wa kilele cha usitawi wayo. Ilikuwa zaidi mrudisho au mwendelezo wa hiyo serikali ya kale kuliko kuwa milki mpya.

      4. Milki ya Mashariki ilikuwa na mafanikio gani, lakini kulitukia nini kwa sehemu kubwa ya lililokuwa eneo la Roma ya kale katika Afrika Kaskazini, Hispania, na Siria?

      4 Milki ya Mashariki ya Roma, yenye kitovu katika Konstantinopo, iliendelea ikiwa na uhusiano wenye wasiwasi na Milki ya Magharibi. Katika karne ya sita, maliki wa Mashariki Justiniani 1 aliweza kushinda sehemu kubwa ya Afrika ya Kaskazini, na pia akaingilia Hispania na Italia. Katika karne ya saba, Justiniani 2 alikombolea Milki hiyo maeneo ya Makedonia ambayo yalikuwa yameshindwa na wanamakabila wa Kislavi. Hata hivyo, Kufikia karne ya nane eneo kubwa la zamani la Roma ya kale katika Afrika Kaskazini, Hispania, na Siria lilikuwa limekuja chini ya milki mpya ya Islamu na hivyo likapita kutoka udhibiti wa Konstantinopo na Roma pia.

      5. Ingawa jiji la Roma lilianguka 410 W.K., ilikuwaje kwamba ilichukua karne nyingi zaidi kabla ya visehemu vyote vya Milki ya Roma ya kisiasa kutoweka katika mandhari ya ulimwengu?

      5 Jiji la Konstanipo lenyewe lilidumu kwa muda mrefu zaidi kidogo. Liliokoka mashambulizi ya mara nyingi kutoka kwa Waajemi, Waarabu, Wabulgari, na Warusi mpaka mwishowe katika 1203 likaangushwa—si na Waislamu bali na Wakrusedi kutoka Magharibi. Ingawa hivyo, katika 1453, lilikuja chini ya mamlaka ya mtawala Mwislamu wa Ottomani Mehmedi 2 na upesi likawa jiji kuu la Milki ya Ottomani, au ya Kituruki. Hivyo, ijapokuwa jiji la Roma lilianguka katika 410 W.K., ilichukua karne nyingi zaidi kabla ya visehemu vyote vya Milki ya Roma ya kisiasa kutoweka katika mandhari ya ulimwengu. Na hata hivyo, uvutano wayo bado ulitambulikana katika milki za kidini zenye msingi wa upapa wa Roma na makanisa ya Orthodoksi ya Mashariki.

      6. Ni milki zipi mpya kabisa zilizotokea, na ni ipi iliyopata kuwa yenye kufanikiwa zaidi sana?

      6 Hata hivyo, kufikia karne ya 15, nchi fulani zilikuwa zikijenga milki mpya kabisa. Ingawa baadhi ya serikali hizi mpya za kibepari zilipatikana katika maeneo ambayo hapo kwanza yalikuwa makoloni ya Roma, milki zazo hazikuwa mwendelezo vivi hivi wa Milki ya Roma. Ureno, Hispania, Ufaransa, na Uholanzi zote zikawa makao ya milki zilizotapakaa sana. Lakini iliyofanikiwa zaidi sana ilikuwa Uingereza, ambayo ikaja kusimamia milki kubwa mno ambayo juu yayo ‘jua halikutua kamwe.’ Milki hii ilienea katika nyakati mbalimbali juu ya sehemu kubwa ya Amerika Kaskazini, Afrika, India, na Esia Kusini-mashariki, pamoja na maeneo ya Pasifiki Kusini.

      7. Serikali ya ulimwengu ya uwili ilikujaje kuwako, na Yohana alisema ni kwa muda gani ‘kichwa’ au serikali ya ulimwengu ya saba ingeendelea?

      7 Kufikia karne ya 19, baadhi ya makoloni katika Amerika Kaskazini yalikuwa yamekwisha kujitenga na Uingereza yakaunda United States ya Amerika yenye kujitawala. Kisiasa, hitilafu fulani ziliendelea kati ya taifa jipya na iliyokuwa nchi-mama yao. Hata hivyo, vita ya ulimwengu ya kwanza ilizilazimisha hizo nchi zote mbili kutambua masilahi yazo ya pamoja na zikatia nguvu uhusiano maalumu kati yazo. Hivyo, namna ya serikali ya ulimwengu ya uwili ikatokea, ikiwa inafanyizwa na United States ya Amerika, sasa ikiwa ndilo taifa la ulimwengu lenye ukwasi zaidi sana, na Uingereza, kao la milki ya ulimwengu iliyo kubwa zaidi sana. Basi, hiki, ndicho ‘kichwa’ cha saba, au serikali kubwa ya ulimwengu, ambayo inaendelea mpaka ndani ya wakati wa mwisho na katika maeneo ambamo Mashahidi wa ki-siku-hizi wa Yehova walijiimarisha kwanza. Kikilinganishwa na utawala mrefu wa kichwa cha sita, hiki cha saba ‘chabaki kitambo kifupi’ mpaka Ufalme wa Mungu uangamizapo mataifa yote.

      Kwa Nini Huitwa Mfalme wa Nane?

      8, 9. Malaika anamwitaje hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu na ni katika njia gani huchipuka kutoka kwa wafalme saba?

      8 Malaika anamweleza Yohana zaidi hivi: “Na hayawani-mwitu ambaye alikuwako lakini hayuko, yeye pia mwenyewe ni mfalme wa nane, lakini huchipuka kutoka kwa wale saba, na yeye huenda zake ndani ya uharibifu.” (Ufunuo 17:11, NW) Hayawani-mwitu wa ufananisho rangi-nyekundu-nyangavu “huchipuka kutoka” kwa vichwa saba; yaani, yeye anazaliwa na, au yuko kwa sababu ya vichwa hivyo vya ‘hayawani-mwitu kutoka bahari,’ ambaye hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu ni mfano wake. Kwa njia gani? Basi, katika 1919 serikali ya Uingereza-Amerika ilikuwa ndiyo kichwa chenye kutawala. Vile vichwa sita vilivyotangulia vilikuwa vimeanguka, nacho cheo cha serikali kubwa ya ulimwengu yenye kutawala kilikuwa kimepitishwa kwenye kichwa hiki cha uwili na sasa kikawa katika kitovu chacho. Hiki kichwa cha saba, kikiwa ndicho mwakilishi wa sasa wa mstari wa serikali za ulimwengu, kilikuwa ndicho kani yenye kutenda katika kusimamisha Ushirika wa Mataifa na kingali ndicho mwendelezaji na mtegemezaji kifedha mkuu wa Umoja wa Mataifa. Hivyo, kwa njia ya ufananisho hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu—mfalme wa nane—“huchipuka kutoka” kwa vile vichwa saba vya kwanza. Ikionwa katika njia hii, taarifa ya kwamba yeye alichipuka kutoka kwa vichwa saba inapatana vizuri na ufunuo wa mapema zaidi kwamba hayawani-mwitu mwenye pembe mbili mithili ya mwana-kondoo (Serikali ya Ulimwengu Uingereza-Amerika, kichwa cha saba cha hayawani-mwitu wa kwanza) alihimiza kufanyizwa kwa huo mfano na akaupa uhai.—Ufunuo 13:1, 11, 14, 15.

      9 Kwa kuongezea, washiriki wa kwanza kabisa wa Ushirika wa Mataifa walikuwamo, pamoja na Uingereza, serikali ambazo zilitawala katika makao ya baadhi ya vichwa vilivyotangulia, yaani, Ugiriki, Irani (Uajemi), na Italia (Roma). Hatimaye, serikali zenye kutawala maeneo yaliyodhibitiwa na serikali za ulimwengu sita zilizotangulia zikaja kuwa washiriki waungaji mkono wa mfano wa hayawani-mwitu. Katika maana hii, vilevile, ingeweza kusemwa kwamba huyu hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu alichipuka kutoka kwa serikali za ulimwengu saba.

      10. (a) Inaweza kusemwaje kwamba hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu “yeye pia mwenyewe ni mfalme wa nane”? (b) Kiongozi mmoja wa nchi zilizokuwa Muungano wa Sovieti alionyeshaje uungaji-mkono wake wa Umoja wa Mataifa?

      10 Angalia kwamba hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu “yeye pia mwenyewe ni mfalme wa nane.” Hivyo, Umoja wa Mataifa leo unakusudiwa uonekane kuwa serikali ya ulimwengu. Nyakati fulani hata umetenda hivyo, ukituma majeshi uwanjani kusuluhisha magomvi ya kimataifa, kama vile katika Korea, Peninsula ya Sinai, nchi fulani za Kiafrika, na Lebanoni. Lakini huo ni mfano tu wa mfalme. Kama vile mfano wa kidini, huo hauna uvutano au uwezo halisi isipokuwa ule ambao unapewa na wale ambao waliutokeza na wanaouabudu. Katika pindi fulani, hayawani-mwitu huyu wa ufananisho huonekana dhaifu; lakini hajapatwa kamwe na aina ya kuachwa kwa wingi na washiriki wenye maelekeo ya udikteta ambao walifanya Ushirika wa Mataifa utetereke na kutumbukia ndani ya abiso. (Ufunuo 17:8) Ingawa anashikilia maoni yanayotofautiana sana katika maeneo mengine, kiongozi mmoja mashuhuri wa nchi zilizokuwa Muungano wa Sovieti katika 1987 alijiunga na mapapa wa Roma katika kuonyesha uungaji-mkono wa UM. Yeye hata alitaka kuwe na “mfumo mpana wa usalama wa kimataifa” wenye kutegemea UM. Kama Yohana ajifunzavyo upesi, wakati utakuja ambapo UM utatenda kwa mamlaka kubwa. Kisha huo, katika zamu yao, “huenda zake ndani ya uharibifu.”

      Wafalme Kumi kwa Saa Moja

      11. Malaika wa Yehova anasema nini juu ya pembe kumi zilizo juu ya hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu wa ufananisho?

      11 Katika sura ya Ufunuo iliyotangulia, malaika, wa sita na wa saba walimimina mabakuli ya kasirani ya Mungu. Hivyo sisi tuliarifiwa kwamba wafalme wa dunia wanakusanywa kwenye vita ya Mungu kwenye Har–Magedoni na kwamba ‘Babuloni Mkubwa apaswa kukumbukwa katika mwono wa Mungu.’ (Ufunuo 16:1, 14, 19, NW) Sasa tutajifunza kirefu zaidi jinsi hukumu za Mungu juu ya hawa zitatekelezwa. Sikiliza tena malaika wa Yehova anaponena kwa Yohana. “Na pembe kumi ambazo wewe uliona humaanisha wafalme kumi, ambao bado kupokea ufalme, lakini wao hupokea mamlaka wakiwa wafalme saa moja pamoja na hayawani-mwitu. Hawa wana fikira moja, na hivyo wao humpa hayawani-mwitu nguvu na mamlaka yao. Hawa watapigana na Mwana-Kondoo, lakini, kwa sababu yeye ni Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme, Mwana-Kondoo atashinda wao. Pia, wale wenye kuitwa na wachaguliwa na waaminifu pamoja na yeye watafanya hivyo.”—Ufunuo 17:12-14, NW.

      12. (a) Pembe kumi ni picha ya nini? (b) Ni jinsi gani pembe kumi za ufananisho ‘hazikuwa zimepokea ufalme’? (c) Pembe kumi za ufananisho zinakuwaje na “ufalme” sasa, na ni kwa muda gani?

      12 Pembe kumi ni picha ya serikali zote za kisiasa ambazo zinatawala sasa katika mandhari ya ulimwengu na ambazo huunga mkono hayawani-mwitu. Ni nchi chache sana zilizoko sasa ambazo zilijulikana katika siku ya Yohana. Na zile zilizojulikana, kama Misri na Uajemi (Irani), leo zina muundo wa kisiasa ulio tofauti kabisa. Kwa sababu hiyo, katika karne ya kwanza, ‘pembe kumi hazikuwa zimepokea ufalme.’ Lakini sasa katika siku ya Bwana, zina “ufalme,” au mamlaka ya kisiasa. Milki kubwa-kubwa za kikoloni zilipoanguka, hasa tangu vita ya ulimwengu ya pili, mataifa mengi mapya yamezaliwa. Hizi, pamoja na serikali ambazo zimeimarika muda mrefu, lazima zitawale pamoja na hayawani-mwitu kwa kipindi kifupi—“saa moja” tu—kabla Yehova hajakomesha mamlaka zote za kisiasa za ulimwengu kwenye Har–Magedoni.

      13. Ni katika njia gani pembe kumi zina “fikira moja,” na hiyo huhakikisha mwelekeo gani kwa Mwana-Kondoo?

      13 Leo, utukuzo wa taifa ndio mojapo kani zenye nguvu zaidi sana zinazosukuma pembe kumi hizi. Zina “fikira moja” kwa kuwa hizo zinataka kuhifadhi enzi zao za kitaifa badala ya kukubali Ufalme wa Mungu. Hilo ndilo lilikuwa kusudi lao katika kuchangia Ushirika wa Mataifa na tengenezo la Umoja wa Mataifa katika ile mara ya kwanza—kuhifadhi amani ya ulimwengu na hivyo kulinda salama kuwako kwazo. Mwelekeo kama huo unahakikisha kwamba pembe kumi zitapinga Mwana-Kondoo, “Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme,” kwa sababu Yehova amekusudia kwamba Ufalme wake chini ya Yesu Kristo hivi karibuni utachukua mahali pa falme hizi.—Danieli 7:13, 14; Mathayo 24:30; 25:31-33, 46.

      14. Inawezekanaje kwa watawala wa ulimwengu kupigana na Mwana-Kondoo, na tokeo litakuwa nini?

      14 Bila shaka, watawala wa ulimwengu huu hawawezi kufanya kitu chochote dhidi ya Yesu mwenyewe. Yeye yumo mbinguni, mbali sana wasimoweza kumfikia. Lakini ndugu za Yesu, wabakio wa mbegu ya mwanamke, wangali duniani na inaonekana wazi wanaumizika. (Ufunuo 12:17) Nyingi za pembe zimekwisha onyesha uhasama mkali kuwaelekea, na katika njia hii zimepigana na Mwana-Kondoo. (Mathayo 25:40, 45) Ingawa hivyo, karibuni, wakati utakuja wa Ufalme wa Mungu ‘kuponda-ponda na kuweka mwisho kwenye falme hizi zote.’ (Danieli 2:44, NW) Ndipo, wafalme wa dunia watakuwa katika pigano hadi tamati pamoja na Mwana-Kondoo, kama tutakavyoona karibuni. (Ufunuo 19:11-21) Lakini hapa tunajifunza mambo ya kutosha kung’amua kwamba mataifa hayatafanikiwa. Ingawa hayo pamoja na hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu wa UM wana “fikira moja” yao, wao hawawezi kumshinda “Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme” aliye mkubwa, wala hawawezi kushinda “wale wenye kuitwa na wachaguliwa na waaminifu pamoja na yeye,” kutia ndani wafuasi wapakwa-mafuta wake ambao wangali duniani. Hawa pia watakuwa wamekwisha shinda kwa kushika ukamilifu katika kujibu mashtaka maovu ya Shetani.—Warumi 8:37-39; Ufunuo 12:10, 11.

      Kuteketeza Kahaba

      15. Malaika anasema nini juu ya kahaba na mwelekeo na tendo la pembe kumi na hayawani-mwitu kuelekea yeye?

      15 Watu wa Mungu sio peke yao wanaochukiwa na pembe kumi. Malaika sasa anavuta uangalifu wa Yohana kwenye kahaba: “Na yeye anasema kwangu mimi: ‘Maji ambayo wewe uliona, ambapo kahaba anaketi, humaanisha vikundi vya watu na umati wa watu na mataifa na ndimi. Na pembe kumi ambazo wewe uliona, na hayawani-mwitu, hizi zitachukia kahaba na zitafanya yeye kuwa mwenye kuteketezwa na mwenye uchi, na zitakula kabisa sehemu zake zenye mnofu na zitachoma yeye kabisa kabisa kwa moto.’”—Ufunuo 17:15, 16, NW.

      16. Ni kwa nini Babuloni Mkubwa hataweza kutegemea maji yake yamuunge mkono wa himaya wakati serikali za kisiasa zinapomgeukia?

      16 Kama vile Babuloni wa kale alivyotegemea ulinzi wa maji yake, Babuloni Mkubwa leo anategemea washiriki wake wengi mno “vikundi vya watu na umati wa watu na mataifa na ndimi.” Kwa kufaa malaika huelekeza uangalifu wetu kwenye hao kabla ya kusimulia tukio lenye kugutusha: Serikali za kisiasa za dunia hii zitamgeukia kijeuri Babuloni Mkubwa. “Vikundi vya watu na umati wa watu na mataifa na ndimi” wote hao watafanya nini wakati huo? Tayari watu wa Mungu wanaonya Babuloni Mkubwa kwamba maji ya mto Eufrati yatakauka. (Ufunuo 16:12) Mwishowe maji hayo yatakauka kabisa. Hayo hayataweza kumpa kahaba kizee mwenye kunyarafisha tegemezo lolote lenye kufaa katika saa yake ya uhitaji ulio mkubwa zaidi sana.—Isaya 44:27; Yeremia 50:38; 51:36, 37.

      17. (a) Ni kwa sababu gani ukwasi wa Babuloni Mkubwa hautamwokoa? (b) Mwisho wa Babuloni Mkubwa utakuwaje wenye aibu kabisa? (c) Mbali na pembe kumi, au mataifa moja moja, ni nini kingine kinachojiunga katika jeuri dhidi ya Babuloni Mkubwa?

      17 Kwa hakika, ukwasi mkubwa mno wa vitu vya kimwili hautaweza kumwokoa Babuloni Mkubwa. Huenda hata ukaharakisha kuharibiwa kwake, kwa kuwa njozi huonyesha kwamba wakati hayawani-mwitu na pembe kumi wanapomwonyesha chuki yao watamvua majoho yake ya kifalme na vito vyake vyote vya thamani. Wao watapora ukwasi wake. ‘Wanamfanya kuwa uchi,’ wakifichua kiaibu tabia yake halisi. Mteketezo wee! Pia mwisho wake ni wenye aibu kabisa. Wanamharibu, na ‘kula sehemu zake zenye mnofu,’ wakimwacha mifupa mitupu isiyo na uhai. Mwishowe, wao ‘humchoma kabisa kabisa kwa moto.’ Yeye huchomwa kabisa kama mwenye ugonjwa wa tauni, bila hata maziko ya heshima! Si mataifa yale tu, kama yanavyowakilishwa na pembe kumi, yanayomharibu kahaba mkubwa, bali pia “hayawani-mwitu,” kumaanisha UM wenyewe, hujiunga nayo katika kuonyesha jeuri hii. Utatoa idhini yao ili dini bandia iharibiwe. Yaliyo mengi ya yale mataifa 190 na zaidi yaliyo ndani ya UM yameonyesha tayari, kwa kiolezo chayo cha kupiga kura, uhasama wayo kuelekea dini, hasa ile ya Jumuiya ya Wakristo.

      18. (a) Ni uwezekano gani wa mataifa kugeukia dini za Kibabuloni ambao tayari umeonekana? (b) Ni nini itakayokuwa sababu ya msingi ya shambulio la ujumla juu ya kahaba mkubwa?

      18 Ni kwa nini hayo yangemtenda kijeuri hivyo hawara wao wa zamani? Sisi tumeona katika historia ya hivi majuzi uwezekano kama huo wa kugeukia dini ya Kibabuloni. Upinzani rasmi wa kiserikali umepunguza sana uvutano wa dini katika nchi kama vile China na nchi zilizokuwa Muungano wa Sovieti. Katika maeneo ya Kiprotestanti ya Ulaya, ubaridi wenye kuenea pote na mashaka vimeyaacha makanisa yakiwa tupu, hivi kwamba karibu dini imekufa. Milki kubwa mno ya Kikatoliki imegawanywa na uasi na kutoafikiana ambavyo viongozi wake wameshindwa kutuliza. Ingawa hivyo, haitupasi kupoteza mwono wa uhakika wa kwamba hili shambulio la mwisho kabisa, la ujumla juu ya Babuloni Mkubwa linakuja likiwa wonyesho wa hukumu ya Mungu isiyobadilika juu ya kahaba mkubwa.

      Kufikiliza Fikira ya Mungu

      19. (a) Utekelezo wa hukumu ya Yehova dhidi ya kahaba mkubwa unaweza kutolewaje kielezi na hukumu yake dhidi ya Yerusalemu asi-imani katika 607 K.W.K.? (b) Hali ya ukiwa, ya kutokaliwa ya Yerusalemu baada ya 607 K.W.K. ilitangulia kutoa tamathali ya nini kwa siku yetu?

      19 Yehova anatekelezaje hukumu hii? Hii inaweza kutolewa kielezi na tendo la Yehova dhidi ya watu wake waasi-imani katika nyakati za kale, ambao kuwahusu yeye alisema: “Katika manabii wa Yerusalemu mimi nimeona vitu vibaya sana, kufanya uzinzi na kutembea katika ubandia; na wao wameimarisha mikono ya watenda maovu ili kwamba isiwapase kurudi, kila mmoja kutoka ubaya wake mwenyewe. Kwangu mimi wao wote wamekuwa kama Sodoma, na wakaaji wake ni kama Gomora.” (Yeremia 23:14, NW) Katika 607 K.W.K., Yehova alitumia Nebukadneza ‘avue mavazi, atwae vitu vizuri, na aache uchi na bila nguo’ jiji hilo lenye uzinzi wa kiroho. (Ezekieli 23:4, 26, 29, NW) Yerusalemu la wakati huo lilikuwa kigezo cha Jumuiya ya Wakristo ya leo, na kama alivyoona Yohana katika njozi ya mapema zaidi, Yehova ataipa Jumuiya ya Wakristo na dini nyingine yote bandia adhabu inayofanana na hiyo. Ukiwa, hali ya kutokaliwa ya Yerusalemu baada ya 607 K.W.K. huonyesha vile Jumuiya ya Wakristo ya kidini itakavyoonekana baada ya kuvuliwa ukwasi wayo na kufichuliwa kiaibu. Na sehemu inayobaki ya Babuloni Mkubwa haitakuwa afadhali.

      20. (a) Yohana anaonyeshaje kwamba kwa mara nyingine tena Yehova atatumia watawala wa kibinadamu kutekeleza hukumu? (b) “Fikira” ya Mungu ni nini? (c) Ni katika njia gani mataifa yatafikiliza “fikira moja,” yayo lakini kwa kweli ni fikira ya nani itatimizwa?

      20 Kwa mara nyingine tena Yehova anatumia watawala wa kibinadamu kutekeleza hukumu. “Kwa maana Mungu alitia hilo ndani ya mioyo yao kufikiliza fikira yake, hata kufikiliza fikira yao moja kwa kumpa ufalme wao hayawani-mwitu, mpaka hapo maneno ya Mungu yatakuwa yametimilizwa.” (Ufunuo 17:17, NW) “Fikira” ya Mungu ni nini? Kupangia wafishaji wa Babuloni Mkubwa waungane pamoja, ili kumharibu kabisa. Bila shaka, matilaba ya watawala katika kumshambulia yatakuwa kufikiliza “fikira moja” yao wenyewe. Wao watahisi kwamba ni kwa masilahi yao ya utukuzaji wa taifa kumgeukia huyo kahaba mkubwa. Huenda wakaja kuona kule kuendelea kwa dini iliyopangwa kitengenezo ndani ya mipaka yao kuwa tisho kwa enzi zao. Lakini Yehova atakuwa kwa kweli akiongoza mambo kwa werevu; wao watafikiliza fikira yake kwa kuharibu kwa dharuba moja adui yake mzinzi wa muda mrefu!—Linga Yeremia 7:8-11, 34.

      21. Kwa kuwa hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu atatumiwa katika kuharibu Babuloni Mkubwa, kwa wazi mataifa yatafanya nini kwa habari ya Umoja wa Mataifa?

      21 Ndiyo, mataifa yatatumia hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu, Umoja wa Mataifa, katika kuharibu Babuloni Mkubwa. Wao hawatendi kwa utangulizi wao wenyewe, kwa maana Yehova hutia ndani ya mioyo yao “hata kufikiliza fikira moja yao kwa kumpa ufalme wao hayawani-mwitu.” Wakati ujapo, kwa wazi mataifa yataona uhitaji wa kuimarisha Umoja wa Mataifa. Itakuwa kana kwamba, wanaupa meno, wakiupa mamlaka yoyote na nguvu waliyo nayo ili kwamba uweze kugeukia dini bandia na kupiga vita kwa kufaulu dhidi yayo “mpaka hapo maneno ya Mungu yatakuwa yametimilizwa.” Hivyo, kahaba wa kale atakuja kwenye mwisho wake kabisa. Na apotelee mbali!

      22. (a) Kwenye Ufunuo 17:18, ni nini kinachoashiriwa kwa njia ambayo malaika humalizia ushahidi wake? (b) Mashahidi wa Yehova wanaitikiaje kufumbuliwa kwa fumbo hilo?

      22 Kana kwamba anakazia uhakika wa kutekelezwa kwa hukumu ya Yehova juu ya milki ya ulimwengu ya dini bandia, malaika anamalizia ushahidi wake kwa kusema: “Na mwanamke ambaye wewe uliona anamaanisha jiji kubwa ambalo lina ufalme juu ya wafalme wa dunia.” (Ufunuo 17:18, NW) Kama Babuloni wa wakati wa Belshaza, Babuloni Mkubwa “amepimwa uzani katika mizani na akapatikana anapungukiwa.” (Danieli 5:27, The New English Bible) Kufishwa kwake kutakuwa kwepesi na kwa kukata maneno. Nao Mashahidi wa Yehova wanaitikiaje kufumbuliwa kwa fumbo la kahaba mkubwa na la hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu? Wao huonyesha bidii katika kupiga mbiu ya siku ya hukumu ya Yehova, huku wakijibu “kwa upendezi” watafutaji wa ukweli wenye mioyo myeupe. (Wakolosai 4:5, 6; Ufunuo 17:3, 7, NW) Kama vile sura yetu ifuatayo itakavyoonyesha, wote wenye kutamania kuokoka wakati kahaba mkubwa anapofishwa lazima watende, na kutenda chakachaka!

      [Picha katika ukurasa wa 252]

      Mfuatano wa Serikali Saba za Ulimwengu

      MISRI

      ASHURU

      BABULONI

      UMEDI-UAJEMI

      UGIRIKI

      ROMA

      UINGEREZA-AMERIKA

      [Picha katika ukurasa wa 254]

      “Yeye pia mwenyewe ni mfalme wa nane”

      [Picha katika ukurasa wa 255]

      Wakimgeuzia Mwana-Kondoo visogo vyao, “wao humpa hayawani-mwitu nguvu na mamlaka yao”

      [Picha katika ukurasa wa 257]

      Jumuiya ya Wakristo ikiwa ndiyo sehemu kuu ya Babuloni Mkubwa itashabihi Yerusalemu la kale kuwa gofu kabisa

  • Jiji Kubwa Lateketezwa
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Sura ya 36

      Jiji Kubwa Lateketezwa

      Njozi ya 12—Ufunuo 18:1–19:10

      Habari: Anguko na uharibifu wa Babuloni Mkubwa; ndoa ya Mwana-Kondoo yatangazwa

      Wakati wa utimizo: Kutoka 1919 mpaka baada ya ile dhiki kubwa

      1. Ni nini kitakachotia alama mwanzo wa dhiki kubwa?

      CHA GHAFULA, chenye kugutusha, chenye kuteketeza—ndivyo kitakuwa kifo cha Babuloni Mkubwa! Kitakuwa mojapo matukio yenye msiba mkuu zaidi sana katika historia yote, kikifanyiza mwanzo wa “dhiki kubwa kama ambayo haijapata kutokea tangu mwanzo wa ulimwengu mpaka sasa, la, wala haitatukia tena.”—Mathayo 24:21, NW.

      2. Ingawa milki za kisiasa zimeinuka na zikaanguka, ni milki ya aina gani ambayo imedumu?

      2 Dini bandia imekuwapo kwa muda mrefu. Imekuwapo bila kikomo tangu siku za Nimrodi mwenye kiu cha damu ambaye alipinga Yehova na akaanzisha watu kujenga Mnara wa Babeli. Yehova alipovuruga ndimi za waasi hao na kuwatawanya juu ya dunia, dini bandia ya Babuloni ilienda pamoja nao. (Mwanzo 10:8-10; 11:4-9) Tangu hapo, milki za kisiasa zimeinuka na zikaanguka, lakini dini ya Kibabuloni imedumu. Imechukua sura na maumbo mengi, ikiwa milki ya ulimwengu ya dini bandia, Babuloni Mkubwa aliyetolewa unabii. Sehemu yake yenye kutokeza zaidi sana ni Jumuiya ya Wakristo, ambayo ilikua kutokana na mchanganyo wa mafundisho ya Kibabuloni ya mapema zaidi na mafundisho ya “Ukristo” ulioasi imani. Kwa sababu ya historia ndefu, ndefu mno ya Babuloni Mkubwa, watu wengi wanaliona kuwa jambo gumu kuitikadi kwamba itaangamizwa wakati wowote.

      3. Ufunuo unathibitishaje hukumu ya maangamizi ya dini bandia?

      3 Kwa hiyo inafaa kwamba yaupasa Ufunuo uthibitishe hukumu ya uangamivu wa dini bandia kwa kutupatia maelezo mawili yenye mambo mengi ya kuanguka kwake na matukio yanayofuata yakiongoza kwenye kufanywa ukiwa wake mkubwa. Sisi tumekwisha kumwona yeye akiwa ndiye “kahaba mkubwa” ambaye mwishowe anateketezwa na wale ambao hapo zamani walikuwa wapenzi wake wa milki ya kisiasa. (Ufunuo 17:1, 15, 16, NW) Sasa, katika njozi nyingine bado, sisi tutamwona akiwa jiji, kifananisho cha kidini cha Babuloni wa kale.

      Babuloni Mkubwa Aanguka

      4. (a) Yohana anafuata kuona njozi gani? (b) Sisi tunaweza kumtambuaje malaika, na ni kwa nini inamfaa yeye atangaze anguko la Babuloni Mkubwa?

      4 Yohana aendelea na simulizi, akituambia: “Baada ya vitu hivi mimi nikaona malaika mwingine akishuka kutoka katika mbingu, akiwa na mamlaka kubwa; na dunia ilinururishwa kutokana na utukufu wake. Na yeye akalia kwa sauti imara, kusema: ‘Yeye ameanguka! Babuloni Mkubwa ameanguka.’” (Ufunuo 18:1, 2a, NW) Hii ni mara ya pili kwa Yohana kusikia tangazo hilo la kimalaika. (Ona Ufunuo 14:8.) Hata hivyo, wakati huu umaana walo umekaziwa na utukufu wa huyo malaika wa kimbingu, kwa kuwa utukufu wake unanururisha dunia kwa ujumla! Yeye anaweza kuwa nani? Karne nyingi mapema nabii Ezekieli, akiripoti juu ya njozi ya kimbingu, alitaarifu kwamba “dunia yenyewe iling’aa kwa sababu ya utukufu [wa Yehova].” (Ezekieli 43:2, NW) Malaika pekee wa kung’aa kwa utukufu unaolinganika na wa Yehova angekuwa Bwana Yesu, ambaye ni “ule mrudisho wa utukufu [wa Mungu] na uwakilisho barabara wa kuwako kwake kwenyewe.” (Waebrania 1:3, NW) Katika 1914, Yesu alipata kuwa Mfalme mbinguni, na tangu wakati huo amekuwa akitumia mamlaka juu ya dunia akiwa Mfalme na Hakimu mshirika wa Yehova. Inafaa, basi, kwamba imempasa yeye atangaze kuanguka kwa Babuloni Mkubwa.

      5. (a) Malaika huyo anatumia nani kutoa habari ya anguko la Babuloni Mkubwa? (b) Hukumu ilipoanza juu ya wale wenye kudai kuwa “nyumba ya Mungu,” Jumuiya ya Wakristo ilikuwa hali gani?

      5 Malaika huyu mwenye mamlaka kubwa anatumia nani katika kutoa habari kama hizo zenye kushangaza mbele ya aina ya binadamu? Kwani, ni wale watu wenyewe ambao wanaachiliwa likiwa tokeo la anguko hilo, wale wapakwa-mafuta wabakio duniani, jamii ya Yohana. Kutoka 1914 mpaka 1918, hao waliteseka sana mikononi mwa Babuloni Mkubwa, lakini katika 1918 Bwana Yehova na “mjumbe wa agano [la Kiabrahamu]” wake, Yesu Kristo, alianza hukumu pamoja na “nyumba ya Mungu,” wale wenye kudai kuwa Wakristo. Hivyo Jumuiya ya Wakristo iliyoasi imani ililetwa kwenye jaribio. (Malaki 3:1; 1 Petro 4:17, NW) Hatia ya damu yayo kubwa mno iliyopata wakati wa vita ya ulimwengu ya kwanza, ushiriki wayo katika kunyanyasa mashahidi waaminifu wa Yehova, na itikadi zayo za Kibabuloni havikuisaidia katika wakati wa hukumu yayo; wala hapana sehemu nyingine yoyote ya Babuloni Mkubwa iliyostahili kibali cha Mungu.—Linga Isaya 13:1-9.

      6. Inaweza kusemwaje kwamba Babuloni Mkubwa alikuwa ameanguka kufikia 1919?

      6 Hivyo kufikia 1919 Babuloni Mkubwa alikuwa ameanguka, kufungulia njia watu wa Mungu waachiliwe na warudishwe, kana kwamba kwa siku moja, kwenye bara lao la ufanisi wa kiroho. (Isaya 66:8) Kufikia mwaka huo, Yehova Mungu na Yesu Kristo, Dario Mkubwa Zaidi na Sairasi Mkubwa Zaidi, walikuwa wameongoza mambo kwa werevu ili kwamba dini bandia isiweze tena kuwashikilia watu wa Yehova. Haingeweza tena kuwazuia wasimtumikie Yehova na kujulisha kwa wote ambao yamkini kusikia kwamba Babuloni Mkubwa aliye kama kahaba amehukumiwa uangamivu na kwamba kutetewa kwa enzi kuu ya Yehova kumekaribia karibu.—Isaya 45:1-4; Danieli 5:30, 31.

      7. (a) Ingawa Babuloni Mkubwa hakuharibiwa katika 1919, Yehova alimwonaje? (b) Babuloni Mkubwa alipoanguka katika 1919, tokeo lilikuwa nini kwa watu wa Yehova?

      7 Ni kweli, Babuloni Mkubwa hakuangamizwa katika 1919—kama vile jiji la Babuloni la kale halikuangamizwa katika 539 K.W.K. wakati lilipoanguka mikononi mwa majeshi ya Sairasi Mwajemi. Lakini kwa maoni ya Yehova, tengenezo hilo lilikuwa limeanguka. Yeye alikuwa amepata hukumu mbaya ya kimahakama, akingojea kufishwa; kwa hiyo dini bandia haingeweza kushikilia tena watu wa Yehova katika utekwa. (Linga Luka 9:59, 60.) Hao waliachiliwa wakatumikie wakiwa mtumwa mwaminifu na mwenye uangalifu wa Bwana-Mkubwa wakitoa chakula cha kiroho kwa wakati unaofaa. Wao walikuwa wamepokea hukumu ya ‘Mmefanya vema’ nao walipewa utume wajishughulishe tena na kazi ya Yehova.—Mathayo 24:45-47; 25:21, 23; Matendo 1:8, NW.

      8. Ni tukio gani ambalo mlinzi wa Isaya 21:8, 9 hupigia mbiu, na ni nani leo anayetolewa kivuli na mlinzi huyo?

      8 Mileani nyingi zilizopita Yehova alitumia manabii wengine watabiri tukio hili kubwa lenye kuanzisha muda maalumu. Isaya alisema juu ya mlinzi ambaye “aliendelea kuita kwa sauti kubwa kama simba: ‘Juu ya mnara wa lindo, O Yehova, mimi ninasimama daima mchana, na kwenye kilindio changu mimi nimewekwa mausiku yote.’” Na ni tukio gani analotambua mlinzi huyo na kupiga mbiu kwa ujasiri kama wa simba? Hili: “Yeye ameanguka! Babuloni ameanguka, na mifano yote ya kuchongwa ya miungu yake [Yehova] amevunja hadi kwenye dunia!” (Isaya 21:8, 9, NW) Mlinzi huyu anatolea kivuli vizuri jamii ya Yohana leo ambayo ni yenye kuamka kabisa, inapotumia gazeti Mnara wa Mlinzi na vichapo vingine vya kitheokrasi kuvumisha kotekote habari za kwamba Babuloni ameanguka.

      Mshuko wa Babuloni Mkubwa

      9, 10. (a) Uvutano wa dini ya Kibabuloni umepatwa na mpunguo gani tangu Vita ya Ulimwengu 1? (b) Malaika mwenye nguvu anaelezaje hali ya kuanguka ya Babuloni Mkubwa?

      9 Anguko la Babuloni wa kale katika 539 K.W.K. lilikuwa mwanzo wa mshuko mrefu ambao ulimalizikia katika ukiwa wake. Hali kadhalika, tangu vita ya kwanza ya ulimwengu, uvutano wa dini ya Kibabuloni umeshuka sana kwa kadiri ya tufe lote. Kufuata vita ya ulimwengu ya pili, ibada ya Shinto ya maliki ilikatazwa katika Japani. Katika China, serikali ya Kikomunisti hudhibiti uwekwaji rasmi na utendaji wote wa kidini. Katika Ulaya kaskazini ya Kiprotestanti, watu walio wengi wamekuwa wasiopendezwa na dini. Na hivi majuzi Kanisa Katoliki la Roma limedhoofishwa na mifarakano na kutopatana kwa ndani katika milki yalo ya tufe lote.—Linga Marko 3:24-26.

      10 Pasipo shaka miendo hii yote ni sehemu ya ‘kukauka kwa mto Eufrati’ katika kutayarishia shambulio linalokuja la kivita juu ya Babuloni Mkubwa. ‘Kukauka’ huku kunaonyeshwa, vilevile, katika tangazo la papa la Oktoba 1986 kwamba lazima kanisa ‘liwe mwomba-ombaji tena’—kwa sababu ya upungufu mkubwa mno. (Ufunuo 16:12) Hususa tangu 1919 Babuloni Mkubwa amekuwa akifichuliwa atazamwe na wote kuwa yeye ni bara-tupu la kiroho, kama malaika mwenye nguvu anavyotangaza hapa: “Na yeye amekuwa mahali pa kukaa roho waovu na mahali pa kujibanza kila pumzi isiyo safi na mahali pa kujibanza kila ndege asiye safi na mwenye kuchukiwa!” (Ufunuo 18:2b, NW) Karibuni atakuwa bara-tupu kama hilo kihalisi, akiwa ukiwa kama magofu ya Babuloni katika Iraki ya leo.—Ona pia Yeremia 50:25-28.

      11. Ni katika maana gani Babuloni Mkubwa amekuwa “mahali pa kukaa roho waovu” na ‘mahali pa kujibanza pumzi zisizo safi na pa ndege wasio safi’?

      11 Neno “roho waovu” hapa inaelekea ni mrudisho wa neno “roho waovu wenye umbo-mbuzi” (se‘i·rimʹ) linalopatikana katika elezo la Isaya kuhusu Babuloni aliyeanguka: “Na huko mizuka ya mikoa isiyo na maji kwa hakika italala chini, na nyumba zayo lazima zijawe na tai-bundi. Na huko mbuni lazima wakae, na roho waovu wenye umbo-mbuzi wenyewe wataenda wakirukaruka huko.” (Isaya 13:21, NW) Huenda isirejezee roho waovu halisi bali wanyama wakaa-jangwani wenye nywele za matimutimu ambao mwonekano wao ulifanya watazamaji wafikirie roho waovu. Katika magofu ya Babuloni Mkubwa, kuwako kitamathali kwa wanyama kama hao, pamoja na hewa tuli (“pumzi isiyo safi”) yenye sumu, na ndege wasio safi, huashiria hali yake ya kiroho iliyokufa. Yeye hatolei aina ya binadamu mataraja yoyote ya uhai.—Linga Waefeso 2:1, 2.

      12. Hali ya Babuloni Mkubwa hulandaje unabii wa Yeremia katika sura ya 50?

      12 Hali yake hulanda pia unabii wa Yeremia: “‘Kuna upanga dhidi ya Wakaldayo,’ ni tamko la Yehova, ‘na dhidi ya wakaaji wa Babuloni na dhidi ya wana-wafalme wake na dhidi ya wenye hekima wake. . . . Kuna mteketezo juu ya maji yake, na ni lazima yakaushwe kabisa. Kwa maana ni bara la mifano ya kuchongwa, na kwa sababu ya njozi zao zenye kujaa kikuli wao huendelea kutenda kikichaa. Kwa hiyo mizuka ya mikoa isiyo na maji itakaa pamoja na wanyama wenye kulia, na ndani yake yeye lazima mbuni wakae; naye hatakaliwa tena kamwe milele, wala yeye hatakaa kizazi baada ya kizazi.’” Ibada ya sanamu na kuimbwa kwa sala za kurudiwarudiwa hakuwezi kumwokoa Babuloni Mkubwa asipatwe na lipo linaloshabihi kuangushwa kwa Sodoma na Gomora na Mungu.—Yeremia 50:35-40, NW.

      Divai Yenye Kuamsha Harara

      13. (a) Malaika mwenye nguvu avutaje uangalifu kwenye mweneo mpana wa ukahaba wa Babuloni Mkubwa? (b) Ni utovu wa adili gani ulioenea sana katika Babuloni wa kale unaopatikana pia katika Babuloni Mkubwa?

      13 Kisha malaika mwenye nguvu anaelekeza uangalifu kwenye mweneo mpana wa ukahaba wa Babuloni Mkubwa, akipiga mbiu hivi: “Kwa sababu ya divai yenye kuamsha harara ya uasheratia wake mataifa yote yameanguka yakiwa majeruhi, na wafalme wa dunia walifanya uasherati na yeye, na wauza-bidhaa wasafiri wa dunia wakawa na utajiri kwa sababu ya nguvu za anasa yake isiyo ya aibu.” (Ufunuo 18:3, NW) Yeye amefundisha mataifa yote ya aina ya binadamu katika njia zake zisizo safi za kidini. Katika Babuloni wa kale, kulingana na mwanahistoria Herodoto, kila mwanamwali alitakwa aufanyize uasherati ubikira wake katika ibada ya hekalu. Kufikia leo hii ufisadi wa kingono wenye kukirihisha unaonyeshwa kitaswira katika sanamu-choro zilizoharibiwa na vita kwenye Angkor Wat katika Kampuchea na katika mahekalu katika Khajuraho, India, ambazo huonyesha mungu wa Kihindu Vishnu akizungukwa na mandhari za kimahaba zenye kunyarafisha. Katika United States, mafumbuo ya utovu wa adili ambayo yalitetemesha ulimwengu wa waevanjeli wa TV katika 1987, na tena katika 1988, pamoja na ufunuo wa zoea lenye kuenea pote la ugoni-jinsia-moja wa wahudumu wa kidini, hutoa kielezi kwamba hata Jumuiya ya Wakristo huvumilia mazidio yenye kugutusha ya uasherati halisi. Hata hivyo, mataifa yote yamekuwa majeruhi ya aina ya uasherati mbaya hata zaidi.

      14-16. (a) Ni uhusiano gani usio halali wa dini-siasa uliotukia katika Italia ya Ufashisti? (b) Wakati Italia ilipovamia Abisinia, ni taarifa gani walizotoa maaskofu wa Kanisa Katoliki la Roma?

      14 Sisi tumekwisha pitia uhusiano haramu wa dini-siasa uliomweka Hitla katika mamlaka katika Ujeremani ya Nazi. Mataifa mengine pia yalitaabika kwa sababu ya dini kujidukiza katika mambo ya kiserikali. Mathalani, Katika Italia ya Ufashisti, katika Februari 11, 1929, Mwafaka wa Laterani ulitiwa sahihi na Mussolini na Kardinali Gasparri, ukifanya Jiji la Vatikani kuwa dola lenye enzi. Papa Pius 11 alidai kwamba yeye alikuwa ‘ameirudisha Italia kwa Mungu, na Mungu akamrudisha kwa Italia.’ Je! huo ulikuwa ni ukweli? Fikiria yaliyotokea miaka sita baadaye. Katika Oktoba 3, 1935, Italia ilivamia Abisinia, ikidai kwamba lilikuwa “bara la kishenzi ambalo lilikuwa lingali linazoea utumwa.” Ni nani, kwa kweli, aliyekuwa wa kishenzi? Je! Kanisa Katoliki lililaumu vikali ushenzi wa Mussolini? Ingawa papa alitoa taarifa zisizoeleweka, maaskofu wake walisema wazi kabisa katika kubariki majeshi yenye silaha ya Italia “bara-baba” lao. Katika kitabu The Vatican in the Age of the Dictators, Anthony Rhodes huripoti hivi:

      15 “Katika Barua ya Uchungaji yake ya Oktoba 19 [1935], Askofu wa Udine [Italia] aliandika, ‘Si la wakati unaofaa wala lenye kufaa kwa sisi kutamka yanayofaa na yasiyofaa ya kisa hiki. Wajibu wetu tukiwa Waitalia, na hata hivyo zaidi tukiwa Wakristo ni kuchangia fanikio la silaha zetu.’ Askofu wa Padua aliandika katika Oktoba 21, ‘katika hizi saa ngumu ambazo sisi tunazipitia, sisi tunawaomba nyinyi mwe na imani katika watawala wetu na majeshi yenye silaha.’ Oktoba 24, Askofu wa Kremona aliweka wakfu bendera kadhaa za kijeshi na akasema: ‘Baraka ya Mungu na iwe juu ya askari-jeshi hawa ambao, juu ya udongo wa Kiafrika, watashinda mabara mapya na yenye rutuba kwa ajili ya ubunifu wa Italia, na hivyo kuwaletea utamaduni wa Kiroma na Kikristo. Italia na isimame kwa mara nyingine tena ikiwa mshauri wa ulimwengu kwa ujumla.’”

      16 Abisinia ikatwaliwa kinguvu, kwa baraka ya makasisi wa Katoliki ya Roma. Je! yeyote wa hawa angeweza kudai, katika maana yoyote, kwamba wao walikuwa kama mtume Paulo katika kuwa ‘bila hatia ya damu ya watu wote’?

      17. Hispania ilitesekaje kwa sababu ya viongozi wa kidini wayo kushindwa ‘kufua panga zao ziwe majembe ya plau’?

      17 Ongezea Ujeremani, Italia, na Abisinia taifa jingine ambalo limekuwa jeruhi kwa uasherati wa Babuloni Mkubwa—Hispania. Vita ya Wenyewe kwa Wenyewe ya 1936-39 katika bara hilo, kwa sehemu, ilianzishwa kwa sababu ya serikali ya kidemokrasi kuchukua hatua ya kupunguza nguvu kubwa mno za Kanisa Katoliki la Roma. Vita hiyo ilipoanza, Franko, kiongozi Mfashisti Mkatoliki wa majeshi ya Kimapinduzi, alijieleza mwenyewe kuwa “Jenerali Mkuu wa Kikristo wa Krusedi Takatifu,” jina la cheo ambalo baadaye aliacha. Mamia ya maelfu kadhaa ya Wahispania walikufa katika kupigana. Mbali na hilo, kulingana na kadirio dogo, Wateteaji wa Taifa wa Franko walikuwa wameua kimakusudi wanachama 40,000 wa Popular Front, hali hao wa pili nao walikuwa wameua kimakusudi makasisi—watawa wa kiume, mapadri, watawa wa kike, na makasisi wapya 8,000. Hilo ndilo ogofyo na msiba wa vita ya wenyewe kwa wenyewe, ikionyesha hekima ya kutii maneno haya ya Yesu: “Rudisha upanga wako mahali pao, kwa maana wale wote ambao huchukua upanga watapotelea mbali kwa upanga.” (Mathayo 26:52, NW) Ni jambo lenye kunyarafisha kama nini kwamba Jumuiya ya Wakristo hujiingiza katika umwagaji-damu mkubwa hivyo! Kweli kweli viongozi wayo wa kidini wameshindwa kabisa kabisa ‘kufua panga zao ziwe majembe ya plau’!—Isaya 2:4, NW.

      Wauza-Bidhaa Wasafiri

      18. Ni nani walio “wauza-bidhaa wasafiri wa dunia”?

      18 Ni nani walio “wauza-bidhaa wasafiri wa dunia”? Pasipo shaka sisi tungewaita leo wachuuzi, wanabiashara wakubwa-wakubwa, walanguzi chapuchapu na biashara kubwa-kubwa. Hii si kusema kwamba ni kosa kufanya biashara halali. Biblia huandaa shauri la hekima kwa watu wa biashara, ikiwaonya dhidi ya utovu wa haki, pupa, na kadhalika. (Mithali 11:1; Zekaria 7:9, 10; Yakobo 5:1-5) Pato lililo kubwa zaidi ni “kujitoa kwa ajili ya Mungu pamoja na ujitoshelevu.” (1 Timotheo 6:6, 17-19, NW) Hata hivyo, ulimwengu wa Shetani haufuati kanuni za uadilifu. Ufisadi ni tele. Unapatikana katika dini, katika siasa—na katika biashara kubwa-kubwa. Wakati kwa wakati vyombo vya habari hufichua kashifa, kama vile maofisa wa serikali wa vyeo vya juu kutumia vibaya mali ya serikali na kuuza silaha kimagendo.

      19. Ni mambo hakika gani ya uchumi wa ulimwengu husaidia kueleza sababu kwa nini wauza-bidhaa wasafiri wa dunia hupata mtajo usiopendeleka katika Ufunuo?

      19 Uchuuzi wa kimataifa wa silaha unapanda juu sana kupita dola 1,000,000,000,000 kila mwaka, huku mamia ya mamilioni ya wanadamu wakinyimwa lazima za maisha. Hilo ni baya vya kutosha. Lakini silaha huonekana kuwa tegemezo la msingi la uchumi wa ulimwengu. Katika Aprili 11, 1987, makala moja katika Spectator ya London iliripoti hivi? “Kuhesabu viwanda vinavyohusiana moja kwa moja, kazi 400,000 zinahusika katika U.S. na 750,000 katika Ulaya. Lakini ajabu ni kwamba, kadiri daraka la kijamii na kiuchumi la kuunda silaha linavyoongezeka, lile swali hasa la kama waundaji wanakingwa vizuri limesahauliwa.” Faida kubwa mno zinapatikana kadiri mabomu na silaha nyinginezo zinachuuzwa kotekote duniani, hata na kwa wanaoweza kuwa maadui. Siku moja huenda mabomu hayo yakarudi katika mteketeo wa moto kuwaharibu wale wanaoyauza. Ni kinyume kama nini! Ongezea hilo ulanguzi unaohusika katika biashara hii ya silaha. Katika United States pekee, kulingana na Spectator, “kila mwaka kwa njia isiyoelezeka Pentagoni hupoteza silaha na vifaa vya thamani ya dola milioni 900.” Si ajabu kwamba wauza-bidhaa wa dunia wanatajwa isivyopendeleka katika Ufunuo!

      20. Ni kielelezo gani kinachoonyesha kujihusisha kwa dini katika mazoea yenye ufisadi ya shughuli za biashara?

      20 Kama ilivyotabiriwa na malaika mwenye utukufu, dini imehusika sana katika mazoea yenye ufisadi ya biashara. Mathalani, kuna kujihusisha kwa Vatikani katika anguko la Banco Ambrosiano katika 1982. Kesi hiyo imejikokota muda wote wa miaka ya 1980, lile swali ambalo halijajibiwa likiwa: Fedha zilienda wapi? Katika Februari 1987 mahakimu wa Milani walitoa waranti ili makasisi watatu wa Vatikani wakamatwe, kutia na askofu mkuu mmoja Mwamerika, kwa mashtaka ya kwamba wao walikuwa washiriki kwenye ufilisi wenye udanganyifu, lakini Vatikani ilitupilia mbali ombi la kuwakabidhi wakahukumiwe. Katika Julai 1987, katikati ya makelele ya kuteta, zile waranti zilibatilishwa na Mahakama ya Rufani ya juu zaidi sana kwa msingi wa mwafaka wa zamani kati ya Vatikani na serikali ya Italia.

      21. Sisi twajuaje kwamba Yesu hakuwa na uhusiano na mazoea ya kibiashara yenye kutilika mashaka ya siku yake, lakini sisi tunaona nini leo katika dini ya Kibabuloni?

      21 Je! Yesu alijihusisha katika mazoea ya kibiashara yenye kutilika mashaka ya siku yake? La. Yeye hata hakuwa mwenye mali yoyote, kwa maana yeye alikuwa “hana mahali pa kulaza chini kichwa chake.” Mtawala mmoja kijana tajiri alishauriwa na Yesu hivi: “Uza vitu vyote ulivyo navyo na kugawia maskini, na wewe utakuwa na hazina katika mbingu; na uje uwe mfuasi wangu.” Hilo lilikuwa shauri jema, kwa maana lingaliweza kumwondolea mbali wasiwasi wote juu ya mambo ya kibiashara. (Luka 9:58; 18:22, NW) Kwa kutofautisha, dini ya Kibabuloni mara nyingi ina mafungamano mabaya na biashara kubwa-kubwa. Mathalani, katika 1987 Albany Times Union liliripoti kwamba msimamizi wa mambo ya kifedha wa akidayosisi ya Miami, Florida, U.S.A., alikubali kwamba kanisa lina hisa katika makampuni ambayo hufanyiza silaha za nyukilia, sinema zisizofaa, na sigareti.

      “Ondokeni Katika Yeye, Watu Wangu”

      22. (a) Sauti kutoka katika mbingu inasema nini? (b) Ni nini kilichoongoza kwenye mshangilio wa watu wa Mungu katika 537 K.W.K., na katika 1919?

      22 Maneno yanayofuata ya Yohana yanaelekeza kwenye utimizo zaidi wa kigezo cha kiunabii: “Na mimi nikasikia sauti nyingine kutoka katika mbingu ikisema: ‘Ondokeni katika yeye, watu wangu, ikiwa nyinyi hamtaki kushiriki pamoja na yeye katika madhambi yake, na ikiwa nyinyi hamtaki kupokea sehemu ya tauni zake.’” (Ufunuo 18:4, NW) Unabii wa anguko la Babuloni wa kale katika Maandiko ya Kiebrania unatia ndani pia amri ya Yehova kwa watu wake: “Kimbieni mtoke katikati ya Babuloni.” (Yeremia 50:8, 13, NW) Hali moja na hiyo, kwa sababu ya ukiwa unaokuja wa Babuloni Mkubwa, watu wa Mungu wanahimizwa sasa waponyoke. Katika 537 K.W.K. fursa ya kuponyoka kutoka Babuloni ilileta mshangilio mkubwa upande wa Waisraeli waaminifu. Katika njia iyo hiyo, kuachiliwa kwa watu wa Mungu kutoka utekwa wa Babuloni Mkubwa kuliongoza kwenye mshangilio upande wao. (Ufunuo 11:11, 12) Na tangu wakati huo mamilioni ya wengine yametii amri hiyo wakimbie.

      23. Sauti kutoka katika mbingu inakaziaje umuhimu wa kukimbia kutoka katika Babuloni Mkubwa?

      23 Je! ni jambo la muhimu kweli kweli kadiri hiyo kukimbia kutoka katika Babuloni Mkubwa, kujiondoa katika uanachama wa dini za ulimwengu na kujitenga kabisa? Ndivyo, kwa maana sisi tunahitaji kuchukua oni la Mungu juu ya dubwana hili la kale la kidini, Babuloni Mkubwa. Yeye hakuepa kumwita kahaba mkubwa. Kwa hiyo sasa sauti kutoka katika mbingu inamwarifu Yohana zaidi hivi kuhusu malaya huyu: “Kwa maana madhambi yake yametungamana pamoja moja kwa moja hadi kwenye mbingu, na Mungu amekumbuka matendo yake yasiyo ya haki. Rudisha kwa yeye hata kama vile yeye mwenyewe alirudisha, na fanya kwa yeye mara mbili ya vile yeye alifanya, ndiyo, mara mbili ya hesabu ya alivyofanya; katika kikombe ambacho ndani yacho yeye aliweka mchanganyiko wekea yeye mara mbili ya mchanganyiko huo. Kwa kadiri ambayo yeye alijitukuza mwenyewe na akaishi katika anasa ya kutoona aibu, kwa kadiri hiyo mpe yeye teso na ombolezo. Kwa maana katika moyo wake yeye hufuliza kusema, ‘Mimi naketi nikiwa malkia, na mimi si mjane, na mimi sitaona kamwe ombolezo.’ Hiyo ndiyo sababu katika siku moja tauni zake zitakuja, kifo na ombolezo na njaa kuu, na yeye atachomwa kabisa kwa moto, kwa sababu Yehova Mungu, ambaye alihukumu yeye, ni imara sana.”—Ufunuo 18:5-8, NW.

      24. (a) Ni lazima watu wa Mungu wakimbie kutoka Babuloni Mkubwa ili waepuke nini? (b) Wale wanaoshindwa kukimbia kutoka katika Babuloni Mkubwa wanashiriki naye madhambi gani?

      24 Ni maneno yenye nguvu, hayo! Kwa hiyo tendo linatakwa. Yeremia alihimiza watu katika siku yake watende, akisema: “Kimbieni kutoka katikati ya Babuloni, . . . kwa maana ni wakati wa kisasi ambacho ni cha Yehova. Kuna tendeo ambalo yeye analipa kurudisha kwa yeye. Ondokeni katikati yake, O watu wangu, na kila mmoja aandalilie nafsi yake mponyoko kutoka kasirani yenye kuwaka ya Yehova.” (Yeremia 51:6, 45, NW) Katika njia kama hiyo, sauti kutoka katika mbingu inaonya watu wa Mungu leo wakimbie kutoka Babuloni Mkubwa ili wasipokee sehemu ya tauni zake. Hukumu za Yehova zilizo kama tauni juu ya ulimwengu huu, kutia na Babuloni Mkubwa, zinapigiwa mbiu sasa. (Ufunuo 8:1–9:21; 16:1-21) Watu wa Mungu wanahitaji kujitenga wenyewe na dini bandia ikiwa wao wenyewe hawataki kupatwa na tauni hizi na mwishowe kabisa wafe naye. Waaidha, kubaki ndani ya tengenezo hilo kungewafanya washiriki katika madhambi yake. Wao wangekuwa na hatia kama yeye ya uzinzi wa kiroho na ya kumwaga damu “ya wale wote ambao wamechinjwa juu ya dunia.”—Ufunuo 18:24, NW; linga Waefeso 5:11; 1 Timotheo 5:22.

      25. Ni katika njia zipi watu wa Mungu waliondoka katika Babuloni wa kale?

      25 Ingawa hivyo, ni jinsi gani watu wa Mungu huondoka katika Babuloni Mkubwa? Katika kisa cha Babuloni wa kale, Wayahudi walikuwa sharti wafanye safari halisi kutoka katika jiji la Babuloni moja kwa moja hadi Bara la Ahadi. Lakini zaidi ya hilo lilihusika. Kiunabii Isaya aliambia Waisraeli hivi: “Geukeni mbali, geukeni mbali, ondokeni humo, msiguse kitu kisicho safi; ondokeni katikati yake, jitunzeni wenyewe safi, nyinyi ambao mnapeleka vyombo vya Yehova.” (Isaya 52:11, NW) Ndiyo, wao walipaswa waache mazoea yote yasiyo safi ya dini ya Kibabuloni ambayo yangeelekea kuitia kutu ibada yao kwa Yehova.

      26. Wakristo Wakorintho walitiije maneno haya, ‘Ondokeni kutoka miongoni mwao na mwache kabisa kugusa kitu kisicho safi’?

      26 Mtume Paulo alinukuu maneno ya Isaya katika barua yake kwa Wakorintho, akisema: “Msipate kuwa wenye kufungiwa nira isivyofaa pamoja na wasioitikadi. Kwa maana ni ushirika gani uadilifu unao pamoja na ukosefu wa kutii sheria? Au ni hisa gani nuru inayo pamoja na giza? . . . ‘Kwa hiyo ondokeni kutoka miongoni mwao, na kujitenga nyinyi wenyewe,’ asema Yehova, ‘Na acheni kabisa kugusa kitu kisicho safi.’” Haikuwa lazima Wakristo wa Korintho waache Korintho ili watii amri hiyo. Hata hivyo, wao walikuwa na lazima ya kuepuka kihalisi mahekalu yasiyo safi ya dini bandia, pamoja na kujitenga wenyewe kiroho na matendo yasiyo safi ya waabudu sanamu hao. Katika 1919 watu wa Mungu walianza kukimbia kutoka katika Babuloni Mkubwa kwa njia hiyo, wakijisafisha wenyewe mabaki yoyote ya mafundisho na mazoea yasiyo safi. Hivyo, waliweza kutumikia yeye wakiwa watu wake waliosafishwa.—2 Wakorintho 6:14-17, NW; 1 Yohana 3:3.

      27. Ni milingano gani iliyopo kati ya hukumu juu ya Babuloni wa kale na juu ya Babuloni Mkubwa?

      27 Anguko la Babuloni wa kale na ukiwa uliofuata lilikuwa adhabu kwa ajili ya madhambi yake. “Kwa maana moja kwa moja hukumu zake zimefika katika zile mbingu.” (Yeremia 51:9, NW) Hali moja na hiyo, madhambi ya Babuloni Mkubwa “yametungamana pamoja moja kwa moja hadi kwenye mbingu,” ili ziangaliwe na Yehova mwenyewe. Yeye ana hatia ya utovu wa haki, ibada ya sanamu, utovu wa adili, uonevu, unyakuzi, na uuaji kimakusudi. Anguko la Babuloni wa kale lilikuwa kwa sehemu, kisasi kwa yale ambayo lilikuwa limefanyia hekalu la Yehova na waabudu wa kweli wake. (Yeremia 50:8, 14; 51:11, 35, 36) Anguko la Babuloni Mkubwa na uharibifu wake utakaofuata hali moja na hiyo huonyesha kisasi kwa yale ambayo yeye amefanyia waabudu wa kweli katika muda wote wa karne zilizopita. Kweli kweli, uharibifu wake wa mwisho kabisa ni mwanzo wa “siku ya kisasi upande wa Mungu wetu.”—Isaya 34:8-10; 61:2, NW; Yeremia 50:28.

      28. Ni kiwango gani cha haki anachotumia Yehova kwa Babuloni Mkubwa, na kwa sababu gani?

      28 Chini ya Sheria ya Musa, ikiwa Mwisraeli aliiba kutoka wananchi wenzake, alikuwa sharti alipe ili kurudisha angalau maradufu katika kufidia. (Kutoka 22:1, 4, 7, 9) Katika uharibifu unaokuja wa Babuloni Mkubwa, Yehova atatumia kiwango kinacholinganika na hicho cha haki. Yeye atapokea maradufu ya yale aliyotoa. Hakutakuwa na rehema kwa sababu Babuloni Mkubwa hakuonyesha rehema yoyote kwa majeruhi wake. Yeye alijilisha kidusia juu ya watu wa dunia ili kujidumisha mwenyewe katika “anasa ya kutoona aibu.” Sasa yeye atateseka na kuomboleza. Babuloni wa kale alihisi alikuwa katika hali ya usalama kabisa, akijigamba: “Mimi sitaketi kama mjane, na mimi sitajua hasara ya watoto.” (Isaya 47:8, 9, 11, NW) Babuloni Mkubwa huhisi yu salama. Lakini uharibifu wake, ulioamriwa na Yehova ambaye “ni imara sana,” utatukia chakachaka, kana kwamba “katika siku moja”!

      [Maelezo ya Chini]

      a New World Translation Reference Bible, kielezi cha chini.

      [Sanduku katika ukurasa wa 263]

      “Wafalme . . . Walifanya Uasherati na Yeye”

      Mapema katika miaka ya 1800 wauza-bidhaa wa Ulaya walikuwa wakiingiza kimagendo ndani ya China viasi vikubwa vya kasumba. Katika Machi 1839 maofisa Wachina walijaribu kukomesha uchuuzi huo usio halali kwa kukamata masanduku 20,000 ya dawa hiyo ya kulevya kutoka kwa wauza-bidhaa Waingereza. Hili liliongoza kwenye wasiwasi kati ya Uingereza na China. Mahusiano kati ya nchi hizo mbili yalipozorota, baadhi ya wamisionari Waprotestanti walihimiza Uingereza kwenda vitani, kwa taarifa kama hizi zifuatazo:

      “Jinsi magumu haya yanavyoshangilisha moyo wangu kwa sababu mimi nafikiri huenda serikali ya Uingereza ikakasirishwa vikali, na Mungu, katika nguvu Zake huenda akavunjavunja migogoro inayozuia gospeli ya Kristo isiingie China.”—Henrietta Shuck, misionari wa Baptisti ya Kusini.

      Hatimaye, vita ikafyatuka—vita ambayo leo hujulikana kuwa Vita ya Kasumba. Kwa moyo wote wamisionari walichochea Uingereza kwa maelezo kama haya:

      “Mimi nalazimika kutazama nyuma juu ya hali ya sasa ya mambo sana sana si kuwa ni shauri la kasumba au la Uingereza, kuwa ndilo kusudi kubwa la Mwelekezo wa Kimungu ili kufanya uovu wa mwanadamu utii makusudi Yake ya rehema kuelekea China katika kupenya ukuta wayo wa kujitenga.”—Peter Parker, misionari Mkongrigeshonali.

      Misionari mwingine Mkongrigeshonali, Samuel W. Williams, aliongeza hivi: “Mkono wa Mungu ni wazi katika yale yote ambayo yamefanyika kwa jinsi ya kutokeza, na sisi hatutii shaka kwamba Yeye ambaye alisema alikuja kuleta upanga juu ya dunia amekuja hapa na kwamba ni kwa ajili ya uharibifu mwepesi wa maadui Wake na kusimamishwa kwa ufalme Wake. Yeye atapindua na kupindua mpaka Yeye awe amemthibitisha Mwana-Mfalme wa Amani.”

      Kwa mintarafu ya chinjo lenye kuogofya la wanataifa Wachina, misionari J. Lewis Shuck aliandika: “Mimi huona mandhari kama hizo . . . kuwa ala za Bwana za moja kwa moja katika kuondolea mbali takataka ambayo inazuia usongaji mbele wa Ukweli wa Kimungu.”

      Misionari Mkongrigeshonali Elijah C. Bridgman aliongeza: “Mara nyingi Mungu ametumia mkono imara wa mamlaka ya kiserikali ili kutayarisha njia kwa ajili ya ufalme Wake . . . Chombo katika nyakati hizi zenye maana ni cha kibinadamu; nguvu yenye kuelekeza ni ya kimungu. Gavana mkuu wa mataifa yote ametumia Uingereza kuadhibu na kunyenyekeza China.”—Manukuu yamechukuliwa kutoka “Ends and Means,” 1974, insha ya Stuart Creighton Miller iliyotangazwa katika The Missionary Enterprise in China and America (Durusi la Harvard lililohaririwa na John K. Fairbank).

      [Picha katika ukurasa wa 264]

      “Wauza-Bidhaa Wasafiri . . . Wakawa na Utajiri”

      “Kati ya 1929 na mfyatuko wa Vita ya Ulimwengu 2, [Bernadino] Nogara [msimamizi wa mambo ya kifedha wa Vatikani] aligawia Vatikani jiji kuu na mawakili wa Vatikani kufanya kazi katika maeneo ya namna namna ya uchumi wa Italia—hasa katika nguvu za umeme, mawasiliano ya simu, karidhi na kazi za benki, njia za reli ndogondogo, na ufanyizaji wa zana za kilimo, saruji, na nyuzi za nguo za kubuniwa. Nyingi za shughuli hizi zilifanikiwa.

      “Nogara alinyakua kampuni kadhaa kutia na La Società Italiana della Viscosa, La Supertessile, La Società Meridionale Industrie Tessili, na La Cisaraion. Akiunganisha hizi kuwa kampuni moja, ambayo aliita CISA-Viscosa na akaiweka chini ya usimamizi wa Baron Francesco Maria Oddasso, mmojapo makabwela wa Vatikani wenye kuitibariwa zaidi sana, kisha Nogara akaongoza mambo kwa werevu ili kampuni hiyo mpya itwaliwe na [kampuni] ya Italia iliyo kubwa zaidi sana ya kufanyiza nguo, SNIA-Viscosa. Hatimaye faida za Vatikani katika SNIA-Viscosa zikakua zikawa kubwa zaidi na zaidi, na baada ya wakati Vatikani ikachukua udhibiti—kama inavyoshuhudiwa na uhakika wa kwamba baadaye Baron Oddasso akawa makamu wa msimamizi.

      “Ndivyo Nogara akapenya ndani ya kiwanda cha nguo. Yeye alipenya ndani ya viwanda vingine katika njia nyingine nyingine, kwa maana Nogara alikuwa mwenye vitimbi vingi. Mtu huyu asiye na ubinafsi . . . pengine alifanya mengi zaidi kutia uhai katika uchumi wa Italia kuliko mwanabiashara mwingine yeyote mmoja katika historia ya Italia . . . Benito Mussolini hakuweza kamwe kupata kabisa milki ambayo yeye aliotea ndoto, lakini yeye aliwezesha Vatikani na Bernadino Nogara kubuni utawala wa aina nyingine.”—The Vatican Empire, cha Nino Lo Bello, kurasa 71-3.

      Hiki ni kielelezo kimoja tu cha ushirikiano wa karibu karibu kati ya wauza-bidhaa wa dunia na Babuloni Mkubwa. Si ajabu kwamba wauza-bidhaa hawa wataomboleza wakati mshirika wao wa kibiashara atakapokuwa hayupo tena!

      [Picha katika ukurasa wa 259]

      Wanadamu walipoenea katika dunia yote, walichukua dini ya Kibabuloni pamoja nao

      [Picha katika ukurasa wa 261]

      Jamii ya Yohana, kama mlinzi, hupiga mbiu kwamba Babuloni ameanguka

      [Picha katika ukurasa wa 266]

      Magofu ya Babuloni wa kale yanaonya kimbele juu ya angamio linalokuja la Babuloni Mkubwa

  • Kuomboleza na Kushangilia Mwisho wa Babuloni
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Sura ya 37

      Kuomboleza na Kushangilia Mwisho wa Babuloni

      1. “Wafalme wa dunia” watatendaje kwa kuitikia uharibifu wa ghafula wa Babuloni Mkubwa?

      MWISHO wa Babuloni ni habari njema kwa watu wa Yehova, lakini mataifa yanauonaje? Yohana anatuambia: “Na wafalme wa dunia ambao walifanya uasherati na yeye na wakaishi katika anasa yenye utovu wa aibu watatoa machozi na kujipigapiga wenyewe kwa kihoro juu yake, wanapotazama moshi kutoka kuchomwa kwake, huku wao wakisimama mbali kwa sababu ya hofu yao ya teso lake na kusema, ‘Ni vibaya mno, ni vibaya mno, wewe jiji kubwa, Babuloni wewe jiji imara, kwa sababu katika saa moja hukumu yako imewasili!’”—Ufunuo 18:9, 10, NW.

      2. (a) Kwa kuwa pembe kumi za ufananisho za hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu zitamharibu Babuloni Mkubwa, ni kwa nini “wafalme wa dunia” wanahuzunikia mwisho wake? (b) Ni kwa nini hao wafalme wenye kihoro husimama mbali na jiji lililohukumiwa maangamizi?

      2 Tendo-mwitikio la mataifa huenda likaonekana kuwa la kushangaza kwa sababu ya uhakika wa kwamba Babuloni aliharibiwa na zile pembe kumi za ufananisho za hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu. (Ufunuo 17:16) Lakini Babuloni atakapokuwa hayupo, kwa wazi “wafalme wa dunia” watang’amua jinsi alivyokuwa mwenye mafaa kwao katika kutuliza watu na kuwatiisha. Viongozi wa kidini wamejulisha wazi vita kuwa vitakatifu, wakatenda wakiwa mawakili wa kuandikisha askari-jeshi, na wakahubiri vijana waingie katika mapigano. Dini imeandaa kisetiri cha utakatifu ambacho nyuma yacho watawala wafisadi wameendesha mambo katika kukandamiza makabwela. (Linga Yeremia 5:30, 31; Mathayo 23:27, 28.) Hata hivyo, angalia kwamba wafalme hawa wenye kihoro sasa wanasimama mbali na hilo jiji lenye kuhukumiwa maangamizi. Wao hawakaribii vya kutosha ili kuliauni. Wao wanahuzunikia kuona linaenda lakini hawahuzuniki vya kutosha kujihatarisha kwa ajili yalo.

      Wauza-Bidhaa Watoa Machozi na Kuomboleza

      3. Ni nani wengine wanaojutia kupita kwa Babuloni Mkubwa, na Yohana hutoa sababu zipi juu ya hilo?

      3 Wafalme wa dunia sio pekee wanaojutia kupita kwa Babuloni Mkubwa. “Pia, wauza-bidhaa wasafiri wa dunia wanatoa machozi na kuomboleza juu ya yeye, kwa sababu hakuna wa kununua tena bidhaa yao kamili, bidhaa kamili ya dhahabu na fedha na jiwe la thamani na lulu na kitani nzuri na zambarau na hariri na rangi-nyekundu-nyangavu; na kila kitu katika mbao zenye kutiwa manukato na kila aina ya kitu cha meno ya tembo na kila aina ya kitu kutokana na mbao iliyo ya thamani kubwa zaidi sana na cha shaba na cha chuma na cha marimari; pia mdalasini na vikolezo vya Kihindi na uvumba na mafuta yaliyotiwa harufu nzuri na ubani na divai na mafuta ya zeituni na unga safi sana na ngano na ng’ombe na kondoo, na farasi na makochi na watumwa na nafsi za kibinadamu. Ndiyo, na tunda zuri ambalo nafsi yako ilitamani limeondoka kutoka kwa wewe [Babuloni Mkubwa], na vitu vitamu-vitamu vyote na vitu vya umaridadi vimepotelea mbali kutoka kwa wewe, na watu hawatavipata tena kamwe.”—Ufunuo 18:11-14, NW.

      4. Ni kwa nini “wauza-bidhaa wasafiri” hutoa machozi na kuombolezea mwisho wa Babuloni Mkubwa?

      4 Ndiyo, Babuloni Mkubwa alikuwa rafiki ya karibu na mteja mwema wa wauza-bidhaa wenye ukwasi. Mathalani, kwa muda wa karne zilizopita nyumba za watawa-waume, nyumba za watawa wa kike na makanisa ya Jumuiya ya Wakristo zimejipatia kiasi kikubwa mno cha dhahabu, fedha, mawe ya thamani, mbao za thamani, na namna nyinginezo za ukwasi wa vitu vya kimwili. Na zaidi, baraka ya kidini imetolewa juu ya shamrashamra za ununuzi wa kianasa na karamu za ulafi, ulevi na uasherati zinazoandamana na mwadhimisho wa Krismasi wenye kuvunjia Kristo heshima na siku nyinginezo zinazoitwa eti takatifu. Wamisionari wa Jumuiya ya Wakristo wamepenya ndani ya mabara ya mbali, wakafungua masoko mapya kwa ajili ya “wauza-bidhaa wasafiri” wa ulimwengu huu. Katika Japani ya karne ya 17, Ukatoliki, uliokuja pamoja na wachuuzi hata ulijihusisha katika vita vyenye uhasama wa daima. Ikiripoti juu ya vita yenye kukata maneno chini ya kuta za ngome ya Osaka, The Encyclopædia Britannica hutaarifu hivi: “Vikosi vya Tokugawa vilijikuta vikipigana dhidi ya adui ambaye bendera zake zilikuwa zimepambwa kwa msalaba na mifano ya Mwokozi na ya [Mt.] James, mtakatifu mfadhili wa Hispania.” Chamkano yenye kushinda ilinyanyasa na karibu imalize Ukatoliki katika bara hilo. Ushiriki wa kanisa katika mambo ya ulimwengu leo vilevile hautaliletea baraka.

      5. (a) Sauti kutoka katika mbingu inaelezaje zaidi kuomboleza kwa hao “wauza-bidhaa wasafiri”? (b) Ni kwa nini wauza-bidhaa ‘wanasimama mbali’ pia?

      5 Sauti kutoka katika mbingu inasema zaidi hivi: “Wauza-bidhaa wasafiri wa vitu hivi, ambao wakawa na utajiri kutokana na yeye, watasimama mbali kwa sababu ya hofu yao ya teso lake na watatoa machozi na kuomboleza, kusema, ‘Ni vibaya mno, ni vibaya mno—jiji kubwa, lililovikwa kitani nzuri na zambarau na rangi-nyekundu-nyangavu, na kurembwa kitajiri kwa madoido ya dhahabu na jiwe la thamani na lulu, kwa sababu katika saa moja utajiri mwingi hivyo umeteketezwa!’” (Ufunuo 18:15-17a, NW) Kwa sababu ya kuharibiwa kwa Babuloni Mkubwa, “wauza-bidhaa” wanaombolezea hasara ya mshirika wa kibiashara huyo. Kwa kweli, “ni vibaya mno, ni vibaya mno” kwao. Hata hivyo, angalia kwamba sababu za kuomboleza kwao ni za ubinafsi kabisa na kwamba wao—kama vile wafalme—‘husimama mbali.’ Wao hawakaribii sana vya kutosha ili wasaidie Babuloni Mkubwa.

      6. Sauti kutoka katika mbingu inaelezaje kuomboleza kwa makapteni wa meli na mabaharia, na ni kwa nini wao hutoa machozi?

      6 Simulizi laendelea: “Na kila kapteni wa meli na kila mtu ambaye husafiri kwa meli kokote, mabaharia na wale wote ambao hupata riziki kwa bahari, walisimama mbali na kupiga kilio kikuu walipotazama moshi wa kuchomwa kwake na kusema, ‘Ni jiji gani lililo kama jiji kubwa?’ Na wao wakatupa mavumbi juu ya vichwa vyao na kupiga kilio kikuu, wakitoa machozi na kuomboleza, na wakasema, ‘Ni vibaya mno, ni vibaya mno—jiji kubwa, ambalo katika hilo wale wote wenye mashua kwenye bahari, wakawa na utajiri kwa sababu ya ughali walo, kwa kuwa katika saa moja limeteketezwa!’” (Ufunuo 18:17b-19, NW) Babuloni wa kale alikuwa jiji la kibiashara na alikuwa na kundi kubwa la meli. Hali moja na hiyo, Babuloni Mkubwa hufanya biashara nyingi sana kwa kutumia “maji mengi” ya watu wake. Hiyo huandaa kuajiriwa kwa raia wake wengi wa kidini. Uharibifu wa Babuloni Mkubwa utakuwa dharuba ya kiuchumi kama nini kwa watu hawa! Hakutakuwa kamwe na chimbuko jingine la riziki kama yeye.

      Kushangilia Juu ya Utowesho Wake

      7, 8. Sauti kutoka katika mbingu inafikiaje upeo wa ujumbe wayo kuhusu Babuloni Mkubwa, na ni nani watakaoitikia maneno hayo?

      7 Babuloni wa kale alipopinduliwa na Wamedi na Waajemi, Yeremia alisema kiunabii hivi: “Na juu ya Babuloni mbingu na dunia na wale wote walio ndani yazo kwa hakika watapiga kilio kikuu kwa kushangilia.” (Yeremia 51:48, NW) Wakati Babuloni Mkubwa aharibiwapo, sauti kutoka katika mbingu inafikisha ujumbe wayo kwenye upeo kwa kusema juu ya Babuloni Mkubwa hivi: “Uwe na nderemo juu yake, O mbingu, pia nyinyi watakatifu na nyinyi mitume na nyinyi manabii, kwa sababu kwa hukumu Mungu ametoza adhabu kutoka kwake kwa ajili ya nyinyi!” (Ufunuo 18:20, NW) Yehova na malaika watapendezwa sana kuona utowesho wa adui wa kale wa Mungu, kama vile watakavyopendezwa mitume na wale manabii Wakristo wa mapema, ambao kwa sasa wamefufuliwa na wamechukua cheo chao katika ule mpango wa wazee 24.—Linga Zaburi 97:8-12.

      8 Kweli kweli, “watakatifu” wote,—wawe wamefufuliwa kwenda kwenye mbingu au wangali wanaendelea kuishi duniani—watapiga kilio kikuu kwa shangwe, kama vile utakavyofanya umati mkubwa wa kondoo wengine unaoshirikiana nao. Baada ya wakati kupita, watu wote waaminifu wa zamani watafufuliwa ndani ya mfumo mpya wa mambo, na wao vilevile watajiunga katika kushangilia. Watu wa Mungu hawakujaribu kujilipiza kisasi wenyewe juu ya wanyanyasaji wao wa dini bandia. Wao wamekumbuka maneno ya Yehova: “Kisasi ni changu mimi; mimi nitalipa, asema Yehova.” (Warumi 12:19; Kumbukumbu 32:35, 41-43, NW) Basi, Yehova amelipa sasa. Damu yote iliyomwagwa na Babuloni Mkubwa itakuwa imekwisha lipizwa kisasi.

      Kuvurumisha Jiwe Kubwa la Kusagia

      9, 10. (a) Sasa malaika kabambe anafanya na kusema nini? (b) Ni tendo gani kama hilo linalofanywa na huyo malaika wa Ufunuo 18:21 lilitukia katika siku ya Yeremia, na hilo lilitoa dhamana gani? (c) Tendo linalochukuliwa na malaika kabambe aliyeonwa na Yohana linatoa dhamana gani?

      9 Jambo ambalo Yohana anafuata kuona linathibitisha kwamba hukumu ya Yehova juu ya Babuloni Mkubwa ni ya kukata maneno: “Na malaika kabambe akainua juu jiwe kama jiwe kubwa la kusagia na kulivurumisha ndani ya bahari, kusema: ‘Hivyo kwa mtupo wa kasi sana Babuloni jiji kubwa atavurumishwa chini, na yeye hatapatikana kamwe tena.’” (Ufunuo 18:21, NW) Katika wakati wa Yeremia, tendo kama hilo likiwa na maana kubwa ya kiunabii lilifanywa. Yeremia alivuviwa aandike katika kitabu “mabaa yote ambayo yangekuja juu ya Babuloni.” Yeye alimpa Seraya kitabu na kumwambia asafiri hadi Babuloni. Huko, akifuata maagizo ya Yeremia, Seraya alisoma julisho-wazi dhidi ya jiji hilo: “O Yehova, wewe mwenyewe umesema dhidi ya mahali hapa, ili kupakatilia mbali pasipate kuwa na mkazi ndani yapo, ama binadamu ama hata mnyama wa nyumbani, bali kwamba pawe mahali patupu tu penye ukiwa hadi wakati usio dhahiri.” Kisha Seraya akafungilia jiwe kwenye kitabu na kukitupa ndani ya mto Eufrati, akisema: “Hivi ndivyo Babuloni litazama chini na halitainuka kamwe kwa sababu ya baa ambalo mimi ninaleta juu yake.”—Yeremia 51:59-64, NW.

      10 Kutupwa kwa kitabu ndani ya mto kikiwa kimefungiliwa jiwe kulikuwa dhamana kwamba Babuloni lingetumbukia ndani ya hali ya kutokomea kabisa, lisipate kupona kamwe. Kuona kwa mtume Yohana malaika kabambe akifanya tendo linalofanana na hilo hali kadhalika ni dhamana yenye nguvu kwamba kusudi la Yehova kuelekea Babuloni Mkubwa litatimizwa. Hali ya kuangamia kabisa ya Babuloni wa kale leo hushuhudia kwa nguvu sana kitakachoangukia dini bandia katika wakati ujao ulio karibu.

      11, 12. (a) Sasa malaika kabambe anahutubiaje Babuloni Mkubwa? (b) Yeremia alitoaje unabii kuhusu Yerusalemu lililoasi imani, na huo uliashiria nini kwa ajili ya siku yetu?

      11 Sasa malaika kabambe anahutubia Babuloni Mkubwa, kusema hivi: “Na sauti ya waimbaji ambao hujifuatanisha kwa kinubi na ya wanamuziki na ya wanafilimbi na ya wanatarumbeta haitasikiwa tena kamwe ndani ya wewe, na hakuna fundi wa kazi ya uchumi yoyote ambaye atapatikana tena wakati wowote ndani ya wewe, na hakuna sauti ya jiwe la kusagia itakayosikika tena wakati wowote ndani yako, na hakuna nuru ya taa ambayo itaangaza tena wakati wowote ndani ya wewe, na hakuna sauti ya bwana-arusi na ya bibi-arusi ambayo itasikiwa tena wakati wowote ndani ya wewe; kwa sababu wauza-bidhaa wasafiri wako walikuwa ndio watu wenye vyeo vya juu wa dunia, kwa maana kwa zoea lako la uwasiliano na roho mataifa yote yaliongozwa vibaya.”—Ufunuo 18:22, 23, NW.

      12 Kwa semi zinazolinganika, Yeremia alitoa unabii kuhusu Yerusalemu asi-imani: “Mimi nitaharibu kutoka wao mvumo wa mchachawo na mvumo wa kushangilia, na sauti ya bwana-arusi na sauti ya bibi-arusi, na mvumo wa kinu cha mkono na nuru ya taa. Na bara hili lote lazima liwe mahali palipoteketezwa na kitu cha kutia kimako.” (Yeremia 25:10, 11, NW) Ikiwa ndiyo sehemu kuu ya Babuloni Mkubwa, Jumuiya ya Wakristo itakuwa magofu yasiyo na uhai, kama vile imeonyeshwa wazi sana na ukiwa wa Yerusalemu baada ya 607 K.W.K. Jumuiya ya Wakristo ambayo wakati mmoja ilishangilia kwa moyo mkunjufu na ikashughulika kwa kelele ya kila siku itajikuta yenyewe ikiwa imeshindwa na kutupiliwa mbali.

      13. Ni badiliko gani la ghafula linalomfikilia Babuloni Mkubwa, na tokeo ni nini kwa “wauza-bidhaa wasafiri” wake?

      13 Kweli kweli, kama vile malaika huyo anavyomwambia Yohana, Babuloni Mkubwa wote atageuka kutoka milki ya ulimwengu yenye nguvu, na kuwa bara-ukiwa kavu mithili ya mahame. “Wauza-bidhaa” wake, kutia na mamilionea wa vyeo vya juu, wametumia dini yake kwa kujinufaisha kibinafsi au kama kisetiri cha mabaya, na hao viongozi wa kidini wameliona kuwa jambo lenye kufaidi kushiriki pamoja nao katika umashuhuri huo. Lakini wauza-bidhaa hao hawatakuwa tena na Babuloni Mkubwa akiwa mshirika wao katika kufanya mabaya. Yeye hatayapofusha macho tena mataifa ya dunia kwa mazoea ya mafumbo yake ya kidini.

      Hatia ya Damu Yenye Kutisha

      14. Ni nini anayotoa malaika kabambe kuwa ndiyo sababu ya ukali wa hukumu ya Yehova, na Yesu alisema nini hali moja na hivyo wakati alipokuwa duniani?

      14 Kwa kumalizia, malaika kabambe amwambia Yohana sababu ya Yehova kumhukumu Babuloni Mkubwa kwa ukali hivyo. “Ndiyo,” asema malaika, “katika yeye ilipatikana damu ya manabii na ya watakatifu na ya wale wote ambao wamechinjwa juu ya dunia.” (Ufunuo 18:24, NW) Alipokuwa duniani, Yesu aliambia viongozi wa kidini kwamba wao walistahili kutozwa hesabu kwa ajili ya “damu yote yenye uadilifu iliyomwagwa juu ya dunia, kutoka damu ya Abeli mwadilifu” na kuendelea. Kulingana na hilo, kizazi hicho kombokombo kiliharibiwa katika 70 W.K. (Mathayo 23:35-38, NW) Leo, kizazi kingine cha wanadini kinabeba hatia ya damu kwa ajili ya kunyanyasa watumishi wa Mungu.

      15. Kanisa Katoliki katika Ujeremani ya Nazi lilikuwaje na hatia ya damu katika visa viwili?

      15 Katika kitabu chake The Catholic Church and Nazi Germany, Guenter Lewy anaandika: “Wakati Mashahidi wa Yehova walipokandamizwa katika Bavaria Aprili 13 [1933] Kanisa hata lilikubali mgawo liliopewa na Wizara ya Elimu na Dini wa kuripoti juu ya washiriki wa farakano hilo walioendelea kuzoea dini hiyo iliyokatazwa.” Hivyo Kanisa Katoliki linashiriki daraka la kupelekwa kwa maelfu ya Mashahidi kwenye kambi za mateso; mikono yalo imetiwa madoa ya damu ya uhai wa mamia ya Mashahidi ambao walinyongwa. Wakati Mashahidi vijana, kama Wilhelm Kusserow, walipoonyesha kwamba wangekufa kijasiri kwa kupigwa risasi na kikosi cha wapiga risasi, Hitla aliamua kwamba kikosi cha wapiga risasi hakikuwafaa wakataaji kidhamira; kwa hiyo Wolfgang ndugu ya Wilhelm, akiwa na umri wa miaka 20, alikufa kwa njia ya gilotini. Wakati ule ule, Kanisa Katoliki lilikuwa likiwatia moyo vijana Wakatoliki Wajeremani wafe katika jeshi la bara-baba lao. Hatia ya damu ya hilo kanisa yaonekana wazi!

      16, 17. (a) Ni hatia gani ya damu ambayo ni lazima Babuloni Mkubwa ashtakiwe, na Vatikani ilikuwaje na hatia ya damu kuhusu Wayahudi waliouawa katika michinjo-chinjo ya Kinazi? (b) Ni katika njia gani moja ambayo kwayo dini bandia ina lawama kwa ajili ya kuuawa kwa mamilioni ya watu katika mamia ya vita katika nyakati zetu?

      16 Hata hivyo, unabii unasema kwamba lazima Babuloni Mkubwa ashtakiwe kwa damu ya “wale wote ambao wamechinjwa juu ya dunia.” Hakika hilo limekuwa kweli katika nyakati za ki-siku-hizi. Mathalani, kwa kuwa hila ya Katoliki ndiyo iliyomsaidia Hitla apate mamlaka katika Ujeremani, Vatikani inashiriki hatia ya damu iliyo mbaya sana juu ya Wayahudi milioni sita waliokufa katika michinjo-chinjo ya Kinazi. Na zaidi, katika nyakati zetu, watu zaidi ya milioni mia moja wameuawa katika mamia ya vita. Je! dini bandia ina lawama kwa habari hii? Ndiyo, kwa njia mbili.

      17 Njia moja ni kwamba vita vingi vinahusiana na tofauti za kidini. Mathalani, jeuri katika India kati ya Waislamu na Wahindu katika 1946-48 ilichochewa na dini. Mamia ya maelfu ya maisha yalipotea. Pambano kati ya Iraki na Irani katika miaka ya 1980 lilihusiana na tofauti za kimafarakano, kukiwa na mamia ya maelfu waliouawa. Jeuri kati ya Wakatoliki na Waprotestanti katika Ailandi ya Kaskazini imetwaa maelfu ya maisha. Akichunguza uwanja huu, mleta habari za magazetini C. L. Sulzberger alisema hivi katika 1976: “Ni ukweli wenye kuhuzunisha kwamba pengine nusu au zaidi ya vita vinavyopiganwa sasa kotekote katika ulimwengu ama kwa wazi ni mapambano ya kidini ama yanahusu mabishano ya kidini.” Kweli kweli, imekuwa hivyo muda wote wa historia yenye msukosuko ya Babuloni Mkubwa.

      18. Ni ipi njia ya pili ambayo kwayo dini za ulimwengu zina hatia ya damu?

      18 Ni ipi ile njia nyingine? Kwa maoni ya Yehova, dini za ulimwengu zina hatia ya damu kwa sababu hizo hazikufundisha kwa kusadikisha wafuasi wazo ukweli wa matakwa ya Yehova kwa ajili ya watumishi wake. Hizo hazikufundisha watu kwa kusadikisha kwamba waabudu wa kweli lazima wamwige Yesu Kristo na kuonyesha wengine upendo bila kujali asili yao ya kitaifa. (Mika 4:3, 5; Yohana 13:34, 35; Matendo 10:34, 35; 1 Yohana 3:10-12) Kwa sababu dini ambazo zinajumlika kuwa Babuloni Mkubwa hazikufundisha vitu hivi, wafuasi wazo wamevutwa kuingizwa ndani ya kizingo cha vita vya kimataifa. Lo! jinsi hilo lilivyokuwa wazi katika vile vita viwili vya ulimwengu vya nusu ya kwanza ya karne ya 20, ambavyo vyote viwili vilianza katika Jumuiya ya Wakristo na vikatokeza kuchinjana kwa wanadini! Ikiwa wote wanaodai kuwa Wakristo wangalishikamana na kanuni za Biblia, vita hivyo havingaliweza kutukia kamwe.

      19. Ni hatia ya damu gani yenye kutisha sana anayobeba Babuloni Mkubwa?

      19 Yehova anaweka lawama la umwagaji-damu huu wote kwenye nyayo za Babuloni Mkubwa. Ikiwa viongozi wa kidini, hasa wale walio katika Jumuiya ya Wakristo, wangalifundisha watu wao ukweli wa Biblia, umwagaji-damu mkubwa sana hivyo haungalitukia. Kwa kweli, basi, kwa njia ya moja kwa moja au isiyo ya moja kwa moja, Babuloni Mkubwa—yule kahaba mkubwa na milki ya ulimwengu ya dini bandia—lazima amjibu Yehova si kwa ajili ya “damu ya manabii na ya watakatifu” tu ambao yeye amenyanyasa na akaua bali pia kwa ajili “ya wale wote ambao wamechinjwa juu ya dunia.” Kweli kweli Babuloni Mkubwa anabeba hatia ya damu yenye kutisha sana. Na apotelee mbali wakati uharibifu wake unapotukia!

      [Sanduku katika ukurasa wa 270]

      Gharama ya Kuridhiana

      Guenter Lewy anaandika katika kitabu chake The Catholic Church and Nazi Germany: “Kama Ukatoliki wa Ujeremani tangu mwanzo ungalishikamana na mwongozo wa kupinga kwa dhati utawala wa Nazi, historia ya ulimwengu ingaliweza kuchukua mwendo tofauti. Hata kama mng’ang’ano huu ungalikosa mwishowe kabisa kumshinda Hitla na kuzuia uhalifu wake mwingi, kwa oni hili ungaliinua sana hadhi ya kiadili ya Kanisa hilo. Gharama ya kibinadamu kwa ukinzani huu ingalikuwa kubwa bila kukanika, lakini dhabihu hizo zingalikuwa zimetolewa kwa ajili ya kusudi kubwa zaidi ya yote. Hitla akiwa haungwi mkono nyumbani, yamkini hangalithubutu kwenda vitani na kihalisi mamilioni ya maisha yangaliokolewa. . . . Wakati Wajeremani wapinga Unazi walipoteswa mpaka kifo katika kambi za mateso za Hitla, wakati weledi wa Polandi walipochinjwa, wakati mamia ya maelfu ya Warusi walipokufa kama tokeo la kutendwa kama Untermenschen [nusu-binadamu] wa Kislavi, na wakati binadamu 6,000,000 walipouawa kimakusudi kwa kuwa ‘si Waarya,’ maofisa wa Kanisa Katoliki katika Ujeremani walitegemeza utawala uliokuwa ukifanya uhalifu huu. Papa katika Roma, kichwa cha kiroho na mwalimu wa kiadili mkuu zaidi ya wote wa Kanisa Katoliki la Roma, alikaa kimya.”—Kurasa 320, 341.

      [Picha katika ukurasa wa 268]

      “Ni vibaya mno, ni vibaya mno,” wasema watawala

      [Picha katika ukurasa wa 268]

      “Ni vibaya mno, ni vibaya mno,” wasema wauza-bidhaa

  • Sifuni Yah kwa Hukumu Zake!
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Sura ya 38

      Sifuni Yah kwa Hukumu Zake!

      1. Yohana anasikia maneno gani “kama sauti kubwa ya umati mkubwa katika mbingu”?

      BABULONI MKUBWA hayupo tena! Kwa kweli hizi ni habari zenye shangwe. Si ajabu kwamba Yohana anasikia mipaazo yenye furaha katika mbingu! “Baada ya vitu hivi mimi nikasikia kilichokuwa kama sauti kubwa ya umati mkubwa katika mbingu. Wao walisema: ‘Halleluyah!a Wokovu na utukufu na nguvu ni za Mungu wetu, kwa sababu hukumu zake ni za kweli na za uadilifu. Kwa maana yeye ametekeleza hukumu juu ya kahaba mkubwa ambaye alifisidi dunia kwa uasherati wake, na yeye amelipiza kisasi cha damu ya watumwa wake katika mkono wake.’ Na mara hiyo kwa mara ya pili wao wakasema: ‘Halleluyah!b Na ule moshi kutoka kwake huendelea kupaa milele na milele.’”—Ufunuo 19:1-3, NW.

      2. (a) Neno “Halleluyah” humaanisha nini, na Yohana kulisikia mara mbili kufikia hapa huonyesha nini? (b) Ni nani anayepokea utukufu kwa kuharibu Babuloni Mkubwa? Fafanua.

      2 Halleluyah kweli kweli! Neno hilo humaanisha “Sifuni Yah, nyinyi watu,” “Yah” ikiwa ni namna ya kifupi cha jina la kimungu, Yehova. Tunakumbushwa hapa waadhi ya mtunga zaburi: “Kila kitu chenye kupumua—acheni kisifu Yah. Sifuni Yah, nyinyi watu!” (Zaburi 150:6, NW) Kusikia kwa Yohana korasi ya kimbingu yenye kuchachawa ikiimba “Halleluyah!” mara mbili kufikia hapa katika Ufunuo huonyesha mwendeleo wa ufunuo wa kimungu wa ukweli. Mungu wa Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo ndiye Mungu yule yule wa Maandiko ya Kiebrania ya mapema zaidi, na Yehova ndilo jina lake. Mungu aliyesababisha anguko la Babuloni wa kale amehukumu na akaharibu sasa Babuloni Mkubwa. Mpeni utukufu kwa tendo hilo la uhodari! Nguvu iliyoongoza kwa werevu kuanguka kwake ilikuwa yake badala ya kuwa ya mataifa ambayo yeye alitumia kuwa vyombo vya kumwacha ukiwa. Yatupasa sisi kumsifu Yehova pekee kwa ajili ya wokovu.—Isaya 12:2; Ufunuo 4:11; 7:10, 12.

      3. Ni kwa sababu gani kahaba mkubwa amestahili sana hukumu yake?

      3 Ni kwa sababu gani kahaba mkubwa amekuwa mwenye kustahili sana hukumu hii? Kulingana na Sheria ambayo Yehova alitoa kwa Noa—na kupitia yeye kwa aina ya binadamu yote—kumwaga damu kimakusudi kunataka hukumu ya kifo. Taarifa hiyo ilitolewa tena katika Sheria ya Mungu kwa Israeli. (Mwanzo 9:6; Hesabu 35:20, 21) Zaidi ya hilo, chini ya Sheria ya Musa uzinzi wa kiroho na wa kimwili ulistahilisha kifo. (Walawi 20:10; Kumbukumbu 13:1-5) Kwa maelfu ya miaka, Babuloni Mkubwa amekuwa na hatia ya damu, na yeye ni mwasherati mbaya sana. Mathalani, sera ya Kanisa Katoliki la Roma ya kukataza mapadri walo kuoa imetokeza utovu wa adili mbaya sana upande wa wengi wao, na ni wengi wa hawa leo ambao wameambukizwa UKIMWI. (1 Wakorintho 6:9, 10; 1 Timotheo 4:1-3) Lakini madhambi yake makubwa, ‘yakitungamana pamoja moja kwa moja hadi mbinguni,’ ni matendo yalo yenye kugutusha ya uasherati wa kiroho—tendo hili la pili ni katika kufundisha mafundisho bandia na kujipanga upande mmoja na wanasiasa wafisadi. (Ufunuo 18:5) Kwa kuwa adhabu yake mwishowe imemfikilia, halaiki kubwa ya kimbingu sasa yarudisha mwangwi wa pili wa Halleluyah!

      4. Ni nini kinachofananishwa na uhakika wa kwamba moshi kutoka Babuloni Mkubwa “huendelea kupaa milele na milele”?

      4 Babuloni Mkubwa amewashwa moto kama jiji lililoshindwa, na moshi wa kutoka kwake “huendelea kupaa milele na milele.” Wakati jiji halisi linapochomwa na majeshi yenye ushindi, moshi huendelea kupaa kwa muda ambao majivu ni yenye moto. Yeyote anayejaribu kulijenga tena linapoendelea kutoa moshi atachomwa tu na yale magofu yenye kutoa moshi. Kwa kuwa moshi kutoka kwake utainuka “milele na milele” katika kuonyesha hukumu yake yenye kukata maneno, hakuna yeyote atakayeweza wakati wowote kurudisha jiji hilo lenye dhambi. Dini bandia imetoweka milele na milele. Halleluyah, kweli kweli!—Linga Isaya 34:5, 9, 10.

      5. (a) Wazee 24 na viumbe hai wanne wanafanya na kusema nini? (b) Ni kwa sababu gani kibwagizo cha Halleluyah ni cha kimelodia kuliko korasi za Halleluyah zinazoimbwa katika makanisa ya Jumuiya ya Wakristo?

      5 Katika njozi ya mapema zaidi, Yohana aliona kuzunguka kiti cha ufalme viumbe hai wanne, pamoja na wazee 24 ambao ni picha ya warithi wa Ufalme wakiwa katika cheo chao kitukufu cha kimbingu. (Ufunuo 4:8-11) Sasa yeye anawaona tena na wao wanangurumisha Halleluyah ya tatu juu ya uharibifu wa Babuloni Mkubwa: “Na wale wazee ishirini na wanne na viumbe hai wanne wakaanguka chini na kuabudu Mungu aketiye juu ya kiti cha ufalme, na kusema: ‘Ameni! Halleluyah.’”c (Ufunuo 19:4, NW) Basi, korasi tukufu hii ya Halleluyah ni katika kuongezea ule “wimbo mpya” wa sifa kwa Mwana-Kondoo. (Ufunuo 5:8, 9, NW) Wao wanaimba sasa kibwagizo cha ushindi wenye utukufu, wakimpa Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu utukufu wote kwa sababu ya ushindi wake wenye kukata maneno juu ya kahaba mkubwa, Babuloni Mkubwa. Halleluyah hizi zimelia kimelodia kwa mbali zaidi sana kuliko korasi za Halleluyah zozote zilizopata kuimbwa katika makanisa ya Jumuiya ya Wakristo ambamo Yehova, au Yah, amevunjiwa heshima na akadharauliwa. Wimbaji wa kinafiki kama huo unaoshutumu jina la Yehova umekomeshwa sasa milele!

      6. Ni “sauti” ya nani inayosikiwa, nayo inahimiza nini, na ni nani wanaoshiriki katika kuitikia?

      6 Ilikuwa katika 1918 ndipo Yehova alianza kuthawabisha ‘wale wanaohofu jina lake, wadogo na wakubwa’—wa kwanza wa hawa wakiwa wa wale Wakristo wapakwa-mafuta ambao walikuwa wamekufa wakiwa waaminifu, na ambao yeye alifufua na akawaweka katika vyeo vya kimbingu vya wazee 24. (Ufunuo 11:18, NW) Wengine hujiunga na hawa katika kuimba Halleluyah, kwa kuwa Yohana huripoti hivi: “Pia, sauti moja ikatokea katika kiti cha ufalme na kusema: ‘Mwe mkisifu Mungu wetu, nyinyi nyote watumwa wake, ambao huhofu yeye, wadogo na wakubwa.’” (Ufunuo 19:5, NW) Hii ni “sauti” ya Mneni wa Yehova, Mwana wake mwenyewe, Yesu Kristo, ambaye husimama “katikati ya kiti cha ufalme.” (Ufunuo 5:6, NW) Si mbinguni tu bali pia hapa duniani, “nyinyi nyote watumwa wake” shirikini katika kuimba, jamii ya Yohana iliyopakwa mafuta ikiwa inachukua uongozi duniani. Ni kwa kuchachawa kulikoje hawa hushiriki katika kutii amri: “Mwe mkisifu Mungu wetu”!

      7. Baada ya Babuloni Mkubwa kuharibiwa, ni nani watakaokuwa wakisifu Yehova?

      7 Ndiyo, wale wa umati mkubwa pia huhesabiwa wanapewa namba pia miongoni mwa watumwa hawa. Tangu 1935 hawa wamekuwa wakitoka katika Babuloni Mkubwa na wameona utimizo wa ahadi ya Mungu: “Yeye atabariki wale ambao huhofu Yehova, wadogo na wakubwa.” (Zaburi 115:13, NW) Wakati Babuloni Mkubwa aharibiwapo, mamilioni yao watajiunga katika ‘kusifu Mungu wetu’—pamoja na jamii ya Yohana na wingi wote wa kimbingu. Baadaye, wale wenye kufufuliwa duniani, wawe hapo kwanza walikuwa mashuhuri au la, bila shaka wataimba Halleluyah zaidi wanapojifunza kwamba Babuloni Mkubwa ametoweka milele. (Ufunuo 20:12, 15) Sifa yote imwendee Yehova kwa ushindi wake wenye kishindo juu ya kahaba huyo wa tangu zamani!

      8. Korasi za sifa zilizoshuhudiwa na Yohana zapaswa kutupa sisi kichochezi gani sasa, kabla ya Babuloni Mkubwa kuharibiwa?

      8 Hayo yote yanatupa sisi kichochezi kama nini tushiriki katika kazi ya Mungu leo! Watumishi wote wa Yah na wajitoe wenyewe kwa moyo na nafsi kutangaza hukumu za Mungu, pamoja na tumaini tukufu la Ufalme, sasa, kabla ya Babuloni Mkubwa kuondolewa katika kiti na kuharibiwa.—Isaya 61:1-3; 1 Wakorintho 15:58.

      ‘Halleluyah—Yehova Ni Mfalme!’

      9. Ni kwa sababu gani Halleluyah ya mwisho ni yenye mvumo kamili, ni ya sauti timilifu, na ya hali ya juu sana?

      9 Kuna sababu zaidi kwa kushangilia, kama vile Yohana aendeleavyo kutuambia: “Na mimi nikasikia kilichokuwa kama sauti ya umati mkubwa na kama mvumo wa maji mengi na kama mvumo wa ngurumo kubwa. Zikasema: ‘Halleluyah,d kwa sababu Yehova Mungu wetu, Mweza Yote, ameanza kutawala akiwa mfalme.’” (Ufunuo 19:6, NW) Halleluyah hii ya mwisho ndiyo inayofanya mbiu iwe yenye miraba minne, au yenye ulingano. Ni mvumo wa kimbingu wenye nguvu, wa hali ya juu kuliko korasi yoyote ya kibinadamu, yenye fahari ya kifalme zaidi ya poromoko la maji lolote la kidunia, na yenye kuvuvia hofu zaidi kuliko ngurumo yoyote ya kidunia. Mamiriadi ya sauti za kimbingu yanasherehekea uhakika wa kwamba “Yehova Mungu wetu, Mweza Yote, ameanza kutawala akiwa mfalme.”

      10. Ni katika maana gani inaweza kusemwa kwamba Yehova huanza kutawala akiwa mfalme baada ya mteketeo wa Babuloni Mkubwa?

      10 Ingawa hivyo, inakuwaje kwamba Yehova huanza kutawala? Mamileani yamepita tangu mtunga zaburi alipotangaza: “Mungu ni Mfalme wangu tangu zamani za kale.” (Zaburi 74:12, NW) Umaliki wa Yehova ulikuwa wa kale hata wakati huo, kwa hiyo korasi hiyo ya ulimwengu wote mzima ingewezaje kuimba kwamba “Yehova . . . ameanza kutawala akiwa mfalme”? Katika maana ya kwamba wakati Babuloni Mkubwa anapoharibiwa, Yehova hatakuwa tena na mshindani huyo mwenye kimbelembele akikengeusha utii kwake akiwa ndiye Mwenye Enzi Kuu ya Ulimwengu Wote Mzima. Dini bandia haitachochea tena watawala wa dunia wampinge. Wakati Babuloni wa kale alipoanguka kutoka utawala wa ulimwengu, Sayuni ilisikia mbiu ya ushindi: “Mungu wako amekuwa mfalme!” (Isaya 52:7, NW) Baada ya Ufalme kuzaliwa katika 1914, wazee 24 walipiga mbiu hii: “Sisi twashukuru wewe, Yehova Mungu . . . kwa sababu wewe umechukua nguvu kuu zako na umeanza kutawala ukiwa mfalme.” (Ufunuo 11:17, NW) Sasa, baada ya mteketeo wa Babuloni Mkubwa, kilio kinatamkwa tena: “Yehova . . . ameanza kutawala akiwa mfalme.” Hakuna kamungu kalikofanyizwa na mwanadamu kanakobaki kagombee enzi kuu ya Yehova, Mungu wa kweli!

      Ndoa ya Mwana-Kondoo Imekaribia!

      11, 12. (a) Yerusalemu wa kale liliitaje Babuloni wa kale, kuweka kiolezo gani kwa habari ya Yerusalemu Jipya na Babuloni Mkubwa? (b) Masongamano ya kimbingu huimba na kutangaza nini kwa ushindi juu ya Babuloni Mkubwa?

      11 “Wewe mwanamke adui yangu”! Hivyo ndivyo Yerusalemu, mahali pa hekalu la ibada ya Yehova, liliita Babuloni mwabudu sanamu. (Mika 7:8, NW) Hali moja na hiyo, “jiji takatifu, Yerusalemu Jipya,” ambalo ni bibi-arusi mwenye washiriki 144,000, limekuwa na kila sababu ya kuita Babuloni Mkubwa kuwa adui yake. (Ufunuo 21:2) Lakini hatimaye huyo kahaba mkubwa amepatwa na msiba, janga, na angamio. Mazoea yake ya kuwasiliana na roho na wanajimu wake hayakumwokoa. (Linga Isaya 47:1, 11-13.) Ni ushindi mkubwa, kweli kweli, kwa ajili ya ibada ya kweli!

      12 Kahaba mwenye kunyarafisha Babuloni Mkubwa, akiwa ametoweka milele, sasa uangalifu waweza kuelekezwa juu ya bibi-arusi bikira safi wa Mwana-Kondoo! Kwa sababu hiyo, masongamano ya kimbingu yaimba kwa mchachawo katika kusifu Yehova: “Acheni sisi tushangilie na tufurikwe na shangwe, na acheni sisi tumpe yeye utukufu, kwa sababu ndoa ya Mwana-Kondoo imewasili na mke wake amejitayarisha mwenyewe. Ndiyo, amepewa ruhusa kujipamba kwa kitani nyangavu, safi, nzuri sana, kwa maana kitani nzuri sana husimama kwa ajili ya matendo ya uadilifu ya watakatifu.”—Ufunuo 19:7, 8, NW.

      13. Ni tayarisho gani kwa ajili ya ndoa ya Mwana-Kondoo limetukia kwa karne zote?

      13 Kwa muda wa karne zote, Yesu amefanya tayarisho lenye upendo kwa ajili ya ndoa hii ya kimbingu. (Mathayo 28:20; 2 Wakorintho 11:2) Yeye amekuwa akisafisha 144,000 wa Israeli wa kiroho ili “yeye aweze kujiletea yeye mwenyewe kundi katika umaridadi walo, bila kuwa na doa au kunyanzi au lolote la vitu kama hivyo, bali kwamba limepaswa kuwa takatifu na bila waa.” (Waefeso 5:25-27, NW) Wakitaka kufikia “zawadi ya mwito wa juu wa Mungu,” kila Mkristo mpakwa-mafuta amelazimika kuvua utu wa zamani pamoja na mazoea yao, na kuvaa utu mpya wa Kikristo, na kufanya matendo ya uadilifu “kwa nafsi yote kama kwa Yehova.”—Wafilipi 3:8, 13, 14; Wakolosai 3:9, 10, 23, NW.

      14. Shetani amejaribuje kuchafua wanaotazamiwa kuwa washiriki wa mke wa Mwana-Kondoo?

      14 Kutoka Pentekoste 33 W.K. na kuendelea, Shetani alitumia Babuloni Mkubwa akiwa chombo chake katika kujaribu kuchafua wanaotazamiwa kuwa washiriki wa mke wa Mwana-Kondoo. Kufikia mwisho wa karne ya kwanza, yeye alikuwa amepanda mbegu za dini ya Kibabuloni katika kundi. (1 Wakorintho 15:12; 2 Timotheo 2:18; Ufunuo 2:6, 14, 20) Mtume Paulo anaeleza wale ambao walikuwa wakipindua imani kwa maneno haya: “Kwa maana watu kama hao ni mitume bandia, wafanya kazi wadanganyifu, wakijigeuza umbile wenyewe kuwa mitume wa Kristo. Na si ajabu, kwa maana Shetani mwenyewe huendelea kujigeuza umbile mwenyewe kuwa malaika wa nuru.” (2 Wakorintho 11:13, 14, NW) Katika karne zilizoandama, Jumuiya ya Wakristo asi-imani, kama sehemu inayobaki ya Babuloni Mkubwa, ilijivisha yenyewe mavazi ya utajiri na pendeleo, “zambarau na rangi-nyekundu-nyangavu, . . . dhahabu na jiwe la thamani na lulu.” (Ufunuo 17:4, NW) Viongozi wayo wa kidini na mapapa waliandamana na maliki wenye kiu cha kumwaga damu kama vile Konstantino na Charlemagne. Yeye hakupambwa kamwe kwa “matendo ya uadilifu ya watakatifu.” Akiwa bibi-arusi bandia, kwa kweli yeye alikuwa kipeo cha udanganyi wa kishetani. Hatimaye, yeye ametoweka milele!

      Mke wa Mwana-Kondoo Amejitayarisha

      15. Kutiwa muhuri hutukiaje, na ni jambo gani linalotakwa kwa Wakristo wapakwa-mafuta?

      15 Basi sasa, baada ya karibu miaka 2,000, wote 144,000 wa jamii ya bibi-arusi wamejiweka wenyewe tayari. Lakini ni kwenye pindi gani ya wakati inaweza kusemwa kwamba ‘mke wa Mwana-Kondoo amejitayarisha’? Kwa kuendelea, kutoka Pentekoste 33 W.K. wapakwa-mafuta wenye kuitikadi “walitiwa muhuri kwa roho takatifu iliyoahidiwa,” hii ni kwa kutazamia “siku ya kuachiliwa kupitia ukombozi” iliyokuwa ikija. Kama mtume Paulo alivyolisema jambo hilo, Mungu “pia ameweka muhuri wake juu yetu na ametupa sisi ishara ya kitakachokuja, yaani, roho, katika mioyo yetu.” (Waefeso 1:13; 4:30; 2 Wakorintho 1:22, NW) Kila Mkristo aliyepakwa mafuta ‘ameitwa na akachaguliwa,’ na amejithibitisha mwenyewe kuwa ‘mwaminifu.’—Ufunuo 17:14, NW.

      16. (a) Kutiwa muhuri kwa mtume Paulo kulitimilizwa wakati gani, na sisi tunajuaje? (b) Ni wakati gani mke wa Mwana-Kondoo atakuwa ‘amejitayarisha’ kikamili?

      16 Baada ya miongo ya mtihani, Paulo mwenyewe angeweza kujulisha wazi: “Mimi nimepiga vita njema, mimi nimekimbia mwendo hadi mwisho, mimi nimeshika imani. Kutoka wakati huu na kuendelea taji la uadilifu limehifadhiwa kwa ajili yangu mimi, ambalo Bwana, hakimu mwadilifu, atanipa mimi ikiwa thawabu katika siku hiyo, hata hivyo si mimi pekee, bali pia wale wote ambao wamependa udhihirisho wake.” (2 Timotheo 4:7, 8, NW) Kutiwa muhuri kwa mtume kunaonekana kulikuwa kumekamilika, hata ingawa alikuwa angali katika mnofu na bado angekabili ufia-imani. Hali moja na hiyo, wakati lazima uje ambao wale wote wanaobaki duniani wa wale 144,000 watakuwa wamekwisha kutiwa muhuri mmoja mmoja kuwa wao ni wa Yehova. (2 Timotheo 2:19) Huo utakuwa ndio wakati ambao mke wa Mwana-Kondoo atakuwa amekwisha jitayarisha kabisa—walio wengi sana wa 144,000 wakiwa wamekwisha pokea thawabu yao ya kimbingu na wale ambao wangali duniani wakiwa wamekwisha kukubaliwa mwishowe na kutiwa muhuri kuwa ni waaminifu.

      17. Ni lini ndoa ya Mwana-Kondoo inapoweza kutukia?

      17 Kufikia hapa katika jedwali ya wakati ya Yehova, wakati kutiwa muhuri kwa wale 144,000 kumefikia ukamilisho, malaika huachilia pepo nne za dhiki kubwa. (Ufunuo 7:1-3) Kwanza, hukumu inatekelezwa juu ya Babuloni Mkubwa aliye mithili ya kahaba. Kisha Kristo mwenye ushindi anasonga kwa haraka kwenye Har–Magedoni kuharibu sehemu inayobaki ya tengenezo la Shetani lililo duniani na, mwishowe, kutia Shetani na roho waovu wake ndani ya abiso. (Ufunuo 19:11–20:3) Ikiwa bado kuna wapakwa-mafuta wowote ambao wanaokoka wakiwa duniani, pasipo shaka wataingia ndani ya thawabu yao ya kimbingu upesi baada ya Kristo kukamilisha ushindi wake, wakajiunge na washiriki wenzao wa jamii ya bibi-arusi. Ndipo wakati uliowekwa na Mungu ufikapo, ndoa ya Mwana-Kondoo yaweza kutukia!

      18. Zaburi ya 45 huthibitishaje mfuatano wa matukio kwa habari ya ndoa ya Mwana-Kondoo?

      18 Simulizi la kiunabii katika Zaburi 45 (NW) linaeleza utaratibu wa matukio. Kwanza Mfalme aliyetawazwa apanda akawashinde maadui wake. (Mistari 1-7) Kisha ndoa yafanywa, bibi-arusi wa kimbingu akiwa anaandamana duniani na waandamani wake mabikira, umati mkubwa. (Mistari 8-15) Halafu ndoa yazaa matunda, aina ya binadamu iliyofufuliwa yainuliwa kwenye ukamilifu chini ya uangalizi wa “wana-wafalme katika dunia yote.” (Mistari 16, 17) Lo! ni baraka zilizoje zinazoandamana na ndoa ya Mwana-Kondoo!

      Wenye Furaha ni Wale Walioalikwa

      19. Ni ipi iliyo furaha ya nne ya zile saba katika Ufunuo, na ni nani wanaoshiriki furaha ii hii?

      19 Sasa Yohana anarekodi furaha ya nne ya zile saba katika Ufunuo: “Na yeye [malaika ambaye amekuwa akifunulia Yohana vitu hivi] aniambia mimi: ‘Andika: Wenye furaha ni wale ambao wamealikwa kwenye mlo wa jioni wa ndoa ya Mwana-Kondoo.’ Pia, yeye aniambia mimi: ‘Hizi ndizo semi za kweli za Mungu.’” (Ufunuo 19:9, NW)e Wale walioalikwa kwenye “mlo wa jioni wa ndoa ya Mwana-Kondoo” ni washiriki wa jamii ya bibi-arusi. (Linga Mathayo 22:1-14.) Shirika la ki-bibi-arusi lililopakwa mafuta lashiriki furaha ya kuwa limepokea mwaliko huu. Walio wengi wa waalikwa tayari wamekwenda kwenye mbingu, mahali pa mlo wa jioni wa ki-ndoa. Wale ambao wangali duniani ni wenye furaha, vilevile, kwamba wao wana mwaliko huo. Mahali pao katika mlo wa jioni wa ki-ndoa kwenye mbingu pako salama. (Yohana 14:1-3; 1 Petro 1:3-9) Wakati wanapofufuliwa kwenda kwenye mbingu, ndipo bibi-arusi mzima, aliyeungamanika, ataanza na kuendelea kushiriki pamoja na Mwana-Kondoo katika ndoa yenye furaha ipitayo zote.

      20. (a) Ni nini maana ya maneno haya: “Hizi ni semi za kweli za Mungu”? (b) Yohana aliathiriwaje na maneno ya malaika, na itikio la malaika lilikuwa nini?

      20 Malaika huongeza kwamba “hizi ndizo semi za kweli za Mungu.” Neno hili “kweli” linatafsiri a·le·thi·nosʹ la Kigiriki na humaanisha “halisi” au “-a kutegemeka.” Kwa kuwa semi hizi kwa kweli zinatoka kwa Yehova, ni zenye kuaminika na zenye kutegemeka. (Linga 1 Yohana 4:1-3; Ufunuo 21:5; 22:6.) Akiwa mmoja aliyealikwa kwa karamu hiyo ya ndoa, lazima Yohana awe alijawa na shangwe kwa kusikia hilo na kwa kufikiria baraka zilizokuwa mbele kwa ajili ya jamii ya bibi-arusi. Kwa kweli, yeye alivutwa sana hivi kwamba malaika akalazimika kumshauri yeye, kama asimuliavyo Yohana: “Ndipo mimi nikaanguka chini mbele ya nyayo zake ili kuabudu yeye. Lakini yeye aniambia mimi: ‘Uwe mwangalifu! Usifanye hivyo! Mimi ni mtumwa mwenzako tu na wa ndugu zako ambao wana kazi ya ushahidi kwa Yesu. Abudu Mungu.’”—Ufunuo 19:10a, NW.

      21. (a) Ufunuo hufumbua nini kwa habari ya malaika? (b) Inawapasa Wakristo kuwa na mwelekeo gani kwa malaika?

      21 Katika kitabu chote cha Ufunuo ushahidi wenye kutokeza umetolewa juu ya uaminifu na bidii-endelevu ya malaika. Wao wanahusika katika njia ya ukweli uliofunuliwa. (Ufunuo 1:1) Wao wanafanya kazi pamoja na wanadamu katika kuhubiri habari njema na kumimina tauni za ufananisho. (Ufunuo 14:6, 7; 16:1) Wao walipigana wakiwa upande wa Yesu katika kumtupa Shetani na malaika zake kutoka katika mbingu, na watapigana wakiwa upande wake tena kwenye Har–Magedoni. (Ufunuo 12:7; 19:11-14) Kweli kweli, wao wanaweza kuingia mbele za Yehova mwenyewe. (Mathayo 18:10; Ufunuo 15:6) Hata hivyo, wao ni watumwa wanyenyekevu tu wa Mungu. Hakuna nafasi katika ibada safi ya kuabudu malaika au hata kwa ibada ya kadiri, kuelekeza ibada kwa Mungu kupitia “mtakatifu” fulani au malaika. (Wakolosai 2:18) Wakristo wanaabudu Yehova pekee, wakifanya maombi yao kupitia jina la Yesu.—Yohana 14:12, 13.

      Daraka la Yesu Katika Unabii

      22. Malaika husema nini kwa Yohana, na maneno hayo yanamaanisha nini?

      22 Ndipo malaika asema: “Kwa maana kutoa ushahidi kwa Yesu ndiko kunakovuvia kutoa unabii.” (Ufunuo 19:10b, NW) Jinsi gani hivyo? Hii humaanisha kwamba unabii wote uliovuviwa hutokezwa kwa sababu ya Yesu na daraka analotimiza katika makusudi ya Yehova. Unabii wa kwanza katika Biblia uliahidi kuja kwa mbegu. (Mwanzo 3:15) Yesu akawa Mbegu hiyo. Mafunuo yaliyofuata yalijenga jengo kubwa la ukweli wa kiunabii juu ya ahadi hii ya msingi. Mtume Petro alimwambia Kornelio asiye Myahudi mwenye kuamini: “Kwake yeye [Yesu] manabii wote hutoa ushahidi.” Yapata miaka 20 baadaye, mtume Paulo alisema: “Si kitu ahadi za Mungu ni nyingi kadiri gani, zote zimekuwa Ndiyo kwa njia yake yeye [Yesu].” (2 Wakorintho 1:20, NW) Baada ya miaka mingine 43, Yohana mwenyewe anatukumbusha: “Ukweli ulikuja kupitia Yesu Kristo.”—Yohana 1:17, NW.

      23. Ni kwa nini cheo cha juu na mamlaka kubwa ya Yesu havipunguzi ibada tunayompa Yehova?

      23 Je! hili lakengeusha kwa njia yoyote ibada tunayompa Yehova? La. Kumbuka maneno ya kutahadharisha ya malaika: “Abudu Mungu.” Yesu hajaribu kamwe kushindana na Yehova. (Wafilipi 2:6) Ni kweli, malaika wote huambiwa “wamsujudu” Yesu, na ni lazima uumbaji wote utambue cheo chake cha juu ili “kwa jina la Yesu kila goti lipigwe.” Lakini angalia, hili ni “kwa utukufu wa Mungu Baba” na kwa agizo lake. (Waebrania 1:6; Wafilipi 2:9-11) Yehova alimpa Yesu mamlaka yake kubwa, na kwa kukubali mamlaka hiyo, sisi tunampa Mungu utukufu. Ikiwa sisi tunakataa kutii utawala wa Yesu, ni sawa na kumkataa Yehova Mungu mwenyewe.—Zaburi 2:11, 12.

      24. Ni matukio gani mawili yenye kupiga butaa ambayo sisi tunafikiria, na kwa hiyo ni maneno gani ambayo sisi tunapaswa kusema?

      24 Hivyo, basi, acheni sisi kwa umoja tuseme yale maneno ya utangulizi ya Zaburi 146 mpaka 150: “Sifuni Yah, nyinyi watu!” Korasi ya Halleluyah na ingurume katika kutazamia ushindi wenye shangwe wa Yehova juu ya milki ya ulimwengu ya dini bandia ya Kibabuloni! Na shangwe na ienee pote ndoa ya Mwana-Kondoo ikaribiapo!

      [Maelezo ya Chini]

      a New World Translation Reference Bible, kielezi cha chini.

      b New World Translation Reference Bible, kielezi cha chini.

      c New World Translation Reference Bible, kielezi cha chini.

      d New World Translation Reference Bible, kielezi cha chini.

      e Ona pia Ufunuo 1:3; 14:13; 16:15, NW.

      [Picha katika ukurasa wa 273]

      “Waraka kwa Sodoma na Gomora”

      Chini ya hiki kichwa kikuu, Daily Telegraph ya London ya Novemba 12, 1987, iliripoti juu ya mjadala mbele ya Baraza Kuu la Kanisa la Uingereza. Huo ulitaka “Wakristo” wagoni-jinsia-moja waondolewe katika kanisa. Mwandikaji habari za nyusipepa Godfrey Barker alitaarifu hivi: “Askofu Mkuu wa Kantabari jana alionelea kwa huzuni: ‘Ikiwa [Mtakatifu] Paulo angaliandikia Kanisa la Uingereza waraka, sisi twaweza kuuliza kwa kufaa ingekuwa barua ya aina gani.’” Bw. Barker mwenyewe alitoa elezo hili: “Waraka kwa Sodoma na Gomora ndilo jibu,” na akaongeza: “Dakt. Runcie [askofu mkuu] aliwaza ingesomeka kama Warumi, [Sura ya] 1.”

      Huyo mwandikaji alinukuu maneno ya Paulo kwenye Warumi 1:26-32: “Hivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu. . . . Wanaume nao . . . wakawakiana tamaa wakiyatenda yasiyopasa . . . wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao.” Yeye alimalizia: “[Mtakatifu] Paulo alihangaikia tu wale watu walio vitini. Tatizo la Dakt. Runcie ni wale watu walio katika mimbari.”

      Kwa nini askofu mkuu ana tatizo kama hilo? Vichwa vikubwa katika Daily Mail ya London ya Oktoba 22, 1987, vilikuwa vimejulisha wazi: “‘Vikari mmoja kati ya watatu ni mgoni-jinsia-moja’ . . . Kampeni ya kuwatoa nje wagoni-jinsia-moja ‘ingefunga Kanisa la Uingereza.’” Ripoti hizo zilinukuu maneno ya “reverendi” katibu mkuu wa Chama cha Wakristo Wagoni-Jinsia-Moja wa Kike na wa Kiume akisema: “Ikiwa mjadala huu ungekubaliwa ungeangamiza Kanisa, na Askofu Mkuu wa Kantabari anajua hivyo. Kama tarakimu ya ujumla, sisi tunaitikadi kati ya asilimia 30 na 40 ya viongozi wa kidini wa Kanisa la Uingereza ni wagoni-jinsia-moja. Na wao ndio watu watendaji zaidi katika kuchangia huduma ya Kanisa.” Idadi zinazozidi kupungua za waenda-kanisani pasipo shaka kwa sehemu ni wonyesho wa kunyarafu huduma hiyo ya ugoni-jinsia-moja inayoongezeka sana.

      Baraza kuu la kanisa liliamuaje? Idadi kubwa ya washiriki 388 (asilimia 95 ya viongozi wa kidini) ilipiga kura kwa kupendelea mjadala uliopunguzwa nguvu. Kuhusu hilo, The Economist ya Novemba 14, 1987, iliripoti hivi: “Kanisa la Uingereza linapinga mazoea ya ugoni-jinsia-moja, lakini si sana. Baraza kuu, bunge la kanisa, kwa kufikiria viongozi wa kidini wagoni-jinsia-moja, liliamua juma lililopita kwamba matendo ya ugoni-jinsia-moja, tofauti na uasherati na uzinzi, si dhambi: ‘yanapungukiwa tu kilicho bora’ kwamba ‘uhusiano wa ngono ni tendo la kujitoa kabisa linalofaa kufanywa ndani ya uhusiano wa ndoa wenye kufaa.’” Ikitofautisha msimamo wa Askofu Mkuu wa Kantabari na taarifa ya waziwazi ya mtume Paulo kwenye Warumi 1:26, 27, The Economist ilionyesha nukuu la maneno ya Paulo juu ya maelezo haya “[Mtakatifu] Paulo alijua aliyofikiri.”

      Yesu Kristo pia alijua aliyofikiri na akayataarifu kwa maneno yaliyo wazi. Yeye alisema kwamba ‘ingevumilika zaidi kwa bara la Sodoma katika Siku ya Hukumu’ kuliko kwa wanadini walioupiga teke ujumbe wake. (Mathayo 11:23, 24, NW) Yesu alikuwa hapa akitumia mubaalagha (usemi uliotiwa chumvi) kuonyesha kwamba wale viongozi wa kidini waliokataa Mwana wa Mungu na fundisho lake walikuwa na hatia hata zaidi ya Wasodoma. Yuda 7 hutaarifu kwamba hao Wasodoma walipatwa na “adhabu ya kihukumu ya moto wa milele,” kumaanisha uharibifu wa milele. (Mathayo 25:41, 46) Basi, itakuwa kali kama nini hukumu ya wale wanaoitwa eti viongozi Wakristo ambao kwa upofu huongoza makundi yao yaliyopofushwa mbali na viwango vya juu vya kiadili vya Ufalme wa Mungu na kuwaingiza ndani ya njia endekevu, pujufu za ulimwengu huu! (Mathayo 15:14) Kuhusu dini bandia, Babuloni Mkubwa, sauti kutoka katika mbingu inaita kwa uharaka: “Ondokeni katika yeye, watu wangu, ikiwa nyinyi hamtaki kushiriki pamoja na yeye katika dhambi yake, na ikiwa nyinyi hamtaki kupokea sehemu ya tauni zake.”—Ufunuo 18:2, 4, NW.

      [Picha katika ukurasa wa 275]

      Mbingu yavuma kwa Halleluyah nne, zikimsifu Yah kwa ajili ya ushindi wake wa mwisho kabisa juu ya Babuloni Mkubwa

  • Mwanavita-Mfalme Asherehekea Ushindi Kwenye Har–Magedoni
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Sura ya 39

      Mwanavita-Mfalme Asherehekea Ushindi Kwenye Har–Magedoni

      Njozi ya 13—Ufunuo 19:11-21

      Habari: Yesu aongoza majeshi ya mbinguni kuharibu mfumo wa mambo wa Shetani

      Wakati wa utimizo: Baada ya uharibifu wa Babuloni Mkubwa

      1. Har–Magedoni ni nini, na ni nini kinachoongoza kwayo?

      HAR–MAGEDONI—neno lenye kuogopesha kwa wengi! Lakini kwa wapenda uadilifu, ni dalili ya siku ambayo imengojewa muda mrefu wakati ambapo Yehova atatekeleza hukumu ya mwisho kabisa juu ya mataifa. Si vita ya mwanadamu bali ni “vita ya ile siku kubwa ya Mungu Mweza Yote”—siku yake ya kisasi dhidi ya watawala wa dunia. (Ufunuo 16:14, 16; Ezekieli 25:17, NW) Dhiki kubwa itakuwa imekwisha kuanza na ukiwa wa Babuloni Mkubwa. Kisha, akihimizwa na Shetani, hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu pamoja na pembe zake kumi atakaza shambulio lake juu ya watu wa Yehova. Ibilisi, akiwa na hasira-kisasi zaidi ya wakati mwingine wowote juu ya tengenezo la Mungu lililo kama mwanamke, ameazimia kutumia mabaradhuli wake katika kupiga vita mpaka mwisho juu ya wabakio wa mbegu ya mwanamke. (Ufunuo 12:17) Hii ndiyo fursa ya mwisho ya Shetani!

      2. Gogu wa Magogu ni nani, na Yehova anamwongozaje kwa werevu ashambulie watu Wake mwenyewe?

      2 Shambulio la ukatili la Ibilisi limeelezwa waziwazi katika Ezekieli sura ya 38. Hapo, Shetani aliyeshushwa anaitwa “Gogu wa bara la Magogu.” Yehova anatia kulabu za ufananisho kwenye taya za Gogu, akimvuta yeye na jeshi la kivita lake kubwa kwenye shambulio. Yeye hufanyaje hivyo? Kwa kumfanya Gogu aone Mashahidi Wake kuwa kikundi cha watu wasio na ulinzi ‘kimekusanywa pamoja kutoka katika mataifa, kimoja ambacho kinarundika ukwasi na mali, wale ambao wanakaa katika kitovu cha dunia.’ Hao hushikilia kitovu cha jukwaa duniani wakiwa kama kikundi kimoja cha watu ambacho kimekataa kuabudu hayawani-mwitu na mfano wake. Imara yao ya kiroho na ufanisi humkasirisha Gogu kijeuri. Kwa hiyo Gogu na jeshi la kivita lake kubwa, kutia hayawani-mwitu kutoka bahari pamoja na pembe kumi zake, wanaomoka kwa wingi wapate windo. Hata hivyo, tofauti na Babuloni Mkubwa, watu safi wa Mungu wanafurahia himaya ya kimungu!—Ezekieli 38:1, 4, 11, 12, 15; Ufunuo 13:1, NW.

      3. Yehova anaondolea mbali majeshi ya kivita ya Gogu jinsi gani?

      3 Yehova huondoleaje mbali Gogu na umati wake wote? Sikiliza! “‘Mimi nitaita upanga uje dhidi yake kotekote katika mkoa wangu wote wa milima,’ ndilo tamko la Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu. ‘Dhidi ya ndugu yake mwenyewe upanga wa kila mmoja utakuja kuwa.’” Lakini wala silaha za nyukilia wala zile za kawaida hazitafua dafu katika pigano hilo, kwa maana Yehova ajulisha wazi: “Mimi nitajileta mwenyewe ndani ya hukumu pamoja na yeye, kwa ugonjwa wa kipuku na kwa damu; na mvua kubwa yenye kufurika na mvua-mawe, na moto na salfa mimi nitanyesha chini juu yake na juu ya vikosi vyake na juu ya vikundi vingi vya watu ambao watakuwa pamoja na yeye. Na kwa hakika mimi nitajikuza mwenyewe na kujitakasa mwenyewe na kujifanya mwenyewe kujulikana mbele ya macho ya mataifa mengi; na wao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.”—Ezekieli 38:21-23; 39:11, NW; linga Yoshua 10:8-14; Waamuzi 7:19-22; 2 Nyakati 20:15, 22-24; Ayubu 38:22, 23.

      Mmoja Aitwaye “Mwaminifu na Wa-kweli”

      4. Yohana huelezaje habari ya Yesu Kristo akiwa katika mpango wa kivita?

      4 Yehova aita upanga uje. Ni nani anayepungapunga upanga huu? Turudiapo Ufunuo, sisi tunapata jibu katika njozi nyingine bado yenye kusisimua. Mbele ya macho ya Yohana mbingu zinafunguka kufunua kitu fulani ambacho ni chenye kuvuvia hofu kikweli—Yesu Kristo mwenyewe akiwa katika mpango wa kivita! Yohana anatuambia: “Na mimi nikaona mbingu zimefunguka, na, tazama! farasi mweupe. Na mmoja aketiye juu yake anaitwa Mwaminifu na Wa-kweli, na yeye anahukumu na kuendeleza vita katika uadilifu. Macho yake ni mwali wa moto, na juu ya kichwa chake pana mataji mengi.”—Ufunuo 19:11, 12a, NW.

      5, 6. Ni nini kinachoashiriwa na (a) “farasi mweupe”? (b) jina “Mwaminifu na Wa-kweli”? (c) macho kama “mwali wa moto”? (d) “mataji mengi”?

      5 Kama katika njozi ya mapema zaidi ya wapanda-farasi wanne, huyu “farasi mweupe” ni ufananisho unaofaa wa vita yenye uadilifu. (Ufunuo 6:2, NW) Na ni yupi wa wana wa Mungu ambaye angekuwa mwadilifu zaidi ya Mwanavita huyu? Akiwa “anaitwa Mwaminifu na Wa-kweli,” lazima yeye awe “shahidi mwaminifu na wa kweli,” Yesu Kristo. (Ufunuo 3:14, NW) Yeye hufanya vita ili kutekeleza hukumu za uadilifu za Yehova. Hivyo, yeye anatenda akiwa katika cheo chake cha Hakimu aliyewekwa rasmi na Yehova, cha kuwa “Mungu Mwenye Nguvu.” (Isaya 9:6, NW) Macho yake yanavuvia hofu, kama “mwali wa moto,” akitarajia uharibifu wenye moto unaokuja wa maadui wake.

      6 Mataji mengi hupamba kichwa cha Mwanavita-Mfalme huyu. Hayawani-mwitu ambaye Yohana aliona akitoka katika bahari alikuwa na mataji kumi, yakiwa ni picha ya utawala wake wa kitambo wa mandhari ya kidunia. (Ufunuo 13:1, NW) Ingawa hivyo, Yesu ana “mataji mengi.” Utawala wake wenye utukufu haulandiki, kwa kuwa yeye ni “Mfalme wa wale ambao hutawala wakiwa wafalme na Bwana wa wale ambao hutawala wakiwa mabwana.”—1 Timotheo 6:15, NW.

      7. Jina lililoandikwa alilo nalo Yesu ni jipi?

      7 Elezo la Yohana laendelea: “Yeye ana jina lililoandikwa ambalo hakuna mmoja ajuaye ila yeye mwenyewe.” (Ufunuo 19:12b, NW) Tayari Biblia husema juu ya Mwana wa Mungu kwa majina kama Yesu, Imanueli, na Mikaeli. Lakini “jina” lake lisilotajwa laonekana kuwa lasimamia cheo na mapendeleo ambayo Yesu anafurahia wakati wa siku ya Bwana. (Linga Ufunuo 2:17.) Isaya, akieleza habari ya Yesu tangu 1914, anasema: “Jina lake ataitwa Mshauri wa Ajabu, Mungu Mwenye Nguvu, Baba wa Milele, Mwana-Mfalme wa Amani.” (Isaya 9:6, NW) Mtume Paulo alishirikisha jina la Yesu na mapendeleo ya juu sana ya utumishi wakati alipoandika: “Mungu alimkweza [Yesu] kwenye cheo cha juu sana na kwa fadhili akampa yeye jina ambalo liko juu ya kila jina jingine, ili kwamba katika jina la Yesu kila goti lipaswe kupigwa.”—Wafilipi 2:9, 10, NW.

      8. Ni kwa sababu gani ni Yesu tu anayeweza kujua hilo jina lililoandikwa, na yeye anashiriki na nani baadhi ya mapendeleo yake ya juu sana?

      8 Mapendeleo ya Yesu hayana kifani. Isipokuwa Yehova mwenyewe, ni Yesu tu anayeweza kufahamu linalomaanishwa na kuwa na cheo kama hicho cha juu. (Linga Mathayo 11:27.) Kwa hiyo, kati ya viumbe wote wa Mungu, ni Yesu tu anayeweza kuthamini jina hilo. Hata hivyo, Yesu anatia ndani bibi-arusi wake katika baadhi ya mapendeleo haya. Kwa hiyo yeye anatoa ahadi hii: “Yeye ambaye hushinda . . . mimi nitaandika juu ya yeye . . . hilo jina jipya langu.”—Ufunuo 3:12, NW.

      9. Ni nini kinachoonyeshwa na (a) Yesu kuwa ‘amepambwa vazi la nje lililonyunyiziwa damu’? (b) Yesu kuitwa “Neno la Mungu”?

      9 Yohana anaongeza: “Na yeye amepambwa vazi la nje lililonyunyiziwa damu, na jina analoitwa yeye ni Neno la Mungu.” (Ufunuo 19:13, NW) Hii ni “damu” ya nani? Ingeweza kuwa damu ya uhai ya Yesu, iliyomwagwa kwa ajili ya aina ya binadamu. (Ufunuo 1:5) Lakini, katika muktadha huu inaelekea zaidi inarejezea damu ya maadui wake ambayo inamwagwa wakati hukumu za Yehova zinapotekelezwa juu yao. Sisi tunakumbushwa juu ya njozi ya mapema zaidi ambayo katika hiyo mzabibu wa dunia unavunwa na kukanyagwa katika shinikizo kubwa la divai ya kasirani ya Mungu hata damu inafika “mpaka juu kabisa kwenye hatamu za wale farasi”—kuashiria ushindi mkubwa juu ya maadui wa Mungu. (Ufunuo 14:18-20, NW) Hali kadhalika, damu iliyonyunyiziwa juu ya vazi la nje la Yesu huthibitisha kwamba ushindi wake ni wa kukata maneno na ni kamili. (Linga Isaya 63:1-6.) Sasa Yohana anasema tena juu ya Yesu kuwa anaitwa kwa jina. Wakati huu ni jina linalojulikana sana—“Neno la Mungu”—likimtambulisha huyu Mwanavita-Mfalme kuwa Mneni na Championi Mkuu wa ukweli wa Yehova.—Yohana 1:1; Ufunuo 1:1, NW.

      Wanavita Wenzi wa Yesu

      10, 11. (a) Yohana anaonyeshaje kwamba Yesu hayuko peke yake katika pigano? (b) Ni nini kinachoonyeshwa na uhakika wa kwamba farasi ni weupe na wapanda-farasi wamevaa “kitani nyeupe, nzuri safi”? (c) Ni nani walio sehemu ya “majeshi” ya kimbingu?

      10 Yesu hayuko peke yake katika kupiga pigano hili. Yohana anatuambia: “Pia, majeshi ambayo yalikuwa katika mbingu yalikuwa yakifuata yeye juu ya farasi weupe, na wao walikuwa wamevaa kitani nyeupe, nzuri, safi.” (Ufunuo 19:14, NW) Uhakika wa kwamba farasi ni “weupe” huonyesha vita ni ya uadilifu. “Kitani nyeupe” inawafaa wapanda-farasi wa Mfalme, na weupe wenye kumeta ulio safi huonyesha msimamo safi, wa uadilifu mbele za Yehova. Ni nani, basi, walio sehemu ya “majeshi” haya? Bila shaka, ni kutia ndani malaika watakatifu. Ilikuwa mapema katika siku ya Bwana kwamba Mikaeli na malaika zake walivurumisha Shetani na roho waovu wake kutoka katika mbingu. (Ufunuo 12:7-9) Na zaidi, “malaika wote” watamtumikia Yesu anapoketi juu ya kiti cha ufalme chake chenye utukufu na kuendelea kuhukumu mataifa na vikundi vya watu wa dunia. (Mathayo 25:31, 32) Hakika, katika vita hii ya kukata maneno, wakati hukumu za Mungu zinapotekelezwa mpaka mwisho, malaika wa Yesu wataandamana tena na yeye.

      11 Wengine vilevile watahusishwa. Alipokuwa akipeleka ujumbe wake kwa kundi la Thiatira, Yesu aliahidi: “Na yeye ambaye hushinda na kushika matendo yangu kuteremka mpaka mwisho mimi nitampa mamlaka juu ya mataifa, na yeye atachunga watu kwa ufito wa chuma hivi kwamba wao watavunjwa vipande vipande kama vyombo vya udongo wa mfinyanzi, sawasawa na ambavyo mimi nimepokea kutoka kwa Baba yangu.” (Ufunuo 2:26, 27, NW) Pasipo shaka, wakati ufikapo, wale wa ndugu za Kristo ambao tayari wako katika mbingu watashiriki katika kuchunga watu wa mataifa kwa ufito huo wa chuma.

      12. (a) Je! watumishi wa Mungu duniani watashiriki katika kupigana kwenye Har–Magedoni? (b) Watu wa Yehova walio duniani wanahusishwaje katika Har–Magedoni?

      12 Ingawa hivyo, namna gani watumishi wa Mungu walio hapa duniani? Jamii ya Yohana haitashiriki sehemu yoyote kwa kutenda katika pigano kwenye Har–Magedoni; wala waandamani wenzao washikamanifu, vikundi vile vya watu kutoka mataifa yote ambavyo vimekuwa vikimiminika kwenye nyumba ya kiroho ya ibada ya Yehova. Binadamu hawa wote wenye kuamanika wamekwisha fua panga zao zikawa majembe ya plau. (Isaya 2:2-4, NW) Hata hivyo, wao wanahusishwa sana! Kama vile tumekwisha kuona, watu wa Yehova wanaoonekana hawana ulinzi ndio wanaoshambuliwa kikatili na Gogu na umati wake wote. Hiyo ndiyo ishara kwa Mwanavita-Mfalme wa Yehova, akiungwa mkono na majeshi yaliyo katika mbingu, aanze kupiga vita ya kuulia mbali kabisa dhidi ya mataifa hayo. (Ezekieli 39:6, 7, 11; linga Danieli 11:44–12:1.) Wakiwa watazamaji, watu wa Mungu duniani watapendezwa sana. Har–Magedoni itamaanisha wokovu wao, na wao wataishi kwa umilele wakiwa wamekuwa mashahidi wenye kujionea vita kubwa ya Yehova ya utetezi.

      13. Sisi twajuaje kwamba Mashahidi wa Yehova hawapingi serikali yote?

      13 Hii inamaanisha kwamba Mashahidi wa Yehova hupinga serikali yote? Sivyo kabisa! Wao wanatii shauri la mtume Paulo: “Acheni kila nafsi iwe katika utii kwa mamlaka za juu zaidi.” Wao wanang’amua kwamba maadamu huu mfumo uliopo unaendelea, hizo “mamlaka za juu zaidi” ziko kwa ruhusa ya Mungu kwa ajili ya kudumisha kadiri fulani ya utaratibu katika jamii ya kibinadamu. Hivyo, Mashahidi wa Yehova hulipa kodi zao, hutii sheria, huheshimu maagizo ya kuendesha magari barabarani, hujiandikisha, na kadhalika. (Warumi 13:1, 6, 7, NW) Na zaidi, wao hufuata kanuni za Biblia kuwa wenye kusema ukweli na haki; wakionyesha upendo wa jirani; wakijenga jamaa zenye nguvu na uadilifu; na kuzoeza watoto wao wawe wananchi walio kielelezo chema. Katika njia hii wao hawalipi tu “Kaisari vitu vya Kaisari, bali vitu vya Mungu kwa Mungu” pia. (Luka 20:25; 1 Petro 2:13-17, NW) Kwa kuwa Neno la Mungu huonyesha kwamba mamlaka za kiserikali za ulimwengu huu ni za kitambo tu, Mashahidi wa Yehova hujitayarisha sasa kwa ajili ya maisha kamili zaidi, yaliyo maisha halisi, yatakayofurahiwa karibuni chini ya utawala wa Ufalme wa Kristo. (1 Timotheo 6:17-19) Ingawa wao hawatashiriki sehemu katika kupindua serikali za ulimwengu huu, Mashahidi wanapatwa na woga wa heshima ya kimungu juu ya yale ambayo Neno la Mungu lililovuviwa, Biblia Takatifu, husema kuhusu hukumu ambayo Yehova anakaribia kutekeleza kwenye Har–Magedoni.—Isaya 26:20, 21; Waebrania 12:28, 29.

      Kwenye Pigano la Mwisho Kabisa!

      14. Ni nini kinachofananishwa na “upanga mkali mrefu” unaotokeza katika kinywa cha Yesu?

      14 Yesu anakamilisha ushindi wake kwa mamlaka gani? Yohana atuarifu: “Na katika kinywa chake unatokeza upanga mkali mrefu kwamba yeye apate kupiga mataifa kwa huo, na yeye atayachunga kwa ufito wa chuma.” (Ufunuo 19:15a, NW) Huo “upanga mkali mrefu” huwakilisha mamlaka ambayo Yesu amepewa na Mungu ya kutoa amri za kufisha wote wanaokataa kuunga mkono Ufalme wa Mungu. (Ufunuo 1:16; 2:16) Mfananisho huu ulio dhahiri unalingana na maneno ya Isaya? “Yeye [Yehova] aliendelea kufanya kinywa changu kama upanga mkali. Katika uvuli wa mkono wake yeye ameficha mimi. Na hatua kwa hatua yeye alifanya mimi kuwa mshale uliokwatuliwa.” (Isaya 49:2, NW) Hapa Isaya alionyesha kivuli cha Yesu, ambaye hupiga mbiu ya hukumu za Mungu na kuzitekeleza, kana kwamba kwa mshale usiokosea.

      15. Kufikia hapa katika wakati, ni nani watakuwa wamekwisha fichuliwa na kuhukumiwa ili kuonyesha mwanzo wa nini?

      15 Kufikia hapa katika wakati, Yesu atakuwa tayari ametenda katika kutimiza maneno ya Paulo: “Ndipo, kweli kweli, mwasi-sheria atafunuliwa, ambaye Bwana Yesu atamwondolea mbali kwa roho ya kinywa chake na kumfanya kuwa si kitu kwa udhihirisho wa kuwapo kwake.” Ndiyo, kuwapo (Kigiriki, pa·rou·siʹa) kwa Yesu kumeonyeshwa kutoka 1914 na kuendelea kwa kufichuliwa na kuhukumiwa kwa mtu wa uasi-sheria, viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo. Kuwapo huko kutadhihirishwa kwa njia yenye kutokeza wakati pembe kumi za hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu zitakapotekeleza hukumu hiyo na kuiharibu Jumuiya ya Wakristo, pamoja na sehemu inayobaki ya Babuloni Mkubwa. (2 Wathesalonike 2:1-3, 8, NW) Huo utakuwa ndio mwanzo wa dhiki kubwa! Baada ya hapo, Yesu ageuza uangalifu wake kwenye sehemu inayobaki ya tengenezo la Shetani, kupatana na unabii huu: “Ni lazima yeye apige dunia kwa ufito wa kinywa chake; na kwa roho ya midomo yake yeye ataweka mwovu kwenye kifo.”—Isaya 11:4, NW.

      16. Zaburi na Yeremia huelezaje habari ya daraka la Mwanavita-Mfalme wa Yehova?

      16 Mwanavita-Mfalme, akiwa mwekwa rasmi wa Yehova, atafanya utofautisho kati ya wale watakaookoka na wale watakaokufa. Yehova, akisema kiunabii kwa Mwana huyu wa Mungu, anasema: “Wewe utavunja wao [watawala wa dunia] kwa fimbo ya kifalme ya chuma, kana kwamba ni chombo cha mfinyanzi wewe utavunja wao vipande vipande.” Na Yeremia anawaambia viongozi kama hao wafisadi wa kiserikali na watumishi wao, akisema: “Zomeni, nyinyi wachungaji, na kuguta! Na kugaagaa huku na huku, nyinyi wenye fahari ya kifalme wa kundi, kwa sababu siku zenu za kuchinja na za kutawanya kwenu zimetimizwa, na ni lazima nyinyi mwanguke kama chombo chenye kutamanika!” Hata watawala hao wawe wameonekana kuwa wenye kutamanika kama nini kwa ulimwengu mbovu, dharuba moja kutoka kwa fimbo ya kifalme ya Mfalme itawavunjavunja, kama kuvunja chombo chenye kuvutia. Itakuwa kama vile Daudi alitoa unabii kuhusu Bwana Yesu: “Fimbo ya imara yako Yehova atapeleka nje kutoka Sayuni, kusema: ‘Enda hali ukitiisha katikati ya maadui wako.’ Yehova mwenyewe kwenye mkono wako wa kulia kwa hakika atavunja wafalme vipande vipande katika siku ya kasirani yake. Yeye atatekeleza hukumu miongoni mwa mataifa; yeye atasababisha ujazi wa miili mifu.”—Zaburi 2:9, 12; 83:17, 18; 110:1, 2, 5, 6; Yeremia 25:34, NW.

      17. (a) Yohana huelezaje tendo la kufisha la Mwanavita-Mfalme? (b) Simulia baadhi ya unabii ambao huonyesha jinsi siku ya kasirani ya Mungu itakavyokuwa yenye kuleta baa kwa mataifa?

      17 Mwanavita-Mfalme huyu mwenye nguvu huonekana tena katika mandhari inayofuata ya njozi: “Yeye hukanyaga vilevile shinikizo la divai ya kasirani ya hasira-kisasi ya Mungu Mweza Yote.” (Ufunuo 19:15b, NW) Katika njozi moja iliyotangulia, Yohana alikuwa tayari ameona kukanyagwa kwa “shinikizo la divai ya kasirani ya Mungu.” (Ufunuo 14:18-20, NW) Isaya pia hueleza habari ya shinikizo la divai la kufisha, na manabii wengine wanasimulia jinsi siku ya kasirani ya Mungu itakavyokuwa yenye kuleta baa kwa mataifa yote.—Isaya 24:1-6; 63:1-4; Yeremia 25:30-33; Danieli 2:44; Sefania 3:8; Zekaria 14:3, 12, 13; Ufunuo 6:15-17.

      18. Nabii Yoeli hufumbua nini kwa habari ya Yehova kuhukumu mataifa yote?

      18 Nabii Yoeli anashirikisha shinikizo la divai na Yehova akija ‘kuhukumu mataifa yote kuzunguka huku na huku.’ Na Yehova ndiye anayetoa amri, bila shaka kwa Hakimu mshirika Wake, Yesu, na majeshi yake ya kimbingu: “Tupeni mundu ndani, kwa maana vuno limeiva. Njooni, shukeni, kwa maana shinikizo la divai limejaa. Yale mapipa kwa kweli yanafurika; kwa maana ubaya umekuwa tele. Umati wa watu, umati wa watu umo katika uwanda-bonde wa uamuzi, kwa maana siku ya Yehova iko karibu katika ule uwanda-bonde wa uamuzi. Jua na mwezi vyenyewe kwa hakika vitakuwa na utusitusi, na nyota hasa kwa kweli zitaondoa uangavu wazo. Na kutoka Sayuni Yehova mwenyewe atanguruma, na kutoka Yerusalemu yeye atatoa sauti yake. Na mbingu na dunia kwa hakika zitasukasuka; lakini Yehova atakuwa kimbilio kwa watu wake, na ngome kwa wana wa Israeli. Na nyinyi watu mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova Mungu wenu.”—Yoeli 3:12-17, NW.

      19. (a) Swali lililoulizwa kwenye 1 Petro 4:17 litajibiwaje? (b) Ni jina gani ambalo limeandikwa juu ya vazi la nje la Yesu, na ni kwa nini linathibitika kuwa lenye kufaa?

      19 Hiyo itakuwa siku ya maangamizi, kweli kweli, kwa mataifa na wanadamu wasiotii lakini siku ya muawana kwa wote ambao wamefanya kimbilio lao kuwa Yehova na Mwanavita-Mfalme wake! (2 Wathesalonike 1:6-9) Hukumu ambayo ilianza na nyumba ya Mungu katika 1918 itakuwa imeendelea kufikia upeo wayo, ikijibu swali kwenye 1 Petro 4:17 NW: “Utakuwa nini mwisho wa wale ambao si watiifu kwa habari njema za Mungu?” Mshindi mtukufu atakuwa amekwisha kanyaga shinikizo la divai mpaka mwisho, akionyesha kwamba yeye ndiye yule Mmoja aliyekwezwa ambaye kwa habari zake Yohana alisema: “Na juu ya vazi lake la nje, hata juu ya paja lake, yeye ana jina lililoandikwa, Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana.” (Ufunuo 19:16, NW) Yeye amejithibitisha kuwa mwenye nguvu zaidi sana ya mtawala yeyote wa kidunia, mfalme au bwana yeyote wa kibinadamu. Adhama na umaridadi wake unapita wote. Yeye amepanda “katika kusudi la ukweli na unyenyekevu na uadilifu” na amesherehekea ushindi kwa wakati wote! (Zaburi 45:4, NW) Juu ya vazi lake lililonyunyiziwa damu limeandikwa jina alilopewa na Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu, ambaye yeye ni Mteteaji wake!

      Ule Mlo wa Jioni Mkubwa wa Mungu

      20. Yohana anaelezaje habari ya “mlo wa jioni mkubwa wa Mungu,” hilo likitukumbusha unabii gani wa mapema zaidi, lakini unaofanana na huo?

      20 Katika njozi ya Ezekieli, baada ya uharibifu wa umati wa Gogu, ndege na wanyama wa mwitu wanaalikwa kwenye karamu! Wao wanaondolea mandhari-bara mizoga kwa kula miili mifu ya maadui wa Yehova. (Ezekieli 39:11, 17-20) Maneno yanayofuata ya Yohana yanatukumbusha kwa udhahiri unabii huo wa mapema zaidi: “Na mimi nikaona pia malaika mmoja akisimama katika jua, na yeye akalia kwa sauti kubwa na kusema kwa ndege wote ambao huruka katika mbingu ya kati: ‘Njooni hapa, kusanyikeni pamoja kwenye mlo wa jioni mkubwa wa Mungu, kwamba nyinyi mpate kula sehemu zenye mnofu za wafalme na sehemu zenye mnofu za makamanda wa kivita na sehemu zenye mnofu za wanaume wakakamavu na sehemu zenye mnofu za farasi na za wale walioketi juu yao, na sehemu zenye mnofu za wote, za watu huru na pia za watumwa na za wadogo na wakubwa.’”—Ufunuo 19:17, 18, NW.

      21. Ni nini kinachoonyeshwa na (a) “malaika akisimama katika jua”? (b) uhakika wa kwamba wafu wanaachwa wamelala chini? (c) orodha ya wale ambao maiti zao zingeachwa zimelala chini? (d) usemi “mlo wa jioni mkubwa wa Mungu”?

      21 Malaika “akisimama katika jua,” mahali penye amri kwa ajili ya kuvuta usikivu wa ndege wote. Yeye anawaalika wawe tayari kulafua mnofu wa wale ambao karibu kuuawa na Mwanavita-Mfalme na majeshi yake ya kimbingu. Uhakika wa kwamba wafu wataachwa usoni pa nchi unaonyesha kwamba watakufa kwa aibu mbele ya watu wote. Kama Yezebeli wa kale, hawatakuwa na maziko yenye kuheshimika. (2 Wafalme 9:36, 37) Orodha ya wale ambao maiti zao zingeachwa zimelala huko huonyesha masafa ya uharibifu: wafalme, makamanda wa kivita, wanaume wakakamavu, watu huru, na watumwa. Hakuna wa kuachwa. Kila alama ya ulimwengu mwasi unaopinga Yehova itaondolewa mbali. Baada ya hii, hakutakuwako tena bahari isiyotulia ya wanadamu waliovurugika. (Ufunuo 21:1) Huu ndio “mlo wa jioni mkubwa wa Mungu,” kwa kuwa Yehova ndiye anayealika ndege hao waushiriki.

      22. Yohana anatoaje muhtasari wa mwendo wa ile vita ya mwisho?

      22 Yohana anatoa muhtasari wa mwendo wa vita hiyo ya mwisho: “Na mimi nikaona hayawani-mwitu na wafalme wa dunia na majeshi yao wamekusanyika pamoja kufanya vita na mmoja aketiye juu ya farasi na majeshi yake. Na hayawani-mwitu akabambwa, na pamoja na yeye nabii bandia ambaye alifanya mbele yake ishara ambazo kwa hizo yeye aliongoza vibaya wale ambao walipokea alama ya hayawani-mwitu na wale ambao hutoa ibada kwa mfano wake. Wakiwa wangali hai, wao wawili walivurumishwa ndani ya ziwa lenye moto ambalo huwaka salfa. Lakini wanaobaki waliuliwa mbali kwa upanga mrefu wa mmoja aketiye juu ya farasi, upanga ambao ulitokeza katika kinywa chake. Na ndege wote wakashiba sehemu zenye mnofu zao.”—Ufunuo 19:19-21, NW.

      23. (a) Ni katika maana gani “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi” inapiganwa kwenye “Har–Magedoni”? (b) Ni onyo gani ambalo “wafalme wa dunia” wameshindwa kutii, kukiwa na tokeo gani?

      23 Baada ya kumiminwa kwa bakuli la sita la hasira-kisasi ya Yehova, Yohana aliripoti kwamba “wafalme wa ulimwengu wote” walikusanywa na propaganda ya roho waovu kwenye “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi.” Hiyo inapiganwa kwenye Har–Magedoni—si mahali halisi, bali ni ile hali ya tufe lote ambayo hutaka hukumu ya Yehova itekelezwe. (Ufunuo 16:12, 14, 16, UV) Sasa Yohana aona mipororo ya pigano. Hapo, waliojipanga dhidi ya Mungu, ni “wafalme [wote] wa dunia na majeshi yao.” Kwa ukaidi wao wamekataa kujitiisha wenyewe kwa Mfalme wa Yehova. Yeye aliwapa onyo lenye haki katika huu ujumbe wake uliovuviwa: “Mbusuni Mwana, kwamba [Yehova] asipate kutiwa ukali na nyinyi msipate kupotea kutoka njia.” Wakiwa hawakutii utawala wa Kristo ni lazima wafe.—Zaburi 2:12, NW.

      24. (a) Ni hukumu gani inayotekelezwa juu ya hayawani-mwitu na juu ya nabii bandia, na ni katika maana gani wao “wakiwa wangali hai”? (b) Kwa nini “ziwa la moto” lazima liwe la kitamathali?

      24 Hayawani-mwitu mwenye vichwa saba na pembe kumi kutoka katika bahari, akiwakilisha tengenezo la kisiasa la Shetani, anatumbukizwa ndani ya usahaulifu kabisa, na pamoja na yeye aenda nabii bandia, serikali ya saba ya ulimwengu. (Ufunuo 13:1, 11-13; 16:13) Wakiwa wangali “hai,” au wangali wanatenda katika umoja wao wa kuwapinga watu wa Mungu duniani, wao wanatupwa ndani ya “ziwa la moto.” Je! hili ni ziwa halisi la moto? La, kama vile hayawani-mwitu na nabii bandia wasivyokuwa wanyama halisi. Badala ya hivyo, ni ufananisho wa uharibifu kamili wa mwisho kabisa, mahali ambako hakuna kurudi. Humo ndimo, baadaye, kifo na Hadesi, pamoja na Ibilisi mwenyewe, vitavurumishwa. (Ufunuo 20:10, 14, NW) Kwa hakika si tanuri la mateso ya milele kwa waovu, kwa kuwa wazo lenyewe la mahali kama hapo ni lenye kukirihika kwa Yehova.—Yeremia 19:5; 32:35; 1 Yohana 4:8, 16.

      25. (a) Ni nani wale ambao “waliuliwa mbali kwa upanga mrefu wa mmoja aketiye juu ya farasi”? (b) Je! tutazamie kwamba hao waliouliwa mbali watakuwa na ufufuo?

      25 Wengine wote ambao hawakuwa sehemu ya serikali moja kwa moja lakini hata hivyo walikuwa sehemu isiyoongoleka ya ulimwengu huu mfisadi wa aina ya binadamu, wao hali kadhalika ‘wanauliwa mbali kwa upanga mrefu wa mmoja aketiye juu ya farasi.’ Yesu atawatamka kuwa wanastahili kifo. Kwa kuwa kwa habari yao ziwa la moto halikutajwa, je! tutaraji kwamba watafufuliwa? Hakuna mahali tunapoambiwa kwamba wenye kufishwa wakati huo na Hakimu wa Yehova wanapaswa kufufuliwa. Kama Yesu mwenyewe alivyotaarifu, wote wale ambao si “kondoo” wanaenda zao “katika moto wa milele uliotayarishwa kwa ajili ya Ibilisi na malaika zake,” yaani, “katika kukatiliwa mbali kwa milele.” (Mathayo 25:33, 41, 46, NW) Hii huileta kwenye upeo “siku ya hukumu na ya kuharibiwa kwa watu wasiohofu Mungu.”—2 Petro 3:7; Nahumu 1:2, 7-9; Malaki 4:1, NW.

      26. Taarifu kifupi tokeo la Har–Magedoni.

      26 Katika njia hii, tengenezo lote la kidunia la Shetani laja kwenye ukomo. “Mbingu za kwanza” za utawala wa kisiasa zimepitilia mbali. “Dunia,” mfumo ulioonekana kuwa wa kudumu ambao Shetani amejenga kwa muda wa karne zilizopita, sasa imeharibiwa kabisa. “Bahari,” tungamo la wanadamu waovu wenye kupingana na Yehova, haipo tena. (Ufunuo 21:1; 2 Petro 3:10, NW) Ingawa hivyo, ni nini ambacho Yehova ameweka akiba kwa ajili ya Shetani mwenyewe? Yohana huendelea kutusimulia.

  • Kuponda Kichwa cha Nyoka
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Sura ya 40

      Kuponda Kichwa cha Nyoka

      Njozi ya 14—Ufunuo 20:1-10

      Habari: Kutiwa kwa Shetani ndani ya abiso, Utawala wa Mileani, mtihani wa mwisho kabisa wa wanadamu, na kuharibiwa kwa Shetani

      Wakati wa utimizo: Kutoka mwisho wa dhiki kubwa hadi kuharibiwa kwa Shetani

      1. Utimizo wa unabii wa kwanza wa Biblia umeendeleaje?

      JE! WEWE wakumbuka unabii wa kwanza wa Biblia? Ulitamkwa na Yehova Mungu aliposema kwa Nyoka: “Mimi nitaweka uadui kati ya wewe na mwanamke na kati ya mbegu yako na mbegu yake. Yeye atachubua wewe katika kichwa na wewe utachubua yeye katika kisigino.” (Mwanzo 3:15, NW) Sasa utimizo wa unabii huo waja kwenye upeo wao! Sisi tumefuatilia historia ya vita ya Shetani dhidi ya tengenezo la Yehova la kimbingu lililo kama mwanamke. (Ufunuo 12:1, 9) Mbegu ya kidunia ya Nyoka, pamoja na dini, siasa, na biashara kubwa-kubwa yayo, imerundika mnyanyaso wenye ukatili juu ya mbegu ya mwanamke, Yesu Kristo na wafuasi wake wapakwa-mafuta 144,000, hapa duniani. (Yohana 8:37, 44; Wagalatia 3:16, 29) Shetani alimpiga Yesu kwa kifo chenye maumivu makali. Lakini hiki kilithibitika kuwa kama kidonda cha kisigino, kwa maana Mungu alimfufua Mwana wake mwaminifu siku ya tatu.—Matendo 10:38-40.

      2. Shetani huchubuliwaje, na ni jambo gani linaloipata mbegu ya Shetani ya kidunia?

      2 Vipi Nyoka na mbegu yake? Wapata 56 W.K. mtume Paulo aliandika barua ndefu kwa Wakristo katika Roma. Katika kuimalizia, yeye aliwatia moyo kwa kusema: “Kwa upande wake, Mungu ambaye hutoa amani ataponda Shetani chini ya nyayo zenu karibuni.” (Warumi 16:20, NW) Hii ni zaidi ya kuchubua juujuu tu. Shetani atapondwapondwa! Hapa Paulo alitumia neno la Kigiriki, syn·triʹbo, hilo linamaanisha kuchubua katika hali kama ya ute, kukanyagakanyaga chini ya nyayo, kuharibu kabisa kwa kupondaponda. Kwa habari ya sehemu ya kibinadamu ya mbegu ya Nyoka, hii inatazamiwa ipatwe na tauni halisi katika siku ya Bwana, ikifikia upeo kwenye dhiki kubwa katika kupondwapondwa kabisa kwa Babuloni Mkubwa na ile mifumo ya kisiasa ya ulimwengu, pamoja na wategemezaji wayo wa kifedha na kivita. (Ufunuo, sura za 18 na 19) Hivyo Yehova analeta kwenye upeo uadui kati ya mbegu mbili. Mbegu ya mwanamke husherehekea ushindi juu ya mbegu ya kidunia ya Nyoka, na mbegu hiyo inakuwa haipo tena!

      Shetani Atiwa Ndani ya Abiso

      3. Yohana anatuambia ni nini kitakachompata Shetani?

      3 Basi, ni nini kilicho akibani kwa ajili ya Shetani mwenyewe na roho waovu wake? Yohana hutuambia: “Na mimi nikaona malaika mmoja akija chini kutoka katika mbingu mwenye ufunguo wa abiso na mnyororo mkubwa katika mkono wake. Na yeye akakamata drakoni, nyoka wa awali kabisa, ambaye ndiye Ibilisi na Shetani, na akamboba yeye kwa miaka elfu moja. Na yeye alimvurumisha ndani ya abiso na akaifunga na akatia kalafati juu yake, ili asipate kuongoza vibaya mataifa tena mpaka miaka elfu ilipokuwa imekwisha. Baada ya vitu hivi ni lazima yeye aachwe legelege kwa kitambo kidogo.”—Ufunuo 20:1-3, NW.

      4. Ni nani aliye malaika mwenye ufunguo wa abiso, na sisi twajuaje?

      4 Malaika huyu ni nani? Ni lazima yeye awe na nguvu nyingi mno kuweza kumwondolea mbali adui mkuu wa Yehova. Yeye ana “ufunguo wa abiso na mnyororo mkubwa.” Je! hiyo haitukumbushi njozi ya mapema zaidi? Ee, ndiyo, yule mfalme juu ya nzige anaitwa “malaika wa abiso”! (Ufunuo 9:11, NW) Kwa hiyo hapa sisi tunaona Mteteaji Mkuu wa Yehova, Yesu Kristo aliyetukuzwa, akitenda. Huyu malaika mkuu ambaye alitupa Shetani kutoka katika mbingu, ambaye alihukumu Babuloni Mkubwa, na ambaye aliondolea mbali “wafalme wa dunia na majeshi yao” kwenye Har–Magedoni hakika hangekaa kando aruhusu malaika mwingine mdogo zaidi apige dharuba kuu hii ya kutia Shetani katika abiso!—Ufunuo 12:7-9; 18:1, 2; 19:11-21, NW.

      5. Malaika wa abiso hushughulikaje na Shetani Ibilisi, na kwa nini?

      5 Drakoni mkubwa mwenye rangi-moto alipovurumishwa chini kutoka katika mbingu, alisemwa kuwa ndiye “nyoka wa awali kabisa, mmoja ambaye huitwa Ibilisi na Shetani, ambaye anaongoza vibaya dunia nzima yote inayokaliwa.” (Ufunuo 12:3, 9, NW) Sasa, wakati wa kukamatwa kwake na kutiwa ndani ya abiso, yeye ameelezwa tena kwa ukamili kuwa ndiye “drakoni, nyoka wa awali kabisa, ambaye ndiye Ibilisi na Shetani.” Huyu ambaye ni mmezaji, mdanganyaji, mchongezi, na mpinzani mwenye sifa mbaya sana anafungwa mnyororo na kuvurumishwa “ndani ya abiso,” ambayo inashindikwa ndi ndi ndi na kutiwa kalafati kikiki, “ili asipate kuongoza vibaya mataifa tena.” Huku kutiwa kwa Shetani ndani ya abiso ni kwa muda wa miaka elfu moja, wakati huo uvutano wake juu ya aina ya binadamu utakuwa haupo tena kama wa mfungwa aliye ndani ya gereza la shimo lenye kina kirefu. Malaika wa abiso anamwondolea mbali kabisa Shetani asiwe na mgusano wowote na Ufalme wa uadilifu. Lo! ni kitulizo kama nini kwa aina ya binadamu!

      6. (a) Kuna ithibati gani kwamba roho waovu pia huenda ndani ya abiso? (b) Sasa ni nini kinachoweza kuanza, na kwa nini?

      6 Inakuwaje kwa roho waovu? Wao vilevile “wamewekwa kwa ajili ya hukumu.” (2 Petro 2:4, NW) Shetani huitwa “Beelzebubu mtawala wa roho waovu.” (Luka 11:15, 18; Mathayo 10:25, NW) Kwa sababu ya kumwunga mkono Shetani kwa muda mrefu, je! wao wasipasishwe hukumu iyo hiyo? Kwa muda mrefu abiso imekuwa kitu cha kuogopwa na roho waovu hao; pindi moja Yesu alipokabiliana nao, wao “walifuliza kusihi yeye asiagize wao waende ndani ya abiso.” (Luka 8:31, NW) Lakini Shetani anapotiwa ndani ya abiso, kwa hakika malaika zake watavurumishwa ndani ya abiso pamoja naye. (Linga Isaya 24:21, 22.) Baada ya Shetani na roho waovu kutiwa ndani ya abiso, Utawala wa Miaka Elfu wa Yesu Kristo unaweza kuanza.

      7. (a) Ni katika hali gani Shetani na roho waovu wake watakuwa wakiwa ndani ya abiso, na sisi twajuaje? (b) Je! Hadesi na abiso ni kitu kile kile? (Ona kielezi cha chini.)

      7 Je! Shetani na roho waovu wake watakuwa wakitenda wakiwamo ndani ya abiso? Basi, kumbuka hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu, mwenye vichwa saba ambaye “alikuwako, lakini hayuko, na bado yu karibu kupanda nje ya abiso.” (Ufunuo 17:8, NW) Alipokuwa katika abiso, ‘alikuwa hayuko.’ Alikuwa hatendi, hajongei, kwa madhumuni na makusudi yote alikuwa amekufa. Hali kadhalika, mtume Paulo akinena juu ya Yesu, alisema: “‘Ni nani atakayeshuka kuingia ndani ya abiso?’ yaani, kumleta juu Kristo kutoka kwa wafu.” (Warumi 10:7, NW) Akiwa katika abiso hiyo, Yesu alikuwa amekufa.a Basi, inapatana na akili kukata shauri kwamba Shetani na roho waovu wake watakuwa katika hali ya kutotenda kama ya kifo kwa muda wa miaka elfu ya kutiwa kwao ndani ya abiso. Hizo ni taarifa njema kama nini kwa wapenda uadilifu!

      Mahakimu kwa Miaka Elfu Moja

      8, 9. Sasa Yohana hutuambia nini juu ya wale wanaoketi juu ya viti vya ufalme, nao ni akina nani?

      8 Baada ya miaka elfu, Shetani anaachiliwa kutoka katika abiso kwa kitambo kifupi. Kwa nini? Kabla ya kutoa jibu, Yohana anarudisha uangalifu wetu kwenye mwanzo wa kipindi hicho cha wakati. Tunasoma: “Na mimi niliona viti vya ufalme, na kulikuwako wale walioketi juu yavyo, na nguvu za kuhukumu zilipewa kwao.” (Ufunuo 20:4a, NW) Ni nani hawa wanaoketi juu ya viti vya ufalme na kutawala katika mbingu pamoja na Yesu aliyetukuzwa?

      9 Wao ni “watakatifu” ambao Danieli alieleza habari yao kuwa wakitawala katika Ufalme pamoja na Mmoja aliye “kama mwana wa binadamu.” (Danieli 7:13, 14, 18, NW) Wao ndio wale wale wazee 24 wanaoketi juu ya viti vya ufalme vya kimbingu katika kuwapo hasa kwa Yehova. (Ufunuo 4:4) Wao ni kutia ndani mitume 12, ambao Yesu aliwapa ahadi hii: “Katika uumbaji-upya wakati Mwana wa binadamu anaketi chini juu ya kiti cha ufalme chake chenye utukufu, nyinyi ambao mmefuata mimi mtaketi nyinyi wenyewe pia juu ya viti vya ufalme kumi na viwili, mkihukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.” (Mathayo 19:28, NW) Wangetia ndani Paulo pia, pamoja na Wakristo Wakorintho ambao walibaki wakiwa waaminifu. (1 Wakorintho 4:8; 6:2, 3) Wao ni kutia ndani, vilevile, washiriki wa kundi la Laodikia ambao walishinda.—Ufunuo 3:21.

      10. (a) Sasa Yohana huelezaje habari ya wafalme 144,000? (b) Kutokana na aliyotuambia Yohana mapema zaidi, wafalme 144,000 hutia ndani nani?

      10 Viti vya ufalme—144,000 vyote pamoja—vimetayarishwa kwa ajili ya hawa washindi wapakwa-mafuta ambao ‘wamenunuliwa kutoka miongoni mwa aina ya binadamu wakiwa matunda ya kwanza kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo.’ (Ufunuo 14:1, 4, NW) “Ndiyo,” aendelea Yohana, “mimi niliona nafsi za wale waliouawa kwa shoka kwa ajili ya ushahidi waliotoa kwa Yesu na kwa ajili ya kusema juu ya Mungu, na wale ambao hawakuwa wameabudu wala hayawani-mwitu wala mfano wake na ambao hawakuwa wamepokea alama juu ya kipaji cha uso wao na juu ya mkono wao.” (Ufunuo 20:4b, NW) Miongoni mwa wafalme hao, basi, wamo wale Wakristo wafia-imani ambao mapema zaidi, wakati wa kufunguliwa kwa kifungo cha kwanza, walimwuliza Yehova angengoja muda gani zaidi ili alipize kisasi cha damu yao. Wakati huo, walipewa joho jeupe na kuambiwa wangojee kitambo kidogo. Lakini sasa kisasi cha damu yao kimekwisha lipizwa kupitia kuteketezwa kwa Babuloni Mkubwa, na mataifa kuharibiwa na Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana, na Shetani kutiwa ndani ya abiso.—Ufunuo 6:9-11; 17:16; 19:15, 16, NW.

      11. (a) Sisi tuueleweje usemi “waliouawa kwa shoka”? (b) Ni kwa nini inaweza kusemwa kwamba wote 144,000 walikufa kifo cha dhabihu?

      11 Je! mahakimu wa kifalme hawa wote 144,000 ‘waliuawa kwa shoka’ kimwili? Yaelekea, ni wachache wao kwa kulinganisha waliouawa hivyo kwa maana halisi. Ingawa hivyo, usemi huu bila shaka unakusudiwa kutia ndani Wakristo wapakwa-mafuta wote waliovumilia ufia-imani kwa njia moja au nyingine.b (Mathayo 10:22, 28) Kwa hakika, Shetani angependa wote wauawe kwa shoka, lakini, kwa kweli, si ndugu wote wapakwa-mafuta wa Yesu wanaokufa wakiwa wafia-imani. Wengi wao huuawa na ugonjwa au uzee. Hata hivyo, hao pia ni wa kile kikundi ambacho Yohana anaona sasa. Kifo cha wao wote, kwa maana fulani, ni cha dhabihu. (Warumi 6:3-5) Kwa kuongezea, hakuna hata mmoja wao aliyekuwa sehemu ya ulimwengu. Kwa sababu hiyo, wao wote wamechukiwa na ulimwengu, maana yake, wakawa wafu katika macho yao. (Yohana 15:19; 1 Wakorintho 4:13) Hakuna hata mmoja wao aliyeabudu hayawani-mwitu au mfano wake, na walipokufa, hakuna hata mmoja wao aliyechukua alama ya hayawani. Wao wote walikufa wakiwa washindi.—1 Yohana 5:4; Ufunuo 2:7; 3:12; 12:11.

      12. Yohana anaripoti nini juu ya wafalme 144,000, na kuja kwao kwenye uhai kunatukia lini?

      12 Sasa washindi hawa waishi tena! Yohana aripoti: “Na wao wakaja kwenye uhai na wakatawala wakiwa wafalme pamoja na Kristo kwa miaka elfu moja.” (Ufunuo 20:4c, NW) Je! hii inamaanisha kwamba mahakimu hawa hawafufuliwi mpaka baada ya uharibifu wa mataifa na Shetani na roho waovu wake kutiwa ndani ya abiso? Hapana. Walio wengi wao tayari wako hai sana, kwa kuwa walipanda farasi pamoja na Yesu dhidi ya mataifa kwenye Har–Magedoni. (Ufunuo 2:26, 27; 19:14) Kweli kweli, Paulo alionyesha kwamba ufufuo wao unaanza upesi baada ya kuwapo kwa Yesu kuanza katika 1914 na kwamba baadhi yao hufufuliwa mbele ya wengine. (1 Wakorintho 15:51-54; 1 Wathesalonike 4:15-17) Kwa hiyo, kuja kwao kwenye uhai kunatukia kwa kipindi fulani cha wakati wanapopokea mmoja mmoja zawadi ya uhai usioweza kufa katika mbingu.—2 Wathesalonike 1:7; 2 Petro 3:11-14.

      13. (a) Inatupasa tuoneje miaka elfu ambayo katika hiyo 144,000 hutawala, na kwa nini? (b) Papiasi wa Hierapolisi aliionaje miaka elfu? (Ona kielezi cha chini.)

      13 Kutawala na kuhukumu kwao kutakuwa kwa miaka elfu moja. Je! hii ni miaka elfu moja halisi, au inatupasa tuione kwa njia ya ufananisho kuwa ni kipindi kirefu cha wakati, kisichodhihirishwa? “Maelfu” yaweza kumaanisha hesabu kubwa isiyodhihirishwa, kama vile kwenye 1 Samweli 21:11. Lakini hapa “elfu” ni halisi, kwa kuwa inaonekana mara tatu katika Ufunuo 20:5-7 kama ile “miaka elfu.” Paulo aliita wakati huu wa hukumu “siku moja” alipotaarifu: “Yeye [Mungu] ameweka siku moja ambayo katika hiyo yeye anakusudia kuhukumu dunia inayokaliwa kwa uadilifu.” (Matendo 17:31, NW) Kwa kuwa Petro anatuambia kwamba siku moja kwa Yehova ni kama miaka elfu moja, inafaa kwamba hii Siku ya Hukumu iwe miaka elfu moja halisi.c—2 Petro 3:8, NW.

      Mabaki ya Wafu

      14. (a) Yohana hupachika taarifa gani juu ya “mabaki ya wafu”? (b) Semi za mtume Paulo zinanururishaje usemi ‘kuja kwenye uhai’?

      14 Ingawa hivyo, hawa wafalme watahukumu nani ikiwa, kama vile mtume Yohana anapachika hapa, “(mabaki ya wafu hayakuja kwenye uhai mpaka miaka elfu ilipokuwa imekwisha)”? (Ufunuo 20:5a, NW) Tena, usemi huu ‘kuja kwenye uhai’ wapasa ueleweke kulingana na muktadha. Usemi huu unaweza kuwa na maana tofautitofauti katika hali tofautitofauti. Mathalani, Paulo alisema juu ya Wakristo wenzake wapakwa-mafuta: “Ni nyinyi Mungu alifanya kuwa hai ingawa nyinyi mlikuwa wafu katika madhambi yenu.” (Waefeso 2:1, NW) Ndiyo, Wakristo wapakwa-mafuta kwa roho ‘walifanywa kuwa hai,’ hata katika karne ya kwanza, wakijulishwa kuwa waadilifu kwa msingi wa imani yao katika dhabihu ya Yesu.—Warumi 3:23, 24.

      15. (a) Mashahidi wa kabla ya Ukristo walifurahia msimamo gani pamoja na Mungu? (b) Kondoo wengine ‘hujaje kwenye uhai,’ na ni wakati gani wao watamiliki dunia kwa maana iliyo kamili zaidi sana?

      15 Hali moja na hiyo, mashahidi wa Yehova wa kabla ya Ukristo walijulishwa wazi kuwa waadilifu kwa habari ya kuwa na urafiki na Mungu; na Abrahamu, Isaka, na Yakobo walisemwa kuwa ‘wakiishi’ hata ingawa walikuwa wafu kimwili. (Mathayo 22:31, 32; Yakobo 2:21, 23) Hata hivyo, wao na wale wengine wote ambao wanafufuliwa, pamoja na umati mkubwa wa kondoo wengine waaminifu ambao wataokoka Har–Magedoni na watoto wowote ambao huenda wakazaliwa kwa hawa katika ulimwengu mpya, itakuwa ni lazima bado wainuliwe kwenye ukamilifu wa kibinadamu. Hilo litatimizwa na Kristo na wafalme na makuhani washirika wake wakati wa Siku ya Hukumu ya miaka elfu, kwa msingi wa dhabihu ya ukombozi ya Yesu. Kufikia mwisho wa hiyo Siku, “mabaki ya wafu” yatakuwa yamekwisha ‘kuja kwenye uhai’ katika maana ya kwamba watakuwa binadamu wakamilifu. Wanapoupita mtihani, Mungu atajulisha wazi kuwa wanastahili kuishi milele, wakiwa waadilifu katika maana iliyo kamili kabisa. Wataona utimizo kamili wa ahadi: “Waadilifu wenyewe watamiliki dunia, na wao wataishi milele juu yayo.” (Zaburi 37:29, NW) Lo! ni wenye kupendeza kama nini wakati ujao, kwa ajili ya aina ya binadamu yenye utii!

      Ule Ufufuo wa Kwanza

      16. Yohana huelezaje habari ya ufufuo wanaoupata wale wanaotawala pamoja na Kristo, na kwa nini?

      16 Kurudi sasa kwa wale ambao ‘walikuja kwenye uhai na wakatawala wakiwa wafalme pamoja na Kristo,’ Yohana aandika: “Huu ndio ufufuo wa kwanza.” (Ufunuo 20:5b) Ni wa kwanza jinsi gani? Ni “ufufuo wa kwanza” kwa habari ya wakati, kwa maana wale wanaoupata ni “matunda ya kwanza kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo.” (Ufunuo 14:4, NW) Pia ni wa kwanza kwa umaana, kwa kuwa wale wanaoushiriki wanakuwa watawala wenzi wa Yesu katika Ufalme wake wa kimbingu na wanahukumu mabaki ya aina ya binadamu. Kwa kumalizia, ni wa kwanza katika ubora. Isipokuwa Yesu Kristo mwenyewe, hao wanaoinuliwa katika ufufuo wa kwanza ndio viumbe pekee wanaosemwa katika Biblia kuwa wanapokea kutokufa.—1 Wakorintho 15:53; 1 Timotheo 6:16.

      17. (a) Yohana huelezaje habari ya taraja lenye kubarikiwa la Wakristo wapakwa-mafuta? (b) “Kifo cha pili” ni nini, na kwa nini “hakina mamlaka” juu ya washindi 144,000?

      17 Ni taraja lenye baraka kama nini kwa ajili ya hawa wapakwa-mafuta! Kama anavyojulisha wazi Yohana? “Mwenye furaha na mtakatifu ni yeyote aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza; juu ya hawa kifo cha pili hakina mamlaka.” (Ufunuo 20:6a, NW) Kama vile Yesu alivyoahidi Wakristo katika Smirna, washindi hawa ambao wanashiriki “ufufuo wa kwanza” hawatakuwa katika hatari ya kupata dhara kutoka “kifo cha pili,” ambacho humaanisha utowesho, uharibifu pasi na tumaini la ufufuo. (Ufunuo 2:11; 20:14, NW) Kifo cha pili “hakina mamlaka” juu ya washindi kama hao, kwa maana wao watakuwa wamekwisha kuvaa kutofisidika na kutokufa.—1 Wakorintho 15:53.

      18. Yohana anasema nini sasa juu ya watawala wapya wa dunia, nao watatimiza nini?

      18 Ni tofauti kama nini na wafalme wa dunia wakati wa muda wa mamlaka ya Shetani! Hawa wametawala kwa muda usiozidi miaka 50 au 60 na walio wengi wao kwa miaka michache tu. Wengi wao wamekandamiza aina ya binadamu. Kwa vyovyote, mataifa yangenufaikaje daima chini ya watawala wenye kubadilika sikuzote na sera zenye kubadilika sikuzote? Kwa kutofautisha, Yohana husema kwa habari ya watawala wapya wa dunia: “Lakini wao watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, na watatawala wakiwa wafalme pamoja na yeye kwa miaka elfu.” (Ufunuo 20:6b, NW) Wakiwa pamoja na Yesu, watafanyiza serikali iliyo pekee kwa miaka elfu moja. Utumishi wao wa kikuhani, katika kutumia ubora wa dhabihu kamilifu ya kibinadamu ya Yesu, utainua binadamu watiifu wafikie ukamilifu wa kiroho, kiadili na kimwili. Utumishi wao wa kifalme utatokeza kujengwa kwa jamii ya kibinadamu ya tufe lote inayoonyesha uadilifu na utakatifu wa Yehova. Wakiwa mahakimu kwa miaka elfu moja, wao, pamoja na Yesu, wataongoza kwa upendo wanadamu waitikifu kuelekea mradi wa uhai wa milele.—Yohana 3:16.

      Mtihani wa Mwisho

      19. Kufikia mwisho wa Utawala wa Miaka Elfu hali ya dunia na ya aina ya binadamu itakuwaje, na sasa Yesu anafanya nini?

      19 Kufikia mwisho wa Utawala wa Miaka Elfu, dunia yote itakuwa imekuja kushabihi Edeni ya awali kabisa. Itakuwa ni Paradiso halisi. Aina ya binadamu iliyo kamilifu haitahitaji tena kuhani mkuu wa kuiombea mbele za Mungu, kwa kuwa alama zote za dhambi ya Adamu zitakuwa zimekwisha kuondolewa na adui ya mwisho, kifo, kuletwa kwenye si kitu. Ufalme wa Kristo utakuwa umekwisha kufikia kusudi la Mungu la kuumba ulimwengu mmoja wenye serikali moja. Kufikia hatua hii, Yesu ‘akabidhi ufalme kwa Mungu na Baba yake.’—1 Wakorintho 15:22-26, NW; Warumi 15:12.

      20. Yohana anatuambia ni nini kitakachotukia unapokuwa wakati wa ule mtihani wa mwisho?

      20 Sasa ni wakati wa mtihani wa mwisho kabisa. Je! ulimwengu huo mkamilifu wa aina ya binadamu utasimama imara katika ukamilifu wao, tofauti na wale binadamu wa kwanza katika Edeni? Yohana atuambia yanayotukia: “Sasa mara miaka elfu inapokwisha, Shetani ataachwa legelege nje ya gereza lake, na yeye ataenda nje kuongoza vibaya yale mataifa katika kona nne za dunia, Gogu na Magogu, kukusanya hayo pamoja kwenye vita. Hesabu ya hawa ni kama mchanga wa bahari. Na wao walisonga mbele juu ya upana wa dunia na kuzingira kambi ya watakatifu na jiji lenye kupendwa.”—Ufunuo 20:7-9a, NW.

      21. Kwa jitihada yake ya mwisho, Shetani anaendeleaje, na kwa nini haipasi kutushangaza kwamba wengine watafuata Shetani hata baada ya Utawala wa Miaka Elfu?

      21 Jitihada ya mwisho ya Shetani itakuwaje? Yeye anadanganya “yale mataifa katika kona nne za dunia, Gogu na Magogu,” na kuyaongoza kwenye “vita.” Ni nani angeweza kuchukua upande wa Shetani baada ya miaka elfu moja ya utawala wa kitheokrasi wenye shangwe, wenye kujenga? Basi, usisahau kwamba Shetani aliweza kuongoza vibaya Adamu na Hawa wakamilifu walipokuwa wakifurahia uhai katika Paradiso ya Edeni. Na yeye aliweza kupotosha malaika wa kimbingu ambao walikuwa wameona matokeo mabaya ya uasi wa awali kabisa. (2 Petro 2:4; Yuda 6) Kwa hiyo tusishangae kwa vile baadhi ya wanadamu wakamilifu watarubuniwa wafuate Shetani hata baada ya utawala wa Ufalme wa Mungu wa miaka elfu wenye kupendeza.

      22. (a) Ni nini kinachoonyeshwa na usemi “yale mataifa katika kona nne za dunia”? (b) Kwa nini waasi huitwa “Gogu na Magogu”?

      22 Biblia huwaita waasi hawa “mataifa katika kona nne za dunia.” Hii haimaanishi kwamba aina ya binadamu itakuwa imekwisha gawanyikana-gawanyikana tena na kuwa mataifa yaliyo pekee. Inaonyesha tu kwamba hawa watajitenga wenyewe kutoka kwa wale washikamanifu, na waadilifu wa Yehova na kudhihirisha roho ile ile mbaya ambayo mataifa yanaonyesha leo. Wao ‘watafikiria njama yenye kudhuru,’ kama alivyofanya Gogu wa Magogu katika unabii wa Ezekieli, wakiwa na mradi wa kuharibu serikali ya kitheokrasi iliyo duniani. (Ezekieli 38:3, 10-12, NW) Kwa sababu hiyo, wao huitwa “Gogu na Magogu.”

      23. Ni nini kinachoonyeshwa na uhakika wa kwamba hesabu ya waasi ni “kama mchanga wa bahari”?

      23 Hesabu ya wale wanaojiunga na Shetani katika uasi wake itakuwa “kama mchanga wa bahari.” Huo ni wingi gani? Hakuna hesabu iliyotangulia kuwekwa rasmi. (Linga Yoshua 11:4; Waamuzi 7:12.) Hesabu ya mwisho yenye jumla ya waasi itategemea jinsi kila mtu mmoja mmoja atakavyotenda kwa kuitikia hila za ujanja za Shetani. Ingawa hivyo, pasi na shaka, watakuwa hesabu kubwa, kwa kuwa watahisi ni wenye nguvu vya kutosha kushinda “kambi ya watakatifu na jiji lenye kupendwa.”

      24. (a) Ni nini lililo “jiji lenye kupendwa” nalo linaweza kuzingirwaje? (b) Ni nini kinachowakilishwa na “kambi ya watakatifu”?

      24 “Jiji lenye kupendwa” lazima liwe jiji ambalo Yesu Kristo aliyetukuzwa anasema juu yalo kwa wafuasi wake kwenye Ufunuo 3:12 na ambalo yeye anaita “jiji la Mungu wangu, Yerusalemu jipya ambalo hushuka kutoka katika mbingu kutoka kwa Mungu wangu.” Kwa kuwa hili ni tengenezo la kimbingu, kani hizo za kidunia zingewezaje ‘kulizingira’? Ni kwa vile wao huzingira “kambi ya watakatifu.” Kambi huwa nje ya jiji; kwa hiyo, “kambi ya watakatifu” lazima iwakilishe wale walio duniani nje ya mahali pa kimbingu pa Yerusalemu Jipya ambao kwa ushikamanifu hutegemeza mpango wa Yehova wa kiserikali. Wakati waasi hao walio chini ya Shetani wanaposhambulia wale waaminifu, Bwana Yesu huona hilo kuwa ni shambulio juu ya yeye. (Mathayo 25:40, 45) “Yale mataifa” yatajaribu kufutilia mbali yote ambayo Yerusalemu Jipya la kimbingu limetimiza katika kufanya dunia paradiso. Hivyo kwa kushambulia “kambi ya watakatifu,” wao wanashambulia pia “jiji lenye kupendwa.”

      Ziwa la Moto na Salfa

      25. Yohana anaelezaje tokeo la shambulio la waasi juu ya “kambi ya watakatifu,” na litamaanisha nini kwa Shetani?

      25 Je! jitihada hii ya mwisho kabisa ya Shetani itafaulu? Hakika sivyo—kama vile shambulio ambalo Gogu wa Magogu anatazamiwa kufanya juu ya Israeli wa kiroho katika siku yetu halitafaulu! (Ezekieli 38:18-23) Yohana anaeleza waziwazi tokeo: “Lakini moto ulikuja chini kutoka katika mbingu na ukameza wao. Na Ibilisi ambaye alikuwa anawaongoza vibaya alivurumishwa ndani ya ziwa la moto na salfa, ambamo wote wawili hayawani-mwitu na nabii bandia tayari walikuwa.” (Ufunuo 20:9b-10a, NW) Badala ya kutiwa ndani ya abiso tu, wakati huu Shetani, nyoka wa awali kabisa, atapondwapondwa kikweli asiweko, atasagwasagwa tikitiki, atoweshwe kabisa kabisa kana kwamba kwa moto.

      26. Ni kwa nini “ziwa la moto na salfa” haviwezi kuwa mahali halisi pa mateso?

      26 Sisi tumekwisha ona kwamba hilo “ziwa la moto na salfa” halingeweza kuwa mahali halisi pa mateso. (Ufunuo 19:20) Ikiwa Shetani angepaswa apate mateso yenye maumivu makali humo kwa umilele wote, Yehova angelazimika kumhifadhi hai. Hata hivyo, uhai ni zawadi, si adhabu. Kifo ndicho adhabu ya dhambi, na kulingana na Biblia, viumbe wafu hawahisi maumivu. (Warumi 6:23; Mhubiri 9:5, 10) Waaidha, tunasoma baadaye kwamba kifo chenyewe, pamoja na Hadesi, vinatupwa ndani ya ziwa ilo hilo la moto na salfa. Hakika, Kifo na Hadesi haviwezi kuona umivu.—Ufunuo 20:14.

      27. Kilichopata Sodoma na Gomora hutusaidiaje sisi kuelewa usemi wa ziwa la moto na salfa?

      27 Yote haya yanaongezea kani lile oni la kwamba ziwa la moto na salfa ni la ufananisho. Na zaidi, mtajo wa moto na salfa hurudisha akilini hukumu ya Sodoma na Gomora ya kale, yaliyoharibiwa na Mungu kwa sababu ya uovu wayo mkubwa sana. Wakati wayo ulipofika, “Yehova alifanya mvua inye salfa na moto kutoka kwa Yehova, kutoka katika mbingu, juu ya Sodoma na Gomora.” (Mwanzo 19:24, NW) Kilichopata majiji hayo kinaitwa “adhabu ya kihukumu ya moto wa milele.” (Yuda 7, NW) Hata hivyo, majiji hayo hayakupatwa na mateso ya milele. Badala ya hivyo, yalifutiliwa mbali, yakaondolewa kabisa kwa wakati wote, pamoja na wakazi wayo wafasiki. Majiji hayo hayako leo, na hakuna yeyote anayeweza kusema kwa uhakika mahali yalipokuwa.

      28. Ziwa la moto na salfa ni nini, na ni jinsi gani si kama kifo, Hadesi, na abiso?

      28 Kupatana na hili, Biblia yenyewe hueleza maana ya ziwa la moto na salfa: “Hii humaanisha kifo cha pili, ziwa la moto.” (Ufunuo 20:14, NW) Kwa wazi ni sawa na Gehena ambayo Yesu alisema juu yayo, mahali waovu wanapobaki wameharibiwa, si kuteswa milele. (Mathayo 10:28) Ni uharibifu kabisa, ulio kamili bila tumaini la ufufuo. Hivyo, ingawa kuna funguo za kifo, Hadesi na abiso, hakuna mtajo wa ufunguo wa kufungua ziwa la moto na salfa. (Ufunuo 1:18; 20:1) Halitaachilia kamwe mateka walo.—Linga Marko 9:43-47.

      Kuteswa Mchana na Usiku Milele

      29, 30. Yohana anasema nini juu ya Ibilisi pamoja na hayawani-mwitu na nabii bandia, nalo hili lielewekeje?

      29 Akirejezea Ibilisi pamoja na hayawani-mwitu na nabii bandia, sasa Yohana hutuambia: “Na wao watateswa mchana na usiku milele na milele.” (Ufunuo 20:10b, NW) Hili lingeweza kumaanisha nini? Kama ilivyokwisha kutajwa, si kimantiki kusema kwamba mifananisho, kama vile hayawani-mwitu na nabii bandia, pamoja na kifo na Hadesi, ingeweza kupatwa na teso kwa njia halisi. Kwa sababu hiyo, sisi hatuna sababu ya kuitikadi kwamba Shetani atakuwa akiteseka kwa umilele wote. Yeye apaswa kutoweshwa.

      30 Neno la Kigiriki ambalo limetumiwa hapa kwa “tesa,” ba·sa·niʹzo, humaanisha kwanza kabisa “kutahini (madini) kwa kipimio.” “Kuhoji kwa kutumia teso” ni maana ya pili. (The New Thayer’s Greek-English Lexicon of the New Testament) Katika muktadha, utumizi wa neno hili la Kigiriki huonyesha kwamba kinachompata Shetani kitatumika, kwa umilele wote, kuwa kipimio juu ya suala la uhalali na uadilifu wa utawala wa Yehova. Suala hilo la utawala wa enzi kuu litakuwa limekwisha malizwa mara moja kwa wakati wote. Kukaidi enzi kuu ya Yehova hakutahitaji tena kamwe kutahiniwe kwa kipindi kirefu cha wakati ili kuthibitishwe kuwa kosa.—Linga Zaburi 92:1, 15.

      31. Maneno mawili ya Kigiriki yanayohusiana na lile linalomaanisha “teso” hutusaidiaje kuelewa adhabu anayopata Shetani Ibilisi?

      31 Kwa kuongezea, neno linalohusiana ba·sa·ni·stesʹ, “mtesi,” linatumiwa katika Biblia kumaanisha “mtunza-jela.” (Mathayo 18:34, Kingdom Interlinear) Kupatana na hili, Shetani atatiwa gerezani milele katika ziwa la moto; hataachiliwa kamwe. Kwa kumalizia, katika Septuagint ya Kigiriki ambayo Yohana aliijua vizuri, neno linalohusiana baʹsa·nos linatumiwa kurejezea utwezo unaoongoza kwenye kifo. (Ezekieli 32:24, 30) Hilo linatusaidia kuona kwamba adhabu anayopata Shetani ni kifo chenye kutweza, cha milele katika ziwa la moto na salfa. Kazi zake zinakufa pamoja naye.—1 Yohana 3:8

      32. Ni adhabu gani ambayo roho waovu watapata na sisi twajuaje?

      32 Tena, roho waovu hawatajwi katika mstari huu. Je! wao wataachiliwa pamoja na Shetani mwishoni mwa miaka elfu na kisha wapate adhabu ya kifo cha milele pamoja naye? Ithibati inajibu ndiyo. Katika fumbo la maneno juu ya kondoo na mbuzi, Yesu alisema kwamba mbuzi wangeenda zao waingie “katika moto wa milele uliotayarishwa kwa ajili ya Ibilisi na malaika zake.” (Mathayo 25:41, NW) Usemi “moto wa milele” lazima urejezee ziwa la moto na salfa ambamo Shetani anavurumishwa. Malaika za Ibilisi walitupwa nje kutoka katika mbingu pamoja naye. Kwa wazi, walienda ndani ya abiso pamoja naye mwanzoni mwa Utawala wa Miaka Elfu. Kwa kupatana, basi, wao wataharibiwa pia pamoja naye katika ziwa la moto na salfa.—Mathayo 8:29.

      33. Ni habari gani ya mwisho ya Mwanzo 3:15 itakayotimizwa wakati huo, na sasa roho ya Yehova yavuta uangalifu wa Yohana kwenye jambo gani?

      33 Kwa njia hii, fasili ya mwisho ya unabii uliorekodiwa kwenye Mwanzo 3:15 inatimizwa. Shetani anapovurumishwa ndani ya hilo ziwa la moto, yeye atakuwa mfu kama nyoka ambaye kichwa chake kimesagwa chini ya kisigino cha chuma. Yeye na roho waovu wake watakuwa wameenda milele. Hawatajwi zaidi ya hapo katika kitabu cha Ufunuo. Sasa, ikiwa imekwisha ondolea mbali hawa kiunabii, roho ya Yehova inavuta uangalifu kwenye jambo lenye upendezi wa umuhimu kwa wale ambao hupokea tumaini la kidunia: Utawala wa kimbingu wa “Mfalme wa wafalme” na “wale wenye kuitwa na wachaguliwa na waaminifu pamoja na yeye” utaitokezea nini aina ya kibinadamu? (Ufunuo 17:14, NW) Ili kujibu, Yohana anaturudisha tena kwenye mwanzo wa Utawala wa Miaka Elfu.

      [Maelezo ya Chini]

      a Maandiko mengine husema kwamba Yesu alikuwa katika Hadesi alipokuwa mfu. (Matendo 2:31, NW) Hata hivyo, haitupasi kukata maneno kwamba Hadesi na abiso sikuzote ni kitu kile kile. Ingawa hayawani-mwitu na Shetani huenda ndani ya abiso, ni wanadamu pekee ndio husemwa kuwa wanaenda kwenye Hadesi, wanamokuwa wamelala katika kifo mpaka ufufuo wao.—Ayubu 14:13; Ufunuo 20:13, NW.

      b Shoka (Kigiriki, peʹle·kus) laonekana kuwa ndilo lililokuwa chombo cha kimapokeo cha kufisha katika Roma, ingawa kufikia siku ya Yohana upanga ulitumiwa kikawaida zaidi. (Matendo 12:2) Kwa hiyo, neno la Kigiriki lililotumiwa hapa, pe·pe·le·kis·meʹnon (“-liouawa kwa shoka”), lamaanisha tu “-liouawa.”

      c Kwa kupendeza, Papiasi wa Hierapolisi, ambaye anaeleweka kuwa alipokea mengine ya maarifa ya Biblia yake kutoka kwa wanafunzi wa Yohana, mwandikaji wa Ufunuo, anaripotiwa na mwanahistoria wa karne ya nne Eusebio kuwa aliitikadi katika Utawala wa Miaka Elfu halisi wa Kristo (ijapokuwa Eusebio hakuafikiana naye hata kidogo).—The History of the Church, Eusebio, 3, 39.

      [Picha katika ukurasa wa 293]

      Ile Baharifu. Yaelekea ndiko yalikokuwa Sodoma na Gomora

      [Picha katika ukurasa wa 294]

      “Mimi nitaweka uadui kati ya wewe na mwanamke na kati ya mbegu yako na mbegu yake. Yeye atachubua wewe katika kichwa na wewe utachubua yeye katika kisigino”

  • Siku ya Hukumu ya Mungu—Matokeo Yayo Yenye Shangwe!
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Sura ya 41

      Siku ya Hukumu ya Mungu—Matokeo Yayo Yenye Shangwe!

      Njozi ya 15—Ufunuo 20:11–21:8

      Habari: Ufufuo wa watu wote, Siku ya Hukumu, na baraka za mbingu mpya na dunia mpya

      Wakati wa utimizo: Utawala wa Miaka Elfu

      1. (a) Aina ya binadamu ilipoteza nini wakati Adamu na Hawa walipofanya dhambi? (b) Ni kusudi gani la Mungu ambalo halijabadilika, na twajuaje?

      TUKIWA wanadamu, tuliumbwa tuishi milele. Kama Adamu na Hawa wangalitii amri za Mungu, hawangalikufa. (Mwanzo 1:28; 2:8, 16, 17; Mhubiri 3:10, 11) Lakini walipofanya dhambi, walipoteza ukamilifu na uhai kwa ajili yao wenyewe na pia kwa ajili ya wazao wao, na kifo kikaja kutawala juu ya aina ya binadamu kikiwa adui asiyehurumia. (Warumi 5:12, 14; 1 Wakorintho 15:26) Hata hivyo, kusudi la Mungu la kuwa na wanadamu wakamilifu wakiishi milele juu ya dunia paradiso halikubadilika. Kwa sababu ya upendo wake mwingi kwa aina ya binadamu, yeye alituma duniani Mwana wake mzaliwa pekee, Yesu, ambaye alitoa uhai wake mkamilifu wa kibinadamu uwe ukombozi kwa ajili ya “wengi” wa wazao wa Adamu. (Mathayo 20:28; Yohana 3:16) Sasa Yesu anaweza kutumia huu ubora wa kisheria wa dhabihu yake ili kurudisha wanadamu wenye kuitikadi kwenye ukamilifu wa uhai katika dunia paradiso. (1 Petro 3:18; 1 Yohana 2:2) Aina ya binadamu ina sababu tukufu kama nini ya ‘kujawa na shangwe na kushangilia’!—Isaya 25:8, 9, NW.

      2. Yohana anaripoti nini kwenye Ufunuo 20:11, na “kiti cha ufalme kikubwa cheupe” ni nini?

      2 Shetani akiwa amefungiwa ndani ya abiso, Utawala wa Miaka Elfu wa Yesu unaanza. Sasa ni “siku” ambayo katika hiyo Mungu “anakusudia kuhukumu dunia inayokaliwa kwa uadilifu kwa mtu mmoja ambaye yeye ameweka rasmi.” (Matendo 17:31, NW; 2 Petro 3:8) Yohana ajulisha wazi: “Na mimi nikaona kiti cha ufalme kikubwa cheupe na mmoja aliyeketi juu yacho. Kutoka mbele zake dunia na mbingu zikakimbilia mbali, na mahali hapakupatikana kwa ajili yazo.” (Ufunuo 20:11, NW) Hiki “kiti cha ufalme kikubwa cheupe” ni nini? Hakiwezi kuwa kingine kuliko kikalio cha hukumu cha “Mungu Hakimu wa wote.” (Waebrania 12:23, NW) Sasa yeye atahukumu aina ya binadamu kwa habari ya ni nani atanufaika na dhabihu ya ukombozi ya Yesu.—Marko 10:45.

      3. (a) Ni nini kinachoonyeshwa na uhakika wa kwamba kiti cha ufalme cha Mungu kinasemwa kuwa “kikubwa” na “cheupe”? (b) Ni nani watakuwa wakihukumu kwenye Siku ya Hukumu, na kwa msingi gani?

      3 Kiti cha ufalme cha Mungu ni “kikubwa,” kikikazia ukuu wa Yehova akiwa Bwana Mwenye Enzi Kuu, na ni “cheupe,” kuvuta uangalifu kwenye uadilifu wake usio na kasoro. Yeye ndiye Hakimu wa mwisho kabisa wa aina ya binadamu. (Zaburi 19:7-11; Isaya 33:22; 51:5, 8) Hata hivyo, yeye amempa Yesu Kristo wakala wa kufanya kazi ya kuhukumu: “Baba hahukumu yeyote kabisa, bali yeye ameaminisha Mwana kuhukumu kote.” (Yohana 5:22, NW) Pamoja na Yesu ni washirika wake 144,000, ambao “nguvu za kuhukumu zilipewa kwao . . . kwa miaka elfu moja.” (Ufunuo 20:4, NW) Hata hivyo, viwango vya Yehova ndivyo vinaamua kitakachompata kila mtu mmoja mmoja wakati wa Siku ya Hukumu.

      4. Maana yake nini kwamba “dunia na mbingu zikakimbilia mbali”?

      4 Ni jinsi gani “dunia na mbingu zikakimbilia mbali”? Hii ni mbingu ile ile ambayo iliondoka kama hati-kunjo wakati wa kufunguliwa kifungo cha sita—serikali za kibinadamu zenye kutawala ambazo “zimewekwa akiba kwa ajili ya moto na zinawekwa kwa ajili ya siku ya hukumu na ya kuharibiwa kwa watu wasiohofu Mungu.” (Ufunuo 6:14; 2 Petro 3:7, NW) Dunia ni mfumo wa mambo uliopangwa kitengenezo ulio chini ya utawala huu. (Ufunuo 8:7) Uharibifu wa hayawani-mwitu na wafalme wa dunia na majeshi yao, pamoja na wale waliopokea alama ya hayawani-mwitu na wale waliotoa ibada kwa mfano wake, hutia alama ya kukimbilia mbali kwa hii mbingu na dunia. (Ufunuo 19:19-21) Hukumu ikiwa imetekelezwa juu ya dunia na mbingu za Shetani, Hakimu Mkuu aamuru kuwe na Siku ya Hukumu nyingine.

      Siku ya Hukumu ya Miaka Elfu

      5. Baada ya dunia ya kale na mbingu ya kale kukimbilia mbali, ni nani wanaobaki kuhukumiwa?

      5 Ni nani wanaobaki wahukumiwe baada ya dunia ya kale na mbingu ya kale kukimbilia mbali? Si mabaki wapakwa-mafuta wa 144,000, kwa maana hawa wamekwisha hukumiwa na kutiwa muhuri. Ikiwa wapakwa-mafuta wowote bado watakuwa duniani baada ya Har–Magedoni, lazima wafe muda mfupi baada ya hapo na kupokea thawabu yao ya kimbingu kwa ufufuo. (1 Petro 4:17; Ufunuo 7:2-4) Hata hivyo, mamilioni ya umati mkubwa ambayo sasa yametoka katika dhiki kubwa yanasimama kwa wazi “mbele ya kiti cha ufalme.” Hawa wamekwisha kuhesabiwa kuwa waadilifu kwa ajili ya kuokolewa kwa sababu ya imani yao katika damu iliyomwagwa ya Yesu, lakini hukumu yao lazima iendelee kupitia muda wote wa miaka elfu kadiri Yesu aendeleavyo kuwaongoza kwenye “vibubujiko vya maji ya uhai.” Kisha, wakiwa wamekwisha rudishwa kwenye ukamilifu wa kibinadamu na baada ya hapo kutahiniwa, wao watajulishwa wazi kuwa waadilifu katika maana iliyo kamili zaidi sana. (Ufunuo 7:9, 10, 14, 17, NW) Watoto ambao huenda wakaokoka dhiki kubwa na watoto wowote wanaozaliwa kwa umati mkubwa wakati wa Mileani hali kadhalika watahitaji kuhukumiwa wakati wa miaka elfu.—Linga Mwanzo 1:28; 9:7; 1 Wakorintho 7:14.

      6. (a) Ni msongamano gani anaoona Yohana, na ni nini linaloonyeshwa na maneno “wakubwa na wadogo”? (b) Mamilioni yasiyohesabika yaliyo katika kumbukumbu la Mungu pasipo shaka yatatokezwaje?

      6 Hata hivyo, Yohana aona msongamano mwingine wenye hesabu kubwa zaidi sana kuliko umati mkubwa wenye kuokoka. Utakuwa na hesabu yenye kufika maelfu ya mamiloni! “Na mimi nikaona wafu, wakubwa na wadogo, wakisimama mbele ya kiti cha ufalme na hati-kunjo zilifunguliwa.” (Ufunuo 20:12a, NW) “Wakubwa na wadogo” hutia ndani walio mashuhuri pamoja na wasio mashuhuri sana wa wanadamu ambao wameishi na wakafa kwenye dunia hii wakati wa miaka 6,000 iliyopita. Katika Gospeli ambayo Yohana aliandika muda mfupi baada ya Ufunuo, Yesu alisema kwa habari ya Baba yake: “Naye akampa [Yesu] amri ya kufanya hukumu kwa sababu ni Mwana wa Adamu. Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake. Nao watatoka.” (Yohana 5:27-29) Ni mradi mkubwa ajabu kama nini—kutangua vifo na makaburi ya muda wote wa historia! Hapana shaka hayo mamilioni yasiyohesabika yaliyo katika kumbukumbu la Mungu watatokezwa hatua kwa hatua hivi kwamba umati mkubwa—ambao ni wachache sana kwa kulinganisha—utaweza kushughulikia matatizo ambayo huenda yatazuka kwa sababu huenda mwanzoni wafufuliwa wakaelekea kufuata mtindo wao wa maisha ya kale, pamoja na udhaifu wa mnofu wao na mielekeo.

      Nani Wanainuliwa na Kuhukumiwa?

      7, 8. (a) Ni hati-kunjo gani inayofunguliwa, na ni jambo gani linalotukia baada ya hapo? (b) Ni kwa akina nani hakutakuwa na ufufuo?

      7 Yohana anaongeza: “Lakini hati-kunjo nyingine ikafunguliwa; ndiyo hati-kunjo ya uhai. Na wafu walihukumiwa kutoka kwa vile vitu vilivyoandikwa katika hati-kunjo kulingana na matendo yao. Na bahari ikatoa wafu wale walio ndani yayo na kifo na Hadesi vikatoa wafu wale walio ndani yavyo na wao walihukumiwa mmoja mmoja kulingana na matendo yao.” (Ufunuo 20:12b, 13, NW) Tamasha yenye kusisimua kweli kweli! ‘Bahari, kifo, na Hadesi’ kila mojapo inatimiza sehemu, lakini angalia kwamba semi hizi si za pekee baina yazo zenyewe.a Wakati Yona alipokuwa tumboni mwa samaki mmoja na kwa hiyo akawa katikati ya bahari, yeye alisema juu yake mwenyewe kuwa alikuwa katika Sheoli, au Hadesi. (Yona 2:2) Ikiwa mtu anashikwa na kifo cha Adamu, basi yaelekea yeye pia yumo katika Hadesi. Maneno haya ya kiunabii yanatoa uhakikisho imara kwamba hakuna hata mmoja atakayekosa kuonwa.

      8 Bila shaka, kuna hesabu isiyojulikana ambayo haitafufuliwa. Miongoni mwa hawa wangekuwa waandishi na Mafarisayo waliomkataa Yesu na mitume, “mtu wa uasi-sheria” wa kidini, na Wakristo wapakwa-mafuta “ambao wameangukia mbali.” (2 Wathesalonike 2:3; Waebrania 6:4-6; Mathayo 23:29-33, NW) Yesu alisema pia juu ya watu walio kama mbuzi wakati wa mwisho wa huu ulimwengu ambao huenda ndani ya “moto wa milele uliotayarishwa kwa ajili ya Ibilisi na malaika zake,” yaani, “kukatiliwa mbali milele.” (Mathayo 25:41, 46, NW) Hakuna ufufuo kwa hao!

      9. Mtume Paulo anaonyeshaje kwamba baadhi yao watapendelewa kipekee katika ufufuo, na hao wanatia ndani akina nani?

      9 Kwa upande mwingine, baadhi yao watapendelewa kipekee katika ufufuo huu. Mtume Paulo alionyesha hivyo wakati aliposema: “Mimi nina tumaini kuelekea Mungu . . . kwamba kutakuja kuwa na ufufuo wa wote walio waadilifu na wasio waadilifu.” (Matendo 24:15, NW) Kwa habari ya ufufuo wa kidunia, “walio waadilifu” watatia ndani wanaume na wanawake waaminifu wa kale—Abrahamu, Rahabu, na wengine wengi—ambao walijulishwa wazi kuwa waadilifu kwa habari ya kuwa na urafiki na Mungu. (Yakobo 2:21, 23, 25) Katika kikundi iki hiki watakuwamo wale kondoo wengine waadilifu ambao walikufa wakiwa waaminifu kwa Yehova katika nyakati za ki-siku-hizi. Yaelekea, washika ukamilifu wote hao watafufuliwa mapema katika Utawala wa Mileani wa Yesu. (Ayubu 14:13-15; 27:5; Danieli 12:13; Waebrania 11:35, 39, 40) Pasi na shaka wengi wa hawa waadilifu waliofufuliwa watapewa migawo ya pendeleo la pekee katika kusimamia kazi kubwa mno ya urudisho katika Paradiso.—Zaburi 45:16; linga Isaya 32:1, 16-18; 61:5; 65:21-23.

      10. Kati ya wale watakaofufuliwa, ni nani “wasio waadilifu”?

      10 Ingawa hivyo, ni nani “wasio waadilifu” wanaotajwa katika Matendo 24:15, NW? Hawa wangetia ndani matungamo ya aina ya binadamu ambayo yamekufa muda wote wa historia, hasa wale ambao waliishi katika ‘nyakati za ujinga.’ (Matendo 17:30) Hawa, kwa sababu ya mahali walipozaliwa au wakati walimoishi, hawakuwa na fursa ya kujifunza kutii penzi la Yehova. Kwa kuongezea, huenda kukawa na baadhi ya waliosikia ujumbe wa wokovu lakini ambao hawakuitikia kikamili katika wakati huo au ambao walikufa kabla ya wao kuendelea kufikia wakfu na ubatizo. Katika ufufuo watu kama hao watahitaji kufanya marekebisho zaidi katika kufikiri na mwendo wao wa maisha ikiwa wao watanufaika na fursa hii kwa ajili ya kupata uhai wa milele.

      Hati-Kunjo ya Uhai

      11. (a) “Hati-kunjo ya uhai” ni nini, na ni majina ya nani yaliyorekodiwa katika hati-kunjo hii? (b) Ni kwa nini hati-kunjo ya uhai itafunguliwa wakati wa Utawala wa Miaka Elfu?

      11 Yohana husema juu ya “hati-kunjo ya uhai.” Hayo ni maandishi ya wale walio katika mstari wa kupokea uhai wa milele kutoka kwa Yehova. Majina ya ndugu wapakwa-mafuta wa Yesu, ya umati mkubwa, na ya watu waaminifu wa kale, kama vile Musa, yameandikwa katika hati-kunjo hii. (Kutoka 32:32, 33; Danieli 12:1; Ufunuo 3:5, NW) Bado kufikia hapa, hakuna hata mmoja wa wale “wasio waadilifu” waliofufuliwa aliye na jina lake limeandikwa katika hati-kunjo ya uhai. Kwa hiyo hati-kunjo ya uhai itafunguliwa wakati wa Utawala wa Miaka Elfu kuruhusu kuandikwa kwa majina ya wengine ambao wanakuja kustahili. Wale ambao majina yao hayapati kuandikwa katika hati-kunjo au kitabu, ya uhai ‘wanavurumishwa ndani ya ziwa la moto.’—Ufunuo 20:15, NW; linga Waebrania 3:19.

      12. Ni nini kitakachoamua kama mtu ataandikisha jina lake katika hati-kunjo ya uhai iliyofunguliwa, na Hakimu mwekwa wa Yehova aliwekaje kielelezo?

      12 Basi, ni nini kitakachoamua kama mtu anapata kuandikisha jina lake katika hati-kunjo ya uhai iliyofunguliwa wakati huo? Sababisho kuu litakuwa lile lile kama lilivyokuwa katika siku ya Adamu na Hawa: utii kwa Yehova. Kama vile mtume Yohana alivyoandikia Wakristo wenzake wapendwa: “Ulimwengu unapitilia mbali na ndivyo na tamaa yao, lakini yeye ambaye hufanya mapenzi ya Mungu hubaki milele.” (1 Yohana 2:4-7, 17, NW) Kwa habari ya utii, Hakimu mwekwa wa Yehova aliweka kielelezo: “Ingawa [Yesu] alikuwa Mwana, yeye alijifunza kutii kutokana na vitu ambavyo yeye aliteseka; na baada ya yeye kuwa amefanywa mkamilifu, yeye alipata kuwa mwenye daraka la wokovu wa milele kwa wale wote wanaotii yeye.”—Waebrania 5:8, 9, NW.

      Kufungua Hati-Kunjo Nyingine

      13. Ni lazima wafufuliwa waonyesheje utii wao, na ni kanuni gani ambazo lazima wafuate?

      13 Ni lazima hawa wafufuliwa waonyesheje utii wao? Yesu mwenyewe alielekeza kwenye amri mbili kubwa, akisema: “Ya kwanza ni, ‘Sikia O Israeli, Yehova Mungu wetu ni Yehova mmoja, na wewe lazima upende Yehova Mungu wako kwa moyo mzima wote na kwa nafsi nzima yote na kwa akili nzima zote na kwa uthabiti mzima wote.’ Ya pili ni hii, ‘Lazima wewe upende jirani yako kama wewe mwenyewe.’” (Marko 12:29-31, NW) Pia kuna kanuni za Yehova zilizoimarishwa vizuri ambazo lazima wafuate, kama vile kukataa katakata kuiba, kusema uwongo, kuua kimakusudi, na utovu wa adili.—1 Timotheo 1:8-11; Ufunuo 21:8.

      14. Ni hati-kunjo gani nyingine zinazofunguliwa, na ni mambo gani yaliyomo?

      14 Hata hivyo, ndipo Yohana ametoka tu kutaja hati-kunjo nyingine ambazo zitafunguliwa wakati wa Utawala wa Mileani. (Ufunuo 20:12) Hizi zitakuwa nini? Nyakati fulani, Yehova ametoa maagizo yaliyo waziwazi katika hali maalumu. Mathalani, katika siku ya Musa yeye aliandaa mfululizo wa sheria zenye mambo mengi-mengi ambazo zilimaanisha uhai kwa Waisraeli ikiwa wangetii. (Kumbukumbu 4:40; 32:45-47) Wakati wa karne ya kwanza, maagizo mapya yalitolewa kusaidia waaminifu kufuata kanuni za Yehova chini ya mfumo wa mambo wa Kikristo. (Mathayo 28:19, 20; Yohana 13:34; 15:9, 10) Sasa Yohana anaripoti kwamba wafu ‘watahukumiwa kutoka kwa vile vitu vilivyoandikwa katika hati-kunjo kulingana na matendo yao.’ Kwa wazi, basi, kufunguliwa kwa hati-kunjo hizi kutatangaza matakwa ya Yehova yenye mambo mengi-mengi kwa ajili ya aina ya binadamu wakati wa miaka elfu. Kwa kutumia katika maisha yao virekebi na amri za hati-kunjo hizo, wanadamu watiifu wataweza kurefusha siku zao, wakifikia mwishowe uhai wa milele.

      15. Ni kampeni ya kielimu ya aina gani itakayohitajiwa wakati wa ufufuo, na yaelekea ufufuo utaendeleaje?

      15 Ni kampeni iliyopanuka kama nini ya elimu ya kitheokrasi itakayohitajiwa! Katika 2005 Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote walikuwa wakiongoza, kwa wastani, mafunzo ya Biblia 6,061,534 katika mahali pa namna namna. Lakini wakati wa ufufuo, mamilioni yasiyohesabika ya mafunzo, msingi wayo ukiwa Biblia na hati-kunjo mpya, yataongozwa bila shaka! Watu wote wa Mungu watahitaji kuwa walimu na kujitahidi wenyewe. Wafufuliwa, kadiri waendeleavyo, pasipo shaka watashiriki programu hii iliyo kubwa mno ya kufundisha. Yaelekea, ufufuo utaendelea katika njia ya kwamba wale walio hai watapata kuwa na shangwe ya kukaribisha na kufundisha washiriki wa jamaa wa zamani na watu waliojuana nao, ambao, nao kwa zamu yao, watapata kukaribisha na kufundisha wengine. (Linga 1 Wakorintho 15:19-28, 58.) Wale Mashahidi wa Yehova zaidi ya milioni sita ambao ni watendaji katika kueneza ukweli leo wanaweka msingi mwema kwa ajili ya mapendeleo wanayotumainia kupata katika wakati wa ufufuo.—Isaya 50:4; 54:13.

      16. (a) Ni majina ya nani ambayo hayataandikwa katika hati-kunjo, au kitabu, ya uhai? (b) Ni nani wale ambao ufufuo wao utathibitika kuwa “wa uhai”?

      16 Kwa habari ya ufufuo wa kidunia, Yesu alisema kwamba ‘wale waliofanya mema hutoka na kuja kwenye ufufuo wa uhai, wale waliozoea vitu vibaya sana kwenye ufufuo wa hukumu.’ Hapa “uhai” na “hukumu” hutofautiana, kuonyesha kwamba wale wafufuliwa ambao ‘huzoea vitu vibaya sana’ baada ya kufundishwa katika Maandiko na hati-kunjo zilizovuviwa huhukumiwa kuwa hawastahili uhai. Majina yao hayataandikwa katika hati-kunjo au kitabu, ya uhai. (Yohana 5:29, NW) Inaweza kuwa hivyo pia kwa wowote ambao hapo kwanza walifuata mwendo wa uaminifu lakini ambao, kwa sababu fulani, wanakengeuka katika wakati wa Utawala wa Miaka Elfu. Majina yanaweza kufutwa. (Kutoka 32:32, 33) Kwa upande mwingine, wale ambao kwa kutii hufuata vitu vilivyoandikwa katika hati-kunjo watatunza majina yao katika rekodi iliyoandikwa, hati-kunjo ya uhai, na kuendelea kuishi. Kwa wao, ufufuo utakuwa umethibitika kuwa “wa uhai.”

      Mwisho wa Kifo na Hadesi

      17. (a) Ni tendo gani zuri ajabu ambalo Yohana anaeleza? (b) Hadesi inaachwa tupu lini? (c) Kifo cha Adamu ‘kitavurumishwa ndani ya ziwa la moto lini’?

      17 Kisha, Yohana anaeleza jambo fulani ambalo kweli ni zuri ajabu! “Na kifo na Hadesi vilivurumishwa ndani ya ziwa la moto. Hii humaanisha kifo cha pili, ziwa la moto. Zaidi ya hayo, yeyote ambaye hakupatikana ameandikwa katika kitabu cha uhai alivurumishwa ndani ya ziwa la moto.” (Ufunuo 20:14, 15, NW) Kufikia mwisho wa Siku ya Hukumu ya mileani, “kifo na Hadesi” vinaondolewa kabisa. Ni kwa nini hili lahusisha miaka elfu moja? Hadesi, ambalo ni kaburi la ujumla la aina ya binadamu, inaachwa ikiwa tupu wakati mtu wa mwisho aliye katika kumbukumbu la Mungu anapofufuliwa. Lakini maadamu binadamu wowote wanatiwa waa na dhambi iliyorithiwa, kifo cha Adamu kingali kipo pamoja nao. Wale wote wanaofufuliwa duniani, pamoja na umati mkubwa unaookoka Har–Magedoni, watahitaji kutii yaliyoandikwa katika hati-kunjo mpaka ubora wa dhabihu ya Yesu uwe umetumiwa kikamili ukiondoa magonjwa, uzee, na udhaifu mwingine uliorithiwa. Ndipo kifo cha Adamu, pamoja na Hadesi, ‘vinapovurumishwa ndani ya ziwa la moto.’ Vitakuwa vimeenda milele!

      18. (a) Mtume Paulo anaelezaje habari ya fanikio la utawala wa Yesu akiwa Mfalme? (b) Yesu hufanya nini na jamaa ya kibinadamu kamilifu? (c) Kunatukia vitu gani vingine mwishoni mwa miaka elfu?

      18 Hivyo, programu ambayo mtume Paulo anaeleza katika barua yake kwa Wakorintho itafikia ukamilisho: “Kwa maana lazima [Yesu] atawale akiwa mfalme mpaka Mungu ameweka maadui wote chini ya nyayo zake. Akiwa ndiye adui wa mwisho, kifo [cha Adamu] kitaletwa kwenye si kitu.” Kwafuata nini? “Wakati vitu vyote vitakuwa vimetiishwa kwake, ndipo Mwana mwenyewe pia atajitiisha mwenyewe kwa Mmoja ambaye alitiisha vitu vyote kwake.” Kwa maneno mengine, Yesu ‘amkabidhi ufalme Mungu na Baba yake.’ (1 Wakorintho 15:24-28, NW) Ndiyo, Yesu, akiwa amekwisha shinda kifo cha Adamu kupitia ubora wa dhabihu ya ukombozi wake, atakabidhi Baba yake, Yehova, jamaa ya kibinadamu kamilifu. Kwa wazi ni hapa mwishoni mwa miaka elfu, ndipo Shetani anaachiliwa na mtihani wa mwisho kabisa unafanyika kuamua ni majina ya nani yatabaki daima yamerekodiwa katika hati-kunjo ya uhai. “Jitahidini wenyewe kisulubu” ili jina lenu liwe miongoni mwayo!—Luka 13:24; Ufunuo 20:5, NW.

      [Maelezo ya Chini]

      a Wale wanaofufuliwa kutoka katika bahari hawangetia ndani wakazi wafisadi wa dunia walioangamia katika Gharika ya siku ya Noa; uharibifu huo ulikuwa wa kukata maneno, kama utakavyokuwa utekelezo wa hukumu ya Yehova katika dhiki kubwa.—Mathayo 25:41, 46; 2 Petro 3:5-7.

      [Picha katika ukurasa wa 298]

      Wafufuliwa “wasio waadilifu” ambao hutii hati-kunjo zinazofunguliwa wakati wa Utawala wa Miaka Elfu huenda wakaandikisha pia majina yao katika ile hati-kunjo ya uhai

  • Mbingu Mpya na Dunia Mpya
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Sura ya 42

      Mbingu Mpya na Dunia Mpya

      1. Yohana anaeleza nini wakati malaika anapomrudisha kwenye mwanzo wa Utawala wa Miaka Elfu?

      NJOZI hii tukufu inaendelea kukunjuka malaika anaporudisha Yohana kwenye mwanzo wa Utawala wa Miaka Elfu. Yeye anaeleza habari gani? “Na mimi nikaona mbingu mpya na dunia mpya; kwa kuwa mbingu ya kwanza na dunia ya kwanza zilikuwa zimepitilia mbali, na bahari haipo tena.” (Ufunuo 21:1, NW) Mandhari yenye kuvutia yaonekana!

      2. (a) Unabii wa Isaya juu ya mbingu mpya na dunia mpya ulitimizwaje juu ya Wayahudi waliorudishwa katika 537 K.W.K.? (b) Twajuaje kwamba kutakuwa na utimizo zaidi wa unabii wa Isaya, na ahadi hii inatimizwaje?

      2 Mamia ya miaka kabla ya siku ya Yohana, Yehova alikuwa amesema kwa Isaya: “Kwa maana hapa mimi naumba mbingu mpya na dunia mpya; na vitu vya kwanza havitarudishwa kwenye akili, wala havitakuja juu kuingia ndani ya moyo.” (Isaya 65:17; 66:22, NW) Unabii huu ulitimizwa kwanza wakati Wayahudi waaminifu waliporudi Yerusalemu katika 537 K.W.K. baada ya uhamisho wao wa miaka 70 katika Babuloni. Katika urudisho huo, wao walifanyiza jamii iliyosafishwa, “dunia mpya,” chini ya mfumo mpya wa kiserikali, “mbingu mpya.” Hata hivyo, mtume Petro alielekeza kwenye utimizo zaidi wa unabii huo, akisema: “Lakini kuna mbingu mpya na dunia mpya ambazo sisi tunangojea kulingana na ahadi yake, na katika hizi uadilifu wapasa kukaa.” (2 Petro 3:13, NW) Yohana sasa anaonyesha kwamba ahadi hii inatimizwa wakati wa siku ya Bwana. “Mbingu ya kwanza na dunia ya kwanza,” mfumo wa mambo uliopangwa kitengenezo wa Shetani ukiwa na muundo wao wa kiserikali wenye kuongozwa na Shetani na roho waovu wake, utapitilia mbali. “Bahari” yenye msukosuko ya aina ya binadamu yenye uovu, yenye kuasi itakoma kuwako. Mahali pazo patachukuliwa na “mbingu mpya na dunia mpya”—jamii mpya ya kidunia chini ya serikali mpya, Ufalme wa Mungu.—Linga Ufunuo 20:11.

      3. (a) Yohana anaeleza habari ya nini, na Yerusalemu Jipya ni nini? (b) Yerusalemu Jipya ‘hujaje chini kutoka katika mbingu’?

      3 Yohana anaendelea: “Mimi nikaona pia jiji takatifu, Yerusalemu Jipya, likija chini kutoka katika mbingu kutoka kwa Mungu na limetayarishwa kama bibi-arusi aliyerembwa kwa ajili ya mume wake.” (Ufunuo 21:2, NW) Yerusalemu jipya ni bibi-arusi wa Kristo, ambaye walio washiriki wake ni Wakristo wapakwa-mafuta ambao hubaki wakiwa waaminifu mpaka kifo na ambao huinuliwa wakawe wafalme na makuhani pamoja na Yesu aliyetukuzwa. (Ufunuo 3:12; 20:6) Kama vile Yerusalemu la kidunia lilivyopata kuwa kao la serikali katika Israeli wa kale, Yerusalemu Jipya lenye uzuri mwingi mno na Bwana-arusi wake huwa ndiyo serikali ya mfumo mpya wa mambo. Hii ndiyo mbingu mpya. ‘Bibi-arusi huja chini kutoka katika mbingu,’ si kihalisi, bali katika maana ya kuelekeza uangalifu kwenye dunia. Bibi-arusi wa Mwana-Kondoo atakuwa mwenzi-msaidizi wake wa kifalme katika kuendesha serikali yenye uadilifu juu ya aina ya binadamu yote. Baraka kweli kweli kwa dunia mpya!

      4. Ni ahadi gani anayofanya Mungu inayofanana na ile aliyofanya kwa taifa jipya lililofanyizwa?

      4 Yohana atuambia zaidi: “Pamoja na hayo mimi nilisikia sauti kubwa kutoka katika kiti cha ufalme ikisema: ‘Tazama! Hema ya Mungu i pamoja na aina ya binadamu, na yeye atakaa pamoja na wao, na wao watakuwa vikundi vya watu wake. Na Mungu mwenyewe atakuwa pamoja na wao.’” (Ufunuo 20:3, NW) Yehova alipofanya agano la Sheria pamoja na taifa la Israeli ambalo wakati huo lilikuwa jipya, yeye aliahidi: “Kwa hakika mimi nitaweka tabenakulo yangu katikati yenu nyinyi, na nafsi yangu haitakirihi nyinyi. Na mimi nitatembea kweli kweli katikati ya nyinyi na kujithibitisha mwenyewe kuwa Mungu wenu, na nyinyi, kwa upande wenu, mtajithibitisha wenyewe kuwa watu wangu.” (Walawi 26:11, 12, NW) Yehova anafanya sasa ahadi inayofanana na hiyo kwa wanadamu waaminifu. Wakati wa Siku ya Hukumu ya miaka elfu, wao watakuwa watu maalumu sana kwake.

      5. (a) Mungu atakaaje na aina ya binadamu wakati wa Utawala wa Mileani? (b) Mungu atakaaje miongoni mwa aina ya binadamu baada ya Utawala wa Miaka Elfu?

      5 Wakati wa Utawala wa Mileani, Yehova ‘atakaa’ miongoni mwa aina ya binadamu katika mpango wa muda, yeye akiwakilishwa na Mwana wake wa kifalme, Yesu Kristo. Hata hivyo, mwishoni mwa Utawala wa Miaka Elfu, wakati Yesu anapomkabidhi Baba yake Ufalme, hakutahitajika mwakilishi au mwombezi wa kifalme. Yehova atakaa kiroho pamoja na “vikundi vya watu wake” katika njia ya kudumu na ya moja kwa moja. (Linga Yohana 4:23, 24.) Ni pendeleo la hali ya juu kama nini kwa ubinadamu uliorudishwa!

      6, 7. (a) Ni ahadi zipi tukufu anazofumbua Yohana, na ni akina nani watakaofurahia baraka hizo? (b) Isaya anaelezaje habari ya paradiso ambayo ni ya kiroho na kimwili pia?

      6 Yohana aendelea kusema: “Na yeye atapangusa kabisa kila chozi kutoka macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala hakutakuwapo kuomboleza wala kuguta wala umivu tena. Vitu vya kwanza vimepitilia mbali.” (Ufunuo 21:4, NW) Kwa mara nyingine tena, tunakumbushwa juu ya ahadi zilizovuviwa za mapema zaidi. Isaya alitazamia pia wakati ambapo kifo na kuomboleza vingekuwa havipo tena na mahali pa kihoro pangechukuliwa na mchachawo. (Isaya 25:8, 35:10; 51:11; 65:19) Yohana anathibitisha sasa kwamba ahadi hizi zina utimizo mzuri ajabu wakati wa Siku ya Hukumu ya miaka elfu. Kwanza umati mkubwa utajifurahisha baraka. “Mwana-Kondoo, aliye katikati ya kiti cha ufalme,” akiendelea kuwachunga, “ataelekeza wao kwenye vibubujiko vya maji ya uhai. Na Mungu atapangusa kabisa kila chozi kutoka macho yao.” (Ufunuo 7:9, 17, NW) Lakini hatimaye wale wote ambao wamefufuliwa na kujizoeza imani katika mpango wa Yehova watakuwako pamoja nao, wakijifurahisha paradiso ambayo ni ya kiroho na kimwili pia.

      7 “Ndipo,” asema Isaya, “macho ya vipofu yatafumbuliwa, na masikio ya viziwi yatazibuliwa.” Naam, “ndipo mtu aliye kilema ataruka-ruka kama kulungu, na ulimi wake aliye bubu utaimba” kwa nderemo. (Isaya 35:5, 6) Wakati huo, pia, “watajenga nyumba, na kukaa ndani yake; watapanda mizabibu, na kula matunda yake. Hawatajenga, akakaa mtu mwingine ndani yake; hawatapanda, akala mtu mwingine; maana kama siku za mti ndivyo zitakavyokuwa siku za watu wangu, na wateule wangu wataifurahia kazi ya mikono yao muda wa siku nyingi.” (Isaya 65:21, 22) Kwa hiyo hawatang’olewa mizizi kutoka dunia.

      8. Yehova mwenyewe anasema nini kwa habari ya kutegemeka kwa ahadi hizi tukufu?

      8 Ni maono ya kimbele yaliyo mazuri kama nini yanayojaa akili zetu tutafakaripo juu ya ahadi hizi! Maandalizi mazuri ajabu yako akibani kwa ajili ya aina ya binadamu yenye uaminifu chini ya serikali yenye upendo ya kimbingu. Je! ahadi hizi ni nzuri mno zisiweze kuwa za kweli? Je! ni ndoto tu za mzee aliyehamishwa kwenye kisiwa cha Patmosi? Yehova mwenyewe anajibu: “Na Mmoja aketiye juu ya kiti cha ufalme akasema: ‘Tazama! Mimi ninafanya vitu vyote kuwa vipya.’ Pia, yeye asema: ‘Andika, kwa sababu maneno haya ni ya uaminifu na ya kweli.’ Na yeye akasema kwa mimi: ‘Yamekwisha tukia! Mimi ndiye Alfa na Omega, mwanzo na mwisho.’”—Ufunuo 21:5, 6a, NW.

      9. Ni kwa nini baraka hizi za wakati ujao zinaweza kuonwa kuwa ni hakika kabisa zitatimizwa?

      9 Ni kana kwamba Yehova mwenyewe alikuwa akitia saini ya dhamana au taitodidi kwenye baraka hizi za wakati ujao kwa ajili ya aina ya binadamu yenye uaminifu. Ni nani anayeweza kuthubutu kushuku Mdhamini kama huyo? Kwani, ahadi hizi za Yehova ni hakika sana hivi kwamba yeye hunena kama tayari zilitimia: “Yamekwisha tukia!” Je! Yehova siye “Alfa na Omega . . . , Mmoja ambaye yuko na ambaye alikuwako na ambaye anakuja, yule Mweza Yote”? (Ufunuo 1:8, NW) Kweli kweli ndiye! Yeye mwenyewe hujulisha wazi: “Mimi ndiye wa kwanza na mimi ndiye wa mwisho, na mbali na mimi hakuna Mungu.” (Isaya 44:6, NW) Akiwa hivyo, yeye anaweza kuvuvia unabii na kuutimiza katika kila jambo dogo-dogo. Jinsi inavyoimarisha imani! Kwa hiyo yeye aahidi: “Tazama! Mimi ninafanya vitu vyote kuwa vipya”? Badala ya kushuku kama maajabu haya yatatukia kweli kweli, hakika ingetupasa tuwe tukitaka kujua: ‘Mimi binafsi inanipasa kufanya nini ili kurithi baraka hizo?’

      “Maji” kwa Wenye Kiu

      10. Ni “maji” gani ambayo Yehova anatoa, nayo yanasimamia nini?

      10 Yehova mwenyewe ndiye anayejulisha wazi: “Yeyote anayeona kiu mimi nitampa kutoka kibubujiko cha maji ya uhai bure.” (Ufunuo 21:6b, NW) Ili kuzima kiu hicho, lazima mtu awe anaona uhitaji wake wa kiroho na awe na nia ya kukubali “maji” ambayo Yehova huandaa. (Isaya 55:1; Mathayo 5:3) “Maji” yapi? Yesu mwenyewe alijibu swali hilo alipokuwa akitoa ushahidi kwa mwanamke kando ya kisima katika Samaria. Yeye alimwambia: “Yeyote ambaye hunywa kutoka maji ambayo mimi nitampa yeye hataona kiu kamwe hata, lakini maji ambayo mimi nitampa yeye yatakuwa ndani ya yeye kibubujiko cha maji kikibubujika kupatia uhai wa milele.” Hicho “kibubujiko cha maji ya uhai” hutiririka kutoka kwa Mungu kupitia Kristo akiwa andalio lake kwa ajili ya kurudisha aina ya binadamu kwenye uhai mkamilifu. Kama mwanamke Msamaria, yatupasa sisi kuwa wenye hamu nyingi kama nini kunywa sana kutokana na kibubujiko hicho! Na kama mwanamke huyo, yatupasa kuwa tayari kama nini kuacha mapendezi ya kidunia na kupendelea kuwaambia wengine habari njema!—Yohana 4:14, 15, 28, 29, NW.

      Wale Wanaoshinda

      11. Ni ahadi gani ambayo Yehova anafanya, na maneno hayo yanatumika kwa nani kwanza?

      11 Wale wanaokunywa ya hayo “maji” yenye kuburudisha lazima pia washinde, kama Yehova aendeleavyo kusema: “Yeyote ambaye anashinda atarithi vitu hivi, na mimi nitakuwa Mungu wake na yeye atakuwa mwana wangu.” (Ufunuo 21:7, NW) Ahadi hii inafanana na ile inayopatikana katika jumbe kwenye makundi saba; kwa sababu hiyo, maneno haya lazima yahusu kwanza wanafunzi wapakwa-mafuta. (Ufunuo 2:7, 11, 17, 26-28; 3:5, 12, 21, NW) Ndugu za kiroho za Kristo katika enzi zote wametazamia kwa hamu nyingi kuwa sehemu ya Yerusalemu Jipya. Wakishinda kama alivyoshinda Yesu, matumaini yao yatatimizwa.—Yohana 16:33.

      12. Ahadi ya Yehova kwenye Ufunuo 21:7 itatimizwaje kuelekea umati mkubwa?

      12 Umati mkubwa kutoka mataifa yote pia watazamia ahadi hii. Lazima wao pia washinde, wakitumikia Mungu kishikamanifu mpaka watoke katika dhiki kubwa. Ndipo wao watakapoingia katika urithi wao wa kidunia, ‘ufalme uliotayarishwa kwa ajili yao tangu kuasisiwa kwa ulimwengu.’ (Mathayo 25:34, NW) Hawa pamoja na wengine wa kondoo wa Bwana wa kidunia ambao hupita mtihani mwishoni mwa miaka elfu huitwa “watakatifu.” (Ufunuo (20:9) Watafurahia uhusiano mtakatifu na wa kibaba na kimwana pamoja na Muumba wao, Yehova Mungu, wakiwa washiriki wa tengenezo lake la ulimwengu wote mzima.—Isaya 66:22; Yohana 20:31; Warumi 8:21.

      13, 14. Ili kurithi ahadi tukufu za Mungu, ni mazoea gani ambayo ni lazima sisi tuepuke kwa dhati, na kwa nini?

      13 Wakiwa na tazamio tukufu hili, ni jambo la maana kama nini kwamba Mashahidi wa Yehova sasa wabaki wakiwa safi bila vitu vyenye kunajisi vya ulimwengu wa Shetani! Sisi twahitaji kuwa imara, wenye dhati, na wenye kuazimia kwamba Ibilisi hatatuburuta kamwe na kutuingiza ndani ya kampuni ambayo Yehova mwenyewe anaeleza hapa? “Lakini kwa habari ya waoga na wale bila imani na wale ambao ni wenye kunyarafisha kwa uchafu wao na wauaji kimakusudi na waasherati na wale ambao huzoea uwasiliano na roho na waabudu sanamu na waongo wote, aria yao itakuwa katika ziwa ambalo huwaka moto na salfa. Hii humaanisha kifo cha pili.” (Ufunuo 21:8, NW) Ndiyo, yeye ambaye angekuwa mrithi lazima aepuke mazoea ambayo yamechafua huu mfumo wa mambo wa kale. Lazima yeye ashinde kwa kubaki akiwa mwaminifu usoni mwa mibano yote na vishawishi.—Warumi 8:35-39.

      14 Jumuiya ya Wakristo, ijapokuwa inadai kuwa bibi-arusi wa Kristo, inatambuliwa kwa mazoea yenye kunyarafisha ambayo Yohana anaeleza hapa. Kwa hiyo inaenda kwenye uharibifu wa milele pamoja na sehemu inayobaki ya Babuloni Mkubwa. (Ufunuo 18:8, 21) Hali kadhalika, wowote wa wapakwa-mafuta au wa umati mkubwa ambao huchukua mazoea kama hayo ya kufanya maovu, au kuanza kutia moyo yafanywe, wakabili uharibifu wa milele. Wakiendelea na matendo haya, hawatarithi ahadi hizi. Na katika dunia mpya, wowote wanaojaribu kuleta mazoea kama hayo wataharibiwa kwa kasi sana, wakiingia ndani ya kifo cha pili bila tumaini la ufufuo.—Isaya 65:20.

      15. Ni nani wenye kutokeza wakiwa washindi, na Ufunuo unaletwa kwenye upeo wa hali ya juu sana kwa njozi gani?

      15 Wenye kutokeza sana wakiwa washindi ni Mwana-Kondoo, Yesu Kristo, na bibi-arusi wake wa 144,000, Yerusalemu Jipya. Inafaa kama nini, basi, kwamba Ufunuo uletwe kwenye upeo wa hali ya juu sana kwa mwono wa mwisho, wa Yerusalemu Jipya wenye kupita ubora wote! Sasa Yohana anaeleza habari ya njozi nyingine moja ya mwisho.

      [Picha katika ukurasa wa 302]

      Katika jamii ya dunia mpya, kutakuwako kazi na ushirika wenye kujaa shangwe kwa wote

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki