Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb16 Septemba uku. 8
  • Epuka Mitego Hii Unapoongoza Funzo la Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Epuka Mitego Hii Unapoongoza Funzo la Biblia
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo (2016)
  • Habari Zinazolingana
  • Kuongoza Funzo la Biblia Nyumbani
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Wasaidie Wanafunzi Wako wa Biblia Wafikie Ubatizo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Fundisha kwa Njia Rahisi
    Wapende Watu—Fanya Wanafunzi
  • Jinsi ya Kufanya Wanafunzi kwa Kutumia Kitabu Ujuzi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo (2016)
mwb16 Septemba uku. 8

MAISHA YA MKRISTO

Epuka Mitego Hii Unapoongoza Funzo la Biblia

Makala Iliyochapishwa
Ndugu anazungumza kupita kiasi anapomfundisha mwanafunzi wake

Kuzungumza Kupita Kiasi: Hupaswi kuhisi kwamba unahitaji kueleza kila kitu. Yesu alitumia maswali kuwasaidia watu wafikiri na kufikia uamuzi unaofaa. (Mt 17:24-27) Maswali yanafanya funzo liwe halisi na kukusaidia kuelewa kile ambacho mwanafunzi wako anaelewa na kuamini. (be 253 ¶3-4) Unapouliza swali, subiri mwanafunzi ajibu. Mwanafunzi anapotoa jibu lisilo sahihi, badala ya kumwambia jibu sahihi, muulize maswali ya ziada ili kumwongoza kwenye jibu sahihi. (be 238 ¶1-2) Zungumza kwa mwendo unaomruhusu mwanafunzi kuelewa mambo mapya.—be 230 ¶4.

Mambo mengi yenye kutatanisha kuhusu kwa nini tunazeeka

Kufanya Habari Iwe Ngumu Kueleweka: Epuka kishawishi cha kueleza habari zote unazojua kuhusu habari unayozungumzia. (Yoh 16:12) Kazia fikira jambo kuu katika fungu. (be 226 ¶4-5) Kumweleza habari nyingi, hata ikiwa zinapendeza, kunaweza kuficha mambo makuu. (be 235 ¶3) Mara tu mwanafunzi anapoelewa jambo kuu, endelea na fungu linalofuata.

Ndugu anazungumzia habari nyingi sana hivi kwamba mwanafunzi anachanganyikiwa

Kuzungumzia Tu Habari: Lengo letu si kumaliza habari fulani, bali ni kufikia moyo wa mwanafunzi. (Lu 24:32) Ili mwanafunzi afaidike kutokana na nguvu za Neno la Mungu, kazia maandiko ya msingi katika somo. (2Ko 10:4; Ebr 4:12; be 144 ¶1-3) Tumia mifano rahisi. (be 245 ¶2-4) Fikiria matatizo ambayo mwanafunzi anakabili na mambo anayoamini, kisha ufanye somo hilo limfae. Uliza maswali kama vile: “Unahisije kuhusiana na yale unayojifunza sasa?” “Jambo hili linatufundisha nini kumhusu Yehova?” “Unafikiri tutapata faida gani kwa kutumia ushauri huu?”—be 238 ¶3-5; 259 ¶1.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki