Mwanzo
11 Sasa dunia yote iliendelea kuwa na lugha moja na maneno ya namna moja. 2 Mwishowe ikawa kwamba walipokuwa wakisafiri kuelekea mashariki, waligundua nchi tambarare ya bondeni katika nchi ya Shinari,+ nao wakakaa huko. 3 Nao wakaanza kuambiana: “Haya! Na tutengeneze matofali tuyachome.” Basi matofali yakawa mawe yao, lakini lami ikawa saruji yao.+ 4 Ndipo wakasema: “Haya! Na tujijengee jiji na pia mnara na kilele chake kiwe mbinguni,+ na tujifanyie jina maarufu,+ tusije tukatawanyika juu ya uso wote wa dunia.”+
5 Yehova akashuka aone jiji na mnara ambao wanadamu walikuwa wamejenga.+ 6 Halafu Yehova akasema: “Tazama! Wao ni kikundi kimoja cha watu na wote wana lugha moja,+ na hivi ndivyo wanavyoanza kufanya. Basi sasa hakuna chochote wanachowazia akilini mwao kufanya kitakachowashinda kufikia.+ 7 Haya! Na tushuke,+ tuvuruge+ lugha yao huko ili wasiweze kusikilizana lugha.”+ 8 Basi Yehova akawatawanya juu ya uso wote wa dunia kutoka huko,+ nao pole kwa pole wakaacha kulijenga lile jiji.+ 9 Hiyo ndiyo sababu liliitwa jina lake Babeli,+ kwa sababu huko ndiko Yehova alikuwa amevuruga lugha ya dunia yote, na kutoka huko Yehova alikuwa amewatawanya+ juu ya uso wote wa dunia.
10 Hii ndiyo historia ya Shemu.+
Shemu alikuwa na umri wa miaka 100 wakati alipomzaa Arpakshadi+ miaka miwili baada ya gharika. 11 Na baada ya kumzaa Arpakshadi, Shemu akaishi miaka 500. Wakati uleule akazaa wana na mabinti.+
12 Naye Arpakshadi akaishi miaka 35. Ndipo akamzaa Shela.+ 13 Na baada ya kumzaa Shela, Arpakshadi akaishi miaka 403. Wakati uleule akazaa wana na mabinti.
14 Naye Shela akaishi miaka 30. Ndipo akamzaa Eberi.+ 15 Na baada ya kumzaa Eberi, Shela akaishi miaka 403. Wakati uleule akazaa wana na mabinti.
16 Naye Eberi akaishi miaka 34. Ndipo akamzaa Pelegi.+ 17 Na baada ya kumzaa Pelegi, Eberi akaishi miaka 430. Wakati uleule akazaa wana na mabinti.
18 Naye Pelegi akaishi miaka 30. Ndipo akamzaa Reu.+ 19 Na baada ya kumzaa Reu, Pelegi akaishi miaka 209. Wakati uleule akazaa wana na mabinti.
20 Naye Reu akaishi miaka 32. Ndipo akamzaa Serugi.+ 21 Na baada ya kumzaa Serugi, Reu akaishi miaka 207. Wakati uleule akazaa wana na mabinti.
22 Naye Serugi akaishi miaka 30. Ndipo akamzaa Nahori.+ 23 Na baada ya kumzaa Nahori, Serugi akaishi miaka 200. Wakati uleule akazaa wana na mabinti.
24 Naye Nahori akaishi miaka 29. Ndipo akamzaa Tera.+ 25 Na baada ya kumzaa Tera, Nahori akaishi miaka 119. Wakati uleule akazaa wana na mabinti.
26 Naye Tera akaishi miaka 70, kisha akamzaa Abramu,+ Nahori+ na Harani.
27 Na hii ndiyo historia ya Tera.
Tera akamzaa Abramu, Nahori na Harani; naye Harani akamzaa Loti.+ 28 Baadaye Harani akafa akiwa angali na baba yake Tera katika nchi ya kuzaliwa kwake, katika Uru+ la Wakaldayo.+ 29 Nao Abramu na Nahori wakajichukulia wake. Jina la mke wa Abramu lilikuwa Sarai,+ na jina la mke wa Nahori lilikuwa Milka+ binti ya Harani, baba ya Milka na baba ya Iska. 30 Lakini Sarai aliendelea kuwa tasa;+ hakuwa na mtoto.
31 Baada ya hapo Tera akamchukua mwana wake Abramu, na mjukuu wake Loti,+ mwana wa Harani, na binti-mkwe wake Sarai,+ mke wa mwana wake Abramu, nao wakaondoka Uru la Wakaldayo pamoja naye ili kwenda katika nchi ya Kanaani.+ Baadaye wakaja Harani+ na kukaa huko. 32 Na siku za Tera zikawa miaka 205. Ndipo Tera akafa huko Harani.