17 “Roho yangu imevunjwa,+ siku zangu zimezimwa;
Uwanja wa makaburi ni kwa ajili yangu.+
2 Hakika ninafanyiwa mzaha,+
Na jicho langu linakaa katikati ya tabia yao ya uasi.
3 Tafadhali, weka rehani yangu kwako.+
Kuna nani mwingine atakayenisalimu kwa mkono+ kuwa rehani?
4 Kwa maana umefunga moyo wao usiwe na busara.+
Ndiyo sababu huwainui.
5 Huenda akawaambia rafiki wachukue mafungu yao,
Lakini macho ya wanawe yataisha nguvu.+
6 Naye ameniweka kuwa neno la kimethali+ la vikundi vya watu,
Hivi kwamba ninakuwa mtu ambaye uso wake ni wa kutemewa mate.+
7 Na jicho langu linaingia giza kutokana na usumbufu+
Na viungo vyangu vyote ni kama kivuli.
8 Watu wanyoofu wanaangalia kwa mshangao,
Na hata mtu asiye na hatia anachacha kwa sababu ya mwasi-imani.
9 Mwadilifu anaendelea kuishika sana njia yake,+
Na mwenye mikono safi+ anaendelea kuongezeka nguvu.+
10 Hata hivyo, ninyi nyote mnaweza kuanza tena. Haya, tafadhali,
Kwa kuwa sioni yeyote mwenye hekima kati yenu.+
11 Siku zangu zimepita,+ mipango yangu imevunjika,+
Tamaa za moyo wangu.
12 Wanaendelea kuweka usiku badala ya mchana:+
‘Nuru iko karibu kwa sababu ya giza.’
13 Nikiendelea kungojea, Kaburi ndilo nyumba yangu;+
Nitatandika kitanda changu gizani.+
14 Nitalipaazia shimo+ sauti, ‘Wewe ni baba yangu!’
Na kumwambia funza,+ ‘Wewe ni mama yangu na dada yangu!’
15 Kwa hiyo, basi, liko wapi tumaini langu?+
Na tumaini langu—ni nani anayeliona?
16 Watashuka chini kwenye mapingo ya Kaburi,
Wakati ambapo sisi, sote pamoja, tutashuka mavumbini.”+