Ayubu
16 Naye Ayubu akajibu, akasema:
2 “Nimesikia mambo mengi kama hayo.
Ninyi nyote ni wafariji wasumbufu!+
4 Mimi mwenyewe pia naweza kusema kama ninyi mnavyosema.
Laiti nafsi zenu zingekuwa mahali ilipo nafsi yangu,
Je, ningeng’aa kwa maneno juu yenu,+
Na je, ningetikisa kichwa changu juu yenu?+
5 Ningewatia ninyi nguvu kwa maneno ya kinywa changu,+
Na faraja ya midomo yangu mwenyewe ingetuliza—.
6 Nikiongea, maumivu yangu mwenyewe hayatulizwi,+
Nami nikiacha kufanya hivyo, ni nini kinachoondoka kwangu?
8 Pia unanikamata. Ni ushahidi,+
Hivi kwamba kukonda kwangu kunasimama juu yangu. Kunashuhudia usoni pangu.
9 Hasira yake imenirarua vipande-vipande, naye anashikilia uadui+ juu yangu.
Anasaga meno yake juu yangu.+
Adui yangu mwenyewe anayanoa macho yake juu yangu.+
10 Wamefungua vinywa vyao wazi juu yangu,+
Wamenipiga mashavu yangu kwa shutuma,
Wanakusanyika juu yangu wakiwa hesabu kubwa.+
12 Nilikuwa nimestarehe, lakini akanitikisa;+
Akanikamata nyuma ya shingo, akanivunja-vunja,
Naye ananiweka kuwa shabaha kwa ajili yake mwenyewe.
13 Wapiga-mishale+ wake wananizunguka;
Anapasua wazi figo+ zangu wala haoni huruma;
Anaimwaga nyongo yangu chini.
14 Anaendelea kunitoboa kama ukuta kwa kunitia tundu baada ya tundu;
Anakimbia juu yangu kama mtu mwenye nguvu.+
19 Pia sasa, tazama! yeye anayenishuhudia yuko mbinguni,
Na shahidi wangu yuko katika sehemu za juu.+