Ayubu
27 Naye Ayubu akatokeza tena neno lake la kimethali,+ akaendelea kusema:
2 “Kama Mungu anavyoishi,+ ambaye ameiondoa hukumu yangu,+
Na kama Mweza-Yote anavyoishi, ambaye ameitia uchungu nafsi yangu,+
3 Pumzi yangu ikiwa bado ni nzima ndani yangu,
Na roho ya Mungu imo ndani ya mianzi ya pua yangu,+
4 Midomo yangu haitasema ukosefu wa uadilifu
Wala ulimi wangu hautatamka udanganyifu!
5 Ni jambo lisilowaziwa kwangu kwamba niwatangaze ninyi kuwa waadilifu!+
Mpaka nitakapokata pumzi, sitajiondolea utimilifu+ wangu!
6 Nimeishikilia haki yangu, nami sitaiachilia;+
Moyo wangu hautanidhihaki kwa ajili ya yoyote ya siku zangu.+
8 Kwa maana ni nini tumaini la mwasi-imani iwapo anamkatilia mbali,+
Iwapo Mungu anachukua nafsi yake kutoka kwake?+
10 Au, je, atapata furaha tele katika Mweza-Yote?
Je, atamwita Mungu nyakati zote?
13 Hilo ndilo fungu la mtu mwovu kutoka kwa Mungu;+
Na urithi wa waonevu watapokea kutoka kwa Mweza-Yote mwenyewe.
14 Wanawe wakiwa wengi, ni kwa ajili ya upanga;+
Na wazao wake wenyewe hawatakuwa na chakula cha kutosha.
15 Waokokaji wake mwenyewe watazikwa wakati wa tauni yenye kufisha,
Na wajane wao wenyewe hawatalia.+
16 Akirundika fedha kama mavumbi,
Naye akitayarisha mavazi kana kwamba ni udongo,
17 Yeye atatayarisha, lakini mwadilifu ndiye atakayevaa,+
Na yeye asiye na hatia ndiye atakayekuwa na fungu katika ile fedha.
19 Atalala akiwa tajiri, lakini hakuna chochote kitakachokusanywa;
Ameyafungua macho yake, lakini hakutakuwa na chochote.+