26 Naye Ayubu akajibu, akasema:
2 “Lo! Jinsi umekuwa msaada kwa mtu asiye na uwezo!
Lo! Jinsi umeokoa mkono usio na nguvu!+
3 Jinsi umemshauri mtu asiye na hekima,+
Nawe umefanya umati ujue hekima inayotumika!
4 Umemwambia nani maneno,
Na ni pumzi ya nani imetoka kwako?
5 Wale wasiojiweza katika kifo wanaendelea kutetemeka
Chini ya maji na wale wanaokaa ndani yake.+
6 Kaburi liko uchi mbele zake,+
Na mahali pa maangamizi hapana kifuniko.
7 Anaitandaza kaskazini juu ya mahali pasipo na kitu,+
Akiitundika dunia pasipo na kitu;
8 Anafunga maji katika mawingu yake,+
Hivi kwamba wingu kubwa halipasuki chini yayo;
9 Anaufunika uso wa kiti cha ufalme,
Anatandaza juu yake wingu lake.+
10 Amechora mviringo juu ya uso wa maji,+
Mpaka mahali ambapo nuru huishia katika giza.
11 Nguzo za mbingu hutikisika,
Nazo hushangaa kwa sababu ya kemeo lake.
12 Kwa uwezo wake ameichochea bahari,+
Naye kwa uelewaji wake amemvunja vipande-vipande+ yule mshambuliaji.+
13 Kwa upepo wake ameng’arisha mbingu,+
Mkono wake umemchoma yule nyoka anayenyiririka.+
14 Tazama! Hizo ndizo kingo za njia zake,+
Nao ni mnong’ono ulioje wa jambo lililosikiwa juu yake!
Lakini kuhusu mngurumo wake wenye nguvu ni nani anayeweza kuonyesha uelewaji?”+