35 Naye Elihu akaendelea kujibu, akasema:
2 “Je, haya ndiyo umeyaona kuwa haki?
Wewe umesema, ‘Uadilifu wangu unazidi wa Mungu.’+
3 Kwa maana unasema, ‘Ni wa faida gani kwako?+
Ninapata faida gani zaidi kuliko nikitenda dhambi?’+
4 Mimi nitakujibu wewe
Na rafiki zako+ pamoja nawe.
5 Tazama juu mbinguni+ uone,
Na yaangalie mawingu,+ kwamba kwelikweli yako juu kuliko wewe.
6 Kwa kweli ukitenda dhambi, ni nini unachotimiza dhidi yake?+
Na maasi yako kwa kweli yakiongezeka, unamtendea nini?
7 Ikiwa kweli uko upande wa haki, unampa nini,
Au, je, yeye anapokea nini kutoka mkononi mwako?+
8 Uovu wako unaweza kuwa juu ya mwanadamu kama wewe,+
Na uadilifu wako kwa mwana wa mtu wa udongo.+
9 Kwa sababu ya ukandamizaji mwingi wanaendelea kuomba msaada;+
Wanaendelea kulia wapewe msaada kwa sababu ya mkono wa wakuu.+
10 Na ingawa hivyo hakuna yeyote ambaye amesema, ‘Yuko wapi Mungu, Mtengenezaji Mkuu wangu,+
Yeye anayetoa muziki wakati wa usiku?’+
11 Ni Yeye anayetufundisha+ sisi kuliko wanyama wa dunia,+
Naye anatufanya tuwe na hekima kuliko hata viumbe vinavyoruka vya mbinguni.
12 Huko wao huendelea kupaaza kilio, lakini yeye hajibu,+
Kwa sababu ya kiburi+ cha wabaya.
13 Yasiyo ya kweli tu ndiyo Mungu hasikii,+
Na Mweza-Yote mwenyewe hayatazami.+
14 Sembuse basi unaposema kwamba humwoni!+
Kesi iko mbele zake, na kwa hiyo unapaswa umngojee kwa hangaiko.+
15 Na sasa kwa sababu hasira yake haijatoza hesabu,+
Yeye pia hakufuatilia kule kuchukua hatua kwa haraka inayopita kiasi.+
16 Na Ayubu mwenyewe hukifungua wazi kinywa chake bure tu;
Anazidisha maneno matupu pasipo ujuzi.”+