Ayubu
34 Naye Elihu akaendelea kujibu, akasema:
2 “Sikilizeni maneno yangu, enyi wenye hekima;
Nanyi mnaojua, nitegeeni sikio.
4 Acheni tujichagulie hukumu;
Acheni tujue yaliyo mema katikati yetu.
6 Je, mimi nasema uwongo juu ya hukumu yangu mwenyewe?
Jeraha langu kali haliponi ingawa hakuna kosa.’+
10 Kwa hiyo nisikilizeni mimi, ninyi watu walio na moyo wenye kufahamu.+
Hasha, Mungu wa kweli asitende kwa uovu,+
Na Mweza-Yote kutenda isivyo haki!+
11 Kwa maana yeye atamlipa+ mtu wa udongo kulingana na matendo yake,
Na kulingana na pito la mwanadamu yeye ataifanya ije juu yake.
13 Ni nani aliyemgawia dunia,
Na ni nani aliyemwekea nchi yenye kuzaa, hiyo yote?
16 Basi ikiwa una uelewaji, sikiliza mambo haya;
Tega sikio kwa sauti ya maneno yangu.
17 Kwa kweli, je, mtu yeyote anayechukia haki ataongoza,+
Na ikiwa mwenye nguvu ni mwadilifu, je, utamtangaza yeye kuwa mwovu?+
19 Yupo Yeye ambaye hajaonyesha upendeleo kwa wakuu
Wala hakumwonyesha mwenye cheo ufikirio kuliko yule wa hali ya chini,+
Kwa maana wao wote ni kazi ya mikono yake.+
20 Wanakufa ghafula,+ katikati ya usiku;+
Watu huyumba-yumba na kupitilia mbali,
Na wenye nguvu huondolewa pasipo mkono wa mtu.+
23 Kwa maana haweki wakati wowote kwa ajili ya mwanadamu yeyote
Aende kwa Mungu hukumuni.
28 Ili kukifanya kilio cha mtu wa hali ya chini kimfikie;
Na hivyo yeye hukisikia kilio cha watu wanaoteseka.+
29 Yeye mwenyewe anaposababisha utulivu, ni nani, basi, anayeweza kulaumu?
Na anapoficha uso wake,+ ni nani anayeweza kumwona,
Iwe ni kuelekea taifa+ au ni kuelekea mwanadamu, yote yakiwa ni mamoja?
31 Kwa maana, je, yeyote atamwambia Mungu mwenyewe,
‘Mimi nimevumilia, ijapokuwa sitendi kwa ufisadi;+
32 Ijapokuwa sioni lolote, nifundishe wewe mwenyewe;
Ikiwa nimetenda ukosefu wowote wa uadilifu,
Sitautenda tena’?+
33 Je, yeye atalilipia kama unavyopenda kwa sababu unakataa hukumu,
Kwa sababu wewe mwenyewe unachagua, wala si mimi?
Unalolijua vema, liseme.