36 Naye Elihu akaendelea kusema:
2 “Nisubiri kidogo, nami nitakutangazia
Kwamba bado kuna maneno ya kusema kwa ajili ya Mungu.
3 Nitachukua ujuzi wangu kutoka mbali,
Nami nitamhesabia uadilifu Muumba wangu.+
4 Kwa maana maneno yangu kwa kweli si uwongo;
Yeye aliye mkamilifu katika ujuzi+ yuko pamoja nawe.
5 Tazama! Mungu ni mwenye nguvu+ wala hatakataa;
Yeye ana uwezo wa nguvu za moyo;
6 Hatamhifadhi hai mtu yeyote aliye mwovu,+
Lakini atatoa hukumu ya wenye kuteseka.+
7 Hataondoa macho yake juu ya mtu yeyote aliye mwadilifu;+
Hata wafalme juu ya kiti cha ufalme+—
Yeye pia atawaketisha milele, nao watainuliwa.
8 Na ikiwa wamefungwa pingu,+
Wanatekwa kwa kamba za mateso.
9 Ndipo atawaambia kuhusu jinsi wanavyotenda
Na makosa yao, kwa sababu wanajivuna sana.
10 Naye atafungua sikio lao ili lisikie himizo,+
Naye atasema kwamba wageuke waache madhara.+
11 Wakitii na kutumikia,
Watakamilisha siku zao katika mema
Na miaka yao katika uzuri.+
12 Lakini wasipotii, watamalizwa+ kwa silaha,+
Nao watakata pumzi bila ujuzi.
13 Na wale walio waasi-imani moyoni wataweka hasira.+
Hawapaswi kulia wapewe msaada kwa sababu amewafunga.
14 Nafsi yao itakufa katika ujana,+
Na uzima wao katikati ya wanaume walio makahaba wa hekaluni.+
15 Atamwokoa mwenye kuteseka katika mateso yake,
Naye atafungua sikio lao katika ukandamizaji huo.
16 Naye hakika pia atakushawishi kutoka katika kinywa cha taabu!+
Mahali penye nafasi,+ wala si penye kufinyana, patakuwa badala yake,
Na faraja ya meza yako itajaa unono.+
17 Wewe hakika utajaa adhabu ya hukumu juu ya mwovu;+
Adhabu ya hukumu na haki zitathibitika.
18 Ili uwe mwangalifu kwamba ghadhabu+ isikushawishi upige makofi ya chuki,
Wala usiache fidia+ kubwa ikupotoshe.
19 Je, kilio chako cha kuomba msaada kitakuwa na matokeo?+ Hapana, wala katika taabu
Hata jitihada zako zote zenye nguvu.+
20 Usipumue kwa kutamani usiku,
Wakati watu wanaporudi kutoka mahali walipo.
21 Jilinde usigeukie jambo lenye kudhuru,+
Kwa maana umelichagua hilo badala ya mateso.+
22 Tazama! kwa nguvu zake, Mungu mwenyewe hutenda kwa njia iliyoinuliwa;
Ni nani aliye mfundishaji kama yeye?
23 Ni nani amemtaka atoe hesabu juu ya njia yake,+
Na ni nani amesema, ‘Wewe umetenda ukosefu wa uadilifu’?+
24 Kumbuka kwamba unapaswa kutukuza utendaji wake+
Ambao wanadamu wameimba juu yake.+
25 Wanadamu wote wameutazama;
Mwanadamu anayeweza kufa anaendelea kutazama toka mbali.+
26 Tazama! Mungu ameinuliwa sana kuliko tunavyoweza kujua;+
Hesabu ya miaka yake haichunguziki.+
27 Kwa maana yeye huyateka matone ya maji;+
Yanajichuja kama mvua yawe ukungu wake,
28 Hivi kwamba mawingu yanadondoka,+
Yanadondoka kwa wingi juu ya wanadamu.
29 Kwa kweli, ni nani anayeweza kuelewa tabaka za mawingu,
Mngurumo kutoka katika kibanda chake?+
30 Tazama! Ametandaza juu yake nuru yake,+
Naye ameifunika mizizi ya bahari.
31 Kwa maana kwa hizo yeye hutetea kesi ya vikundi vya watu;+
Hutoa chakula kwa wingi.+
32 Amefunika umeme katika mikono yake,
Naye huweka amri juu yake dhidi ya mshambuliaji.+
33 Kunguruma+ kwake hueleza habari zake,
Mifugo pia kuhusu yule anayekuja.