Zaburi
Ya Daudi.
144 Na abarikiwe Yehova Mwamba wangu,+
Anayeifundisha mikono yangu kwa ajili ya kupigana,+
Vidole vyangu kwa ajili ya vita;
2 Fadhili zangu zenye upendo na ngome yangu,+
Kilele changu salama na Mwokoaji wangu,+
Ngao+ yangu na Yeye ambaye nimemkimbilia,+
Yule anayevitiisha vikundi vya watu chini yangu.+
7 Unyooshe mikono yako kutoka katika kilele;+
Uniweke huru na kunikomboa kutoka katika maji mengi,+
Kutoka kwa mkono wa wageni,+
8 Ambao kinywa chao kimesema mambo yasiyo ya kweli+
Na ambao mkono wao wa kuume ni mkono wa kuume wa uwongo.+
10 Wewe unayewapa wafalme wokovu,+
Wewe unayemweka Daudi mtumishi wako huru kutokana na upanga wenye kuumiza.+
11 Uniweke huru na kunikomboa kutoka kwa mkono wa wageni,+
Ambao kinywa chao kimesema mambo yasiyo ya kweli+
Na ambao mkono wao wa kuume ni mkono wa kuume wa uwongo,+
12 Wanaosema: “Wana wetu ni kama mimea michanga iliyokua wakati wa ujana wao,+
Binti zetu ni kama nguzo za pembeni zilizochongwa kwa mtindo wa jumba la mfalme,
13 Maghala yetu yamejaa, yakitoa mali za aina moja baada ya nyingine,+
Makundi yetu yanaongezeka kwa maelfu, elfu kumi kwa moja, kwenye barabara zetu,
14 Ng’ombe zetu ni wazito, bila mpasuko wala mimba kutoka,+
Na hakuna kilio katika viwanja vyetu vya watu wote.+