Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora.+ Muziki.
49 Sikieni hili, enyi vikundi vyote vya watu.
Tegeni sikio, enyi wakaaji wote wa mfumo wa mambo,+
2 Enyi wana wa wanadamu, naam, ninyi wana wa binadamu.
Wewe tajiri pamoja nawe maskini.+
3 Kinywa changu mwenyewe kitasema mambo ya hekima,+
Na moyo wangu utatafakari mambo ya uelewaji.+
4 Nitatega sikio langu nisikie maneno ya kimethali;+
Nitafumbua kitendawili+ changu kwa kinubi.
5 Kwa nini niogope katika siku za uovu,+
Wakati ambapo kosa la wanaonipindua linanizingira?+
6 Wale wanaotegemea riziki zao,+
Na ambao wanaendelea kujisifu juu ya wingi wa utajiri wao,+
7 Hakuna hata mmoja wao anayeweza kumkomboa hata ndugu,+
Wala kumpa Mungu fidia kwa ajili yake;
8 (Nayo bei ya ukombozi wa nafsi yao ni yenye thamani sana+
Hivi kwamba imekoma mpaka wakati usio na kipimo)
9 Hivi kwamba yeye aendelee kuishi milele na asilione shimo.+
10 Kwa maana yeye huona kwamba hata wenye hekima wanakufa,+
Mjinga na asiyetumia akili huangamia wote pamoja,+
Nao hulazimika kuwaachia wengine mali yao.+
11 Tamaa yao ya ndani ni kwamba nyumba zao ziwepo mpaka wakati usio na kipimo,+
Maskani zao mpaka kizazi baada ya kizazi.+
Wameyaita mashamba yao kwa majina yao.+
12 Na bado mtu wa udongo, ingawa katika heshima, hawezi kuendelea kukaa;+
Kwa kweli analingana na wanyama ambao wameangamizwa.+
13 Hiyo ndiyo njia ya wale wenye ujinga,+
Na ya wale wanaowafuata ambao wanapendezwa na maneno yao wenyewe. Sela.
14 Kama kondoo, wao wamewekewa Kaburi;+
Kifo chenyewe kitawachunga;+
Nao wanyoofu watawatawala asubuhi,+
Nayo maumbo yao hayatakosa kuchakaa;+
Kaburi badala ya makao yaliyo juu ni kwa ajili ya kila mmoja.+
15 Hata hivyo, Mungu mwenyewe ataikomboa nafsi yangu kutoka katika mkono wa Kaburi,+
Kwa maana atanipokea. Sela.
16 Usiogope kwa sababu mtu fulani anapata utajiri,+
Kwa sababu utukufu wa nyumba yake unaongezeka,+
17 Kwa maana anapokufa hawezi kuchukua kitu chochote;+
Utukufu wake hautashuka chini pamoja naye.+
18 Kwa maana muda wote wa maisha yake alikuwa akiibariki nafsi yake mwenyewe;+
(Na watu watakusifu kwa sababu unajiendeleza vizuri)+
19 Nafsi yake mwishowe inafikia tu kwenye kizazi cha mababu zake.+
Hawataona nuru tena kamwe.+
20 Mtu wa udongo, ingawa katika heshima, ambaye haelewi,+
Kwa kweli analingana na wanyama ambao wameangamizwa.+