Wimbo wa Sulemani
Wimbo wa Sulemani
1 Wimbo ulio bora,+ ambao ni wa Sulemani:+ 2 “Na anibusu kwa busu za kinywa chake,+ maana maonyesho yako ya mapenzi ni bora kuliko divai.+ 3 Maana harufu ya mafuta yako+ ni nzuri. Kama mafuta yanayomiminwa, ndivyo lilivyo jina lako.+ Hiyo ndiyo sababu wanawali wamekupenda. 4 Nivute nyuma yako;+ na tukimbie. Mfalme ameniingiza katika vyumba vyake vya ndani!+ Na tufurahi na kushangilia katika wewe. Na tutaje maonyesho yako ya mapenzi kuliko divai.+ Wamekupenda inavyostahili.+
5 “Mimi ni msichana mweusi, lakini mwenye kupendeza, enyi binti za Yerusalemu,+ kama mahema ya Kedari,+ tena kama vitambaa vya mahema+ ya Sulemani. 6 Msinitazame kwa sababu mimi ni mweusi, kwa sababu jua limeniunguza. Wana wa mama yangu mwenyewe walinikasirikia; waliniweka kuwa mtunzaji wa mashamba ya mizabibu,+ ijapokuwa sikulitunza shamba langu mwenyewe la mizabibu.
7 “Niambie, ewe ambaye nafsi yangu imekupenda,+ mahali unapochunga,+ mahali unapolaza kundi katikati ya mchana. Kwa nini niwe kama mwanamke aliyefungwa nguo za maombolezo kati ya makundi ya wenzako?”
8 “Ikiwa wewe mwenyewe hujui, ewe uliye mrembo zaidi kati ya wanawake,+ nenda mwenyewe katika nyayo za kundi uchunge wana-mbuzi wako kando ya maskani za wachungaji.”
9 “Nimekufananisha na farasi-jike wangu katika magari ya Farao,+ ewe msichana mwenzi wangu.+ 10 Mashavu yako yanapendeza kati ya nywele zilizosukwa, shingo yako katika mkufu wa shanga.+ 11 Tutakufanyia vitaji vya dhahabu,+ pamoja na vifungo vya fedha.”
12 “Maadamu mfalme yupo penye meza yake ya mviringo, marashi+ yangu mwenyewe ya nardo yametoa harufu+ yake nzuri. 13 Kwangu mimi mpenzi wangu ni kama mfuko wa manemane;+ katikati ya maziwa+ yangu atalala usiku kucha. 14 Kama kishada cha hina+ ndivyo alivyo mpenzi wangu kwangu, kati ya mashamba ya mizabibu ya En-gedi.”+
15 “Tazama! Wewe ni mrembo, ewe msichana mwenzi wangu.+ Tazama! Wewe ni mrembo. Macho yako ni kama ya njiwa.”+
16 “Tazama! Wewe ni mrembo,+ mpenzi wangu, pia mwenye kupendeza. Pia kitanda+ chetu ni cha majani. 17 Nguzo za nyumba yetu kuu ni mierezi,+ maboriti yetu ni miberoshi.