1 Timotheo
Ikiwa mwanamume yeyote anajitahidi kufikia cheo cha mwangalizi,+ yeye anatamani kazi njema. 2 Kwa hiyo mwangalizi anapaswa kuwa asiyelaumika,+ mume wa mke mmoja, mwenye kiasi+ katika mazoea, mwenye utimamu wa akili,+ mwenye utaratibu,+ mkaribishaji-wageni,+ mwenye sifa za kustahili kufundisha,+ 3 si mlevi mwenye fujo,+ si mwenye kupiga watu,+ bali mwenye usawaziko,+ si mtaka-vita,+ si mwenye kupenda pesa,+ 4 mwanamume anayeisimamia nyumba yake mwenyewe kwa njia nzuri,+ mwenye watoto wanaojitiisha pamoja na kuchukua mambo kwa uzito wote;+ 5 (kwa kweli ikiwa mtu yeyote hajui jinsi ya kuisimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje kutaniko la Mungu?) 6 si mtu aliyegeuka hivi karibuni,+ asije akajivuna kwa kiburi+ na kuanguka katika hukumu iliyopitishwa juu ya Ibilisi.+ 7 Zaidi ya hayo, anapaswa pia kuwa na ushuhuda mzuri kutoka kwa watu walio nje,+ ili asianguke katika shutuma na mtego+ wa Ibilisi.
8 Vivyo hivyo watumishi wa huduma+ wanapaswa kuwa wenye kuchukua mambo kwa uzito, si wenye ndimi mbili, si wenye kunywa divai nyingi, si wenye pupa ya pato lisilo la haki,+ 9 wakiishika siri takatifu+ ya imani kwa dhamiri safi.+
10 Pia, acha hao wajaribiwe+ juu ya kufaa kwanza, kisha watumike wakiwa wahudumu, kwa kuwa hawana shtaka.+
11 Vivyo hivyo wanawake wanapaswa kuwa wenye kuchukua mambo kwa uzito, si wenye uchongezi,+ wawe wenye kiasi+ katika mazoea, waaminifu katika mambo yote.+
12 Watumishi wa huduma na wawe waume wa mke mmoja,+ wakisimamia kwa njia nzuri watoto na nyumba zao wenyewe.+ 13 Kwa maana wanaume wanaohudumu kwa njia nzuri wanajipatia wenyewe msimamo mzuri+ na uhuru mwingi wa kusema+ katika imani kuhusiana na Kristo Yesu.
14 Ninakuandikia mambo haya, ingawa ninatumaini kuja kwako upesi,+ 15 lakini nikichelewa, ili ujue jinsi unavyopaswa kujiendesha katika nyumba ya Mungu,+ ambayo ni kutaniko la Mungu aliye hai, nguzo na tegemezo+ la ile kweli. 16 Kwa kweli, ni jambo lenye kukubalika kwamba siri takatifu+ ya huu ujitoaji-kimungu ni kubwa: ‘Yeye alifunuliwa katika mwili,+ alitangazwa kuwa mwadilifu katika roho,+ alionekana kwa malaika,+ alihubiriwa kati ya mataifa,+ aliaminiwa katika ulimwengu,+ alipokewa juu katika utukufu.’+