Waebrania
5 Kwa maana kila kuhani mkuu anayechukuliwa kutoka kati ya wanadamu huwekwa rasmi kwa ajili ya wanadamu juu ya mambo yanayohusiana na Mungu,+ ili atoe zawadi na dhabihu kwa ajili ya dhambi.+ 2 Yeye anaweza kuwatendea kwa kiasi wale wasiojua na wanaokosea kwa kuwa yeye pia amezungukwa na udhaifu wake mwenyewe,+ 3 na kwa sababu ya huo ana wajibu wa kutoa matoleo ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe kama vile kwa ajili ya watu.+
4 Pia, mtu huchukua heshima hii, si kwa kupenda kwake mwenyewe,+ bali tu Mungu anapomwita,+ kama Haruni+ pia alivyoitwa. 5 Vivyo hivyo pia Kristo hakujitukuza mwenyewe+ kwa kuwa kuhani mkuu,+ bali alitukuzwa+ na yeye aliyesema hivi kumhusu: “Wewe ni mwanangu; mimi, leo, nimekuwa baba yako.”+ 6 Kama vile anavyosema pia mahali pengine: “Wewe ni kuhani milele kwa mfano wa Melkizedeki.”+
7 Katika siku za mwili wake wenye nyama Kristo alitoa dua na pia maombi+ kwa Yule aliyekuwa na uwezo wa kumwokoa kutoka katika kifo, pamoja na vilio vyenye nguvu+ na machozi, naye akasikiwa vizuri kwa sababu ya kumwogopa+ Mungu. 8 Ijapokuwa yeye alikuwa Mwana, alijifunza kutii kutokana na mambo aliyoteseka;+ 9 na baada ya yeye kufanywa kuwa mkamilifu+ akawa ndiye mwenye daraka la wokovu+ wa milele kwa wale wote wanaomtii,+ 10 kwa sababu Mungu amemwita jina, kuhani mkuu kwa mfano wa Melkizedeki.+
11 Kumhusu yeye sisi tuna mengi ya kusema na yaliyo magumu kufafanuliwa, kwa kuwa mmekuwa wazito katika kusikia kwenu.+ 12 Kwa maana, kwa kweli, ijapokuwa mnapaswa kuwa walimu+ kwa sababu ya wakati, ninyi mnahitaji tena mtu awafundishe tangu mwanzo mambo ya msingi+ ya maneno matakatifu ya Mungu;+ nanyi mmekuwa kama wanaohitaji maziwa, si chakula kigumu.+ 13 Kwa maana kila mtu anayetumia maziwa hafahamu neno la uadilifu, kwa maana yeye ni mtoto mchanga.+ 14 Lakini chakula kigumu ni cha watu wakomavu, cha wale ambao kwa kutumia, nguvu zao za ufahamu+ zimezoezwa kutofautisha yaliyo sawa na yaliyo makosa pia.+