Wafilipi
4 Kwa hiyo, ndugu zangu wapendwa na wenye kuonewa hamu sana, shangwe yangu na taji langu, simameni imara katika njia hii katika Bwana, wapendwa.
2 Euodia namhimiza kwa bidii na Sintike namhimiza kwa bidii wawe wenye akili ileile katika Bwana. 3 Ndiyo, nakuomba wewe pia, mwenzi wa nira halisi, fuliza kuwasaidia wanawake hawa ambao wamepigana sambamba pamoja nami katika habari njema pamoja na Klementi na vilevile wale wengine kati ya wafanyakazi wenzangu, ambao majina yao yamo katika kitabu cha uhai.
4 Sikuzote shangilieni katika Bwana. Mara moja tena hakika nitasema, Shangilieni! 5 Hali yenu ya kukubali sababu na ijulikane kwa watu wote. Bwana yuko karibu. 6 Msihangaikie kitu chochote, bali katika kila jambo kwa sala na dua pamoja na utoaji-shukrani acheni maombi yenu ya bidii yajulishwe kwa Mungu; 7 na amani ya Mungu izidiyo fikira yote kwa ubora italinda mioyo yenu na nguvu zenu za akili kwa njia ya Kristo Yesu.
8 Mwishowe, akina ndugu, mambo yoyote yaliyo ya kweli, mambo yoyote yaliyo ya hangaikio zito, mambo yoyote yaliyo ya uadilifu, mambo yoyote yaliyo safi kiadili, mambo yoyote yaliyo ya kupendeka, mambo yoyote yaliyo ya kusemwa vema, wema wa adili wowote ulioko na jambo lolote la kustahili sifa likiwako, endeleeni kufikiria mambo haya. 9 Mambo mliyojifunza na vilevile mkayapokea na kuyasikia na kuyaona kuhusiana nami, zoeeni kuyafanya haya; na Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi.
10 Nashangilia sana katika Bwana kwamba sasa mwishowe nyinyi mmeamsha fikira yenu kwa niaba yangu, ambayo kwa kweli mlikuwa mkiifikiria, lakini mkakosa fursa. 11 Si kwamba ninasema kwa habari ya kuwa katika uhitaji, kwa maana nimejifunza, kuwa mwenye ujitoshelevu, mwenyewe katika hali zozote nilimo. 12 Kwa kweli najua jinsi ya kupungukiwa na maandalizi, kwa kweli najua jinsi ya kuwa na wingi. Katika kila jambo na katika hali zote nimejifunza siri ya jinsi ya kushiba na pia jinsi ya kuwa na njaa, jinsi ya kuwa na wingi na pia jinsi ya kupatwa na uhitaji. 13 Kwa mambo yote ninayo nguvu kwa njia ya yeye anipaye nguvu.
14 Hata hivyo, mlitenda vema kuwa washiriki pamoja nami katika dhiki yangu. 15 Kwa kweli, nyinyi Wafilipi, mwajua pia kwamba katika mwanzoni mwa kutangaza habari njema, nilipoondoka Makedonia, hakuna kutaniko hata moja lililoshiriki pamoja nami katika jambo la kutoa na kupokea, ila nyinyi peke yenu; 16 kwa sababu, hata katika Thesalonike, nyinyi mlinipelekea kitu fulani mara moja na vilevile mara ya pili kwa ajili ya uhitaji wangu. 17 Si kwamba ninaitafuta zawadi kwa bidii, ila ninatafuta kwa bidii matunda yaletayo sifa zaidi kwenye hesabu yenu. 18 Hata hivyo, mimi nina vitu vyote kwa ukamili na nina wingi. Nimejaa, kwa kuwa sasa nimepokea kutoka kwa Epafrodito vitu vilivyotoka kwenu, harufu inayonukia utamu, dhabihu yenye kukubalika, yenye kupendeza vema kwa Mungu. 19 Naye, Mungu wangu atawajazia kikamili uhitaji wenu wote kwa kadiri ya utajiri wake katika utukufu kwa njia ya Kristo Yesu. 20 Sasa kwa Mungu na Baba yetu uwe utukufu milele na milele. Ameni.
21 Mpeni kila mtakatifu salamu zangu katika muungano na Kristo Yesu. Akina ndugu walio pamoja nami wawapelekea nyinyi salamu zao. 22 Watakatifu wote, lakini hasa wale wa nyumbani mwa Kaisari, wawapelekea nyinyi salamu zao.
23 Fadhili isiyostahiliwa ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na roho ambayo mwaonyesha.