Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 2:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Lakini kuhusu matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula, utakufa hakika.”+

  • Mwanzo 3:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Kwa jasho la uso wako utakula mkate mpaka utakaporudi katika udongo, kwa kuwa ulitolewa katika huo.+ Kwa maana wewe ni mavumbi nawe utarudi mavumbini.”+

  • Zaburi 146:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  4 Roho yake hutoka,+ naye hurudi kwenye udongo wake;+

      Siku hiyo mawazo yake hupotea.+

  • Methali 21:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Mtu anayeiacha njia ya ufahamu,+ atapumzika katika kutaniko la wale wasiojiweza katika kifo.+

  • Mhubiri 6:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Hata ikiwa ameishi miaka elfu moja mara mbili na bado hajaona yaliyo mema,+ je, kila mtu haendi mahali pamoja?+

  • Mhubiri 9:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Kwa maana walio hai wanajua kwamba watakufa;+ lakini wafu, hawajui lolote kamwe,+ wala hawana malipo tena, kwa maana kumbukumbu lao limesahauliwa.+

  • Ezekieli 18:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Tazama! Nafsi zote—ni zangu.+ Kama ilivyo nafsi+ ya baba ndivyo ilivyo nafsi ya mwana—ni zangu.+ Nafsi inayotenda dhambi+—hiyo yenyewe itakufa.+

  • Waroma 6:23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 Kwa maana mshahara ambao dhambi hulipa ni kifo,+ lakini zawadi+ ambayo Mungu hutoa ni uzima wa milele+ kupitia Kristo Yesu Bwana wetu.+

  • 1 Wakorintho 15:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Kwa maana kama vile katika Adamu wote wanakufa,+ vivyo hivyo pia katika Kristo wote watafanywa kuwa hai.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki