7 Na ilaaniwe hasira yao,+ kwa sababu ni katili,+ na ghadhabu yao, kwa sababu hutenda kwa ukali.+ Acheni niwagawanye katika Yakobo na kuwatawanya katika Israeli.+
32 “‘Na kuhusu majiji ya Walawi pamoja na nyumba za majiji ya miliki yao,+ haki ya kukomboa itaendelea mpaka wakati usio na kipimo kwa ajili ya Walawi.+
18“Hakuna fungu au urithi pamoja na Israeli litakalokuja kuwa la makuhani, Walawi,+ kabila zima la Lawi. Matoleo yanayotolewa kwa njia ya moto kwa Yehova, naam, urithi wake, watayala.+
4 Kwa maana wana wa Yosefu walikuwa wamekuwa makabila mawili,+ Manase+ na Efraimu;+ nao hawakuwa wamewapa Walawi fungu katika nchi, isipokuwa majiji+ ya kukaa na viwanja vyao vya malisho kwa ajili ya mifugo yao na mali zao.+
2 kisha wakasema nao huko Shilo+ katika nchi ya Kanaani, wakiwaambia: “Yehova alitoa amri kupitia Musa kwamba sisi tupewe majiji ya kukaa, pamoja na viwanja vyake vya malisho kwa ajili ya wanyama wetu wa kufugwa.”+