7 Baada ya hapo watumishi wa Farao wakamwambia: “Mtu huyu ataendelea kuwa mtego+ kwetu mpaka wakati gani? Waruhusu watu waende zao ili wamtumikie Yehova Mungu wao. Je, bado hujajua kwamba Misri imeangamia?”+
17 Mwishowe Sauli akamwambia Daudi: “Huyu hapa Merabu binti yangu mkubwa zaidi.+ Yeye ndiye nitakayekupa awe mke wako.+ Ila tu jionyeshe kwangu kuwa shujaa na upigane vita vya Yehova.”+ Lakini Sauli alisema moyoni mwake hivi: “Mkono wangu usije juu yake, lakini mkono wa Wafilisti uje juu yake.”+
8 Ulimi wao ni mshale unaoua.+ Huo umesema udanganyifu. Kwa kinywa chake, mtu anaendelea kusema amani pamoja na mwenzake; lakini ndani yake anaweka mavizio yake.”+