7 Naye mtu asiye na msimamo, vyombo vyake ni vibaya;+ yeye ametoa shauri kwa ajili ya matendo ya mwenendo mpotovu,+ kuwavunja wenye kuteseka kwa maneno ya uwongo,+ hata maskini anaposema jambo lililo haki.
3 ninyi ambao pia mmekula nyama ya watu wangu,+ na mmeichuna ngozi yao kutoka kwao, mkaivunja vipande-vipande mifupa yao, na kuiponda vipande-vipande kama kitu kilicho katika chungu chenye mdomo mpana na kama nyama ndani ya chungu cha kupikia.+
14 Kwa fimbo zake mwenyewe ulikichoma+ kichwa cha mashujaa wake wa vita waliposonga kama tufani ili kunitawanya.+ Upeo wao wa raha ulikuwa kama wa wale wanaokusudia kummeza mwenye kuteseka katika maficho.+
4 Tazama! Mishahara iliyo haki ya wafanyakazi waliovuna mashamba yenu lakini ambayo mmeizuilia,+ inaendelea kupaaza kilio,+ na vilio vya kuomba msaada+ vya wavunaji vimeingia masikioni+ mwa Yehova wa majeshi.