Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 1:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Msipendelee katika hukumu.+ Msikilizeni mdogo sawa na mkubwa.+ Msiogope kwa sababu ya mwanadamu,+ kwa maana hukumu ni ya Mungu;+ na kesi ambayo ni ngumu mno kwenu, nileteeni, nami nitaisikiliza.’+

  • 2 Samweli 8:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Na Daudi akaendelea kutawala juu ya Israeli+ yote; na Daudi akaendelea kutoa uamuzi wa hukumu na uadilifu+ kwa ajili ya watu wake wote.+

  • Zaburi 58:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Nao wanadamu watasema:+ “Kwa kweli kuna matunda kwa ajili ya mwadilifu.+

      Kwa kweli kuna Mungu ambaye anahukumu duniani.”+

  • Zaburi 72:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  2 Na atetee kesi ya watu wako kwa uadilifu+

      Na ya watu wako wenye kuteseka kwa hukumu.+

  • Isaya 11:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Naye atawahukumu kwa uadilifu watu wa hali ya chini,+ atakaripia kwa unyoofu kwa ajili ya watu wapole wa dunia. Naye ataipiga dunia kwa fimbo ya kinywa chake;+ na kumuua mwovu kwa roho ya midomo yake.+

  • Yeremia 22:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Yehova amesema hivi: “Toeni haki na uadilifu, nanyi mumkomboe yeye anayenyang’anywa kutoka mkononi mwa mpunjaji; wala msimtendee vibaya mkaaji mgeni yeyote, mvulana asiye na baba au mjane.+ Msiwatendee jeuri yoyote.+ Wala msimwage damu yoyote isiyo na hatia mahali hapa.+

  • Yohana 7:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Acheni kuhukumu kwa sura ya nje, bali hukumuni kwa hukumu ya uadilifu.”+

  • Waebrania 1:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Uliupenda uadilifu, nawe ukauchukia uasi-sheria. Ndiyo sababu Mungu, Mungu wako, alikutia mafuta+ kwa mafuta ya kushangilia kuliko wenzako.”+

  • Ufunuo 19:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Nami nikaona mbingu imefunguliwa, na, tazama! farasi mweupe.+ Na yeye aliyeketi juu yake anaitwa Mwaminifu+ na wa Kweli,+ naye anahukumu na kufanya vita kwa uadilifu.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki