17 Msipendelee katika hukumu.+ Msikilizeni mdogo sawa na mkubwa.+ Msiogope kwa sababu ya mwanadamu,+ kwa maana hukumu ni ya Mungu;+ na kesi ambayo ni ngumu mno kwenu, nileteeni, nami nitaisikiliza.’+
4 Naye atawahukumu kwa uadilifu watu wa hali ya chini,+ atakaripia kwa unyoofu kwa ajili ya watu wapole wa dunia. Naye ataipiga dunia kwa fimbo ya kinywa chake;+ na kumuua mwovu kwa roho ya midomo yake.+
3 Yehova amesema hivi: “Toeni haki na uadilifu, nanyi mumkomboe yeye anayenyang’anywa kutoka mkononi mwa mpunjaji; wala msimtendee vibaya mkaaji mgeni yeyote, mvulana asiye na baba au mjane.+ Msiwatendee jeuri yoyote.+ Wala msimwage damu yoyote isiyo na hatia mahali hapa.+
11 Nami nikaona mbingu imefunguliwa, na, tazama! farasi mweupe.+ Na yeye aliyeketi juu yake anaitwa Mwaminifu+ na wa Kweli,+ naye anahukumu na kufanya vita kwa uadilifu.+