Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 24:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Katika siku yake utampa malipo yake,+ nalo jua lisitue juu yake, kwa sababu yeye yuko katika taabu naye anaiinua nafsi yake kwa malipo yake; ili asimlilie Yehova juu yako,+ na iwe dhambi kwako.+

  • Zaburi 12:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  5 “Kwa sababu ya kuporwa kwao wenye kuteseka, kwa sababu ya kuugua kwao maskini,+

      Nitasimama wakati huu,” asema Yehova.+

      “Nitamweka katika usalama mbali na mtu yeyote anayemdhihaki.”+

  • Methali 17:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Anayemdhihaki maskini anamletea shutuma Mtengenezaji+ wake. Anayeshangilia msiba wa mwingine hatakosa adhabu.+

  • Mhubiri 5:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Ukimwona mtu yeyote maskini akionewa na hukumu+ na uadilifu zikitwaliwa kijeuri katika wilaya ya utawala, usishangazwe na jambo hilo,+ kwa maana aliye juu zaidi kuliko yule aliye juu+ anaangalia,+ na kuna wale walio juu yao.

  • Waroma 15:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Kwa maana hata Kristo hakujipendeza mwenyewe;+ bali kama ilivyoandikwa: “Shutuma za wale waliokuwa wanakushutumu zimeniangukia.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki