5 Ndipo vichwa+ vya upande wa baba vya Yuda na vya Benyamini na makuhani na Walawi wakasimama, ndiyo, kila mmoja ambaye Mungu wa kweli aliiamsha roho+ yake, ili kwenda kujenga upya nyumba ya Yehova,+ iliyokuwa Yerusalemu.
3 “Nami nitakusanya mabaki ya kondoo zangu kutoka katika nchi zote ambako nilikuwa nimewatawanya,+ nami nitawarudisha kwenye uwanja wao wa malisho,+ na hakika wao watazaa na kuwa wengi.+
17 “Kwa hiyo sema, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Pia nitawakusanya ninyi kutoka kwa vikundi vya watu na kuwakusanya ninyi kutoka katika nchi ambazo katikati yake mmetawanywa, nami nitawapa ninyi udongo wa Israeli.+
11 Na wana wa Yuda na wana wa Israeli hakika watakusanywa pamoja katika umoja+ nao kwa kweli watajiwekea kichwa kimoja nao watatoka katika ile nchi,+ kwa maana siku ya Yezreeli+ itakuwa kuu.