Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 29:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 “Na itatukia kwamba wakati ambapo mtu atakuwa amesikia maneno ya kiapo hiki,+ naye amejibariki moyoni mwake, na kusema, ‘Nitakuwa na amani,+ ijapokuwa nitatembea katika ukaidi wa moyo wangu,’+ kwa kusudi la kumfagilia mbali aliyenyweshwa maji vizuri pamoja na mwenye kiu,

  • Yeremia 5:23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 Lakini hawa watu wamekuwa na moyo mgumu na wenye kuasi; wamegeuka kando nao wanaendelea kutembea katika mwendo wao.+

  • Yeremia 23:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Wanawaambia tena na tena wale ambao hawaniheshimu, ‘Yehova amesema: “Ninyi mtakuwa na amani.”’+ Nao wamemwambia kila mtu anayetembea katika ukaidi wa moyo wake,+ ‘Hamtapatwa na msiba wowote.’+

  • Ezekieli 3:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Lakini nyumba ya Israeli, hawatataka kukusikiliza wewe, kwa maana hawataki kunisikiliza mimi;+ kwa sababu wote hao wa nyumba ya Israeli wana vichwa vigumu na mioyo migumu.+

  • Hosea 4:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Kwa maana, kama vile ng’ombe mkaidi, ndivyo Israeli amekuwa mkaidi.+ Je, ni wakati huu kwamba Yehova atawachunga kama vile mwana-kondoo dume katika mahali penye nafasi pana?

  • Zekaria 7:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Nayo mioyo yao+ wakaifanya kuwa kama jiwe gumu ili isitii sheria+ na maneno ambayo Yehova wa majeshi alipeleka kwa roho yake,+ kupitia manabii wa kale;+ hata Yehova wa majeshi akakasirika sana.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki