24 “‘Msijifanye wenyewe kuwa wasio safi kwa lolote la mambo hayo, kwa sababu kwa mambo yote hayo mataifa ninayoyafukuza kutoka mbele yenu yamejifanya yenyewe kuwa si safi.+
33 “‘Nanyi msiichafue nchi mliyo ndani yake; kwa sababu damu ndiyo inayoichafua nchi,+ na kwa ajili ya nchi hakuwezi kuwa na upatanisho kuhusu damu ambayo imemwagwa juu yake isipokuwa kwa damu ya yule anayeimwaga.+
23 maiti yake isibaki usiku kucha juu ya mti;+ bali kwa vyovyote utamzika siku hiyo, kwa sababu mtu aliyetundikwa ni kitu kilicholaaniwa na Mungu;+ nawe usiitie unajisi nchi yako, ambayo Yehova Mungu wako anakupa iwe urithi.+
18 Na, kwanza kabisa, nitalipa kiwango kamili cha kosa+ lao na cha dhambi yao, kwa sababu waliitia nchi yangu unajisi.+ Walikuwa wameujaza urithi wangu mizoga ya machukizo yao na vinyaa vyao.’”+
17 “Mwana wa binadamu, nyumba ya Israeli walikuwa wakikaa katika nchi yao, nao wakaendelea kuichafua kwa njia yao na kwa matendo yao.+ Njia yao imekuwa mbele zangu kama uchafu wa hedhi.+