Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo ya Walawi 18:25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 Kwa hiyo nchi si safi, nami nitaleta adhabu kwa ajili ya kosa lake juu yake, nayo nchi itawatapika wakaaji wake.+

  • Zaburi 106:38
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 38 Kwa hiyo wakaendelea kumwaga damu isiyo na hatia,+

      Damu ya wana wao na binti zao,

      Ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani;+

      Na nchi ikachafuliwa na umwagaji wa damu.+

  • Isaya 24:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Nayo nchi imechafuliwa chini ya wakaaji wake,+ kwa maana wamezivunja sheria,+ wamelibadili sharti,+ wamevunja agano linalodumu mpaka wakati usio na kipimo.+

  • Yeremia 2:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 “Nami mwishowe nikawaleta ninyi katika nchi yenye mashamba ya matunda, ili mle matunda yake na vitu vyake vyema.+ Lakini mkaingia na kuitia unajisi nchi yangu; nanyi mkaufanya urithi wangu kuwa chukizo.+

  • Yeremia 3:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Kuna msemo: “Mwanamume akimwacha mke wake na mke huyo aondoke kwake na kuwa wa mwanamume mwingine, je, mwanamume huyo anapaswa kurudi kwake tena?”+

      Je, nchi hiyo haikutiwa unajisi hakika?+

      “Nawe mwenyewe umefanya ukahaba pamoja na rafiki wengi;+ na je, unapaswa kurudi kwangu mimi?”+ asema Yehova.

  • Yeremia 16:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Na, kwanza kabisa, nitalipa kiwango kamili cha kosa+ lao na cha dhambi yao, kwa sababu waliitia nchi yangu unajisi.+ Walikuwa wameujaza urithi wangu mizoga ya machukizo yao na vinyaa vyao.’”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki