Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 3:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Nami ninashuka ili kuwakomboa kutoka katika mkono wa Wamisri+ na kuwatoa katika nchi hiyo mpaka kwenye nchi nzuri na kubwa, nchi inayotiririka maziwa na asali,+ kwa Wakanaani na Wahiti na Waamori na Waperizi na Wahivi na Wayebusi.+

  • Mambo ya Walawi 20:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Ndipo nikawaambia ninyi:+ “Ninyi mtaimiliki nchi yao, nami nitawapa ninyi ili mwimiliki, nchi inayotiririka maziwa na asali.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu, ambaye nimewatenga kutoka kwa vikundi vya watu.”+

  • Kumbukumbu la Torati 6:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Nawe usikilize, Ee Israeli, nawe uwe mwangalifu kuzitenda,+ ili mambo yakuendee vema+ nanyi mpate kuwa wengi sana, kama vile ambavyo Yehova Mungu wa mababu zako amekuahidi wewe,+ kuhusu nchi inayotiririka maziwa na asali.

  • Yoshua 5:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Kwa maana wana wa Israeli walikuwa wametembea miaka 40+ nyikani, mpaka lilipokwisha taifa lote la wale wanaume wa vita waliotoka Misri ambao hawakuisikiliza sauti ya Yehova, ambao Yehova alikuwa amewaapia kwamba hatawaruhusu kamwe waione nchi+ ambayo Yehova alikuwa amewaapia mababu zao kwamba atatupa sisi,+ nchi inayotiririka maziwa na asali.+

  • Ezekieli 20:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Katika siku hiyo niliuinua mkono+ katika kiapo kwao ili kuwatoa katika nchi ya Misri mpaka katika nchi niliyokuwa nimeipeleleza kwa ajili yao, yenye kutiririka maziwa na asali.+ Hiyo ilikuwa ni pambo la nchi zote.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki