Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Mambo ya Nyakati 36:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Lakini waliendelea kuwadhihaki+ wale wajumbe wa Mungu wa kweli na kuyadharau maneno+ yake na kuwafanyia mzaha+ manabii wake, mpaka ghadhabu+ ya Yehova ikapanda juu ya watu wake, mpaka kukawa hakuna kuponywa.+

  • Nehemia 9:33
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 33 Nawe ni mwadilifu+ kuhusu mambo yote ambayo yametupata, kwa maana umetenda kwa uaminifu,+ lakini sisi ndio tumetenda kwa uovu.+

  • Yeremia 30:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Wale wote wanaokupenda sana ndio wale ambao wamekusahau.+ Si wewe ambaye wanaendelea kukutafuta. Kwa maana nimekupiga kwa pigo la adui,+ kwa adhabu ya mtu mkatili,+ kwa sababu ya wingi wa makosa yako;+ dhambi zako zimekuwa nyingi.+

  • Maombolezo 1:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Yehova ni mwadilifu,+ kwa maana nimekiasi kinywa chake.+

      Sikilizeni sasa, enyi nyote vikundi vya watu, na mwone maumivu yangu.

      Mabikira wangu na vijana wangu wameenda utekwani.+

  • Ezekieli 8:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Naye akaendelea kuniambia: “Je, umeona hili, Ee mwana wa binadamu? Je, ni jambo dogo sana kwa nyumba ya Yuda kufanya machukizo ambayo wamefanya hapa, kwamba waijaze nchi jeuri+ na kwamba wanitie uchungu tena, na tazama, wananyoosha lile chipukizi kuelekea pua yangu?

  • Danieli 9:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Kwako wewe, Ee Yehova, kuna uadilifu, lakini kwetu sisi kuna aibu ya uso kama ilivyo leo hii,+ kwa watu wa Yuda na kwa wakaaji wa Yerusalemu na kwa watu wote wa Israeli, wale walio karibu na wale walio mbali katika nchi zote ambako uliwatawanya kwa sababu ya ukosefu wao wa uaminifu waliokutendea.+

  • Danieli 9:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Ee Yehova, kulingana na matendo yako yote ya uadilifu,+ tafadhali, hasira yako na ghadhabu yako na zigeuke kutoka kwenye jiji lako Yerusalemu, mlima wako mtakatifu;+ kwa maana Yerusalemu na watu wako ni vitu vya kushutumiwa na watu wote wanaotuzunguka+ kwa sababu ya dhambi zetu na kwa sababu ya makosa ya mababu zetu.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki