Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 32:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Kisha akaichukua dhahabu hiyo toka mikononi mwao, naye akaifanya+ kwa kifaa cha kuchongea na kuifanya kuwa sanamu ya kuyeyushwa ya ndama.+ Nao wakaanza kusema: “Huyu ndiye Mungu wako, Ee Israeli, aliyekuongoza kutoka nchi ya Misri.”+

  • Waamuzi 17:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Basi akamrudishia mama yake fedha hizo, kisha mama yake akachukua vipande mia mbili vya fedha akampa fundi wa fedha.+ Naye akatengeneza sanamu ya kuchongwa+ na sanamu ya kuyeyushwa;+ nayo ikawa katika nyumba ya Mika.

  • Isaya 46:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Kuna wale wanaotoa dhahabu kwa wingi katika kikoba, nao hupima fedha kwa mizani. Wanamwajiri fundi wa chuma, naye huifanya kuwa mungu.+ Wanasujudu, ndiyo, wanainama.+

  • Hosea 8:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Wao wenyewe wameweka wafalme,+ lakini si kwa sababu yangu. Wameweka wakuu, lakini mimi sikuwa na habari. Wamejifanyia sanamu+ kwa fedha yao na dhahabu yao, kusudi wakatiliwe mbali.+

  • Hosea 13:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Na sasa wanafanya dhambi zaidi na kujifanyia sanamu ya kuyeyushwa kutoka kwenye fedha+ yao, sanamu kulingana na uelewaji wao wenyewe,+ yote hiyo ni kazi ya mafundi.+ Nao wanaziambia, ‘Acheni wanadamu wanaotoa dhabihu wabusu ndama.’+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki