4 Kisha akaichukua dhahabu hiyo toka mikononi mwao, naye akaifanya+ kwa kifaa cha kuchongea na kuifanya kuwa sanamu ya kuyeyushwa ya ndama.+ Nao wakaanza kusema: “Huyu ndiye Mungu wako, Ee Israeli, aliyekuongoza kutoka nchi ya Misri.”+
4 Basi akamrudishia mama yake fedha hizo, kisha mama yake akachukua vipande mia mbili vya fedha akampa fundi wa fedha.+ Naye akatengeneza sanamu ya kuchongwa+ na sanamu ya kuyeyushwa;+ nayo ikawa katika nyumba ya Mika.
6 Kuna wale wanaotoa dhahabu kwa wingi katika kikoba, nao hupima fedha kwa mizani. Wanamwajiri fundi wa chuma, naye huifanya kuwa mungu.+ Wanasujudu, ndiyo, wanainama.+
4 Wao wenyewe wameweka wafalme,+ lakini si kwa sababu yangu. Wameweka wakuu, lakini mimi sikuwa na habari. Wamejifanyia sanamu+ kwa fedha yao na dhahabu yao, kusudi wakatiliwe mbali.+
2 Na sasa wanafanya dhambi zaidi na kujifanyia sanamu ya kuyeyushwa kutoka kwenye fedha+ yao, sanamu kulingana na uelewaji wao wenyewe,+ yote hiyo ni kazi ya mafundi.+ Nao wanaziambia, ‘Acheni wanadamu wanaotoa dhabihu wabusu ndama.’+