-
1 Samweli 7:3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Na Samweli akaiambia nyumba yote ya Israeli: “Ikiwa mnarudi kwa Yehova+ kwa mioyo yenu yote, ondoeni miungu ya kigeni iliyo katikati yenu+ na pia zile sanamu za Ashtorethi,+ nanyi mwelekeze mioyo yenu kwa Yehova bila kuyumba-yumba, mkamtumikie yeye peke yake,+ naye atawakomboa kutoka mkono wa Wafilisti.”+
-
-
2 Mambo ya Nyakati 30:6Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Kwa hiyo wakimbiaji+ walio na zile barua kutoka katika mkono wa mfalme na wa wakuu+ wake wakaenda katika Israeli yote na Yuda, kulingana na amri ya mfalme, na kusema: “Ninyi wana wa Israeli, rudini+ kwa Yehova Mungu+ wa Abrahamu, Isaka na Israeli, ili yeye arudi kwa wale walioponyoka+ ambao wamebaki kati yenu kutoka katika mkono wa wafalme wa Ashuru.+
-