Hosea
12 “Efraimu anajilisha upepo+ na kufukuza upepo wa mashariki siku nzima.+ Anazidisha uwongo na uporaji.+ Nao hufanya agano na Ashuru,+ na mafuta hupelekwa Misri.
2 “Naye Yehova ana kesi na Yuda,+ kumtoza Yakobo hesabu kulingana na njia zake;+ atamlipa kulingana na matendo yake.+ 3 Alimkamata ndugu yake kwenye kisigino ndani ya tumbo,+ na kwa nguvu zake zenye msukumo alishindana na Mungu.+ 4 Akaendelea kushindana na malaika, naye mwishowe akashinda.+ Alilia, ili apate kujiombea kibali kwa bidii.”+
Alimkuta Betheli,+ na huko Yeye akaanza kusema nasi.+ 5 Na Yehova Mungu wa majeshi,+ Yehova ni ukumbusho wake.+
6 “Na wewe inakupasa kurudi kwa Mungu wako,+ ushike fadhili zenye upendo+ na haki;+ nawe umtumaini Mungu wako sikuzote.+ 7 Mfanya-biashara ana mizani ya udanganyifu mkononi mwake;+ amependa kupunja.+ 8 Na Efraimu anaendelea kusema, ‘Kwa kweli nimekuwa tajiri;+ nimejipatia vitu vyenye thamani.+ Na kuhusu kazi yangu yote ya kutaabika, hawatanipata nikiwa na kosa lililo dhambi.’+
9 “Lakini mimi ni Yehova Mungu wako kuanzia nchi ya Misri.+ Na bado nitakufanya ukae katika mahema kama katika siku za wakati uliowekwa. 10 Nami nilisema na manabii,+ nikazidisha maono, nikaendelea kutoa mifano kupitia mkono wa manabii.+
11 “Mambo ya uchawi,+ pia yasiyo ya kweli,+ yametokea Gileadi. Wametoa dhabihu za ng’ombe katika Gilgali.+ Zaidi ya hayo, madhabahu zao ni kama mafungu ya mawe katika matuta ya shamba.+ 12 Na Yakobo akakimbia kwenda katika nchi ya Siria,+ na Israeli+ akaendelea kutumikia apate mke,+ naye akalinda kondoo apate mke.+ 13 Na Yehova kupitia nabii akaleta Israeli kutoka Misri,+ naye akalindwa kupitia nabii.+ 14 Efraimu alichukiza akatia uchungu,+ na matendo yake ya kumwaga damu anayaacha juu yake mwenyewe,+ na Bwana-Mkuu wake atamlipa yeye shutuma zake.”+